Tatizo ni hao wanaoliongoza kanisa.
Je wamehitimu miongozo ya Kanisa ?
Wakati huu kuna baadhi ya watu wanaanzisha kanisa wakiwa na Sera yao binafsi ya kujipatia kipato toka kwa waumini.
Kanisa linageuzwa kama kampuni ya kuingiza pesa na sio kuhubiri habari njema ya Kristo.
Mtu akiona hana mwelekeo wa kiuchumi basi anaenda Serikalini na anasajiri kanisa.
Vigezo vilivyowekwa na Serikali ili kumruhusu mtu kuanzisha kanisa ni tofauti kabisa na vigezo alivyoviweka Yesu Kristo.
Ndio maana tunaona baadhi ya makanisa waumini wanalishwa nyoka, mhubiri anasimama juu ya watu, wanawake wanavuliwa nguo, wanabakwa, wanazalishwa, nk. na baadhi ya viongozi wa baadhi ya makanisa ya zama hizi.
Mtu anaanzisha kanisa wakati hajasoma hata mstari mmoja wa Biblia na inawezekana hajawahi kuiona na kuishika.
Ndio maana Bwana Yesu alitahadharisha kuwa
" hapo baadae kutatokea manabii wengi wa uwongo, watakaowadanganya wengi na hata waumini kwa mbembwe zao hivyo kabla ya kuwaamini wapimeni maneno yao na matendo yao kama yanalingana na maagizo niliyowaachia "
Leo hii watu wakisikia tu flani kaanzisha kanisa bila kuangalia kushoto na kulia wanajiunga mojakwamoja kwenye ibada zake athari zake ndio hizo.
Nabii Tito alipata waumini haraka haraka na isingekuwa kukatazwa na Serikali leo hii kanisa lake linge jaa waumini.
Wakati muunini anaenda kanisani huku hajui lolote la kwenye Biblia, anakutana na Nabii ambaye naye hajui lolote la kwenye Biblia kama (Nabii Tito)
Hapo mchezo ndipo unapoanza kupendeza.
Kanisa lililo timiza vigezo kamwe haliwezi kuumiza waumini wake.
Kanisa kama la Mchungaji Mwakasege ni mojawapo ya Kanisa lenye vigezo vya Kristo mwenyewe.
Waumini mjihadhari.