Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,790
- 24,382
Nimepitia majina ya timu za taifa kwa mataifa yote ya Afrika nikahisi kuwa Tanzania, Ghana na Kenya inabidi tubadilishe majina yatu; neno "stars" linakuwa monontonous. Somalia na South Sudan wamelitumia pia lakini kwao wamelitumia taifauti na sis. Hebu angalia halafu utoe maoni yako.
- Algeria - The Greens au Desert Warriors (Wapiganaji wa jangwani)
- Angola - Black Sable Antelopes (Tandala Weusi)
- Benin - The Cheetahs (Duma)
- Botswana - The Zebras (Pundamilia)
- Burkina Faso - The Stallions (Farasi wa kiume)
- Burundi- The Swallows (Mbayuwayu)
- Cameroon - The Indomitable Lions (Simba wasiofugika)
- Cape Verde -Blue Sharks (Papa wa bluu)
- Central African Republic - The Wild Beasts (Wanyama pori wakali)
- Chad - Les Sao (Wazawa wa Sao) - Sao ilikuwa ni himaya ya zamani sana huko Chad
- Comoros - The Coelacanths (Hawa ni samaki wanopatikana Comoros, Tanzania, Madagascar na Mozambiki tu; sikuweza kupata jina lao kwa kiswahili)
- Congo (Republic) - The Red Devils (Shetani wekundu)
- Djibouti -Shoremen of the Red Sea (Watu wa pwani ya bahari nyekunu) - Djibout inapakana na bahari nyekundu.
- Congo (DRC)- The Leopards (Chui)
- Egypt (Misri)- The Pharaohs (Watawala wa Zamani wa Misri)
- Equatorial Guinea - National Thunder (Radi ya taifa)
- Eritrea - Red Sea Camels (Ngamia wa bahari Nyekundu) - Eritrea nayo inapakana na bahari nyekundu.
- Eswatini - King's Shield (Ngao ya Mfalme)
- Ethiopia The Walia Ibex (Mbuzi pori)
- Gambia - The Scorpions (Nge)
- Ghana- Black Stars (Nyota nyeusi) ???? !!! ???? !!!
- Guinea - National Elephants (tembo wa taifa)
- Guinnea Bissau - The Dromedaries (Ngamia wenye nundu moja)
- Ivory Coast -The Elephants (Tembo)
- Kenya - Harambee Stars (Nyota za Harambee) ???? !!! ???? !!!
- Lesotho- Crocodiles (Mamba)
- Liberia - The Lone Stars (Nyota wapwekwe)
- Libya - The Mediterranean Knights (Askari maalum wa Mediteraneae) - Libya inapakana na bahari ya Mediteranean.
- Madagascar - Barea (Ng'ombe mkubwa)- Barea ni aina ya ng'ombe wakubwa wanaopatikana Madgascar tu.
- Malawi- The Flames (Ndimi za moto)
- Mali- The Eagles (Tai - ndege siyo vazi)
- Mauritania- Lions of Chinguetti (Simba wa Chinguetti)- Chinguetti ni kijiji fulani huko jangwani ndani ya Mauritania kilichokuwa maarufu sana kwa biashara enzi za zamani.
- Mauritius - The Dodos (Ndege wa Zamani aliyekuwa anapatika Mauritius tu) - Ndege huyu alishatoweka.
- Mayotte - Seahorses (farasi wa majini)
- Morocco - The Atlas Lions (Simba wa jangwani)
- Mozambique - The Mambas (Nyoka wenye sumu kali)
- Namibia - Namibia Warriors (Wapiganaji wa Namibia)
- Niger - Ménas (Mtakatifu Menas wa Misri)
- Nigeriua - Super Eagles (Tai wakubwa kuliko wote)
- Reunion - Club R (Timu R, wakifupisha jina la Reunion)
- Rwanda - Amavubi (manyigu)
- Sao Tome - Warriors of the Equator (wapiganaji wa ikweta) - Timu hii ina majina matatu lakini hili ndilo linajulikana zaidi kwa wapenzi wake, jingine ni The Elephants (tembo), na Falcons and True Parrots Team (timu ya vipanga na kasuku)
- Senegal - Lions of Teranga (Simba wa Teranga) - teranga ina maana ya uungwana na upole, kwa hiyo timu hiyo ni "Simba wa Unngwana"
- Seyschells - The Pirates (maharamia wa baharini)
- Sierra Leone - Leone Stars (Nyota wa Leone). Jina hili linahitaji maelezo marefu kidogo lakini nitaliacha hivyo hivyo kwani unahitaji kujua maana ya "Sierra Leone" kwanza kabla ya kuvuta neno "Leone."
- Somalia - The Ocean Stars (Nyota wa baharini)
- South Africa - Bafana Bafana (Wavulana)
- South Sudan - Bright Stars (Nyota zinazong'ara)
- Sudan - Falcons of Jediane ( Vipanga wa Jediane)- Jadiena kwa kisudani ina maana ya ndege ajulikanye kama secretary bird anyatesfrika kwa kiswhali kama ndege kilemba or karani tamba. Muungano wa kipanga na karani tamba sikuweza kutafasri.
- Tanzania - Taifa Stars (Nyota wa Taifa) ???? !!! ???? !!!
- Togo - The Sparrowhawks (Vipanga wadogo wadogo)
- Tunisia - Eagles of Carthage (Tai wa carthage) - cartahge ni mji wa zamani sana nchini Tunisia ulikuwa na maendeleo sana lakini baadaye ulibomolewa na utawala wa warumi baada ya kukataa kutii amri za mtawala wa roma.
- Uganda - The Cranes (Korongo - ndege siyo korongo la ardhi)
- Zambia - Chipolopolo (Risasi za Shaba)
- Zimbabwe - The Warriors (Wapiganaji)