Majibu ya Tuhuma Dhidi Yangu!

Majibu ya Tuhuma Dhidi Yangu!

Umesema kuwa hujihusishi na uendeshaji wa biashara ya kampuni kama mtendaji wa kila siku.

Kwamba kampuni ya Emergent Africa Ltd ina watumishi wake sehemu mbalimbali.

Anayetakiwa kukanusha hayo madai ni wewe mwenye hisa 40% au ni kampuni ya Emergent Africa Ltd?

Could this be another one man company or a family company?

Could this company be a sham or mere a façade concealing the truth facts?

Would you mind us piercing the corporate veil to know what is going behind?

I was about to ask the question mkubwa. Sasa kigangwallah anajibu kama mwanahisa au msemaji wa kampuni, na alishaeleza kwenye pragragh hapo juu kwamba kampuni ina wafanyakazi wanaojitegemea (separate management unit).
 
Kabla hujawa mbunge three years ago ulikuwa na nini na sasa una nini? Kwanini unatoa maelezo ya miaka hiyo badala ya ku-stick on point?

Jiangalie kama vipi kafungue kesi ya kusafisha jina lako kwani kuna ushaidi mkubwa dhidi yako.

Mwisho jipime!!

anaitumia taasisi ya mama salma {WAMA} Kukwepa kodi na kufanya biashara.
 
kujibu tuhuma umejishusha sana kwa 7bu kwanza umeshndwa kujitetea pili ultakiwa kujibu pale mwandish alipokupgia lakn hukutaka kuongea nae,sasa unataka kutuaminisha nini?
 
Kigwangalla ukimaliza Kujibu hilo soo, jibu na hili na ufujaji soo jipya Kwa Kigwangalla.jpg
 
Hivi mkiishi bila kutuibia ninyi ma CCM mnajisikiaje???
 
moto2012 Kigwa hawez kujibu hayo maswali.. Ataishia kusema kuwa wewe ni Bashe kwa hiyo unataka kumchafua. Huwa anatememea kutetea uovu wake kwa kudai kuwa mahasimu wake wa kisiasa wanamjengea tuhuma kutokana na wivu..

Bashe ni wa Nzega, hata simjui, ni bora nimkomalie Jenister Mhagama mbunge wangu,
 
Mheshimia pole achana na hili gazeti la udaku linaloandika habari bila kuwa na uhakika, maelezo yako yamejitosheleza.
 
Aise mchango wako umenivutia zaidi.


A lie has speed,but truth has endurance

Asante sana, ninaumia sana ninpoona vijana wanatamalaki kwa ofisadi na pia kuzisusa taaluma zao kwa sababu ya siasa!

Wadogo na watoto wetu watajfunza nini?
 
HKigwangalla
JF imeharibiwa na watu wenye roho za husda; nadhani wameshtushwa sana na jitihada zako unazozifanya badala ya kuomba ushauri nao wafanye kitu gani wamegeuka ni watu waliokata tamaa ya maisha hasira zao wanataka kuzimaliza kwako; nakupa pole sana kwa hilo endelea na jitihada zako mradi ukifanikiwa hautawasaidia wana CCM peke yao naamini lengo ni kuwasaidia watanzania wote hususani kina mama na watoto
Chama
Gongo la mboto DSM


Chama, you giving this gentleman a deceitful opinion that will render him fragile. Kwenye maelezo yake amesema day to day activities are shouldered not by him but other people presumably "management". Sasa yeye kama uendeshaji wa kampuni hayumo anaeza kutuhakikishia kuwa waendeshaji wa kampuni hawawezi kutumia kampuni yenye msamaha wa deemed capital goods na kuvileta na kuviuza sokoni? Na kwanini anataka ushahidi wa rist na hankara? Kwenye deal ambazo ni illegal nanai yuko tayari kutoa vielelzo anavyotaka? Wote tunaishi hapa bongo ambapo integrity is questionable and ethics fading away. Na yeye hilo analijua bali anataka kulikwepa. Na kwa sababu amakeuja na hoja nyepesi kama kamba za buibui amekosa consistency kwenye maelezo yake. Mwambie asijihaibishe kwa kuja na majibu yanayokinzana
 
Last edited by a moderator:
Pole sana Mkuu Hkigwangala kama ni kweli umepakaziwa,

lakin tatizo siku za hivi karibuni umekuwa kama mwigulu kwa siasa zako za uropokaji kwa ajili ya kujipendekeza kwa mabwana zako na usipobadilika basi pia usiwe mwepesi wa kulalamika pale utakapoguswa.

BTW: kila kheri.
 
H kigwangala ni Fisadi na mhujumu uchumi. Hiyo aliyofanya inafanywa na MaCCM wengi ndio chanzo cha kuuwa ajira, ubunifu, na ushindani wa kweli wa biashara. Hayamkini hata Ubunge ni rushwa na maisha yake ni Rushwa hawezi kusimamia hata wale aliopata nao udaktari ingawaje yeye kwa jina bandia.

Hawa ndio viongozi wa CCM ukiweza kusoma kwa jina la kuiba huwezi shindwa kuiba lolote au chochote. Kuanzia uraia famba, jina famba, na sasa anatupiga kwenye kodi zetu. 2015 ataijua nguvu ya umma maana yake nini.
 
Hamisi Kigwangallah ni Mbunge, Kitendo chakuja jamvini kudanganya watu kwa sababu ya stori iliyoandikwa na gazeti la Tanzania daima, na kumbeza Mwandishi wa stori hiyo kuwa amedanganya. Sijui Mwandishi huyo kama ataendelea au ataacha, ila kwa sababu ya uongo uliozushwa na Kigwangalla anayejiita Mwadilifu. Huyu kijana ni Mwizi, anadharau watanzania kwa kuwaona ni wajinga, wasio na akili. Kwa maneno yake mwenyewe kwenye tamko lake amesema anamiliki 40%, na 11% ni za mke wake. Aje jamvini kama alivyofanya jana aseme amedanganya TIC au amedanganya jamvini, na kwa manufaa gani anahadaa watu jamvini.......... sio mwadilifu, ananitishia maisha sasa. angalieni mnaomwona Kigwangalla kuwa wa maana kumbe ni wale wale tu, anamtukana mwandishi wa Tanzania daima, kale kajamaa ka Tanzania daima kako makini Kigwangalla omba radhi jamvini, jiuzulu utumishi wa umma, umejivunjia heshima
..huyu kijana muhuni....anataka kudanganya watu..anafikiri wote mazuzu humu....Ukitazama majibu yake anaandika utafikiri hajasoma chuo...daktari mzima aibu tu....Majibu yake anadanganya..maana anajua hata lengo la kutaka kuanzisha chuo ni la kibinafsi...yaani anatumia njia ya kudanganya anaanzisha chuo ili apate hizo tax weivers.....at the end of the day anajipatia materials kwa ajili ya biashara zake.....otherwise kuna sababu gani kwa yeye kudanganya umiliki wa hisa kwenye kampuni yake na mkewe???.....hakuna kinachoweza kuelezea hilo zaidi ya usanii.....kama kawaida yao....huwa wanaanza hivi hivi hawa.....mwishowe wanakua mafisadi wakubwa.....kwa kupitia ccm yao.....
 
Mheshimiwa Mbunge nina swali la nyongeza: Uzalendo wako uko wapi kwa kununua cement ya kigeni wakati inapatikana ndani ya nchi? Kwanini ukanushe wewe hali wewe siyo mtendaji?
 
Kwamba wewe ni graduate wa MD,MPH na MBA kweli its another silly academic ground! Bahati nzuri mimi nimesoma na wewe na ubabaishaji wako haujaanza leo hata darasani ulikuwa mbabaishaji hata kitaaluma ulikuwa unaibia mno. Mimi nakusikitikia kwa namna ulivyoanza kuwa mnafiki lakini 2015 huwezi kubaki salama. Kimsingi huna mvuto tena na wewe ni mwizi tu najua tabia zako na huwezi kuacha. Bwana mdogo nikusihi kwamba umeingia choo cha kike na itakula kwako!
 
Mkuu CHAMA na wewe unaunga mkono upuuzi huu.Ifike mahali tuweke pembeni itikadi zetu za kisiasa kwa ajili ya kuliokoa Taifa letu.Mbali na tuhuma anazo tuhumiwa nazo ziwe za kweli zisiwe za kweli.Ukiyasoma maelezo yake inaonekana ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana kifedha.Mtu ambae hakusitahili hata kusamehewa kulipa kodi na serekali yetu kama ingekuwa makini kama alisamehewa kweli kwa mjibu wa maelezo yake yasiyo na ushahidi.Huu ni upuuzi mwingine tunao upinga unaofanywa na serekali yetu.Mtu mwenye uwezo mkubwa kabisa wa kulipa kodi anasamehewa kulipa kodi huku mwananchi ambae ni masikini kabisa ambae anatakiwa kusaidiwa anapelekewa mgambo kupigwa mabuti ili aweze kulipa kodi kwa nguvu pengine na kufungwa kabisa.Eti tajilri mkubwa kabisa mwenye nazo anasamehewa kulipa kodi na yeye bila hata chembe ya aibu anajitokeza hadharani nimesamehewa kulipa kodi na serekali kwa kisingizio cha kujenga Chuo cha afya.Hicho chuo cha afya kitakuwa kinatoa huduma bure kwa mwananchi?.
chama amejawa na mahaba na CCM.

Yeye ni mtetezi wa chochote kinachomhusisha kiongozi wa CCM au CCM kama taasisi.

Tumeshamwelewa hivyo.
 
1.Kigwangala
2.Nchimbi
3.Kinana
4.Lowasa
5.Sitta
6.Kapuya
Pamoja na wabunge wengine wengi wa CCM mmelifilisi taifa letu kwa kiasi kikubwa sana tena bila hata huruma mnatetea mpaka na ujangili wa wazi ambao nyara zimeshikwa mkononi, kwamba vifaa vya usafiri ni vya Kinana ila bidhaa iliyopakakiwa si yake!Okey endeleeni lakini ipo siku mtakujajuta muda si mrefu, kwa sasa bado dua zetu tunazielekeza kwa Mungu na kuyalaani haya mnayotufanyia
Hata mungu anasema tuwe wapole kiasi
sasa muda si mrefu tutaondoa na hiyo kiasi
Wazee tuanze kutafutana nyumba kwa nyumba,mtu kwa mtu hapo ndipo heshima itapatikana
Sio unajitetea namna hiyo ukafikiri sisi hatuna akili ila wewe unazo ndio maana unamiliki kampuni poa hamna noma hizo fedha si uliokota?
 
Umesema kuwa hujihusishi na uendeshaji wa biashara ya kampuni kama mtendaji wa kila siku.

Kwamba kampuni ya Emergent Africa Ltd ina watumishi wake sehemu mbalimbali.

Anayetakiwa kukanusha hayo madai ni wewe mwenye hisa 40% au ni kampuni ya Emergent Africa Ltd?

Could this be another one man company or a family company?

Could this company be a sham or mere a façade concealing the truth facts?

Would you mind us piercing the corporate veil to know what is going behind?

I agree with you and that was my thought.
 
Back
Top Bottom