Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.
Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?
Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.
Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.
Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.
Reference: https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mgawo-wa-maji-watikisa-mijini-vijijini-3974394
Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
- Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
- Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
- Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
- Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?
Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.
Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.
Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.
Reference: https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mgawo-wa-maji-watikisa-mijini-vijijini-3974394