KERO Wakazi wa Mtaa wa Mshikamano -Mbezi Louis (Dar) hatuna huduma ya maji na Mamlaka zipo kimya

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Huku Mbezi Louis maeneo ya Mtaa wa Mshikamano Jijini Dar es Salaam hakuna maji ni mwezi sasa (Hadi muda naandika andiko hili Februari 10, 2024).

Mara chache yanayoka usiku mwingi, Watu wanasumbuka kuamka mida hiyo na kukuta maji yanayotoka ni machafu balaa.

Imagine kukaa mwezi mzima maji yanasumbua na hakuna taarifa yoyote kutoka kwa mamlaka.

Serikali ya mtaa haitoi taarifa yoyote na DAWASA nao wamekaa kimya. Hii inamaanisha nini kwa wakazi wa huku? Hili joto linaloendelea hapa wanategemea watu wanaishi vipi?

Sasa tunashangaa hatutangaziwi uhaba wa maji wakati mvua zimenyesha kwa muda mrefu sana. Kwani kuna shida gani kutuambia kuwa ratiba ya maji itakuwa ni kila baada ya wiki na yatatoka usiku wa manane tu?

Kwakweli Mbunge wa Ubungo na viongozi wa Halmashauri ya Ubungo wanatuangusha sana jamani.

Tunaomba serikali ifanye kutatua hii changamoto. Kama kuna matengenezo ya mabomba tuambiwe. Kama kuna uhaba wa maji tuambiwe.

Uongozi unaokalia taarifa kwa mtindo huu unatia mashaka sana. Viongozi wa serikali za mtaa hadi Halmashauri wanapaswa kuwajibika kwa hili. Kukalia taarifa si jambo zuri. Ni aidha watuambie hatutapata maji kabisa au watuambie ni lini yatapatikana.

Mtu unataka kujisaidia ila hata ukienda baa nako hakuna maji. Hii si sawa kabisa. Tunataka maji yatoke leo, vinginevyo tujulishwe lini yatatoka lini.

==== =====

Jamii Forums imezungumza na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, Baraka Mwaijande kuhusu changamoto hiyo amesema “Kweli changamto hiyo ipo, uwepo wa changamoto ya umeme umesababisha hali hiyo ya maji.

“Nawasiliana na DAWASA ambao wanafanya kazi kwa bidi kule Ruvu ili huduma ipatikane, kumbuka kuwa mitambo yao inatumia umeme na hivyo kama hakuna umeme wa uhakika basi hata ufanyaji kazi pia unakuwa hauna ubora.

“Madai kuwa kuna maji machafu yanayotoka usiku hilo sijawahi kuliona wala kupata malalamiko hayo.”
 
Kwamba mitambo yao inatumia umeme, umeme unaposumbua mashine hazisukumi maji. Yaani hawa hawajui kuwa ni LAZIMA wawe na mbadala wa umeme wa TANESCO?

Na tatizo hili la Umeme ni cancer, means miaka yote hiyo hawafikirii kuwa na plan B ili ku remedy tatizo hili, why Dar kusijengwe dams za kuvuna maji wakati wa masika,then maji haya yatumike kwa wakazi wa Dar?,je hii ni rocket science kujenga dams?
 
Na CCM watapata kura za kutosha uchaguzi serikali za mitaa na ule mkuu...
 
......kwamba mitambo yao inatumia umeme,umeme unaposumbua machines hazisukumi maji, ngoja niendelee kunywa ulanzi wangu huku lingusenguse, yaani wapumbavu hawa hawajui kuwa ni LAZIMA wawe na mbadala wa umeme wa tanesco?,na tatizo hili la umeme ni cancer, means miaka yote hiyo hawafikirii kuwa na plan B ili ku remedy tatizo hili, why Dar kusijengwe dams za kuvuna maji wakati wa masika,then maji haya yatumike kwa wakazi wa Dar?,je hii ni rocket science kujenga dams?

CCM na serikali yake wanasubiria maji ya mto Ruvu yajae wakati wa masika...
 
Kama kichwa cha habari kinavyosema, wana Mbezi Makabe tumefungiwa mabomba ya maji takriban miezi 6 sasa ila kwa sasa ni muda wa takriban miezi miwili maji hayatoki.

Tumekuwa tunawasiliana na mamlaka ya maji ofisi ya makono juu, menja ambaye ni mwana mama amekuwa anatupa ahadi zisizo tekelezeka, kila siku kisingizio eti kuna tatizo kwenye chanzo cha maji. Naomba mamlaka ziangalie kwa kina suala hili, inaonesha kuna harufu ya hujuma ili wanaouza maji ya mtaani wapate fursa mithili ile hujuma inayosemwa upande wa majenereta. Haiingii akilini wafanyakazi eti wanazunguka mtaani kusoma mita za maji ili hali wanajua maji hayatoki ni miezi sasa.

Mamlaka za serikali , tafadhali angalieni huenda hawa watendaji wana nia mbaya ya kuwagombanisha wananchi na mamlaka za juu.
 
Back
Top Bottom