Majani yenye sumu yadaiwa kuwa chanzo cha ng’ombe 15 kufa wilayani Monduli

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Ng’ombe 15 wamekufa katika kijiji cha Losirwa wilayani Monduli Mkoa wa Arusha wakidaiwa kuwa wamekula majani yenye sumu yaliyoota maeneo mbalimbali kijijini hapo.

Akizungumzia suala hilo mkuu wa wilaya ya Monduli, Fank Mwaisumbe amesema hadi jana zaidi ya ng'ombe 15 wamekufa kwa kula majani hayo.

Ngombe.jpg


"Nimepata taarifa za mifugo kufa kutokana na majani hayo na sasa tumeagiza ifukiwe ili watu wasile mizoga yake kwani ni sumu," amesema akibainisha kuwa uzikaji wa mifugo hiyo unasimamiwa na polisi ili kuhakikisha hakuna watu watakaokula mizoga.

Mmoja wa wafugaji, Lememo Mollel amesema,”hii sio mara ya kwanza mifugo kufa kila baada ya ukame kutokea, mvua zikianza kunyesha majani yenye sumu huota na mifugo wakila hayo majani wanakufa.”

Hata hivyo, aliomba Serikali kusaidia upatikanaji wa malisho ya mifugo hasa kipindi hiki cha ukame.

Daktari wa Mifugo wa shirika la kilimo na chakula la umoja wa mataifa (FAO), Moses Ole-Neselle amesema kufa mifugo kunatokana na kula majani mabichi yenye sumu kutokana na kutokamaa.

"Mifugo inakufa pia kwa sababu bado utumbo haujazoea kula majani mabichi ambayo hayajakomaa baada ya kiangazi kwanza huwa wanaharisha na wengine kufa kabisa," amesema.

Chanzo: Mwananchi
 
15 x 700k = 10,500,000 + mahitaji mengineyo = 14,500,000

hayo majani yataftwe yaangamizwe
 
Hata ukanda huu wa pwani haya majani yanasumbuwa sana hayana chakipindi cha ukame wala kipindi cha malisho mabichi, yanatia hasara hayo balaa mnayama anavimba tumbo na kushindwa kuhema ana kufa kwa taabu sana, yamasha nipotezea Mbuzi wengi sana.
 
Ng’ombe 15 wamekufa katika kijiji cha Losirwa wilayani Monduli Mkoa wa Arusha wakidaiwa kuwa wamekula majani yenye sumu yaliyoota maeneo mbalimbali kijijini hapo.

Akizungumzia suala hilo mkuu wa wilaya ya Monduli, Fank Mwaisumbe amesema hadi jana zaidi ya ng'ombe 15 wamekufa kwa kula majani hayo.

View attachment 2429519

"Nimepata taarifa za mifugo kufa kutokana na majani hayo na sasa tumeagiza ifukiwe ili watu wasile mizoga yake kwani ni sumu," amesema akibainisha kuwa uzikaji wa mifugo hiyo unasimamiwa na polisi ili kuhakikisha hakuna watu watakaokula mizoga.

Mmoja wa wafugaji, Lememo Mollel amesema,”hii sio mara ya kwanza mifugo kufa kila baada ya ukame kutokea, mvua zikianza kunyesha majani yenye sumu huota na mifugo wakila hayo majani wanakufa.”

Hata hivyo, aliomba Serikali kusaidia upatikanaji wa malisho ya mifugo hasa kipindi hiki cha ukame.

Daktari wa Mifugo wa shirika la kilimo na chakula la umoja wa mataifa (FAO), Moses Ole-Neselle amesema kufa mifugo kunatokana na kula majani mabichi yenye sumu kutokana na kutokamaa.

"Mifugo inakufa pia kwa sababu bado utumbo haujazoea kula majani mabichi ambayo hayajakomaa baada ya kiangazi kwanza huwa wanaharisha na wengine kufa kabisa," amesema.

Chanzo: Mwananchi
Pole sana kwa wafugaji ambao wamekuwa wakipoteza wanayama wao kila msimu wa kuanza Mvua

Bahati mbaya ni kwamba kinachofanya wanayama wao wafe kipindi cha kuanza Mvua sio majani yenye sumu bali ni yale majani machanga ambayo yanaota Kwa haraka haraka pindi Mvua zinaponyesha kukiwa na kipindi cha ukame

Majani yanapoota kipindi cha ukame huota yakiwa na kiwango kidogo sana au hayana kabisa madini ya Magnesium na wakati huo huo yanakuwa na kiwango kikubwa sana cha madini ya potassium

Kutokuwepo Kwa madini ya Magnesium au kuwa na wingi wa madini ya potassium hufanya Damu kuwa na madini kiasi kidogo zaidi cha magnesium na kupelekea mnyama kushindwa kucheuwa na tumbo kujaa gas

Baada ya tumbo kuwa limejaa gas ambayo haitoki kufanya tumbo kuvimba sana na kugandamiza baadhi ya organ's ikiwemo mapafu na kufanya mnyama awe na kiasi kidogo cha oxygen katika Damu na kupelekea mnyama kupata suffocation

Mnyama kuanza kutoa mapovu mdomoni na puani na hadi kifo kumkuta, na ubaya hili tatizo mara nyingi huwakumba watu wenye Mifugo mingi kwani anakuwa Hana uwezo wa kuwahudumia majani ya kukata au majani makavu, kwahiyo yeye pamoja na wanayama wake wakiona majani yanaota wanaona mkombozi kafika kumbe ni hatari inawaita

Wahanga wakubwa wa hili tatizo ni Ng'ombe ambao wana watoto kwani wao hupoteza madini ya Magnesium Kwa wingi kwenye maziwa na kupelekea kuwa na upungufu wa kiasi kikubwa wa magnesium katika Damu, japokuwa na Ng'ombe wadogo kinachowaponza ni kuyashambulia Kwa wingi hayo majani

Anyway, solution ni kuacha Kulisha wanayama majani ambayo yanaota baada ya kutoka kwenye ukame japokuwa najua hii ni ngumu sana, na kama utalisha basi wale Kwa kiasi kidogo huku wakipewa na majani makavu Kwa kiasi kikubwa

Na kama hiyo haitoshi uhakikishe unawapa wanayama wako madini ya Magnesium Kwa wingi ambayo wafugaji wamezoea kuita (Epsom salt) au chumvi chumvi at least Kwa siku mara 3 ili kuruhusu gas kutoka katika matumbo

Mbali na hayo ila ni kweli kuna majani ya sumu ambayo waga yanadhuru wanayama endapo wakila Kwa bahati mbaya, ila hii ni mara chache kwani asilimia kubwa ya wafugaji wanajua majani ambayo sio mazuri Kwa Afya ya Mifugo yao na waga hawapitishi wala kuchunga sehemu yenye uwepo wa hayo majani
 
Back
Top Bottom