Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 61,023
- 36,865
Yaani ukitaka kujua unachelewa pita njia za Ubungo, Kimara, Mwenge na Tegeta ndani ya dakika 30 utaona ving'ora kama vinne vimepita na vimulimuli
Nimejiuliza hivi kila gari linatakiwa kuwa na king'ora na kimulimuli? Na ni wakati gani vinatakiwa kutumika?
----
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka madereva wa magari ya Serikali kutojihusisha na matumizi ya ving'ora na vimulimuli bila kuwa na maelekezo maalumu, kwa lengo la kuondoa migogoro wakati wa matumizi ya barabara.
"Wengine wanajiwekea ving'ora bila kuwa na ruhusa ya kutumia, na wengine hata vimulimuli ilhali vimulimuli vimeelekezwa kwa watu maalumu. Lengo ni kuondoa migogoro ya barabarani, ambapo kila mmoja anaonekana kuwa na haki sawa," amesema Waziri Mkuu Majaliwa.
Ameyasema hayo katika kongamano la nne la madereva wa Serikali, lililofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Dodoma, leo Septemba 2 2025.
Aidha, amewataka madereva hao wa Serikali kuepuka matumizi ya namba za magari zisizo halali na kuongeza umakini katika kazi zao ili kuepusha ajali.
Nimejiuliza hivi kila gari linatakiwa kuwa na king'ora na kimulimuli? Na ni wakati gani vinatakiwa kutumika?
----
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka madereva wa magari ya Serikali kutojihusisha na matumizi ya ving'ora na vimulimuli bila kuwa na maelekezo maalumu, kwa lengo la kuondoa migogoro wakati wa matumizi ya barabara.
"Wengine wanajiwekea ving'ora bila kuwa na ruhusa ya kutumia, na wengine hata vimulimuli ilhali vimulimuli vimeelekezwa kwa watu maalumu. Lengo ni kuondoa migogoro ya barabarani, ambapo kila mmoja anaonekana kuwa na haki sawa," amesema Waziri Mkuu Majaliwa.
Ameyasema hayo katika kongamano la nne la madereva wa Serikali, lililofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Dodoma, leo Septemba 2 2025.
Aidha, amewataka madereva hao wa Serikali kuepuka matumizi ya namba za magari zisizo halali na kuongeza umakini katika kazi zao ili kuepusha ajali.