Baikije
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 877
- 1,207
Alichoki angeungana tu na nyoshi..naamini wangerudi kwa kishindo Basi tu
Sent using Jamii Forums mobile app
Alilewa sifa akapiga DOCHI Fuko la Hela.BINAFSI MIE NADHANI WANGEENDA VIZURI NA ASHA BARAKA WANGEKUWA WAMESIMAMIA PAZURI KIDOGO TATIZO UJUAJE SANA NA KUPENDWA KULELEWA !!!!!!!
na ilisambaratika baada ya muda mfupi sana. nilishangaa kweli kwa wakongwe kama wale kushindwa kuelewana kiasi kile. nafikiri ndo hivyo kila mmoja alitaka kuwa juu ya wenzieMafahari wawili hawawezi ishi zizi moja. Si wakumbuka walianzishaga bendi choki,banza na muumini ila ilisambaratika vibaya mno
umenena
'wema hawana maisha'.....dah, umenikumbushia mtaalam Patrick Balisidya (R.I.P) katika ile kitu simple lakini very classic, 'ni mashaka na hangaiko'!Hata Aisha Madinda alishafariki. Nilikuwa napenda kuangalia Twanga sababu yake. Kweli wema hawana maisha
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuhonga wanawake ,kuzaa sana mitaani ,kula ngada na pombe ,kuvaa vizuri, hakuna uwekezajiHivi yale mafuba yote waliyokuwa wanavuna tangu enzi za kina marehemu Mpakanjia yameishia wapi
ni kweli kabisa kiongoziKuhonga wanawake ,kuzaa sana mitaani ,kula ngada na pombe ,kuvaa vizuri, hakuna uwekezaji
Wanamziki wa bendi wote maisha yao yanafanana
Wengi wao mdudu anawatafuna kimya kimya
Sent using Jamii Forums mobile app
mbona hata asha baraka anaishi maisha ya kawaida tu na alidai kwenye interview moja kuwa hawakua wakifaidika
Sent from my iPhone using JamiiForums
Post ya juu hapo kuna mkuu ametype kwamba jamaa ni marehemu!!!
Muongo, interview moja ya Charz baba anasema alikuwa akipata hela ya kutunzwa mpaka laki 3 kwa onyesho moja
Sent using Jamii Forums mobile app
aisha alikutana na fikiri madinda stegini ,ivyo ikawa ngumu kumwachisha, pia fikiri alikuwa peneshee kumzibiti mcheza show ni rahisi
note:FIKIRI naye ni marehemu ,pia aisha hakuwa na mtoto
DoohMapedeshee wengi waliokuwa wanaziwezisha hizi bendi wamepigwa pini na huu utawala wa jpm.unaweza kuhusisha na kufulia kwa wanamziki hawa
Sent from my iPhone using JamiiForums
amtumikiae shetani huchakaa mwishowe.
bali amtumikiae Mungu huhuishwa roho na mwili kila iitwapo leo!
Wakati mwingine shetani tunamsingizia sana, upate pesa usijiwekee msingi mzuri ule bata mpaka shilingi ya mwisho ukichoka umsingizie shetani hapana! Kuna wakati hata yeye huwa anatushangaa wanadamuamtumikiae shetani huchakaa mwishowe.
bali amtumikiae Mungu huhuishwa roho na mwili kila iitwapo leo!
Noma sana..Ndugu zangu wana JF, anayopitia Ali Choki, na wengine ndio mfumo mzima wa Maisha ya watanzania. Wao wanajulikana na ndio maana tunawaona kirahisi walivyokuwa sasa tofauti na zamani
Tusiwabeze ndio mfumo ulivyo. Wazazi wetu sisi wengine walikuwa wakubwa serikalini lakini leo tunachangishana watoto kuwakatia Bima za Afya hawana uwezo tena na Maisha yamewapiga wanatutegemea sisi watoto wao. Tusipojipanga vyema na sisi tutakuwa hivyo hivyo tegemezi kwa watoto wetu. Wakati ni ukuta huwezi kubaki juu milele tecnolojia inabadilika na dunia inabadilika vizazi vinabadilika.
Kuna wengi upande wa wafanyakazi na wakulima, Mapedeshee ukiwaona wamefulia tofauti na kipindi cha nyuma
SOMO MUHIMU: Ukiwa juu jitahidi kuwekeza na kujijenga ili wakati unapobadilika ubaki kuwa juu au usitetereke sana