Sikutaka kusema haya usemayo kwasababu utaambiwa unajidai.Mimi situmii chandarua wala dawa ya mbu lakini sijawahi hata kuumwa na malaria. Huyo mbu ndani anaingia kutafuta nini wakati kutwa mlango umefungwa na akikaa lazima afe mwenyewe kwa njaa.
Hahahaaa.. Mama Sabry pole kwa yaliyo kukutaNdio maana mnaamua kuoa ili mpikiwe,mfuliwe,,manaume ya kitz mengi mavivu kweli
Ha ha ha alafu utafikiri hata ulikuwa busy sana, bhasi tu uvivu wa kupikana baada ya nusu saa mtu anakula
![]()
Ukweli mtupu,
ubachela nikuskia njaa ndo kuanza kupika ni ngumu sana kwanza kwangu haijawahi kutokea napika sina njaa au unapika mchele kilo mbili ili uwe unapasha tu kila unaposkia njaa mboga nayo kama sio mchemsho wa nyama basi ni mayai yamekaangwa wengine maharage tunanunua yaliopikwa jero tu afu unayaunga nyumbani.
Viombo vinaoshwa wakati wa kupika tu siku ukibaki home ndo unaosha viwe visafi.
Demu mpya akija ghetto linakua mbingu ya saba clean as f*
Taulo likichafuka ndo story yake imeisha linakua dekio au kutupwa. Hapo tshirt na mashati yanageuzwa taulo
Wanawake ni muhimu sana tuacheni masihara. Tena ka ulikua unakaa na dem ushazoea anarekebisha kila kitu akiondoka tu wiki ya kwanza utamaintain ya piliaah wapi hamna kitu unarudi kule kule.
Huko ni kutojua kupika wala si ubachela,...ubachela unapika ugali mara mbichi
*Fahamu maisha ya ubachela*
Maisha ya ubachela unaweza kuloweka sufuria ulopikia ugali likakaa na maji wiki nzima yakianza kunuka unamwaga halafu unaweka tena maji mengine..
Hahahha Mara unapika wali unatoa kitu bokoooo.au ugali unapika Mara unga unaisha .inakua haielewek ni uji au ugali
Hahahah karoti za kuunga mafuta ilikuwa mboga kuu . wiki nzima ugali na karoti. Samaki ni marufuku Kununua wale wa kubwa.
Kuna tule tudogodogo unakuta fungu LA samak 10 kwa jero...hahahahaha. Mtaa wa kiboloroni raha sana. Mchele ni robo na hauna mboga. Unapika na nyanya kabisaaa huo wali. Unatoka unanukia nyaya...ni balaa.
Siku moja nililetewa maziwa ya mgando ila yalikuwa na maji.
Nikatoa yale maji nkapikia ugali ili nisave mboga.....hahahahah ilishindikana nikamwaga.....
Acha uzembe wewe, tafuna mboga na ratiba nyingine zifuate
unamshauri kabsa! 