Maisha ya ubachela ni vituko

Maisha ya ubachela ni vituko

hamna kazi ngumu kwa Bachelor kuosha vyombo
 
ukiamka unaamka tu na kukurupuka, Kukunja shuka hukunji wala kutandika usiku ndo unakunguta shuka tu unapiga mbonji
Sijawahi kuamka nisikunje shuka na kutandika kitanda aisee! We differ
 
Kufua, kupika, kilufagia, kuosha vyombo (ingawa huwa situmii vyombo vingi ili nisione uvivu kuosha) hvyo vyote kwangu siyo tatzo. Tatz ni kuweka na kutoa Net tu
 
Mbinu za kukabiliana na changamoto za kuosha vyombo ziko zamani.nilikua nachanganya vyombo vyangu na vya mwenye Nyumba kwenye Caro.mwanae anaosha anajua vyao nikirudi jioni navikuta vimeanikwa nachukua.sema walikuja nishtukia nikawa na mpooza dogo na viela vya vocha anaosha
 
Hahaaaaa Kufagia chini ya uvungu vepee..
Kufua, kupika, kilufagia, kuosha vyombo (ingawa huwa situmii vyombo vingi ili nisione uvivu kuosha) hvyo vyote kwangu siyo tatzo. Tatz ni kuweka na kutoa Net tu
 
Kupika soo sana, nakumbuka mamma alituachaga na dingi home akasonga ugali wakati anazungusha dona ikamwangukia kwenye mkuu akaapa hapiki tena mpaka leo
wazee wetu huwa mbwembwe nyingi ila kwenye kupika ndo zero! Umenikumbusha mzee alipika ugali mtepe enzi hizo, sasa ole uinuke mapema, ni nakoz tu
 
*Fahamu maisha ya ubachela*

Maisha ya ubachelor unaweza kujishaua kufululiza kupika msosi hata mwezi mzima ila vyombo visafi vikiisha ndani unarudi kwenye utaratibu ule ule wa kula chipsi na paja la bukujero.Maisha ya ubachela kila siku tunapoteza vijiko kidogo kidogo kwa kumwaga maji ya ukoko wa ugali.

Maisha ya ubachela unaweza kuloweka sufuria ulopikia ugali likakaa na maji wiki nzima yakianza kunuka unamwaga halafu unaweka tena maji mengine.

Maisha ya ubachela mara nyingine neti hugeuka kuwa hema.Ikichomekwa haichomolewi mpaka siku utakapopata mgeni.

Maisha ya ubachela hufika kipindi mtu unageuka mbwa, unanusa kwanza nguo ili ujue kama unaweza kuipa round ya pili au hapana.
Stupid! huo sio ubachela bali ni uchafu
 
Ndio maana mnaamua kuoa ili mpikiwe,mfuliwe,,manaume ya kitz mengi mavivu kweli
 
Mimi ni fundi mzuri wa kupika ugali ila shida ni suala la kuosha vyombo da! Hapa ndo ninapochoka bila kusahau suala pendwa la kunyoosha nguo hii kwangu nayo ni changamoto sana
 
Back
Top Bottom