Maisha ya Dodoma ni Magumu sana

Wakuu habari za jioni? Wiki hii Nilikuwa DODOMA kwa shughuli za Kiofisi,nimependa jinsi jiji la Dodoma linavyokua kwa kasi,Lakini hali ya maisha inaonekana ni ngumu Sana kuliko Dar es salaam.

Nilitafuta guest house, bodabo whyda akaniambia kuwa vyumba vya bei ya chini ni 20,000/=, nikashangaa Sana kwasababu niliwahi kwenda DSM na nikafanikiwa kupata gesti ya 10,000/=, nzuri tu. Chakula kwa Dodoma ndo usiseme,kipimo changu cha kwanza ni kwa Mama ntilie, maana watu wengi wa hali ya chini huenda huko kununua chakula;

Aise kina bei hatari , Kuna sehemu niliambiwa wali nyama 3,000/=,Ugali nyama 3000/=,Wali samaki 3500/=, Ugari Maharage 2000/= na wali Maharage 2500/=, Sehemu nyingi za Mama Ntilie bei ni hizo.Nilipolala ni karibu na Holly Cross Center inayomilikiwa b

Na Kanisa Katoliki Jimbo kuu la DODOMA,Aise hapo kitimoto ya kukaanga kilo ni 10,000/=,Ya kubanikwa ni 12,000/=,Ndizi moja 500/=. Ugari kuku robo 6000/=. Na vyakula vingine bei zipo juu pia.Haya nikasema Niulize Vipi kuhusu nyumba za kupanga?; Kheee!, Bei nilizotajiwa nilishangaa Sana.Twende Bodaboda aisee Hivi kweli kutoka Holly Cross Center hadi Mkonze mtu anaanza na 6000/=baada ya kuvutana Sana ndo anaishia kwenye 4000/=.

Sijauliza viwanja.Nastaajabu kwasababu miaka ya Nyuma DODOMA haikuwa ghali kiasi hicho.Nilijiuliza swali moja kuwa DODOMA ni wafugaji wazuri wa mifugo sasa Kwanini bei ya Nyama ya ng'ombe ipo juu hivi?? Mnazidiwa na Morogoro ambao hawafugi km ninyi kweli?

Serikali ichunguze Hali hii, kwasababu inachangia kwa kiasi kikubwa sana Watumishi wa wizara waliokuwa wamehamishiwa DODOMA kutoka Dar kutamani kurudi Dar kuliko kuishi DODOMA.Tafadhari Serikali inusuru Hali hii.
Hiyo sio kazi ya serikali

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Kuna wenzio wanalala morena au royal village yaan na hawaulizu bei 😂😂
Tutafute helaa
 
Dar wapi ambako guest ni 10,000? Acha zako
Bonjour kulee bugurni Malapa!! buku jero, tena ile iko safi kweli!!unajichagulia unavotaka, zingine nyuma ya msewe kureee! sewa bar! haya Banana mpaka za elfu tano zipo!! ukienda kureee Masangati temeke karibu na kwa wahaya zipo bei poa! bado mikoroshini ndani huko buku mbili tu!

km haitoshi njia panda majumba sita buku mbili!! ukienda kuleeee salasala kwa wabarikiwe buku, na nyapu za kuchagua Kawe karibu na lango la jeshi ndani huko! buku ila ukiwa mgeni huwezi jua haya!
 
Wakuu habari za jioni? Wiki hii Nilikuwa DODOMA kwa shughuli za Kiofisi,nimependa jinsi jiji la Dodoma linavyokua kwa kasi,Lakini hali ya maisha inaonekana ni ngumu Sana kuliko Dar es salaam.

Nilitafuta guest house, bodabo whyda akaniambia kuwa vyumba vya bei ya chini ni 20,000/=, nikashangaa Sana kwasababu niliwahi kwenda DSM na nikafanikiwa kupata gesti ya 10,000/=, nzuri tu. Chakula kwa Dodoma ndo usiseme,kipimo changu cha kwanza ni kwa Mama ntilie, maana watu wengi wa hali ya chini huenda huko kununua chakula;

Aise kina bei hatari , Kuna sehemu niliambiwa wali nyama 3,000/=,Ugali nyama 3000/=,Wali samaki 3500/=, Ugari Maharage 2000/= na wali Maharage 2500/=, Sehemu nyingi za Mama Ntilie bei ni hizo.Nilipolala ni karibu na Holly Cross Center inayomilikiwa b

Na Kanisa Katoliki Jimbo kuu la DODOMA,Aise hapo kitimoto ya kukaanga kilo ni 10,000/=,Ya kubanikwa ni 12,000/=,Ndizi moja 500/=. Ugari kuku robo 6000/=. Na vyakula vingine bei zipo juu pia.Haya nikasema Niulize Vipi kuhusu nyumba za kupanga?; Kheee!, Bei nilizotajiwa nilishangaa Sana.Twende Bodaboda aisee Hivi kweli kutoka Holly Cross Center hadi Mkonze mtu anaanza na 6000/=baada ya kuvutana Sana ndo anaishia kwenye 4000/=.

Sijauliza viwanja.Nastaajabu kwasababu miaka ya Nyuma DODOMA haikuwa ghali kiasi hicho.Nilijiuliza swali moja kuwa DODOMA ni wafugaji wazuri wa mifugo sasa Kwanini bei ya Nyama ya ng'ombe ipo juu hivi?? Mnazidiwa na Morogoro ambao hawafugi km ninyi kweli?

Serikali ichunguze Hali hii, kwasababu inachangia kwa kiasi kikubwa sana Watumishi wa wizara waliokuwa wamehamishiwa DODOMA kutoka Dar kutamani kurudi Dar kuliko kuishi DODOMA.Tafadhari Serikali inusuru Hali hii.
Umegusa penyewe.kipimocha ughali wa maisha kinaana kwenye mlo wa kila siku
 
Kutokana na mzunguko wa pesa kua chini Dodoma, kwa bei hizo utakua mkoa mgumu sana kwa vijana wanaotafuta maisha.

Ndio maana bado ongezeko la vijana kukimbilia Dar liko pale pale japo serikali imeamua kuhamia huko.

Dodoma itambue kwamba serikali kuhamia huko sio kuifanya iwe bora kuliko Dar, mkoa unatakiwa kuweka mazingira rahisi ya vijana kuwekeza na kutenga maeneo maalumu ya biashara kuvuta wawekezaji wa ndani.

Kuhamasisha uwezekaji wa viwanda, bandari kavu, bonded warehouses itawavuta wengi pia.

Dodoma ina watu wengi waajiriwa, sasa ni muda wa serikali ya mkoa ku balance upande wa pili ipate wafanyabiasha wengi na mzunguko utapanda.
 
Kutokana na mzunguko wa pesa kua chini Dodoma, kwa bei hizo utakua mkoa mgumu sana kwa vijana wanaotafuta maisha.
Naungana na wewe kama chakula tu cha kawaida bei ni hiyo? Wakati Kazi za Deiwakaunafanya kazi tangu asubuhi hadi jioni unalipwa Elfu 7.

Sasa imagine ulipwe elfu 7 then toa hiyo bei yachakulacha mchana na usku ukipuga deshi asubuhi
 
Tunaoishi dodoma na familia zetu zinaenda chooni bila shida ni wanaume kweli kweli mtupe Heshima zetu,

Huku chumba kibaya kibaya tu ili mradi kiwe na umeme na maji ni elfu 50,

Chumba angalau, angalau Single tu elfu 60k au 70k kwa mwezi,
Self kuanzia 80k mpaka 100k huku bili ya maji ikikuelemea,
Ukitaka master, Yenye chumba kimoja, sebure na choo ndani jiandae na kuanzia 150k mpaka 180k kwa mwezi huku bili ya umeme,maji na ya kodi ya jengo ikikuelemea,

Ukitaka Apartment, au Nyumba nzima ya kuanzia vyumba viwili au vitatu yenye sebure, choo ndani, master room moja na jiko jiandae na kuanzia 350K mpaka 500k kwa mwezi.

Usisahau na malipo ya dalali ya mwezi mmoja.

Ukifanikiwa kuishi dodoma mwaka bila shida yeyote basi hakuna mkoa utashindwa kuishi hapa Tanzania.


Cc Zero IQ

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuh
 
Back
Top Bottom