M_tiler
Member
- Dec 6, 2016
- 12
- 18
Habari za majukumu wanajukwaa?
Naimani Mwaka huu umeanza vizuri na matarajio yangu kwenye mwaka huu ni lazima nitoke nje ya mipaka ya Tanzania kwa namna yoyote ile iwe isiwe.
Kabla ya yote, Mimi nimehitimu shahada yangu ya Kwanza tangu. Waka 2019 ktk sekta ya Elimu (Masomo ya kufundishia ni Geography na Kiswahili) na kwa bahati mbaya sijafanikiwa kupata ajira serikalini.
Niliwahi kuajiriwa Private school mwaka 2020 lakini sikufanikiwa kuendelea na kazi kwa muda mrefu kwasababu ya ujira kidogo sana (pesa haikukidhi mahitaji). Mpaka kufikia mwisho wa mwaka 2021 nilishindwa kuvumilia kusindikiza wenzangu kwenye maisha nikakata shauri ya kutafuta fani mbadala ya kuniwezesha kuishi mtaani bila marumbamo na taasisi za wenye nacho.
Katikati ya mwezi wa 11 mwaka 2021 nikajichanganya rasmi mtaani na kuanza vibarua kwenye sekta ya ujenzi, niliegemea upande wa kujenga Tiles, Tanga stones na Marble. Nilifanikiwa kujua haraka hizo kazi kwasababu nilifanya bidii saana na nilijituma kwa udi na uvumba nikapendwa na mafundi wengi hatimaye nikazijua fani hizo mapema sana kulinganisha na wenzangu niliowakuta wanajifunza na nikawaacha wanaendelea kujifunza ilhali mimi tayari nimeshapata fani mbadala na niliyoisomea.
Nilipiga rada kusoma mazingira rafiki ya kazi hizi za ujenzi nikagundua mji sahihi kwangu ambao naweza kufanikiwa kupitia kazi zangu ni Dodoma, basi sikupoteza wakati mwezi wa 5 mwaka 2022 nikaanza safari yangu kutokea mjini Dar es salaam mpaka Dodoma bila hata ya kuwa na mwenyeji na nikabahatika kupata kazi kadhaa kutoka kwa mafundi na hatimaye nikapata pesa ya Kodi na godoro nikayaanza maisha yangu rasmi ya usela.
Mwanzoni naanza maisha yangu ndani ya jiji la Dodoma nilikutana na changamoto ya kila kazi kuwa na bei ndogo, lakini kwakuwa sikuwa na namna nyingine nilifanya bila kusitasita. Kazi nyingi nilizozifanya nilijenga kwa Sh. 4,000 mpaka 3,000 kwa 1m² (kutoka kwa fundi).
Lakini kwa kadri ninavyozidi kuizoea na kufanya kazi zangu kwa ufanisi mkubwa ndivyo bei ya ufundi inazidi kushuka na kuwa ndogo zaidi. Kwasasa bei ya 1m² inafika 2,000 kwa 2,500 (kutoka kwa fundi), ukiringa wenzako wanafanya hata kama kazi haina ubora.
Kiukweli, kwa hali ilivyo kwasasa Dodoma kazi za ujenzi zinaelekea kushuka thanami kila kukicha na kwasasa nimefikiria njia sahihi ya mimi kutoboa ni kutoka nje ya Tanzania na kwenda mbali zaidi.
Najua humu ndani wataalamu ni wengi sana na wenye uchu wa mafanikio ni wengi vilevile wengi wenu mnajua machimbo yenye kupiga pesa nje ya Tanzania. Naombeni ushauri wenu nionesheni nchi sahihi ya kwenda (niko tayari hata kuzamia). Namna ya kufika, hali ya maisha ya huko, shughuli za kuanzia kwa kujitafuta na mengine mengi. Nchi ninazofikiria zaidi ni #South Africa, #Nigeria, #DR Congo, #Ghana, na #Visiwa vya Ushelisheli
Naombeni ushauri(usinitukane please). Kama hauna cha kunishauri ni kheri ukae kimya ila please usinitukane.
Naimani Mwaka huu umeanza vizuri na matarajio yangu kwenye mwaka huu ni lazima nitoke nje ya mipaka ya Tanzania kwa namna yoyote ile iwe isiwe.
Kabla ya yote, Mimi nimehitimu shahada yangu ya Kwanza tangu. Waka 2019 ktk sekta ya Elimu (Masomo ya kufundishia ni Geography na Kiswahili) na kwa bahati mbaya sijafanikiwa kupata ajira serikalini.
Niliwahi kuajiriwa Private school mwaka 2020 lakini sikufanikiwa kuendelea na kazi kwa muda mrefu kwasababu ya ujira kidogo sana (pesa haikukidhi mahitaji). Mpaka kufikia mwisho wa mwaka 2021 nilishindwa kuvumilia kusindikiza wenzangu kwenye maisha nikakata shauri ya kutafuta fani mbadala ya kuniwezesha kuishi mtaani bila marumbamo na taasisi za wenye nacho.
Katikati ya mwezi wa 11 mwaka 2021 nikajichanganya rasmi mtaani na kuanza vibarua kwenye sekta ya ujenzi, niliegemea upande wa kujenga Tiles, Tanga stones na Marble. Nilifanikiwa kujua haraka hizo kazi kwasababu nilifanya bidii saana na nilijituma kwa udi na uvumba nikapendwa na mafundi wengi hatimaye nikazijua fani hizo mapema sana kulinganisha na wenzangu niliowakuta wanajifunza na nikawaacha wanaendelea kujifunza ilhali mimi tayari nimeshapata fani mbadala na niliyoisomea.
Nilipiga rada kusoma mazingira rafiki ya kazi hizi za ujenzi nikagundua mji sahihi kwangu ambao naweza kufanikiwa kupitia kazi zangu ni Dodoma, basi sikupoteza wakati mwezi wa 5 mwaka 2022 nikaanza safari yangu kutokea mjini Dar es salaam mpaka Dodoma bila hata ya kuwa na mwenyeji na nikabahatika kupata kazi kadhaa kutoka kwa mafundi na hatimaye nikapata pesa ya Kodi na godoro nikayaanza maisha yangu rasmi ya usela.
Mwanzoni naanza maisha yangu ndani ya jiji la Dodoma nilikutana na changamoto ya kila kazi kuwa na bei ndogo, lakini kwakuwa sikuwa na namna nyingine nilifanya bila kusitasita. Kazi nyingi nilizozifanya nilijenga kwa Sh. 4,000 mpaka 3,000 kwa 1m² (kutoka kwa fundi).
Lakini kwa kadri ninavyozidi kuizoea na kufanya kazi zangu kwa ufanisi mkubwa ndivyo bei ya ufundi inazidi kushuka na kuwa ndogo zaidi. Kwasasa bei ya 1m² inafika 2,000 kwa 2,500 (kutoka kwa fundi), ukiringa wenzako wanafanya hata kama kazi haina ubora.
Kiukweli, kwa hali ilivyo kwasasa Dodoma kazi za ujenzi zinaelekea kushuka thanami kila kukicha na kwasasa nimefikiria njia sahihi ya mimi kutoboa ni kutoka nje ya Tanzania na kwenda mbali zaidi.
Najua humu ndani wataalamu ni wengi sana na wenye uchu wa mafanikio ni wengi vilevile wengi wenu mnajua machimbo yenye kupiga pesa nje ya Tanzania. Naombeni ushauri wenu nionesheni nchi sahihi ya kwenda (niko tayari hata kuzamia). Namna ya kufika, hali ya maisha ya huko, shughuli za kuanzia kwa kujitafuta na mengine mengi. Nchi ninazofikiria zaidi ni #South Africa, #Nigeria, #DR Congo, #Ghana, na #Visiwa vya Ushelisheli
Naombeni ushauri(usinitukane please). Kama hauna cha kunishauri ni kheri ukae kimya ila please usinitukane.