Mahusiano na Wakwe/Mawifi Nini kifanyike?

Mahusiano na Wakwe/Mawifi Nini kifanyike?


...kiukweli, maisha yamejaa suspicious minds/looks kila mahala unapokwenda. Ni vile weye unavyoweza ya balance maisha yako na kuji adapt haraka haraka na changes.
Challenges huanzia pale;

---mtoto anapowatambua watu wa nyumbani, na kuwa 'mtoro' kwa asiowajua...
---unapopelekwa shule kwa mara ya kwanza, kuanza kujenga urafiki na wanafunzi wenzio, kumzoea mwalimu nk
---unapohamishwa shule/kuingia shule mpya i.e sekondari...unakutana na wanafunzi wapya nk
---unapoingia chuo/vyuoni nk...
---unapoanza kazi/unapobadilisha kazi...kujuana upya na wafanyakazi wapya...nk

Hizo challenges zote ulizopitia na kufaulu ni ishara kwamba ni wewe mwenyewe unashikilia funguo za maelewano,
vipi unataka jamii inayokuzunguka ikuchukulie. Ukiamua kujiweka mwenyewe mwenyewe jamii itakutenga tu.
Ukijifanya too intruisive, jamii nayo itakuchukulia hivyo na kuwa na tahadhari nawe.

La msingi, jiwekee mipaka...nini la kuongea, nini la kutokuongea.
Nini la kufanya, nini la kuliepuka. Tangu mwanzo unajifunza lipi la kujenga,
lipi litabomoa. Hakuna formula ya kuishi na watu kwa jinsi ya mitazamo yao
La msingi, be yourself.

Mke/Mume, ana nafasi kubwa kukusaidia mawazo/maoni ufahamu wa ndugu zake,
Akili kichwani mwako kuhakikisha nawe unatumia busara zako jinsi ya kuishi nao.

Kumradhi, nimepita kuwasabahi tu dada zanguni...hii sredi imekalia ki kitchen party zaidi..lol..

Mbu aksante sana kwa huu ushauri wako. Nimefurahi kuona kumbe ukiwa wewe kama wewe no matter what happens you are yourself inasaidia. I tried that approach sometimes back but nikawa najishuku tu mwenyewe kuwa may be am not doing it right (Kwa watu wengine tu jamiini na si mawifi au wakwe zangu maana hawa hawakuwa na tatizo kabisa)

Ila your last sentence imenigusa. ...... Mbu umesema wote Mke na Mume wana wajibu wa kuyaongoza haya mahusiano....................limenijia wazo ambalo wewe ndio umeliinstigate ..............inapotokea mke wako anakuwa na clashes na Mkwe/wifi yake how do you (kama mume/kaka/mtoto) solve this ili usionekane unapendelea?

Unayosema ni kweli kabisa, lakini inakuwa ngumu mno pale mke anavyojitahidi kadri ya uwezo wake kuwa karibu na wifi zake na mama mkwe lakini bado juhudi zake hizo zisizae matunda yoyote ya kuwa na uhusiano mzuri kati yao. Nayasema haya kwa kuwa nimeshayashuhudia mara nyingi sana na inafikia wakati mke inabidi anyooshe mikono juu na kukubali kushindwa kwamba hawezi kuwa uhusiano mzuri na mawifi zake na mama mkwe. Hawa mawifi na mama mkwe mara nyingi humuona huyo binti "anafaidi sana" au "anamuendesha" mumewe.

Mama Wakwe na Mawifi kama hawatataka kuifuatilia ndoa ya mume (mtoto na kaka yao) labda kila siku iendayo kwa Mungu (Wamekula nini, kamnunulia kanga zipi, kamnunulia gauni la namna gani bei gani, viatu vyake mbona ni ghali mno n.k.) labda hii itasaidia kuwepo na uhusiano mzuri vinginevyo ni utata mtupu ambao unaweza kabisa kuivuruga ndoa hiyo na kuitia dosari kubwa sana na si ajabu kuvunjika.

Pia wapo wake wakorofi ambao mara nyingi hawataki mume asaidie upande wake hata kama ana uwezo mkubwa wa kufanya hivyo, hawa pia wakiacha hii tabia mbaya basi labda kuna uwezekano wa kuwa na "uhusiano" mzuri.
Aksante BaK hapa umetuchambulia vizuri kabisa.......hivi Mwanaume anayeishi ndani ya nyumba ambayo mkewe na in-laws wake wanaclashes zisizokwisha huwa anajisikiaje na which- if I may ask- is the best approach kwa yeye kuletewa mashtaka na kuyaelewa? je mume huyu anapaswa kupata mashtaka kutoka kwa mke au inlaws wa mkewe? na inapotokea mmoja wapo anaku'shtakia' ni approach gani ambayo ni nzuri kuichukua ili usi'haribu' pande mojawapo?

Kwa kweli tuongee ukweli akina dada kabla ya kuolewa huwa mnakuwa mna adabu sana na mnanyenyekea sana.
Sijui ile inakuwaga ni nidhamu ya woga wala sijui ili upate dili la kuolewa na bro au dogo.
Mambo yanabadilika mkisha ingia ndani ya nyumba kuwa miongoni mwa familia yetu dahhh hapo vitimbi na misuguano huanza.
Kama wewe dada ni mnoko au jeuri kwa nini usijionyeshe tu toka mwanzo tujue shemeji yetu mnoko mkiwa katika harakati mnajivika ngozi ya kondoo mkisha zama ndani ndo mnakunjua makucha yenu sasa mashemeji na mawifi wanabaki mdomo wazi hivi ndo huyu huyu kweli aliyekuwa anatuheshimu?? Hapo bado biti la kuwekewa kikwazo cha uhuru wa kwenda kusalimia kwa bro. dahhh

Jamani Fide, sio mara zote bana........sometiomes mke anakuwa innocent kama alivyoingia bali unajikuta anabadilishwa na mambo yalivyo (sisemi ni sawa)
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Hii mada inahitaji utulivu sana mkoloni katumia vibaya akili yangu leo
 
Mada za mwanajamiione bwana, huwa nzito nzito sana. Namshauri awe anazianzisha siku ambayo siyo IJUMAA. Maana wengine siku kama ya leo tunapenda kufanya mambo mepesi mepesi na laini laini.
 
Jamani Fide, sio mara zote bana........sometiomes mke anakuwa innocent kama alivyoingia bali unajikuta anabadilishwa na mambo yalivyo (sisemi ni sawa)

Mi yamenikuta haya shemeji kabla hajaolewa tulikuwa tunaiva kweli kweli
Jamaa alivyo muhifadhi ndani khaa amechange nikijihimu kugongea chai nanyimwa yupo radhi anywe saa 6 wkt mm nimeondoka
 
King'asti umenigusa -Ki ukweli nakubaliana nawewei ila jamani mi naona mawifi na wakwe hawatakiwi kukaa karibu kwa muda mrefu hapo heshima na upendo vitabakia kwa pande zote,binafsi nina mawifi na wakwe ambao ni understanding ila bwana nilijuta pale nilipomkaribisha wifi yangu sehemu ninapofanyia kazi tukawa tumeajiriwa sehemu moja,

kweli maneno yaliyopelekwa kwa wakwe zangu na mr wangu ilikuwa balaa..imagine ilitokea misunderstanding kidogo kisa kakake hajampeleka kazini siku ambayo mimi nilikua naumwa na sikwenda job, ooh mimi ni damu yako mimi mdogo wako lakini unampendelea huyo wakupita...

uzuri kakaye alimweleza ukweli kuwa wewe ulushawahi hata siku moja kuchangia hata mia tano kwaajili ya mafuta ya gari?na kipindi hicho mr alikua shule hana income kivile yani long story....

ila mr wangu alisimama na kuamua kama kichwa cha familia yangu...huku tunakoenda nafikiri kuna haja ya kufundisha watoto wetu wasijichanganye sana na mambo ya nyumba za makaka wao hata wakienda kusalimia sioni haja ya kukaa zaidi ya wiki moja ..!
 
Mbu aksante sana kwa huu ushauri wako. Nimefurahi kuona kumbe ukiwa wewe kama wewe no matter what happens you are yourself inasaidia. I tried that approach sometimes back but nikawa najishuku tu mwenyewe kuwa may be am not doing it right (Kwa watu wengine tu jamiini na si mawifi au wakwe zangu maana hawa hawakuwa na tatizo kabisa)

Ila your last sentence imenigusa. ...... Mbu umesema wote Mke na Mume wana wajibu wa kuyaongoza haya mahusiano....................limenijia wazo ambalo wewe ndio umeliinstigate ..............inapotokea mke wako anakuwa na clashes na Mkwe/wifi yake how do you (kama mume/kaka/mtoto) solve this ili usionekane unapendelea?


Aksante BaK hapa umetuchambulia vizuri kabisa.......hivi Mwanaume anayeishi ndani ya nyumba ambayo mkewe na in-laws wake wanaclashes zisizokwisha huwa anajisikiaje na which- if I may ask- is the best approach kwa yeye kuletewa mashtaka na kuyaelewa? je mume huyu anapaswa kupata mashtaka kutoka kwa mke au inlaws wa mkewe? na inapotokea mmoja wapo anaku'shtakia' ni approach gani ambayo ni nzuri kuichukua ili usi'haribu' pande mojawapo?

...lol...Mwanaume ni kichwa cha familia. Miongozo ya Dini yangu, inanitaka mimi mwanaume niwe hakimu, wakili, walii,...nk

Ili niweze kufit yote hayo, inanibidi niwe msikivu, mchambuzi wa hoja, matakwa na mengineyo mengi yahusuyo pande zote mbili.

Nahakikisha Mke anabakia na cheo chake ---MKE, mama anabakia na cheo na daraja lake kuu---MAMA, na madada wanabakia mawifi na ndugu. Mke wangu hawezi kuwa na maamuzi kama ya Mama yangu au dada zangu, and Vice Versa.
Najua hapo unatamani kuniuliza nani nampa maamuzi mazito zaidi kwenye maisha yangu,...jibu ni; mimi Mwenyewe.
 
Muhanga umepotea sana jamani, kwema?...huyu wangu alikuwa anapewa kichwa na mama yake, cjui kitinda mimba wangu hivi na vile, haaa hata sie wengine vitinda mimba na tunashika adabu zetu panapostahili......

nipo mpendwa weee vijimambo vya hapa na pale tu vinanifanya nipotee potee. ooh mie huwa namwambia mkwe usidhani mwanao ni wa maana sana, hata mie mbele ya mamangu ni wa maana mno maana nae alinibeba tumboni miezi hiyo hiyo 9, asijitie tembo kuwa yeye ndio alibeba mimba miezi mingi zaidi.

halafu wanawake bwana kama tuna laana yaani ukiolewa unaonekana kama vile wa kuja tu iko ck utaondoka, as if umekuja kuhemea shida zako kwa mume, utadhani wewe huna kwenu kwa hiyo ukinyanyasika uwe mpole tu, wangejua hao kaka zao wanatembelea nyota zetu, wengine hata kipato-wise wako juu na wanafanya mambo makubwa kuliko hata hao wanaume,

bac tu mie sometimes huwa nawaangalia nacheka sana kwa sauti, nawaambia ukiona kaka yenu hasemi neno mjue anaujua ukweli na undani wa maisha yetu hathubutu kuchonga domo hapa anajua mie ni nani kwenye maisha yake!
 
...lol...Mwanaume ni kichwa cha familia. Miongozo ya Dini yangu, inanitaka mimi mwanaume niwe hakimu, wakili, walii,...nk

Ili niweze kufit yote hayo, inanibidi niwe msikivu, mchambuzi wa hoja, matakwa na mengineyo mengi yahusuyo pande zote mbili.

Nahakikisha Mke anabakia na cheo chake ---MKE, mama anabakia na cheo na daraja lake kuu---MAMA, na madada wanabakia mawifi na ndugu. Mke wangu hawezi kuwa na maamuzi kama ya Mama yangu au dada zangu, and Vice Versa.
Najua hapo unatamani kuniuliza nani nampa maamuzi mazito zaidi kwenye maisha yangu,...jibu ni; mimi Mwenyewe.

Mbu hebu ngoja nisome tena hii comment mara mbili mbili na kisha nitarudi kuchangia
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mada za mwanajamiione bwana, huwa nzito nzito sana. Namshauri awe anazianzisha siku ambayo siyo IJUMAA. Maana wengine siku kama ya leo tunapenda kufanya mambo mepesi mepesi na laini laini.
unabakiza nguvu na akili za kubalance miguu baada ya kupata ulabu wako wa wikiend!
 
...lol...Mwanaume ni kichwa cha familia. Miongozo ya Dini yangu, inanitaka mimi mwanaume niwe hakimu, wakili, walii,...nk

Ili niweze kufit yote hayo, inanibidi niwe msikivu, mchambuzi wa hoja, matakwa na mengineyo mengi yahusuyo pande zote mbili.

Nahakikisha Mke anabakia na cheo chake ---MKE, mama anabakia na cheo na daraja lake kuu---MAMA, na madada wanabakia mawifi na ndugu. Mke wangu hawezi kuwa na maamuzi kama ya Mama yangu au dada zangu, and Vice Versa.
Najua hapo unatamani kuniuliza nani nampa maamuzi mazito zaidi kwenye maisha yangu,...jibu ni; mimi Mwenyewe.

kama kila mtu angekuwa anaielewa nafasi yake katika maisha ya ndoa ya mtu na anafanya yale tu ambayo yako kwenye nafasi yake naamini kusingekuwa na matatizo kabisa,

shida ni watu kutaka kufachukuliana majukumu, mama anataka abebe nafasi ya umama hata pale ambapo mwanae nae kawa baba nyumbani kwake, na haishii hapo anaingilia hadi majukumu ya mke kwenye family, anabakiza moja tu la kulala na mwanae! madada nao wanataka wawe na majukumuhadi kwenye nyumba, ndoa za kaka zao,

hapo ndio mtafaruku unakoanzia, mke nae anakosa nafasi hata hajielewi ana belong wapi, alipotoka kwao aliambiwa unaenda kuanza family yako akapoteza identity kwao, anaenda kwa mume anakuta nafasi zote zimeshikwa na mkwe na ndugu anabaki ka-hang hapo katikati hajielewi!!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Hii mada inahitaji utulivu sana mkoloni katumia vibaya akili yangu leo

Jamani Mamito pole mpenzi...................usijali mamii hata kusoma tu inatosha. .......netweki isijekata bure. Nimekumiss!

Mada za mwanajamiione bwana, huwa nzito nzito sana. Namshauri awe anazianzisha siku ambayo siyo IJUMAA. Maana wengine siku kama ya leo tunapenda kufanya mambo mepesi mepesi na laini laini.
Masaki soma tu mydia jamani. Afu uache kupenda vilaini laini bana asa utamu wa bia utausikiaje kama akili haijachoka??
Umeona eeeh? Bora tuko wengi ambao tunakiri hilo!
LOL
 
Mi yamenikuta haya shemeji kabla hajaolewa tulikuwa tunaiva kweli kweli
Jamaa alivyo muhifadhi ndani khaa amechange nikijihimu kugongea chai nanyimwa yupo radhi anywe saa 6 wkt mm nimeondoka

Duh ........huyu alikuwa ana lake moyoni mwe!! what a drastic change!!!
Pole Fide ni baahti mbaya tu, sio wote wako hivyo!
 
nipo mpendwa weee vijimambo vya hapa na pale tu vinanifanya nipotee potee. ooh mie huwa namwambia mkwe usidhani mwanao ni wa maana sana, hata mie mbele ya mamangu ni wa maana mno maana nae alinibeba tumboni miezi hiyo hiyo 9,

asijitie tembo kuwa yeye ndio alibeba mimba miezi mingi zaidi. halafu wanawake bwana kama tuna laana yaani ukiolewa unaonekana kama vile wa kuja tu iko ck utaondoka, as if umekuja kuhemea shida zako kwa mume, utadhani wewe huna kwenu kwa hiyo ukinyanyasika uwe mpole tu,

wangejua hao kaka zao wanatembelea nyota zetu, wengine hata kipato-wise wako juu na wanafanya mambo makubwa kuliko hata hao wanaume, bac tu mie sometimes huwa nawaangalia nacheka sana kwa sauti, nawaambia ukiona kaka yenu hasemi neno mjue anaujua ukweli na undani wa maisha yetu hathubutu kuchonga domo hapa anajua mie ni nani kwenye maisha yake!

...dahhh, hapo kwenye red hata mimi nitamshika sikio kaka'ngu "anapotea!"...sio hekima wala busara kuyatamka haya.
Anyway, ni mtizamo tu wa kifikra, ila kwangu mie nahisi kama kuna kaji element ka kibri.
 
...lol...Mwanaume ni kichwa cha familia. Miongozo ya Dini yangu, inanitaka mimi mwanaume niwe hakimu, wakili, walii,...nk

Ili niweze kufit yote hayo, inanibidi niwe msikivu, mchambuzi wa hoja, matakwa na mengineyo mengi yahusuyo pande zote mbili.

Nahakikisha Mke anabakia na cheo chake ---MKE, mama anabakia na cheo na daraja lake kuu---MAMA, na madada wanabakia mawifi na ndugu. Mke wangu hawezi kuwa na maamuzi kama ya Mama yangu au dada zangu, and Vice Versa.
Najua hapo unatamani kuniuliza nani nampa maamuzi mazito zaidi kwenye maisha yangu,...jibu ni; mimi Mwenyewe.

Aksante ninashukuru kwa uwazi huu........... mh lucky she is!!

Just curious Mbu........................inapotokea Mume akijua kuwa Mama yake au dada zake huwa ni watata!! should it be part of the 'pre-marriage/coutiship-go tell- information' package au akae kimya mpaka litokee (kwa kuamini kuwa huwenda huyu wa sasa atabahatika kupata 'kibali' mbele zao?...... the same kwa mwanamke iwapo anajua kabisa kuwa ana dada au mama ambao wana tabia ya kuwascorn wakwe zao aseme mapema kama tahadhari au asubiri likitokea?
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
nipo mpendwa weee vijimambo vya hapa na pale tu vinanifanya nipotee potee. ooh mie huwa namwambia mkwe usidhani mwanao ni wa maana sana, hata mie mbele ya mamangu ni wa maana mno maana nae alinibeba tumboni miezi hiyo hiyo 9, asijitie tembo kuwa yeye ndio alibeba mimba miezi mingi zaidi.

halafu wanawake bwana kama tuna laana yaani ukiolewa unaonekana kama vile wa kuja tu iko ck utaondoka, as if umekuja kuhemea shida zako kwa mume, utadhani wewe huna kwenu kwa hiyo ukinyanyasika uwe mpole tu, wangejua hao kaka zao wanatembelea nyota zetu,

wengine hata kipato-wise wako juu na wanafanya mambo makubwa kuliko hata hao wanaume, bac tu mie sometimes huwa nawaangalia nacheka sana kwa sauti, nawaambia ukiona kaka yenu hasemi neno mjue anaujua ukweli na undani wa maisha yetu hathubutu kuchonga domo hapa anajua mie ni nani kwenye maisha yake!

hahahahha muhanga umenichekesha naona umeamua kulipasua jipu pwaaaaa. Umenikumbusha MTM alishawahikiri hapa kuwa kuna rafiki ambaye alipokuwa akiwa naye mambo yake yalikuwa yanakwenda poa kabisa,

yaani yeye maisha yalikuwa ya raha raha tu (kama sikosei ni ile thread ya whether ni kweli kuna wanawake wenye nyota njema au la) sasa sijui ndo hii nyota unayoizungumzia hapa?! Mwe

Mbu utanisaidia hapa au ndo yale ya Radhi ya mke?? ....Mheshimiwa tafadhali nisaidie majibu ya hili swali la nyongeza!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
King'asti umenigusa -Ki ukweli nakubaliana nawewei ila jamani mi naona mawifi na wakwe hawatakiwi kukaa karibu kwa muda mrefu hapo heshima na upendo vitabakia kwa pande zote,binafsi nina mawifi na wakwe ambao ni understanding ila bwana nilijuta pale nilipomkaribisha wifi yangu sehemu ninapofanyia kazi tukawa tumeajiriwa sehemu moja,kweli maneno yaliyopelekwa kwa wakwe zangu na mr wangu ilikuwa balaa..

imagine ilitokea misunderstanding kidogo kisa kakake hajampeleka kazini siku ambayo mimi nilikua naumwa na sikwenda job, ooh mimi ni damu yako mimi mdogo wako lakini unampendelea huyo wakupita...uzuri kakaye alimweleza ukweli kuwa wewe ulushawahi hata siku moja kuchangia hata mia tano kwaajili ya mafuta ya gari?

na kipindi hicho mr alikua shule hana income kivile yani long story.... ila mr wangu alisimama na kuamua kama kichwa cha familia yangu...huku tunakoenda nafikiri kuna haja ya kufundisha watoto wetu wasijichanganye sana na mambo ya nyumba za makaka wao hata wakienda kusalimia sioni haja ya kukaa zaidi ya wiki moja ..!

Stezu hapo kwenye red mbona alikuwa na hila huyo!!? Unawezajikuta unamtuc 'vibaya' kwa hacra ah.....mie wakupita jamani? But nimependa mumeo alivyokupigania kwani ni wachache wanaoweza kusimamia katika kweli!!

Nadhani pia kuna ukweli kuwa wakiwa mbali unaepusha clashes zisizo na msingi .....ingawa sometimes huwa unakuwa na hamu ya kuwa nao jamani!! Umenikumbusha rafiki yangu mmoja mkwe wake alikuwa kiboko: Alipoolewa tu Mama akajaishi Dar kwa mtoto wake- basi akiona shost kavaa mini skirt anaseeeema, mwanae anamwambia mama kwani amekuvalia wewe?

Mie nimemruhusu! Akaona isiwe tabu bana naye akaanza kuagiza vimini! Ukiwakuta utafikiri mtu na mke mwenzie. Akaja kumtibua zaidi alipomwambia aongeze 'speed' kwani ingekuwa mwanae kaoa kijijini sasa hivi angekuwa na mtoto wa pili (hapo wa kwanza ana mwaka na miezi miwili!!)...........Dada akamjibu...."Wamekua mboga, kuwa kila akija mgeni nachinja kitoweo?' ............ mpaka sasa ni chui na paka!!
 

...dahhh, hapo kwenye red hata mimi nitamshika sikio kaka'ngu "anapotea!"...sio hekima wala busara kuyatamka haya.
Anyway, ni mtizamo tu wa kifikra, ila kwangu mie nahisi kama kuna kaji element ka kibri.

usije ukanielewa vibaya ndugu yangu, what i was trying to say n kuwa hawa madada huwa wanadhani sisi wanawake tunaishi, kuvaa, kuendesha magari, kumiliki kipata nyuma ya migongo ya kaka zao na hilo ndio linalowafanya watuone kama tunawanyonya kaka zao na kuwa hatustahili hivyo tunastahili kunyanyasika hata ndugu wanaweza kukusumbua wanavyotaka wakati hilo si kweli,

some cases hao wanaume wanadepend on wake zao kwa mambo mengi na tukiwapa heshima waonekane ndio head wa familia bado inatugharimu ndio maana nimesema hivyo, na of course mie sifichi mbele ya watu wajingawajinga huwa nina kiburi sana sipendi kukaliwa kichwani abadan
 
hahahahha muhanga umenichekesha naona umeamua kulipasua jipu pwaaaaa. Umenikumbusha MTM alishawahikiri hapa kuwa kuna rafiki ambaye alipokuwa akiwa naye mambo yake yalikuwa yanakwenda poa kabisa, yaani yeye maisha yalikuwa ya raha raha tu (kama sikosei ni ile thread ya whether ni kweli kuna wanawake wenye nyota njema au la) sasa sijui ndo hii nyota unayoizungumzia hapa?! Mwe

Mbu utanisaidia hapa au ndo yale ya Radhi ya mke?? ....Mheshimiwa tafadhali nisaidie majibu ya hili swali la nyongeza!

unajua inakera sana, watu tunaishi kwa kusaidiana na kutegemeana ndani ya nyumba, maendeleo na mafanikio yote tunachangia kwa bidii kabisa, halafu kila mafanikio ndugu wanaona kama vile yanaletwa na wanaume tu na wewe mke unafaidika bure, hapo ndio maana mie yananitokaga hayo maneno nakereka mno, kwa nini tusiache kila nyumba ijiendeshe yenyewe?

tupeane nafasi kila watu wawe na maisha yao uone maendeleo yatakavyopamba moto, wkt mwingine wanawake wasiofikiri sawa sawa hawachangii maendeleo ya familia eti tu kwa kigezo kuwa ooh ndugu hawathamini uwepo wangu, kila kitu wanaona cha ndugu yao tu basi mie sichangii lolote, mie kwangu hilo lalipo nawekeza kwa ajili ya maisha yangu , mume na watoto wangu wengine wasubiri kurithi siku familia nzima tukiingia 6 fts under....
 
Shemeji.....................umenikamilishia mwanzo wa mwisho wa wiki dah........nimecheka sana. Aksante mwkaya kwa observation yako.

Salamu zimefika, nikuchagulie sahani gani??[/QUOTE]

yoyote tu, muhimu iwe imejaa tu na ukila inarambika. sipendi sahani zilizozeeka na kufanya ufa.

bek to ze topik: kwa ninavyowaelewa dada zake Mbu nadhani unahitaji kujifunza mipasho kabla kuvalishwa pete na Mbu. lol
 
Back
Top Bottom