haswaa dear, unachotakiwa ni kuw ana msimamo na mambo yako tu, tenda lile unalotakiwa kutenda timiza wajibu wako, huwezi kuwaridhisha binadamu. na ukiwa na msimamo usioyumba kila mtu atakuelewa hivyo na whether they like you or not itabidi tu wakuaccept kuwa ndio mke wa mtoto/kaka yao.
huwezi kuwa na watu around you ambao wana tabia zile tu unazozitaka wewe, binadamu mmoja anatofautiana na mwingine kwa kiasi kikubwa sana na ukitaka kuzifanyia kazi hizo tofauti zao ili zi-match na matakwa yako utaishia kugombana na watu bure. wachukulie vile walivyo, timiza wajibu wako endelea na maisha yako.
mie huwa namwangalia binti yangu nimemzaa mwenyewe lakini sometimes huwa kuna tabia anazo najaribu kujiuliza kazitoa wapi nashindwa kuelewa na simuelewi, na huyo nimemuweka tumboni 9 months,
sembuse mkwe umemkuta na mvi hadi kwapani, wifi na magego yake 32 mdomoni... aaghh.. spare me, siwezi kwa kweli mie najipenda nafsi yangu ikae kwa amani sitaki kelele zisizo na tija ktk maisha yangu...