Mahusiano na Wakwe/Mawifi Nini kifanyike?

nilimtolea uvivu my dia, niliyakusanya yote cku hiyo nikasema haiwezekani hapana kabisa inatosha sasa liwalo na liwe, nilimuita nikamkalisha chini, kweli nilimtolea nyongo, nilimsema vya kutosha na kumweleza kama anaona yeye ndio wa kunipangia mambo ya nyumbani kwangu bac na afungashe atimue kwao na acrudi daima,

kaka yake atawafata huko walipo, ilileta kasheshe sana lakini ilinisaidia kiac cha kutosha, mama mkwe alikuja juu sana kuhusu hilo nae nilimwambia namaanisha nilichokisema....tuheshimiane, mie sio mke mwenzake bali ni mke wa kaka yake....kuanzia hapo heshima ilianza kushika mkondo wake, kupasua nyongo napo kunahitaji moyo uwe tayari kwa lolote,

ilinilietea kasheshe sana sana na mr lakini nikakomaa nayo....hawa watu(wifi/mkwe) unatakiwa utafute mbeleko special la kuwabebea, sio warahic hata kidogo.

eh nyamayao upo dear... hongera kwa kuuvaa moyo wa chuma ndio inavyotakiwa kwa maisha yetu ya kibongo ya 'mshikamano' bila hivyo utawakuta mawifi hadi chumba chako cha kulala tena juu ya kitanda nako wanapekua mambo!!!
 
nimefurahi kusikia hii habari dearest....kweli yote yawezekana!


cku hizi hata kaka yake mwenyewe anafurahi urafiki wetu ulivyo, mwanzoni aliona cpendi ndugu zake cjui nn na nn mambo kibao achia mbali kusucwa mambo kisa cpendi ndugu, dada yake alivyojirudi kwangu nae akaelewa sasa.....nilimvumilia my dia nikaona sasa hapana.
 
kuna factors nyingi zinapelekea wadogo kujiingiza kwenye ndoa na nikisema wadogo simaanishi eti 10, 14 yrs, namaana 16-22 yrs kwa mikiki mikiki ya maisha ya ndoa za ck hizi kwa kweli huwa ni ngumu sana kumudu, labda muolewaji abahatike kupata familia iliyo na upendo wa kuchukuliana kila mtu kwa jinsi yake otherwise ni tatizo...
Nilikuelewa my dear, I was just thinking aloud.
 
cku hizi hata kaka yake mwenyewe anafurahi urafiki wetu ulivyo, mwanzoni aliona cpendi ndugu zake cjui nn na nn mambo kibao achia mbali kusucwa mambo kisa cpendi ndugu, dada yake alivyojirudi kwangu nae akaelewa sasa.....nilimvumilia my dia nikaona sasa hapana.

that is an achievement mae...hongereni sana!

sasa nyamayao ukikuta mwanaume ambae hataki kusikia changamoto zinazosababiswa na mama au ndugu zake na wewe mwenyewe ndo laini laini hukawii kuikimbia ndoa.
 
that is an achievement mae...hongereni sana!

sasa nyamayao ukikuta mwanaume ambae hataki kusikia changamoto zinazosababiswa na mama au ndugu zake na wewe mwenyewe ndo laini laini hukawii kuikimbia ndoa.
kwa nini ukimbie ndoa bht? kitakachonitoa kwenye ndoa ni mume peke yake, maana ndoa ni maagano yangu na yeye, zaidi ya hapo hakuna cha kunitoa.
 
Kweli kabisa mamito yaani aksante kwa hii rule yako but nadhani kama ndo unaishi nao nyumba moja lazima iko siku utakereka na itakuwa inakusumbua tu. Jamani mie ninavyoipenda amakni na furaha yangu yaani kitu kidogo tu kikiingilia huwa nakuwaga kama nimemwagiwa maji, naumia haswa.......mpaka najichukia sijui ugonjwa!!

Juzi kati hapa, mpenzi aliamka na uchovu, yaani kawa mgonjwa, ukimwuliza anakujibu ni uchovu tu mamii (yuko safarini) lakini siamini nahisi kuna kitu hataki nambia mwe!! sasa sijui ndo kutojiamini au vipi. The same kama naishi na mama mkwe au wifi ikahappen unaamka unamsabahi anakukalia kimya,.....au anakujibu kimkato.nawe hujamkosea na wema unamtendea , mie bado kinanisumbua sana mwenzenu nahic nitakuwa na matatizo!!

hiyo roho yako uniweza mwenyewe......mie nilivyompasulia wifi nyongo mama akawa haniitikii salamu yangu, wifi ndio ucseme, akiamka mdomo kauvuta huo, mie walaaa nimeshawatimizia ninachotakiwa kuwafanyia wao waendelee tu na mchuno, mbona wali surrender wenyewe, namtayarishia mama chakula kama kawaida,

namkaribisha kama kawaida namfanyia yote ninayostahili kumfanyia hayo ya mchuno mie huko cko, kisukuma kilikuwa lugha ya taifa hapo ndani, uzuri cwaelewi bac hata kama wanaicmanga mie haaaa.....
 
nilimtolea uvivu my dia, niliyakusanya yote cku hiyo nikasema haiwezekani hapana kabisa inatosha sasa liwalo na liwe, nilimuita nikamkalisha chini, kweli nilimtolea nyongo, nilimsema vya kutosha na kumweleza kama anaona yeye ndio wa kunipangia mambo ya nyumbani kwangu bac na afungashe atimue kwao na acrudi daima,

kaka yake atawafata huko walipo, ilileta kasheshe sana lakini ilinisaidia kiac cha kutosha, mama mkwe alikuja juu sana kuhusu hilo nae nilimwambia namaanisha nilichokisema....tuheshimiane, mie sio mke mwenzake bali ni mke wa kaka yake....kuanzia hapo heshima ilianza kushika mkondo wake, kupasua nyongo napo kunahitaji moyo uwe tayari kwa lolote,

ilinilietea kasheshe sana sana na mr lakini nikakomaa nayo....hawa watu(wifi/mkwe) unatakiwa utafute mbeleko special la kuwabebea, sio warahic hata kidogo.

Kumbe mkakati huo nao unafaaa...........hongera kwa hilo na Asante.
 
eh nyamayao upo dear... hongera kwa kuuvaa moyo wa chuma ndio inavyotakiwa kwa maisha yetu ya kibongo ya 'mshikamano' bila hivyo utawakuta mawifi hadi chumba chako cha kulala tena juu ya kitanda nako wanapekua mambo!!!

Muhanga umepotea sana jamani, kwema?...huyu wangu alikuwa anapewa kichwa na mama yake, cjui kitinda mimba wangu hivi na vile, haaa hata sie wengine vitinda mimba na tunashika adabu zetu panapostahili......
 
niliwahi kukaa na mama mkwe karibia mwaka............ ni mkorofi balaa. cha kufanya sikubadili maisha yangu. job - home - kama nina appointment na watu natoka na kurudi usiku sana, hata kama bila mwanae. sisi tuna maisha yetu, sometimes natoka na rafiki zangu bila mr, na narudi nitakapoachana nao, yeye kama hana misele atarudi nyumbani mapema.
cha muhimu tu alikuwa anapata kila kinachowezekana na kwa wakati unaowezekana, zaidi ya hapo sikuwa na la kufanya

wakati ule kabla hawajajirekebisha, nilkaa nae kumuuguza, ilikuwa miezi 3 lakini nliona kama miaka 10, gosh....hata nimfanyie nn ilikuwa tabu, jamani jamani nilchoka kwa lawama ikabidi tu nimwambie mr amwambie tu dada yake aje anisaidie, mpaka nlichukua likizo kwa ajili ya kumuuguza lakini wapi...khaaa na muolewe tu jamani mjionee.
 
you ladies got some rich experiences....!!!

Karibu mpenzi tujifunze wote!
Nyamayao,

This was what I was refering to..kuwa unamfanyia kila jema but bado anakuwa mkorofi. Afu nyamayao hakuna kitu kinachouma kama ukite wifi mwenyewe ni mdogo wako mara mbili,

tatu anakudharau kisa umeolewa na kaka yake yaani anakuona huna maana we ni wa kufugwa tu laiti wangejua!! Nlishawahikutana na ambaye yaani yeye alikuwa wa pekee kwa huyo kaka lakini mawifi wa mbali (mama mkubwa'; binamu)

wanakashika masikio yaani kanasomeshwa kwa pesa ya huyo mama (kaka aligawa majukumu kihivyo na pia hakuwaga baba/kaka mzuri wa kujali familia) lakini ndo kila likizo kikija yule amma anahaha!

Na usiombe kaje likizo na mama mkwe akiaccompany kwa kaka yake loh! Yule dada alikuwa anaogopa hata kuvaa vizuri! Na akiona vipi anawagawia hadi zawadi anazoletewa na ndugu zake!! hata sijui aliishiaga wapi yule mdada!
Nyamayao,
........namshukuru MUNGU sikupata wa hivyo mwe!! mbona ningekonda mie! Wangu wako so cooperative yaani nakumbuka enzi zile, mkienda kwenye vikao au mikusanyiko ya familia wao kazi yao ni kuangalia mwonekano wa ndoa za kaka zao through faces..yaani mkiingia tu wanawakagua wakiona hali flan vipi haieleweki (ile kununiana kishkaji) utaskia .......

mh wifi vipi? mbona kama TV ina chenga haikamati?.......basi ukisema tu network search wifi yangu........watakwambia umekjaribu kuelekeza antena mjini wifi? ukisema ndio basi wanakupoze usijali subiri. Mkishamaliza vya kumaliza wanamtania kaka yao kutahamaki mnaondoka mmeshikana mikono! yaani wote wanachangia!

Nafikiri hii ni maalumu maana sometimes bwana kaka zao wanakuwaga kama vichaa !
 
Last edited by a moderator:
exsperience inaonesha wanawake wanapenda sana umbea, sasa kama dada au mama wa mume ni mbea inabidi mume atafute waifu mbea, hakyababu watapendana balaa. hapa jirani kuna mdada na wifi yake wambea ajabu, basi wanapendana mpaka samtaimu wanabadilishana makufuli na masidiria. ama kweli maisha ujanja.

Dah! nawahi paredi, conclusion ya hii post nitatoa next time
napenda pia kuwasalimu MJ1, Nyamayao na Bht kwenye hii sredi bila kumsahau selebriti wa walalahoi TFinest
 
that is an achievement mae...hongereni sana!

sasa nyamayao ukikuta mwanaume ambae hataki kusikia changamoto zinazosababiswa na mama au ndugu zake na wewe mwenyewe ndo laini laini hukawii kuikimbia ndoa.

ucdhubutu.....unaiacha ndoa ukiwa umeshindwana na mume tu sio vinginevyo!
 
exsperience inaonesha wanawake wanapenda sana umbea, sasa kama dada au mama wa mume ni mbea inabidi mume atafute waifu mbea, hakyababu watapendana balaa. hapa jirani kuna mdada na wifi yake wambea ajabu, basi wanapendana mpaka samtaimu wanabadilishana makufuli na masidiria. ama kweli maisha ujanja.

Dah! nawahi paredi, conclusion ya hii post nitatoa next time
napenda pia kuwasalimu MJ1, Nyamayao na Bht kwenye hii sredi bila kumsahau selebriti wa walalahoi TFinest
Aiseee Kumbe dhamana niliyokuwekea imefanya kazi uswahili uliacha una kesi nyingine ya wizi wa masufuria
 
exsperience inaonesha wanawake wanapenda sana umbea, sasa kama dada au mama wa mume ni mbea inabidi mume atafute waifu mbea, hakyababu watapendana balaa. hapa jirani kuna mdada na wifi yake wambea ajabu, basi wanapendana mpaka samtaimu wanabadilishana makufuli na masidiria. ama kweli maisha ujanja.

Dah! nawahi paredi, conclusion ya hii post nitatoa next time
napenda pia kuwasalimu MJ1, Nyamayao na Bht kwenye hii sredi bila kumsahau selebriti wa walalahoi TFinest

Shemeji.....................umenikamilishia mwanzo wa mwisho wa wiki dah........nimecheka sana. Aksante mwkaya kwa observation yako.

Salamu zimefika, nikuchagulie sahani gani??
 
MJ1....kama umejua, ka wifi ni kadogo kangu but kalikuwa kanataka kuniburuta, cku hizi kana heshima huwezi kuamini...hahahaha network search, geuzia antena mjini....hahaha nimecheka kwa nguvu zote.
 
MJ1....kama umejua, ka wifi ni kadogo kangu but kalikuwa kanataka kuniburuta, cku hizi kana heshima huwezi kuamini...hahahaha network search, geuzia antena mjini....hahaha nimecheka kwa nguvu zote.

Acha tu Mamito yaani wale huwaga nawaombea kwa MUNGU kila iitwayo leo, wafanikiwe na kubarikiwa. Nadhani bila wao ningeshakuwaga chizi barabarani. ......maana nilicheza na antena mpaka wenyewe wakakiri kweli wifi hii ya blaza (wanavyomwita wenyewe) ni ya kichina !! wakabwaga manyanga nami nikayatua yangu.
 

...kiukweli, maisha yamejaa suspicious minds/looks kila mahala unapokwenda. Ni vile weye unavyoweza ya balance maisha yako na kuji adapt haraka haraka na changes.
Challenges huanzia pale;

---mtoto anapowatambua watu wa nyumbani, na kuwa 'mtoro' kwa asiowajua...
---unapopelekwa shule kwa mara ya kwanza, kuanza kujenga urafiki na wanafunzi wenzio, kumzoea mwalimu nk
---unapohamishwa shule/kuingia shule mpya i.e sekondari...unakutana na wanafunzi wapya nk
---unapoingia chuo/vyuoni nk...
---unapoanza kazi/unapobadilisha kazi...kujuana upya na wafanyakazi wapya...nk

Hizo challenges zote ulizopitia na kufaulu ni ishara kwamba ni wewe mwenyewe unashikilia funguo za maelewano,
vipi unataka jamii inayokuzunguka ikuchukulie. Ukiamua kujiweka mwenyewe mwenyewe jamii itakutenga tu.
Ukijifanya too intruisive, jamii nayo itakuchukulia hivyo na kuwa na tahadhari nawe.

La msingi, jiwekee mipaka...nini la kuongea, nini la kutokuongea.
Nini la kufanya, nini la kuliepuka. Tangu mwanzo unajifunza lipi la kujenga,
lipi litabomoa. Hakuna formula ya kuishi na watu kwa jinsi ya mitazamo yao
La msingi, be yourself.

Mke/Mume, ana nafasi kubwa kukusaidia mawazo/maoni ufahamu wa ndugu zake,
Akili kichwani mwako kuhakikisha nawe unatumia busara zako jinsi ya kuishi nao.

Kumradhi, nimepita kuwasabahi tu dada zanguni...hii sredi imekalia ki kitchen party zaidi..lol..
 
Tatizo laweza kuwa limeanzishwa na yeyote kati ya hizo pande mbili; muolewaji au wakwe na mawifi. Mfano mimi nimeshaona baadhi ya ndugu zangu wa karibu ambo wameolewa na wana power sana kwa wame zao. Ninachokion japo hao wanawake ni ndugu zangu hata mimi huwa najisikia vibaya. Kwa ufupi wanatake advantage ya kupendwa kwao kuwanyanyasa wakwe na mawifi zao hasa kama familia ya mume haina uwezo.

Cha muhimu ni ku play your part. Ni kosa kubwa sana kuwa mbaguzi kwa maana ya kupendelea ndugu zako kuliko ndugu za mumeo; ukiweza hilo nadhani hata mumeo atakupenda na hicho ndoyo kikubwa. Kama mnasaidia wazazi wenu basi mtoe pesa sawa kwa pande zote mbili. Kama mnaishi na ndugu basi siyo ujaze ndugu zako tu ndani wakija wa mumeo unaanza visa. Otherwise be yourself dont stretch too much kwani mwisho wa siku ndoa ni yenu wawili hao wengine ni third parties. Ila kumbuka kuwa ukigombana na ndugu za mumeo unampa wakati mgumu mumeo na sidhani kama unapenda umpendae awe na wakati mgumu.

Kuna wanaume mpaka wakitaka kupeleka pesa kwao wafanye siri kisa wife atanuna. Huwezi mpeda mumeo ukachukia nduguze hayo ni mapenzi ya kilaghai.

Mimi nilijipanga kuwa mwema kwa wakwe na mawifi zangu na nilisema hata nkipata mume anayetegemewa kwao sitafanya hilo kuwa chanzo cha ugomvi ndani ya nyumba yangu, lakini nadhani Mungu hakupenda kunipa majaribu maishani mwangu ninaishi na mume na wanangu tu na wakwe na wazazi tunawasaidia from a distance kwa kuwa they don't need to live with us.
 
Watu wengi wakioa huwa wanajisahau. Antention inabadilika kabisa, ukaribu aliokuwa nao kwa dada zake na mama yake unapungua!
Hata kama mimi ni mama au dada mtu, lazima nikuone kama wewe ndio umekuja kusababisha utengano wetu! ni dhahiri kuwa sintakupenda.
Cha muhimu ni kuwapenda mama mkwe wako na wifi zako,
Jifunze kukubaliana na kila hali..

Unayosema ni kweli kabisa, lakini inakuwa ngumu mno pale mke anavyojitahidi kadri ya uwezo wake kuwa karibu na wifi zake na mama mkwe lakini bado juhudi zake hizo zisizae matunda yoyote ya kuwa na uhusiano mzuri kati yao. Nayasema haya kwa kuwa nimeshayashuhudia mara nyingi sana na inafikia wakati mke inabidi anyooshe mikono juu na kukubali kushindwa kwamba hawezi kuwa uhusiano mzuri na mawifi zake na mama mkwe. Hawa mawifi na mama mkwe mara nyingi humuona huyo binti "anafaidi sana" au "anamuendesha" mumewe.

Mama Wakwe na Mawifi kama hawatataka kuifuatilia ndoa ya mume (mtoto na kaka yao) labda kila siku iendayo kwa Mungu (Wamekula nini, kamnunulia kanga zipi, kamnunulia gauni la namna gani bei gani, viatu vyake mbona ni ghali mno n.k.) labda hii itasaidia kuwepo na uhusiano mzuri vinginevyo ni utata mtupu ambao unaweza kabisa kuivuruga ndoa hiyo na kuitia dosari kubwa sana na si ajabu kuvunjika.

Pia wapo wake wakorofi ambao mara nyingi hawataki mume asaidie upande wake hata kama ana uwezo mkubwa wa kufanya hivyo, hawa pia wakiacha hii tabia mbaya basi labda kuna uwezekano wa kuwa na "uhusiano" mzuri.
 
Kwa kweli tuongee ukweli akina dada kabla ya kuolewa huwa mnakuwa mna adabu sana na mnanyenyekea sana.
Sijui ile inakuwaga ni nidhamu ya woga wala sijui ili upate dili la kuolewa na bro au dogo.
Mambo yanabadilika mkisha ingia ndani ya nyumba kuwa miongoni mwa familia yetu dahhh hapo vitimbi na misuguano huanza.
Kama wewe dada ni mnoko au jeuri kwa nini usijionyeshe tu toka mwanzo tujue shemeji yetu mnoko mkiwa katika harakati mnajivika ngozi ya kondoo mkisha zama ndani ndo mnakunjua makucha yenu sasa mashemeji na mawifi wanabaki mdomo wazi hivi ndo huyu huyu kweli aliyekuwa anatuheshimu?? Hapo bado biti la kuwekewa kikwazo cha uhuru wa kwenda kusalimia kwa bro. dahhh
 
Back
Top Bottom