Mahusiano makazini . . . Je Unaitwaje??

CPU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
3,863
686
Ndugu zangu wana JF
Leo nina kitu nataka tujadiliane

Maofisini au makazini tunafahamiana na watu wa aina mbalimbali, kuanzia makabila, dini, matabaka, mpaka tabia. Na hata mashuleni na mavyuoni. Kwa mchanganyiko huu tunajikuta tunajenga urafiki na watu mbalimbali. Ngoja nitoe kilichonituma nipost hii topic.

Kule bandarini (TPA) kuna mzee mmoja anaitwa Kirondo Manyanya (his official name) ana umri upatao miaka 48 sasa. Ana watoto wakubwa wa3. Siku moja alimuaga mke wake anaenda kazin siku ya Jmosi ambayo anawahi kurudi. Mke akaingiwa na wasiwasi baada ya kuona mume wake kachelewa kurudi, akawaomba watoto wake wawili waende kazini kwa baba yao maana huenda akawa kapata matatizo huku wao hawajui. Watoto kufika mapokezi, baada ya salamu wakauliza:
"Tumekuja kumuona Mzee Manyanya, yupo?"
Wakajibiwa: "Mzee Manyanya?? Mbona hakuna mtu wa jina hilo hapa? Kwani mnamjuaje"
Wakasema: "Ni baba yetu, anafanya kazi hapa muda mrefu sana"

Basi yule mtu wa mapokezi akaamua amuite mfanyakazi mmoja amuulizie kama anamfahamu Mzee Manyanya.
Yule mfanyakazi akajibu: "Eeh ndio namfahamu"
Yule mtu wa mapokezi akashangaa! "Hee! Mbona simjui??"
Akajibiwa: "Si ndo yule Mzee wa Kujambisha, kwanza nani anamtaka maana hapa hajulikani kwa jina hilo bali ni Mzee wa Kujambisha"
Yule mapokezi akamwambia ni watoto wake. Basi wakaruhusiwa waingie ndani.
Basi yule mfanyakazi akawa hajui alipo, akaamua kuchukua viganja vya mikono yake akabana na mdomo ili ajambishe: "Brruuuuuuuuuuuu"
Mara akasikia jibu: "Wee K*mamakooo"
Kwa kufuata jibu na sauti lilipotokea akawaambia wale watoto: "Baba enu yupo upande huu"
Kufika eneo hilo kukawa na makontena mengi, hawajui alipo. Akajambisha tena: "Brruuuuuuuu"
Wakasikia tena jibu: "Wee K*maaa, unafi*wa"

Basi akajua, huyo mzee yupo kontena lipi akawapeleka tena wale watoto.
Kufika kwenye kontena karibu kabisa na alipo Mzee Manyanya, yule mfanyakazi akajambisha tena: "Bruuuuuu"
Yule Mzee akafura kwa hasira, akagonga lile kontena kwa nguvu na kumfuata aliyejambisha huku akitukana matusi ya nguoni mfululizo.
Ile anatoka tu akakutana uso kwa uso na watoto wake!!!!! Akaamua apoe! Akawauliza: "Mmekuja kufanya nini?"
Wakamjibu mama yao kawatuma waje kumuangalia.
Basi akawaambia yuko salama waende nyumbani. Mzee akaanza kuwasindikiza watoto wake nje, ghalfa tena yule mfanyakazi akajambisha tena: "Bruuuuuu". Yule Mzee kama kawaida, akamwaga matusi mbele ya watoto wake.

Sasa huo ni mfano tu wa baadhi ya majina ambayo watu huitana makazini, maofisin au hata mashuleni na mavyuoni kutokana na mazoea fulani waliyojenga kwako au tabia fulani uliyonayo. Wengine huitwa DOGO, KICHWA, EM BII OO, FISADI n.k.
Je haya majina tunayadhibiti vipi hususani mipaka yake? Kama ni jina la kukudhalilisha tunachukua hatua gani?
Anakuja mgeni chuoni kwako, kazin kwako anasikia unaitwa "Wee kindimu cha jukwaa, leo una wageni ??" Unajisokiaje kudhalilika hivi??
Maoni yetu tafadhali.
 
Kuna mkaka hapa kazini tunamwita Mfadhaiko manake akiona sketi ngeni imetuna kidogo atatamani aende yeye reception kuipokea
 
lmao! funny story! miye kazini saa zingine wananiita dogo, sijui sababu mfupi! ila uzuri kuna boundaries, kama amekuja mgeni jina langu official ndio linalotumika.
 
Mambo ya kazini hayo huwa kuna utani sana,ndo maana wakati wa likizo au w/end huwa tunawamis wafanyakazi wenzetu!
 
Mkuu ukitaka ucheke/ufurahi zaidi fatilia mapenzi/ mahusiano ya kimapenzi kati ya dereva na secretary, au mlinzi na mpishi.. Utacheka! Itokeapo ofisin watu hawa wanauhusiano chakwanza kwao ni kununiana pale moja wao awapo karibu na boss teh!
 
lmao! funny story! miye kazini saa zingine wananiita dogo, sijui sababu mfupi! ila uzuri kuna boundaries, kama amekuja mgeni jina langu official ndio linalotumika.

Duuuh!
Lakin kwa mwanamke sio ishu inalipa nasikia
 
Mkuu ukitaka ucheke/ufurahi zaidi fatilia mapenzi/ mahusiano ya kimapenzi kati ya dereva na secretary, au mlinzi na mpishi.. Utacheka! Itokeapo ofisin watu hawa wanauhusiano chakwanza kwao ni kununiana pale moja wao awapo karibu na boss teh!

Daaah
Mbona humalizii?
Hebu mwaga mauzoefu yako ya hao watu
 
Utani ni mzuri,ukipitiliza ndo matokeo yake hayo,kwa kule TPA inabidi kumsamehe huyo mzee Manyanya-ni tradition ya huko.
 
lmao! funny story! miye kazini saa zingine wananiita dogo, sijui sababu mfupi! ila uzuri kuna boundaries, kama amekuja mgeni jina langu official ndio linalotumika.
yaaani hilo DOGO lomekomaaa,nimelikataaa weeee waaapi,eti kisa sijaoa.....kila anitae uutansikia DOGO,
 
Maeneo yoote ya Ofisi yana utani saana dhidi ya wafanya kazi wenzao.. But ninachojua mara nyingi wahusika automatically huchange pale mgeni hasa mtoto mdogo (Not neccessarily mdogo saana) watu hurudi katika hali zao.. Hao ulotolea mganao wamevuka mpaka Aisee... tena watoto watakua disturbed mpaka waje waelewe ni badae saaaana...
 
Mie wananiita mama ngina!! sielewi jina hili limeanza anza vipi? lakini nimekuwa mtu wa mwisho kulijua hapo ofisini kumbe naitwa muda mrefu sijijui!!! kuna mwanamume mmoja tunamwita 'kitombi' maana hata akiona mdoli wa kike atamani kumtia hapishi chambo baba huyo!!!
 
kuna jamaa alikuwa hajui kuwa anaitwa kiuno

kwa sababu kiuno chake kiko juu juu hivi...

siku moja mbele yake
watu wamejisahau......
ishu ilianza kwa kiuno kumwambia mdada mmoja amwambie mdada mwingine anamwita

wakasahau,
walipokutana mbele yake,ndo wakajisahau kabisa

wakaulizana mbele yake..

wewe si nilikwambia kiuno anakuita??????????

jamaa akauliza kiuno ndo nani?????????lol
 
mimi kazini kuna jamaa anaitwa Mswati akiona sketi tu kosa hata kama amechoka lazima afanye kazi,mwingine tunamwita vuvuzela..anapenda sana sifa na kuongea hovyohovyo,sasa ole wako akusikie unamwita hilo jina umekwisha.
 
Mie wananiita mama ngina!! sielewi jina hili limeanza anza vipi? lakini nimekuwa mtu wa mwisho kulijua hapo ofisini kumbe naitwa muda mrefu sijijui!!! kuna mwanamume mmoja tunamwita 'kitombi' maana hata akiona mdoli wa kike atamani kumtia hapishi chambo baba huyo!!!
Hapo kwenye blue,asije akawa rafiki yangu wa zamani tukiwa chuo,ila tulikuwa tunafupisha tunamuita KITO
 
Back
Top Bottom