Mahakama ya Uhujumu Uchumi: Mvutano mkali kesi ya Mbowe na wenzake. Hatma ya kesi kujulikana Septemba 6

Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu inaendelea kuunguruma kwenye Mahakama ya Uhujumu uchumi , Ambapo mvutano wa kisheria umekuwa mkali hasa baada ya Mapingamizi yaliyowekwa na Mawakili wa Mbowe kuwa ya moto .

Kesi imeahirishwa kwa muda ili kuiruhusu Mahakama kupitia mapingamizi hayo na ufafanuzi wa mawakili wa serikali

View attachment 1922291
Polisi wanapoteza muda tu na kesi hewa
 
Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu inaendelea kuunguruma kwenye Mahakama ya Uhujumu uchumi , Ambapo mvutano wa kisheria umekuwa mkali hasa baada ya Mapingamizi yaliyowekwa na Mawakili wa Mbowe kuwa ya moto .

Kesi imeahirishwa kwa muda ili kuiruhusu Mahakama kupitia mapingamizi hayo na ufafanuzi wa mawakili wa serikali

View attachment 1922291
Serikali inawapa wakati mgumu majaji kama alivyowahi kusema kwa Rais Magufuli mmoja wa majaji wakuu wastaafu.
 
Yaani kamanda tuvushe yuko mahakamani hadi sasa ni ukrasa wa pili tu? Ama kweli makamanda uchwara wamejichokea. Ufipa kwishilia mbali.
 
Kesi hii ni kama Mahakama haitaki vyombo vya habari vishirikishwe kama wadau watakaoifanya Kesi hii ni ya wazi kwa umma. Media zikikaribishwa au kuomba kuwepo ili kuhabarisha umma ingekuwa jambo jema.

Ila sasa media zimebaki kuripoti jinsi gari la karandinga lilivyotinga Mahakamani kwa spidi kali huku askari magereza wakiruka toka ktk landrover defender kama askari wa miavuli ndiyo imekuwa habari kubwa ktk kuripoti kesi ya Mbowe.
  • The normal rule is that criminal proceedings should be conducted publicly.
  • Nonetheless, courts do have power to order that the public be excluded.
  • The exercise of that power, in common with any other derogation from the principles of open justice, should be strictly confined to cases where the public's presence would 'frustrate or render impracticable the administration of justice'.

03 September 2021
Mahakama ya Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi
Dar es Salaam, Tanzania

MBOWE AFIKISHWA MAHAKAMANI TENA, ALIOENDA NAO WAPIGWA PINGU, MAHAKAMA KUTOA UAMUZI



Source : Global TV online


3 Sept 2021
Kesi ya Mbowe wenzake yaanza kuunguruma, wafikishwa Mahakamani chini ya ulinzi mkali


Kesi ya uhujumu Uchumi inayowakabili Mwenyekiti wa Chadema na wenzake watatu wakituhumiwa kujihusisha na vitendo vya Ugaidi leo tena imeanza kuunguruma Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi. Mbowe na wenzake wamefikshwa mahakamani hapa saa 9:00 wakisindikizwa na Askari wa Jeshi la Magereza wenye silaha, huku katika viunga vya mahakama ulinzi ukiwa umeimarishwa vya kutosha kwani askari polisi wenye sare na silaha na wasio na sare wakiwa wametanda kila kona ya mahakama hii kuhakikisha kuwa ulinzi na usalama unadumishwa.
Source: Mwananchi Digital
 
Lissu si alisema hawatamwekea mawakili? Au ndiyo yale yale ya kubadili gia angani
 
Kati ya vitu nimeshuhudia Leo kuwa Kuna watu wanaijua Sheria na wengine wanabebwa na katiba mbovu basi ni leo hii, maana sio kwa umombo ule uliojaa vocabulary za adabu za kisheria Hadi nikatamani kurudi shule loooh
Acha ushamba, kujua umombo siyo kujua sheria
 
Back
Top Bottom