Mahakama ya Mbeya yafuta Kesi dhidi ya Wasanii Bi. Sifa Boniventura na wenzake

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,305
24,200
15 December 2023
Mbeya, Tanzania

WIMBO MNATUONA MANYANI
Hii ni baada ya jamhuri kuamua kutoendelea na kesi hii iliyovuta umma mpana kuijadili huku ikiituhumu serikali kubana uhuru wa kujieleza.

Wasanii waimbaji Sifa Boniventura Bujune, Salome Mwampeta na Hezekiel Miliyashi walifunguliwa mashtaka mwezi September 2023 kwa kusambaza "ujumbe usio sahihi - false information" chini ya kifungu cha sheria Cybercrime Act 2015 baada ya kuimba wimbo unaoshutumu ukatili wa polisi na utawala usio sikivu (police brutality and irresponsive governance).

Katika wimbo wao wenye title : Mnatuona Mayani , mstari wake mmoja uendao kwa ujumbe 'kijana kangolewa jino lake na Polisi bila sababu' jamhuri iliona mstari huo siyo kweli .

Baada ya kesi hiyo kuendeshwa kwa miezi minne katika mahakama ya wilaya ya Mbeya, leo tarehe 14 December 2023 Hakima wa Wilaya ameamua kuifuta baada ya upande wa jamhuri kuonesha haina niya ya kuendelea na kesi hii iliyoshutumiwa na wananchi kutoka kila kona ya nchi.

1702676980580.png


Mbali ya wananchi kushutumu kuminywa kwa haki ya wasanii kuelezea hali ya mambo yanayoendelea katika jamii pia wanataaluma na watetezi wa uhuru wa kujieleza kama wakili msomi Fatma Karume rais wa zamani wa TLS, pia Robert Mwampembwa kutoka taasisi ya kukuza ubunifu pia wakili wa kujitegemee Philip Mwakilima walishutumu kesi hiyo waliyoita haina mashiko zaidi ya kuminya uhuru wa kufikiri na kujieleza kupitia majukwaa mbalimbali.
 
15 December 2023
Mbeya, Tanzania

WIMBO MNATUONA MANYANI
Hii ni baada ya jamhuri kuamua kutoendelea na kesi hii iliyovuta umma mpana kuijadili huku ikiituhumu serikali kubana uhuru wa kujieleza.

Wasanii waimbaji Sifa Boniventura Bujune, Salome Mwampeta na Hezekiel Miliyashi walifunguliwa mashtaka mwezi September 2023 kwa kusambaza "ujumbe usio sahihi - false info" chini ya kifungu cha sheria Cybercrime Act 2015 baada ya kuimba wimbo unaoshutumu ukatili wa polisi na utawala usio sikivu (police brutality and irresponsive governance).

Katika wimbo wao wenye title : Mnatuona Mayani , mstari wake mmoja uendao kwa ujumbe 'kijana kangolewa jino lake na Polisi bila sababu' jamhuri iliona mstari huo siyo kweli .

Baada ya kesi hiyo kuendesha kwa miezi minne katika mahakama ya wilaya ya Mbeya, leo tarehe 14 December 2023 Hakima wa Wilaya ameamua kuifuta baada ya upande wa jamhuri kuonesha haina niya ya kuendelea na kesi hii iliyoshutumiwa na wananchi kutoka kila kona ya nchi.

View attachment 2843685

Mbali ya wananchi kushutumu kuminywa kwa haki ya wasanii kuelezea hali ya mambo yanayoendelea katika jamii pia wanataaluma na watetezi wa uhuru wa kujieleza kama wakili msomi Fatma Karume rais wa zamani wa TLS, pia Robert Mwampembwa kutoka taasisi ya kukuza ubunifu pia wakili wa kujitegemee Philip Mwakilima walishutumu kesi hiyo waliyoita haina mashiko zaidi ya kuminya uhuru wa kufikiri na kujieleza kupitia majukwaa mbalimbali.
Tunamjua aliyekuwa nyuma ya kesi hii ni Tulia. Wana Mbeya wameshikana na binti Yao Bwigane ameanza kuhaha. 2025 sako Kwa bako.
 
Hamas wanapambana na NATO, USA NA ISREAL hadi leo mambo magumu sana kwa umoja huo
 
Hapa siyo mahakamani, nitatoa mbele ya Hakimu hata kama Hakimu wa mchongo.
 
15 December 2023
Mbeya, Tanzania

WIMBO MNATUONA MANYANI
Hii ni baada ya jamhuri kuamua kutoendelea na kesi hii iliyovuta umma mpana kuijadili huku ikiituhumu serikali kubana uhuru wa kujieleza.

Wasanii waimbaji Sifa Boniventura Bujune, Salome Mwampeta na Hezekiel Miliyashi walifunguliwa mashtaka mwezi September 2023 kwa kusambaza "ujumbe usio sahihi - false info" chini ya kifungu cha sheria Cybercrime Act 2015 baada ya kuimba wimbo unaoshutumu ukatili wa polisi na utawala usio sikivu (police brutality and irresponsive governance).

Katika wimbo wao wenye title : Mnatuona Mayani , mstari wake mmoja uendao kwa ujumbe 'kijana kangolewa jino lake na Polisi bila sababu' jamhuri iliona mstari huo siyo kweli .

Baada ya kesi hiyo kuendesha kwa miezi minne katika mahakama ya wilaya ya Mbeya, leo tarehe 14 December 2023 Hakima wa Wilaya ameamua kuifuta baada ya upande wa jamhuri kuonesha haina niya ya kuendelea na kesi hii iliyoshutumiwa na wananchi kutoka kila kona ya nchi.

View attachment 2843685

Mbali ya wananchi kushutumu kuminywa kwa haki ya wasanii kuelezea hali ya mambo yanayoendelea katika jamii pia wanataaluma na watetezi wa uhuru wa kujieleza kama wakili msomi Fatma Karume rais wa zamani wa TLS, pia Robert Mwampembwa kutoka taasisi ya kukuza ubunifu pia wakili wa kujitegemee Philip Mwakilima walishutumu kesi hiyo waliyoita haina mashiko zaidi ya kuminya uhuru wa kufikiri na kujieleza kupitia majukwaa mbalimbali.
Wastage of public funds
84e563410094df35433f3a3fd014f21f.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom