Wapendwa wa Jukwaa hili, naomba niende zaidi ya kile kilichoelezwa kwenye mtiririko huu wa michango kwa leo. Going beyond borders, kama wanavyosema CNN. Ila mimi kwanza natangaza maslahi yangu kwenye suala hili, ili kuepuka unafiki ambao wengi wetu huonesha humu. Mimi ni Mzanzibari na ni Muislam. Nachangia suala ambalo linanihusu na halinuhusu pia. Linanihusu kwa kuwa wanaoongelewa hapa ni Waislam wenzangu walio upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano. Halinihusu kwa kuwa kwetu Zanzibar tayari tunayo Mahakama ya Kadhi na tunakusudia pia kwenda mbele kwa kujiunga na Jumuiya ya OIC, baada ya kurekebisha mawili matatu, ambayo huko nyuma yalituzuia tusijiunge.
Tuangaliane machoni kisha tuambizane ukweli, kwamba kinachotuhangaisha wengi wetu ni udini na hali ya kutokukubali kwamba tuna udini. Hali hii, kwenye saikolojia huitwa 'perplexive complexity'. Inapochanganywa na ile 'superiority complex' ambayo wengi wetu tumejengwa kujiaminisha kwamba Waislam Tanganyika ni raia wa daraja la tatu kwenda chini, unakuwa ugonjwa kamili - absolute abnomality.
Mahakama ya Kadhi imekuzwa na kufanywa liwe jambo kubwa sana, na hoja yoyote inayoletwa kuitetea hukandamizwa kwa kuuhusisha Uislam na westoxicated definitions za ugaidi, mujahidina, na mengine mengi, ambayo hayaelezi chochote zaidi ya Islamophobia, ugonjwa mwengine wa kisaikolojia. Ukweli hasa hauelezwi kwamba huko kwenye Mahakama za Kadhi, kama hapa petu Zanzibar, sheria zinazotambuliwa kuhukumu mambo ya kiraia na kihalifu ni zile za serikali.
Baya zaidi ya yote ni mjadala unapopotoshwa na kuja suala la nani atalipia mahakama hiyo, husemi kwamba hakuna mahakama nyengine ambazo haziwahusu raia wote lakini zinaendeshwa na kulipiwa na serikali hiyo hiyo. Husemi kwamba hakuna miradi mengine mingi ya taasisi za kidini ambazo zinaendeshwa na mfuko wa serikali hiyo hiyo inayolipiwa kodi na raia wote.
Ni woga tu, wapendwa. Woga wa kwamba jamii ya Kiislam Tanganyika imetengwa kando ya mfumo wa utawala na uendeshaji kwa miaka nenda miaka rudi na sasa jamii hii imeanza kujitambua na kujiimarisha kama jamii yenye taasisi zake, ndio unaowafanya wenye imani tafauti ya kidini waone kwamba sasa kuna kundi linakuja kuchukua nafasi yao.
Si kweli kwamba unaowangoza hapa ni uzalendo wa nchi na khofu kwamba ikiwa Waislam wataanzisha mahakama ya kuhukumu mambo yao, Tanganyika itakuwa Jamhuri ya Kiislam kama ya Iran. Munajuwa kwamba hilo haliwezekani na wala halipo kwenye makusudio, ila munajenga picha ya makusudi ili mutimize muradi wenu, kama ambavyo huko nyuma, kwa kutumia njia, mbinu na mikakati tafauti, mulifanikiwa kuwasukuma kando Waislam kwa visingizio vingi, kikiwemo hiki munachokitumia sasa cha kwamba hawana elimu, hawakusoma, hawajui kuongoza.
Kwangu, tafauti ni ya fursa ya kiuchumi na maslahi ya kuutawala mfumo zaidi kuliko lilivyo la kidini.
Nawasilisha