Magufuli: Saddam alikuwa rais wa Kuwait!!

Mature Entry student phenomena ndivyo ilivyo. Kukariri kwa wingi sana ili uonekane uko sawa au zaidi ya direct entry students.
 
Nilishasema huyu bwana kimataifa ni embarrassment kwa nchi yetu bado CCM wakamchagua kugombea urais. Magufuli anaziweza local politics tu za kimataifa hazijui kamwe itabidi wampeleke kwanza chekechea ya siasa za kimataifa.
 
Gazeti la mwananchi mnatakiwa kumuomba radhi mheshimiwa dr. Magufuli kwa kumnukuu vibaya.

Msipofanya hivyo tutaamini mwandishi wenu ameshiriki uovu. Jina la mwandishi ni mpunta wadinya.

Queen esther

nimenukuu ukurasa wa 22 wa gazeti la mwananchi la leo 16/09/2015
para ya kwanza; naomba ninukuu" msifanye mabadiliko kwa pupa kama watu wa libya. Walimwondoa madarakani rais saddam , hapana rais gaddafi maana saddam alikuwa rais wa kuwait"

"magufuli , na lowassa nani atatufaa kwa siasa za nje" ni kichwa cha habari cha article yenyewe.

Magufuli huyu anayejua kila barabara ya nchi hii ameshindwa kujua vitu vya darasa la nne vinavyotokea nje ya mipaka ya tanzania sembuse siasa za kimataifa atazijulia wapi. Kuna uwezekano akashindwa kujua hata majina ya nchi tulizopakana nazo, au kushindwa kujua marekani, india uk nk zipo mabara gani. Kama ni hivyo je atajuaje trouble makers na marafiki wa kweli anaoweza kushirikiana nao katika siasa za dunia. Au ushindi kwanza mengine yatajipa?. Ukiona rais hajui kinachoendelea upande mwingine wa dunia ujue kazi tunayo hivyo tusifanye makosa katika uchaguzi wa mwaka huu la sivyo watanzania woote tutaonekana mambumbumbu.
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, kwa hakika Magufuli anaweza sana kuwa waziri chini ya Raisi mtendaji, lkn magufuli hafiti/hatoshi kuwa Rais wa nchi kwa jinsi alivyo.

Nadhan hii si tu kwakuwa sasa kasimamishwa na CCM la hasha, ila mara nyingi imejadiliwa hapa hata kabla haijajulikana atakuja kuwa mgombea wa uRais kuwa huyu hatoshi.

Ni sawa na useme Chadema apewe Tundu lissu agombee Urais kwa haraka utajua tu lisu anaweza kuwa mtendaji mzuri lakn asifae kuwa kiongozi mkuu wa viongozi wengine.

Hii na kwa magufuli ni ivo ivo, anaweza uwaziri, akiongea kwa style yake ile ya comedic na data za uongo flan basi watu wanafurai na wizara inaenda, lakn sio kuwa Rais wa nchi.

Rais inahtaji mtu makini, anaesoma sana na kuelewa mambo mbali mbali ya ndani na nje, Diplomasia, Uchumi, Siasa, asiekurupuka kusema ili tu apate popularity au watu wajue pia yupo eneo husika.

Magufuli kwa hayo au sifa hizi ana pwaya, lakn namvisha Lowasa Urais, namuona akitenda kwa haiba ya pekee sana, kwanza lowasa anaonekana anajisomea sana na kusoma habari za Dunia ya nje, anajua mambo mengi, ana uzoefu na serikali na uongozi, ni mtulivu sana.

mara nyingi E. Lowasa akiongea katika mahojiano au hotuba yeyote (fatilia) lazima utamsikia akitoa nukuu mbalimbali au akinukuu kauli za viongozi kama Tony Blair, Magreth Thatcher, Frank D loosevet, nk nk

Hii tu inaonesha ni mtu alie na uwanda mpana wa kujua Mambo ya nje, na Diplomatic protocol /issues.

Magufuli si mtulivu hata kidogo, anaongea mara nyingi ili aonekane anajua, au asifiwe kwa kuwa na tarakimu kichwani, na wengi mkifatilia nyingi ni mbwembwe tu si kweli kuwa ndiyo ilivyo.

Magufuli hana exposure nje ya nchi na mambo ya kigeni. Asije akafanya mambo ya Tshangrai aliekutana na Waziri mkuu wa Germany na kuchemsha kila hatua aliopiga.
 
Watanzania bhana yaani mtu aliye takiwa kuwa jela kwa ufisadi eti leo anagombea uraisi wa nchi ni balaa.

Ntawanyima kura yangu CCM kwa sababu serikali yao imeshindwa kumshitaki mahakamani kwa "ufisadi" kwa miaka zaidi ya 7 na sasa mpaka anagombea urais na ana uwezekano mkubwa wa kushinda uchaguzi.
 
Achana naye kalewa pombe huyo hana sera. Tunataka nyumba zetu alizohonga vimada
 
iyo phd gani ya kushindwa kutofautisha iraq na kuwait

Ishu yenyewe ya sadam imeheadiline karibu muongo mmoja na nusu inayohusu iraq na sadam na vita ya marekani.

Hata mtoto wa darasa la kwanza hawezi kufanya seriuos mistake namna hiyo ya kushindwa kujua sadam alikua rais wa wapi na rais wa libya alikua nani maana hilo jambo kila siku lazima liongelewe kwenye habari kuhusu mashariki ya kati.

Madhara ya kukalili sasa mnayaona,magufuri hafai kua rais,ana kichwa chepesi sana.let magufuri be a minister,prime mimister or director general of any public company, sio urais.
 
Back
Top Bottom