Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Na usisahau kua mamlaka kamili alikua hana, kweli alikua mbunge ila pia waziri. Hapo angejifanya msema kweli azma ya urais angeisikia kwenye radio. Ukisha pigia mizinga 21 ndio unaweza kushuhulikia mautumbo kwa uhakika zaidi...... Labda nikusaidie kaka ukijibu tena usisahau jina la lugumi!!!!
Hivi unajua kweli unachosema hapa? Utetezi mwingine wa hovyo...!
 
Kuwalinda Lugumi na kitwanga, pia Mwakyembe juu ya mabehewa chakavu, January Makamba juu ya Madili yake kibao, Dau na Ufujaji pesa za Ujenzi wa daraja na miladi mingine ya NSSF , NIDA , ATC , IPTL , escrow, kivuko kibovu cha mwaka 1978 kununuliwa Kwa bilion 8 , kumbukumbu za uuzaji nyumba za Serikali nk , haya ni mojawapo yanayomkwaza Kwa sasa .

Hivi mtu kama wewe unajua hata sheria ya manunuzi ni kitu gani kweli!?, JF kuna haja ya kureview vigezo vya mtu kukidhi kuwa member, unless kuwe na jukwaa la watu wa aina yako.
 
Alipokuwa kule Arusha (kama wiki mbili zimepita) alisema kuwa wabadhilifu wa Sukari anawajua na majina anayo. Hiki ni kichekesho sana, sasa kama unawafahamu kwa nini usiende kuwakamata, kama sio mambo ya kinafiki ni nini sasa hiki?

Akaenda mbali zaidi akasema"wameficha sukari Mbagala" mazombi wake wakaenda huko, waliporudi wakasema ile sukari inamilikiwa ki halali, kodi imelipiwa na haina shida... Jamaa akaumbuka.
Wewe kweli hata nikikuita mjinga nitakuwa nakusifu. Kwa akili zako hakuna aliyekamatwa? Unafikiri hao waliokuwa wakionekana kwenye Tv walikuwa wanajitokeza wenyewe. Au tafasiri ya kukamatwa kwako ni finyu.
Swala ni kuficha sukari siyo sukari ya magendo? Wewe somo la ufahamu hulijui nakushauri ujifunze, vinginevyo utakuwa mbumbumbu milele na kuendelea kuchangia ujinga. Swala la kuonesha vibali haikuwa hoja hoja ni kwanini sukari ipo na haiuzwi? Uhalali wa kuwa na sukari unao, kwanini hauiuzi kama leseni yako inavyotaka ufanye. Unajuwa wajinga nyie mnaidumaza hii nchi.
 
Suala la sukari kuadimika limemtia doa sana Rais Magufuli.Washauri wake hawakumshauri vizuri.Kitu kingine kama alivyosema mchangiaji mmoja humu,awe makini na media.Si ya kutumia sana na si ya kukaa nayo mbali.Mungu ibariki Tanzania
Cha ajabu nimemsikia Pm alisema serikali itaendelea kuagiza sukari, Sasa kama ndio hivyo kwanini serikali isijishushe na kuruhusu wafanyabiashara waagize sukari
 
Wewe kweli hata nikikuita mjinga nitakuwa nakusifu. Kwa akili zako hakuna aliyekamatwa? Unafikiri hao waliokuwa wakionekana kwenye Tv walikuwa wanajitokeza wenyewe. Au tafasiri ya kukamatwa kwako ni finyu.
Swala ni kuficha sukari siyo sukari ya magendo? Wewe somo la ufahamu hulijui nakushauri ujifunze, vinginevyo utakuwa mbumbumbu milele na kuendelea kuchangia ujinga. Swala la kuonesha vibali haikuwa hoja hoja ni kwanini sukari ipo na haiuzwi? Uhalali wa kuwa na sukari unao, kwanini hauiuzi kama leseni yako inavyotaka ufanye. Unajuwa wajinga nyie mnaidumaza hii nchi.

Na huku umefika Msororo69? Twende kwenye mada.....

Naona kama kawaida yako umechangia kwa lugha ya kejeli na kuudhi kwa kuita mwenzako mjinga

Ngoja nikujibu kwa mtindo huohuo, kwamba, likely wewe ndiye mjinga. Kwa maana mjinga ni yule asiyeelewa na asiye na ufahamu wa jambo au mambo flani. Huyu mtu mmojawapo ni wewe!!

Umesema kwamba hao waliokamatwa na wewe ukawaona kwenye TV ndiyo
walificha sukari na kwa hiyo ni kosa. Hebu tuambie wewe "mwerevu" usiye "mjinga", kesi za hao waliokamatwa ziko mahakama gani eti??

Kwa akili yako wewe mwerevu mtu mwenye kiwanda kukutwa na tani zake kadhaa katika warehouse yake, anakuwa ameficha siyo?

Tena sukari ikiwa imehifadhiwa kihalali kabisa kwa sbb imenunuliwa kihalali kwa kupitia taratibu zote ikiwemo kulipia kodi za serikali

Labda nikutaarifu tu kwamba, hapa Mwanza ndugu zako hawa unaowatetea kwa makosa yao mpaka povu linakutoka mdomoni walikamata tani 27 za mfanyabiashara mmoja tarehe 5/5/2016 kwa hisia hizohizo ulizonazo wewe.

Wameshindwa kuthibitisha kama ilifichwa na badala yake wao wenyewe wameirudisha sukari kwa mwenyewe ili aendelee na biashara yake!!

Maamuzi ya kukurupuka yana madhara yake kikubwa ikiwa ni kupoteza muda na rasrimali za serikali kwa jambo ambalo lilihitaji akili kidogo kulishughulikia!!
 
Mwanzoni mwa utawala wake ilikuwa kila gazeti linamwandika yeye tena vizuri. Vijiwe vyote kuanzia vya kahawa, daladala, bar na maofisini story alikuwa ni yeye tena watu wakimsema kama malaika mkombozi.

Ghafla upepo ukabadilika, watumishi wakaanza kukosoa utumbuaji majipu, wafanyabiashara wakakosoa mbinyo wake kwenye kodi, wanasiasa wakahoji style yake ya uongozi. Wananchi wa kawaida wakanigwa na maisha magumu (ingawa hawa bado wamebakiza kaimani fulani). Vyombo vya habari wanalalamikia kuminywa uhuru wao.

Kiujumla upepo unavuma vibaya kwa JPM naye ameshakiri ugumu wa kiti chake mpaka akasema angejua asingegombea urais. Je, rais wetu amekosea wapi mpaka hali imegeuka mapema hivyo?
Hilo ni kweli mkuu,na wanaomfatilia watagundua usemalo lakini wasiomfatilia na watajua ni yule yule wa kipindi kile ameingia madarakani,kumbe ulikuwa ni moto wa gazeti
 
Mwanzoni mwa utawala wake ilikuwa kila gazeti linamwandika yeye tena vizuri. Vijiwe vyote kuanzia vya kahawa, daladala, bar na maofisini story alikuwa ni yeye tena watu wakimsema kama malaika mkombozi.

Ghafla upepo ukabadilika, watumishi wakaanza kukosoa utumbuaji majipu, wafanyabiashara wakakosoa mbinyo wake kwenye kodi, wanasiasa wakahoji style yake ya uongozi. Wananchi wa kawaida wakanigwa na maisha magumu (ingawa hawa bado wamebakiza kaimani fulani). Vyombo vya habari wanalalamikia kuminywa uhuru wao.

Kiujumla upepo unavuma vibaya kwa JPM naye ameshakiri ugumu wa kiti chake mpaka akasema angejua asingegombea urais. Je, rais wetu amekosea wapi mpaka hali imegeuka mapema hivyo?
Anajua tatizo ni chama chake na yeye mwenye ni zao la hicho chama na hawezi kutenda tofauti na chama, na ndio kiwanda cha majizi,mafisadi na mazembe. hivyo kiwanda kinachotengeneza sumu hakiwezi tengeneza sukari.Viongozi wote waliotoka kwenye hicho chama wana tabia ya kuficha ukweli na kuongea wasichokitenda ndio maana wanapoteza imazi kwa Watanzania muda mfupi tu wa uongozi, na kinachomgharimu ni kufanya jitihada za kuficha uovu wa chama chake kupitia serekali mbaya ni kwamba kwa dunia hii ya utandawazi hataweza.
 
Back
Top Bottom