Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Yaani CCM madudu ni yale yale, huyu Ngosha naye anadhani kuongoza ni ubabe pasi kutumia demokrasia. Mawaziri wake wako kimya sasa, wanashindwa kufanya maamuzi magumu kwa dhamana ya wizara zao kwa hofu ya kutumbuliwa. 2020 hawa mburula ni lazima waende.
 
Nchi hii bila ubabe hamuwezi kwenda!!;angepita japo makotopola ndo mngenyooka zaidi!
 
mpk...

Huu uzi umenigusa. Unajua nini? Huyu Magu mwisho wake utafanana na ule wa Mkapa....ikulu kuungua kwa pasi na nyaraka kutoweka,...kujilimbikizia mali dakika za mwisho wa utawala wake baada ya kuona Unyerere unamshinda. Arudishe bunge letu live tuwahukumu wabunge kwa matendo yao.
 
jamaa miezi karibu saba ikulu hakuna cha maana njia za kumkwamua Mtanzania hazionekani amebaki kutishiya watu kila Nyanja mimi na jiuliza kimempata nini majaliwa mbona haendi na makaratasi tena kwenye taasisi
 
Mwanzoni mwa utawala wake ilikuwa kila gazeti linamwandika yeye tena vizuri. Vijiwe vyote kuanzia vya kahawa, daladala, bar na maofisini story alikuwa ni yeye tena watu wakimsema kama malaika mkombozi.

Ghafla upepo ukabadilika, watumishi wakaanza kukosoa utumbuaji majipu, wafanyabiashara wakakosoa mbinyo wake kwenye kodi, wanasiasa wakahoji style yake ya uongozi. Wananchi wa kawaida wakanigwa na maisha magumu (ingawa hawa bado wamebakiza kaimani fulani). Vyombo vya habari wanalalamikia kuminywa uhuru wao.

Kiujumla upepo unavuma vibaya kwa JPM naye ameshakiri ugumu wa kiti chake mpaka akasema angejua asingegombea urais. Je, rais wetu amekosea wapi mpaka hali imegeuka mapema hivyo?
Unaota mkuu mchana
 
Jibu hoja utakuwa umemsaidia yeye na taifa, mashambulizi kwa mtu aliyeonyesha kile kinachoonekana hayasaidii
Umesema kweli na KISHUJAA nakupa BIG BRAVOOOO,.,,., JAMANI TUWE WAWAZI MTU ANAPOKOSEA SIO KUTOA KASHFA,..,.PERIOOOOD.
 
Kuwalinda Lugumi na kitwanga, pia Mwakyembe juu ya mabehewa chakavu, January Makamba juu ya Madili yake kibao, Dau na Ufujaji pesa za Ujenzi wa daraja na miladi mingine ya NSSF , NIDA , ATC , IPTL , escrow, kivuko kibovu cha mwaka 1978 kununuliwa Kwa bilion 8 , kumbukumbu za uuzaji nyumba za Serikali nk , haya ni mojawapo yanayomkwaza Kwa sasa .
NA KUACHIA DEAL ZA MZEE WA TEZI DUME ZINAENDELEA TENA KWA KASI NA WAARABU NDIO VINARA,BANDARI, FORODHA,WAKALA WA MIZIGO,LAKE OIL NA MENGI TO NAME BUT FEW,,ETI NATUMBUA MAJIPU HAAA WE ACHA TUU,SUKARI SHS 5000 NA INGINE IMEPINDUKA LEO IKAUA PUNDA 19.
 
Amekosea kujitanabahisha kichama na kusahau kwamba raisi ni utumishi wa taifa na si wa CCM. Anachuja kwa kasi kwa sababu anavyozidi kujizamisha ki CCM ndivyo anavyozidi kuuvaa uhusika wa CCM ambaye ndiye adui mkubwa wa Watanzania waliofariki, waliopo na watakaokuwepo. CCM ni adui mkubwa zaidi ya ujinga, umaskini na maradhi, na hakuna mtu atakayejitanabahisha kulinda maslahi ya adui CCM, atabaki kuwa mwema kwa watanzania wenye mateso yasiyosemekana!.

Angetaka kuendele kung'ara, angekaa kwenye nafasi ya raisi ajenge nchi lakini si kusimamia maslahi haramia ya CCM halafu bado Watanzania waendelee kumwamini!.

Wewe ndoo unchuja. JPM HAWEZI CHUJA NA wala hatachuja. Iliyochuja haraka NI CHAMA la manyumbu Yaani CHADEMA
 
NA KUACHIA DEAL ZA MZEE WA TEZI DUME ZINAENDELEA TENA KWA KASI NA WAARABU NDIO VINARA,BANDARI, FORODHA,WAKALA WA MIZIGO,LAKE OIL NA MENGI TO NAME BUT FEW,,ETI NATUMBUA MAJIPU HAAA WE ACHA TUU,SUKARI SHS 5000 NA INGINE IMEPINDUKA LEO IKAUA PUNDA 19.
Na bado itafika ten!;mtaisoma namba!!
 
...katika maisha kuna kupanda na kushuka lkn huyu 'mtukufu' badala ya kupanda alikwea na kawaida ya anayekwea huwa hashuki bali anaporimoka...
"..the harder they come, the harder they go....."
...katika maisha kuna kupanda na kushuka lkn huyu 'mtukufu' badala ya kupanda alikwea na kawaida ya anayekwea huwa hashuki bali anaporimoka...
 
Back
Top Bottom