Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Kuna sababu kama 4 hivi naziona ndizo zinazomfanya achuje haraka hivi:

1. Kushindwa kwake kudili na majipu (wala rushwa wakubwa) na kubaki kuangaika na kesi za kuku. Hii imejionyesha kwa yeye kunywea kwenye swala la Lugumi, Wezi wa Escrow (kutekeleza maamuzi ya Bunge), kuendelea kukumbatia viongozi majizi, HSC na mambo kama hayo.

2. Kuendesha nchi pasipo kufuata utawala wa sheria. Anajiona yeye ndio ultimate decision maker wa kila kitu na hakuna anayejua zaidi yake. Sasa watu wameamua kumuacha afanye kazi zoootee peke yake.



3. Nchi kukosa muelekeo wa kiuchumi. Hii inapelekea kuwa na hali ngumu pasipo sababu. Bado anaangaika na kodi za machinga na mama Ntilie, wakati kule kwenye madini wanawaanchia wazungu wanachukua madhahabu na Almasi bureee kabisa. Hana vyanzo vipya vya kodi zaidi ya kumbana mwananchi wa kawaidi.

4. Kunyima Uhuru wa habari. Hii imejionyeshwa kupitia kukataa kuonyesha Bunge Live kwa sababu ya kuogopa wananchi kuona serikali yake ikikosolewa. Yeye anataka kusifiwa tu, ukimkosoa ni shida.

Mkuu Nkuba25 hakika wewe umeirejesha JF ya wakati uleee mdau kauliza swali zuri,nilitegemea wachangaji wangekuja na hoja nzito badala yake wengi wamekuja na viroja badala ya hoja.

Kiasi fulani nakubaliana na hoja zako hasa hili la kukosa utawala wa sheria nililiona tangu mwanzo nikajisemea Dr Magufuli yeye Rais hapo hapo anafanyakazi za kibunge,wakati mwingine anakuwa yeye mshitaki na yeye Jaji.

Hili la kuminya uhuru wa habari ndio limeniacha hoi bin taabani.Fikiria bila uhuru wa habari hata yeye asingejulikana hata kidogo.Kibaya zaidi anapenda kutumia vyombo vya habari hata mahali pasipo stahili.Mfano unatimua maafisa wa Serekali mbele ya Media tena pasipo kuwapatia nafasi ya kujitetea ?.Kila anachokifanya lazima atumie media sana tena kwa nguvu kubwa lakini Bunge hataki lionekane live ?hataki tuhukumu utendaji wa wabunge wetu tuliowachagua.

Suala la uhaba wa Sukari ni tatizo alilolitengeneza Dr Magufuli lakini lawama anawarushia wafanyabiashara tena anawatuhumu pasipo ushahidi wa uhakika eti walikuwa wakileta sukari ili expire.TBS walikuwa wako wapi,ipo kesi mahakamani kuhusiana na suala hilo kama hakuna basi hapakuwa na sababu ya kuliongelea hata kidogo hasa ukizingatia level yake kama Rais wa JMT.

Suala la Mke wa Dr Mahiga na trafic police hakuwa sawa kumpandisha askari cheo kisa kabisaha na mke wa waziri.Pili Mke wa waziri ni mtu mzima mwenye kuwajibika kwa matendo yake binafsi kumwingiza waziri tena katika mkutano wa wakuu wa jeshi la polisi haikuwa sawa hata kidogo.

Mwisho naanza kuingiwa na woga iwapo hali hii itaachwa kuendelea bila wadau mbali mbali kupaza sauti ya kuonya na kukemea ukiukwaji wa sheria,kanuni na taratibu za kuongoza nchi.
 
Kweli
Hapo unapotoka. Hicho ulichoandika ni nje ya UTAWALA WA SHERIA.Kwa hilo mimi nampongeza Mh kwa kuvumilia na kuchukua muda kujiridhisha. Tuache kulaumu kila mahali!
Kweli kabisa na hilo tumekuwa tukipigania kwamba magufuli afate utawala wa sheria....nafikiri wandani wake wamemuonya pia kwamba anaelekea kwenye anguko kuu....cha ajabu wana Ccm wenzake walikuwa wanamchekelea
 
Mkuu naomba tujadili ishu ya NIDA

Nadhani unakumbuka kuwa Mtendaji mkuu wa NIDA (Dickson Mwaimu) pamoja na wasaidizi wake 3 walisimamishwa kazi kutokana na kile Magufuli alichodai ni ubadhilifu.

Sasa jiulize, kesi ya hawa watu hipo katika mahakama gani, ni kitu gani kinachofanya hadi leo wasifikishwe mahakamani, ni uchunguzi gani unaofanyika mwezi wa 4 sasa.

Huu ni mfano mmoja tu.

Je unakumbuka kesi ya wale jamaa wa TRA? Umeshajiuliza mbona haisikiki tena?
Apo kwa NIDA ni hasara zaidi kapilimba kafukuza watu bila utaratibu sasa fidia ya kuwalipa ni zaidi ya 2 bil
 
Mkuu Nkuba25 hakika wewe umeirejesha JF ya wakati uleee mdau kauliza swali zuri,nilitegemea wachangaji wangekuja na hoja nzito badala yake wengi wamekuja na viroja badala ya hoja.

Kiasi fulani nakubaliana na hoja zako hasa hili la kukosa utawala wa sheria nililiona tangu mwanzo nikajisemea Dr Magufuli yeye Rais hapo hapo anafanyakazi za kibunge,wakati mwingine anakuwa yeye mshitaki na yeye Jaji.

Hili la kuminya uhuru wa habari ndio limeniacha hoi bin taabani.Fikiria bila uhuru wa habari hata yeye asingejulikana hata kidogo.Kibaya zaidi anapenda kutumia vyombo vya habari hata mahali pasipo stahili.Mfano unatimua maafisa wa Serekali mbele ya Media tena pasipo kuwapatia nafasi ya kujitetea ?.Kila anachokifanya lazima atumie media sana tena kwa nguvu kubwa lakini Bunge hataki lionekane live ?hataki tuhukumu utendaji wa wabunge wetu tuliowachagua.

Suala la uhaba wa Sukari ni tatizo alilolitengeneza Dr Magufuli lakini lawama anawarushia wafanyabiashara tena anawatuhumu pasipo ushahidi wa uhakika eti walikuwa wakileta sukari ili expire.TBS walikuwa wako wapi,ipo kesi mahakamani kuhusiana na suala hilo kama hakuna basi hapakuwa na sababu ya kuliongelea hata kidogo hasa ukizingatia level yake kama Rais wa JMT.

Suala la Mke wa Dr Mahiga na trafic police hakuwa sawa kumpandisha askari cheo kisa kabisaha na mke wa waziri.Pili Mke wa waziri ni mtu mzima mwenye kuwajibika kwa matendo yake binafsi kumwingiza waziri tena katika mkutano wa wakuu wa jeshi la polisi haikuwa sawa hata kidogo.

Mwisho naanza kuingiwa na woga iwapo hali hii itaachwa kuendelea bila wadau mbali mbali kupaza sauti ya kuonya na kukemea ukiukwaji wa sheria,kanuni na taratibu za kuongoza nchi.
Mkuu Ngongo

Unajua ku fail ni process. Ku fail hakuji ghafla.

Sasa ukiangalia kuanza kuanguka kwa JPM unatakiwa uangalia kutokea kwenye uchaguzi mkuu.

Amini nakwambia ni ngumu sana kuukata mkono unaokulisha au unaokufanya sasa hivi upate icho chakula.

JPM amewekwa hapo na CCM, chama ambacho kimeoza kwa uchafu wa kila namna. Na wao wanajua ni kwa namna gani wamemuweka hapo.

Sasa, linapokuja swala la kupambana na majizi na mafisadi, maana yake unahatarisha uhai wa chama. Je chama kife kwa sababu ya kumfurahisha JPM? Je JPM yupo juu ya chama? Je vigogo wa CCM wafe njaa kisa JPM? Haya yote hayawezekani. Kamwe hayawezekani.

Kwa muktadha huo, ndio maana utaona JPM anakuwa na mipaka kwenye swala la kupambana na ufisadi na utumbuaji wa majipu. Anakuwa na mipaka kwa sababu yeye hayupo juu ya chama na chama kina wenyewe.

Pia, yatupasa kutambua CCM ina mizizi hadi huko Jeshini, Polisi Magereza usalama etc. Sasa nataka kukueleza kwamba hata JPM mwenyewe hajui vita dhidi ya ufisadi na majizi anapigana na nani, (adui ni nani?)
 
Alikosea siku ile ile alitamka kwenye halaiki kwamba ya Zanzibar haya mhusu na ole wake atakayaleta fyoko fyoko atakiona cha mtema kuni.
 
Lengo lake ni zuri kwa nchi hii kama akipanga vizuri utawala wake ataifikisha nchi pazuri
 
Kwanini asichuje wakati yeye katusababishia sisi walala hoi kuunga chumvi kwenye chai? Huku kwetu Mbaha, wilaya ya Nyasa licha ya kumwona, hatutaki hata kumsikia.
 
Kumteua Nape / kibaya zaidi Nape kuichukua ajenda ya ccm Juu ya uzuiaji Bunge kuonyeshwa live!
n.b
****
Tukumbuke pia ukurupukaji wakati jk akiingia kwa jinsi nchi ilivyokuwa katika blackout ya ukosefu wa umeme!
 
Apo kwa NIDA ni hasara zaidi kapilimba kafukuza watu bila utaratibu sasa fidia ya kuwalipa ni zaidi ya 2 bil
Fidia zitalipwa sana tu.

Ndio maana juzi Makamu wa Rais, Mh Samia aliwaasa Wakuu wa Mikoa na DC kufuata sheria ya utumishi wa umma wanapofukuza/kusimamisha watumishi kazi. Mama wa watu amestuka, na ameamua kunawa mikono.

Mwisho wa siku kitakachotokea ni kwamba, watu wameiba na fidia wanalipwa.
 
Kwa Hapa Uganda bado ndio habari ya mugini..... watu wamekufuru kwa kusema eti kama tunakubali watubadilishie na nyongeza juuu.... nje bado anavuma sana aisee ila ni muhimu akafanyia changamoto za ndani maana huko ndiko alikochaguliwa ....tujifunze ya Kafulila
 
Fidia zitalipwa sana tu.

Ndio maana juzi Makamu wa Rais, Mh Samia aliwaasa Wakuu wa Mikoa na DC kufuata sheria ya utumishi wa umma wanapofukuza/kusimamisha watumishi kazi. Mama wa watu amestuka, na ameamua kunawa mikono.

Mwisho wa siku kitakachotokea ni kwamba, watu wameiba na fidia wanalipwa.
Busara anayoitumia huyu makamu utadhani kuna mchakato wa kumkabidhi nchi unaendelea ndani kwa ndani...
Haiingii akilini jambo lilioasisiwa na rais linaenda kukemewa na kukatazwa na makamu wake.
 
Back
Top Bottom