TANZIA Magambo Makongoro Amefariki Dunia

TANZIA Magambo Makongoro Amefariki Dunia

Ni muhimu taarifa ya kifo iambatishwe na umri alioufukia.
Pumziko La Amani Apate.
 
Mzee naye aache ushubwada! Amejuaje kama wamo humu? Ametaja watu kama 10 hivi wale maarufu waliokuwa pamoja si angewapigia simu tu kuliko kuja kutusumbua hapa!

Mohamed said ni Mzee lakini anaishi Kama MTU wa Karne ya 21.
Alafu kuna vijana wadogo ambao wanaishi kama wazee wa Karne ya 17.

Uhuru wa mtu kujieleza unaelewa maana yake kama angalau ulifika kidato cha nne ukapata ufaulu walau wa D moja ya Civics?
 
Duh aisee hii jf ya siku hizi jamani?
Kwamba wewe uliejiunga humu 2018.

Unadhani JF ya siku hizi ina shida kuliko sisi tulioko humu tangu 2013.

Screenshot_20250521_120734_Chrome.jpg
 
Inaonekana we ni kijitu chenye roho mbaya🤗
Majitu yenye ROHO mbaya ndio yana MDUDE.

Yalipiga SATIVA RISASI ya KICHWA.

Yalimuua AZORY GWANDA.

Yalimuua AKWILINA.

Yalimuua DEUS SOKA.

Yalimpiga Padre Kitima CHUMA cha KICHWA.

Halafu yenyewe YAKIFIWA au YAKIFA yanataka KILA MTU ASIKITIKE.
 
Kuna yule Dada wa USA Linda Beizedenhout amezaa na huyu Magambo anamislead watu kuwa ni mtoto wa Nyerere sasa wengi wanadhani ni Makongoro Nyerere ndio kafa.

Hebu tudadavulie kwa faida ya JF, Chifu Makongoro amefariki kabla Uhuru mwaka 1958, je Nyerere alimchukuwa huyu Magambo Makongoro na kumlea ndio sababu anaonekana ni kama mtoto wa Nyerere wa kumzaa?

Mwisho ningependa kujuwa huyu Magambo Makongoro Uislamu ameupata wapi kama amekulia kwenye familia ya kikatoliki?
Machifu wengi wa zamani walikua waislamu,mfano kina mkwawa,makwaia,mirambo,kinweri,etcusikute hata huyo chief makongoro
 
Huyu Mwamba namkumbuka kumuona kipindi katoka USA na Nywele alikuwa akizipiga Mafuta ya Curl 😀😀

Enzi hizo alijenga ghorofa lake Mbezi Beach na akitumia Wafanyakazi wa Interchick usiku wanamwaga Zege. Jamaa hao wamwaga Zege walikuwa wakimpa sifa Makongoro kwa umahiri wake wa kumwaga Matusi mazito hadi Wakamkubali. Hadhi yake na Matusi yake havikuenda pamoja ila kwa ufupi alikuwa Mtoto wa Mjini hadi basi 😀😀

Alikuwa akiingia speed mno na Pajero lake la hali nzuri kabisa hapo Interchick.

Kipindi hicho wakati Interchick inaanza, yeye alikuwa tayari ni Mkurugenzi wa kampuni nyingine ya huyo huyo Owner iitwayo BANDAG - tire retreaders ambacho kilikuwa Kiwanda cha matairi.
Mzungu owner nadhani alikuwa akiishi Kenya na alikuwa ni Mgeruman au Mwingereza huku akija Dar kwa ndege yake ndogo na kuzunguka hapo juu Interchick na ndiyo anakwenda uwanja wa ndege kutua.

Makongoro alikuwa na ndugu yake hapo Interchick aitwaye Matare. Sijui aliishia wapi?
Pia Mshelisheli Mike kutoka Seychells ndiyo walikuwa Weusi Wazito hapo Interchick.

RIP Makongoro....

MAGAMBO MAKONGORO AMEFARIKI DUNIA

Kwa wanaomfahamu Magambo Makongoro amefariki leo hospitali ya muhimbili, maziko kesho Kisutu Alasiri.

Msiba upo nyumbani kwake Msasani opp na nyumba ya Mzee Rais Mwinyi Mikocheni.
Nimepokea taarifa hiyo hapo juu hivi punde.

Magambo tunajuana toka udogo wetu ni mtoto wa Chief Makongoro.

Tulipokuwa shule tukifanya picnic yeye akitupeleka Kigamboni nyumba ya mapumziko iliyokuwa ya Gavana wakati wa ukoloni na kwa wakati ule baada ya uhuru ikawa iko chini ya Mwalimu Nyerere kama Rais wa Tanzania.

Mwalimu alikuwa haitumii nyumba hii na Magambo yeye kwa ule usuhuba uliokuwa baina ya baba yake na Nyerere alikuwa mtoto wa nyumbani State House.

Nakumbuka siku zile hata jina hili la Ikulu lilikuwa bado.

Magambo alikuwa mwenzetu na mchezo wetu ulikuwa mmoja pamoja na Kleist na mdogo wake Ebby, Yusuf Zialor, Wendo Mwapachu, Bubby Bokhari, Christopher Faraj, Abdallah Mohamed Saleh (Tambaza), Abdul Mtemvu, Edward Makwaia (sasa Chief wa Siha), Abdallah Mgambo, Eyshe na Mariam Max, Erica Kisa, Janet Zebedayo, Haitham Rashid, Esther Mzena wenzetu wengine wengi siwakumbuki.

Wenyewe tukijiita Scorpions na wengi tulikuwa wanafunzi St. Joseph's Convent.
Baadhi wemetangulia mbele ya haki.

Miaka ya kati Magambo alikuwa akifanya kazi Inter King iko Mbezi wanafuga kuku.

Mara ya mwisho miaka michache nyuma mwezi wa Ramadhani tulikutana Masjid Ngazija alikuwa na Abraham Sykes.

Nakumbuka siku ile walinishambulia sana kwa kunichangia ati mie najidai sana na Msikiti Ngazija nauona kama mali yangu nikiwaona wao wanakuja kusali pale roho inaniuma.

Haya ndiyo yalikuwa mapenzi yetu tulikutana lazima tubwatizane huku tunacheka.
Nilipoteana na Magambo kwa muda hatujaonana.

Allah amsamehe na amtie Firdaus.
Amin.

View attachment 3339866
Magambo Makongoro
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom