Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,633
- 6,229
Asante kwa ufafanuzi.Baba yake (au babu yake?) Magambo, Chifu Makongoro, ndiye mtu aliyemuambia baba yake Julius Nyerere, Chifu Nyerere Burito, kwamba huyu mtoto (Kambarage Nyerere) ana akili sana, anafaa kupelekwa shule.
Yule Chifu Makongoro alipokuwa anamtembelea Chifu Nyerere Burito, alikuwa anapata nafasi ya kucheza bao na mtoto wa rafiki yake na Chifu mwenzake, mtoto mwenyewe ndiye Kambarage Nyerere. Chifu Makongoro akaona kuwa huyu mtoto Kambarage anajua sana kucheza bao, anamshinda hata yeye mtu mzima. Chifu Makongoro akamwambia rafiki yake Chifu Nyerere Burito ampeleke huyu mtoto kusoma shule, kwa sababu anaonekana ana akili sana.
Chifu Burito Nyerere kwanza alisita, lakini kaka yake Nyerere aliyeitwa Edward Wanzagi (aliyekuja kuwa Chifu Wanzagi baada ya Chief Burito kufariki) naye pia akamsisitiza Chifu Nyerere Burito (baba yake Edward Wanzagi na Kambarage Nyerere) amuandikishe kuanza shule Kambarage Nyerere. Edward Wanzagi alimpenda sana mdogo wake Kambarage Nyerere.
Hiyo ndiyo historia ya Julius Kambarage Nyerere kuandikishwa shule. Chifu Makongoro alikuwa mtu aliyemshawishi baba yake Kambarage Nyerere ampeleke shule huyu Kambarage Nyerere aliyekuja kuwa rais wa Tanganyika na Tanzania.
Kwa hiyo, utaona familia ya Makongoro imekuwa na ukaribu sana na famikia ya Nyerere tangu enzi za wazee walivyokuwa machifu huko.
Na kwa hwshima ya Chifu Makongoro, Julius Kambarage Nyerere alimuita mmoja wa watoto wake jina hilo la Makongoro, Charles Makongoro Nyerwre. Baba yake Magambo Mako giro ndiyo chanzo cha jina la Charles Makongoro Nyerere, aka "kaka Mako".
Kwa historia zaidi ya uhusiano huu wa famikia za Nyerere na Makongoro soma "Nyerere: The Early Years" cha Profesa Timothy Molony (Edinburgh University).
Poppy Hatonn
Tangu namuona Interchick, niliambiwa kwamba alitunzwa kwenye Familia ya Nyerere ila hawana Undugu.
Interchick alikuwepo pia Matare Joseph Nyerere kama sijachanganya Sirname na hivyo wengi walikuwa wanajua ukweli huo.
Ila nilikuwa sijajua uhusiano wao hadi kukaa na Nyerere yeye na Dr Abdallah (Mhaya) sijui?
Hata hivyo sijawahi kuifuatilia kwa ukaribu historia ya JK Nyerere na hivyo siwezi kusema lolote. Leo walau nimepata somo zaidi maana nilikuwa najua JKN na yeye ni kutoka Familia ya Mtemi.