Mafisadi watashinda! - A somber look

Ninasema watanzania tunashinda kila siku kwa kumaanisha kwamba kila siku tunapiga hatua mbele katika , Kuhoji na kushiriki katika mambo mbali mbali ya maendeleo. Vijana wengi sasa wameshaanza kuamka na kuanza kudai nchi yao. Tupo katika Safari ya Ushindi kuelekea maendeleo, unaweza ukafikiri hatupigi hatua ila mimi ninaona tunapiga hatua.

Ninachompinga mwanakijiji ni ile notion ya kwamba RA ndie anayesababisha umasiki wa Tanzania, Kwanini anaogopa kuitaja CCM ambayo kwa mika 40 bado imeshindwa kutufikisha tunapotaka kufika.

Mwanakijiji ana agenda yake ya siri , Mimi ninamwomba atueleze nafasi ya CCM katika kutupa huo umasikini, pili atuambie nafasi ya CCM katika kumpa nguvu RA .

LeoKweli, pamoja na point zako, nafasi aliyo nayo RA ndani ya hii awamu ya nne si ya kupuuzia hata kidogo. Dr. Slaa alipotaja listi ya mafisadi iliyomhusisha si tu JK mwenyewe bali hata BWM na vigogo wengine, hatukusikia cha waziri wa habari ama utawala bora wakikurupuka. Swala la Richmond lilipowaka moto jitihada zilifanyika kuzima moto wake zilizopelekea Waziri Mkuu pamoja na mawaziri wawili kujiuzulu lakini hakuna aliyemnyoshea vidole RA. Hata Kamati ya Mwakyembe ilishindwa kumhoji RA na kuishia kulalamika tu na siku RA alipotishia kumwaga yote bungeni tulishuhudia jitihada za NEC na kamati ya wabunge wa CCM zikikutanishwa kwa kikao cha dharura sababu ya RA. EPA ilipofumuka serikali iliyowekwa madarakani na wananchi ilikiri kuwa kuna vigogo wasiokamatika na wakiguswa taifa lingeyumba. Kampuni zote zilizohusishwa na wizi wa EPA viongozi wake walichukuliwa hatua isipokuwa zilizohusishwa na RA kama KAGODA. Mh. Mwakyembe alipojibizana na RA, tulishuhudia serikali kupitia mawaziri wake wakiingilia kati na kudai ugomvi wa hawa ungeliipeleka taifa pabaya. Hivi sasa Reginald Mengi amethubutu kuligusa mbuyu RA na tena tumeshuhudia serikali kwa mara nyingine ikiingilia kwa kudai malumbano yao yangeweza kulipeleka taifa kubaya.

Huyu RA ni nani mpaka kulumbana naye kuhatarishe usalama wa taifa. Huyu RA ni nani mpaka jina lake lisipatikane kwenye daftari la usajili wa makampuni yanayodaiwa ni yake. Huyu RA ni nani serikali iliyochaguliwa na wananchi imtetemekee na kumlinda kwa hali yoyote hata ikibidi kumpoteza Gavana Mzima wa Benki. Kujiuliza haya maswali hatutaweza kupata majibu lakini nina hakika tukiacha kumwangalia kama individual na kuanza kumjadili kama institution labda tunaweza tukafikia majibu. Swali what is RA is more appropriate at this stage badala ya who is RA. Kwa nini serikali imwogope na kumlinda RA, what does he represent and who is he representing and why ? Kwa nini Raisi wetu hatulii nyumbani Tanzania na kwa mantiki hiyo hiyo kwa nini aliutaka Uraisi. Kwa nini Mzee wetu Malecela kaanza kupiga filimbi mapema hivi apewe kipindi cha pili. What is the connection between these three - Iran ? I am just talking to myself or just plain day-dreaming - hizi ndoto za mchana zina matatizo, I admit.
 
Kama tunakubaliana kuwa tuko vitani dhidi ya ufisadi na mafisadi,pengine busara zifuatazo za SUN TZU zinaweza kuwa na msaada flani:

All warfare is based on deception. Hence, when able to attack, we must seem unable; when using our forces, we must seem inactive; when we are near, we must make the enemy believe we are far away; when far away, we must make him believe we are near. Hold out baits to entice the enemy. Feign disorder, and crush him.
- Sun Tzu, the Art of War

If your enemy is secure at all points, be prepared for him. If he is in superior strength, evade him. If your opponent is temperamental, seek to irritate him. Pretend to be weak, that he may grow arrogant. If he is taking his ease, give him no rest. If his forces are united, separate them. If sovereign and subject are in accord, put division between them. Attack him where he is unprepared, appear where you are not expected.
- Sun Tzu, the Art of War

If you know the enemy and know yourself, you need not fear the result of a hundred battles. If you know yourself but not the enemy, for every victory gained you will also suffer a defeat. If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle.
- Sun Tzu

The good fighters of old first put themselves beyond the possibility of defeat, and then waited for an opportunity of defeating the enemy. To secure ourselves against defeat lies in our own hands, but the opportunity of defeating the enemy is provided by the enemy himself. Thus the good fighter is able to secure himself against defeat, but cannot make certain of defeating the enemy.
- Sun Tzu

The clever combatant imposes his will on the enemy, but does not allow the enemy's will to be imposed on him.
- Sun Tzu

If we wish to fight, the enemy can be forced to an engagement even though he be sheltered behind a high rampart and a deep ditch. All we need do is attack some other place that he will be obliged to relieve...All we need do is to throw something odd and unaccountable in his way.
- Sun Tzu

Should the enemy strengthen his van, he will weaken his rear; should he strengthen his rear, he will weaken his van; should he strengthen his left, he will weaken his right; should he strengthen his right, he will weaken his left. If he sends reinforcements everywhere, he will everywhere be weak.
- Sun Tzu

We cannot enter into alliances until we are acquainted with the designs of our neighbors.
- Sun Tzu

If we know that our own men are in a condition to attack, but are unaware that the enemy is not open to attack, we have gone only halfway towards victory. If we know that the enemy is open to attack, but are unaware that our own men are not in a condition to attack, we have gone only halfway towards victory. If we know that the enemy is open to attack, and also know that our men are in a condition to attack, but are unaware that the nature of the ground makes fighting impracticable, we have still gone only halfway towards victory.
- Sun Tzu

Sio lengo langu kuwachosha ni hizo busara za mtaalam huyu wa tasnia ya vita bali naamini zinaweza kutusaidia kwa namna flani.​

GIVING UP IS NOT AN OPTION.Hebu tuangalie mifano hii halisi ya kihistoria.Japo tunaweza kudai kuwa "mkoloni hakuondoka",ukweli ni kwamba kuna Watanganyika walipambana na mkoloni (japo naamini hawakutegemea kuwa kuondoka kwa mkoloni kungeibua matatizo mengine kama hili la ufisadi).Ni dhahiri kuwa laiti nationalist/anti-colonial movements zingefika mahala pa "kukubali matokeo" (kuwa hawamwezi mkoloni) basi uhuru usingepatikana.Najua neno "uhuru" linaweza kuzua mjadala mwingine,lakini for the sake ya discussion hii,naomba tuafikiane kuwa Tanganyika eventually ilifanikiwa kupata uhuru Desemba 9,1961.​

Na kama "uhuru" wetu umepoteza maana,basi tunaweza kupata mfano mzuri kutoka sehemu mbalimbali tu:​

  1. Mandela et al walivyokataa katakata kukubali kuwa kwa vile Makaburi wako superior ktk almost kila eneo huko waki-enjoy support ya mataifa makubwa kama US,UK,nk basi bora wabwage manyanga.
  2. Civil right activists huko Marekani wangekubali kuwa Blacks ni inferior kwa ngozi nyeupe,au utumwa ni destiny yao....sote tunajua hali ingekuwaje hivi leo!​
  3. Ukomunisti katika nchi zilizokuwa zikipata patronage ya USSR ulikuwa sio tu mfumo dhalimu lakini uliominya kila mwanya wa kuubomoa...KGB walikuwa wakinusa kila particle kuhakikisha ukomunisti unadumu milele.....sote tunafahamu what happened!​
  4. Kwa mfano wa nyumbani,uvamizi wa Idd Amini 1978-79.Hivi tungekubali kushindwa,leo hii si tungekuwa na wakati mgumu pengine zaidi ya huu tulionao ndani ya mafisadi (though that's not to say ufisadi ni lesser evil compared to ushenzi wa Amin).​
  5. Kidini,laiti Yesu angekubali kutii matakwa ya wale waliomwona adui na tishio kwa himaya zao,ukombozi (kwa sie tunaoamini hivyo) usingepatikana.Japo aliuawa,lakini (tukiweka kando maelezo ya kibiblia) vifo vya mashujaa wengi vimepelekea kuleta mabadiliko miaka mingi baada ya vifo hivyo.Martin Luther,Kennedy,Yitzak Rabbin (japo huyu jitihada zake bado hazijazaa matunda),nk.​
Binafsi,nakubaliana na analysis nzima ya Mzee Mwanakijiji.Kujumuika nao sio ufumbuzi kwa vile itakuwa mithili ya kufungua jar lenye swine flu wakati wa cyclone...tunajua matokeo yake.Kutegemea kuwabomoa kutoka ndani sio healthy strategy kwa vile ufisadi ni mithili ya HIV Infection,atakayelogwa kuji-infect consciously asitegemee kusalimika.Bado hakuna tiba!​





Giving up?Throwing in the towel?Quitting?Absolutely not solution!Ufisadi ni curable infection like malaria;inatibika (please refer kwenye mifano ya hapo juu).Tukielekeza nguvu kwenye udhibiti wa mazingira yanayozalisha parasite (breeding ground ya mafisadi) na mahala panapowapatia ustawi (need I mention that I'm referring to CCM?),pamoja na mkakati mmoja nitaoupendekeza hapa chini,tunaweza kufanikiwa....Ila ni muhimu kukumbuka kuwa mafanikio dhidi ya uzalimu ni tofauti na ujauzito,kwamba usually ni miezi tisa....au sawa na urefu wa siku (masaa 24).Instead,mapambano ya aina hii licha ya kuchukua muda mrefu kufanikiwa,yanapaswa kuwa continuous kwa kipindi chote cha maisha ya wapambanaji.Ni kama itapotokea,hypothetically,tiba ya ukimwi then watu wakaendeleza ngono zembe,ni dhahiri tatizo linaweza kuja kuwa kubwa zaidi ya awali.Na hilo tumeshuhudia baada ya kupata uhuru.Tulijisahau tukidhani mapambano yamekamilika na matokeo ndio haya:leo tunahoji kama kweli tulipata uhuru!

Proposal:Hivi kuna Watanzania wangapi wameshawahi kuwabana wanaowapa jeuri watawala?(naomba usiseme kwanini nisiwe mfano badala ya kutaka wengine wafanye hivyo.I'm currently working on this).Kwanini misukumo ya Wabongo kukutana yearly kwenye sijui memorial bash (or something like that) huko Columbus au Houston zisigeuke kuwa kum-bana senator flani au member of house of representatives kupata perspective ya watanzania wanyanyasika na sio version ya watawala?

Kwanini,kwa hapa UK,jitihada za kufungua matawi ya CCM zisipate counter-efforts za kuwabana MPs katika maeneo tunayoishi kuwahabarisha hawa donors kuwa tunahitaji msaada wao!

Efforts za aina hiyo ziki-duplicate sehemu mbalimbali zinaweza kuzaa matunda.Tukumbuke kuwa huko Iran, Shah Reza Pahlavi aliishia kung'oka (na ultimately kufanikiwa kwa Islamic Revolution 1979) kwa jitihada za kutoka nje (Ayatollah Khomeini alihamasisha revolution hiyo akiwa uhamishoni France)...

Sounds too hypothetical?Well,hypotheses zinaweza kutoka kuwa mere assumptions na kuwa testable theories palipo na dhamira ya dhati.Tukumbuke,we have everything to lose if we surrender,and everything to gain if we eventually win.

(Hiyo proposal is just one of many.I know,inaweza kuwa one of the dumbest proposals you've ever come across kwenye forum hii,lakini mfano wa namna gani hata dumbest ideas could end up bringing desired changes ni namna Hitler alivyowa-motivate (or fool) Germans kuhusu Jews na matatizo yaliyokuwa yakiikabili nchi hiyo.Hapa simaanishi kuwa Hitler was right but najaribu kuonyesha namna gani hata mawazo ya "kipuuzi" in the absense of mawazo yanavyoweza kusaidia kuleta mabadiliko).
 
Last edited:
I myself I can take out RA,

You can not!
that why I believe if CCM wants they can too.

No they can not..

And if you dont believe me PM me and I will give you a stratergy which will take you only three 3 weeks make him history in Tanzanian politics.

if you could do that.. you'll be my hero!

But I need a proof why CCM cant take him out.

because they are incapable of cutting the branch on which they sit on. Hakuna mtu ndani ya CCM mwenye uwezo huo, period. Proof, he is still there!
 
You can not!

if you could do that.. you'll be my hero!

I can take him out very easily. I am sure you ... I can
I will need a post strategy of cleaning the rest of Mafisadi first , because I dont belive he is the only and that he is the main problem, I belive almost 80% of Kamati Kuu it has to go. If you only tell me how we gona do that. I promise I will pass you a stratergy which will take you very short time to map him out of the political map of Tanzania.
 
I can take him out very easily. I am sure you ... I can
I will need a post strategy of cleaning the rest of Mafisadi first , because I dont belive he is the only and that he is the main problem, I belive almost 80% of Kamati Kuu it has to go. If you only tell me how we gona do that. I promise I will pass you a stratergy which will take you very short time to map him out of the political map of Tanzania.

don't worry about the rest of them.. most of them stand or fall with RA. So.. lets deal with this one first and you'll see how many he'll take down with him.. about 40 of them..!! The whole group that met at EL Dodoma usiku wa kuamkia Alhamisi ile..

I wish you knew what is going on..
 
Huyu RA ni nani mpaka kulumbana naye kuhatarishe usalama wa taifa. Huyu RA ni nani mpaka jina lake lisipatikane kwenye daftari la usajili wa makampuni yanayodaiwa ni yake. Huyu RA ni nani serikali iliyochaguliwa na wananchi imtetemekee na kumlinda kwa hali yoyote hata ikibidi kumpoteza Gavana Mzima wa Benki. Kujiuliza haya maswali hatutaweza kupata majibu lakini nina hakika tukiacha kumwangalia kama individual na kuanza kumjadili kama institution labda tunaweza tukafikia majibu. Swali what is RA is more appropriate at this stage badala ya who is RA. Kwa nini serikali imwogope na kumlinda RA, what does he represent and who is he representing and why ? Kwa nini Raisi wetu hatulii nyumbani Tanzania na kwa mantiki hiyo hiyo kwa nini aliutaka Uraisi. Kwa nini Mzee wetu Malecela kaanza kupiga filimbi mapema hivi apewe kipindi cha pili. What is the connection between these three - Iran ? I am just talking to myself or just plain day-dreaming - hizi ndoto za mchana zina matatizo, I admit.

i bet you.. utakuwa umesomea masomo ya Sayansi!
 
don't worry about the rest of them.. most of them stand or fall with RA. So.. lets deal with this one first and you'll see how many he'll take down with him.. about 40 of them..!! The whole group that met at EL Dodoma usiku wa kuamkia Alhamisi ile..

I wish you knew what is going on..

Is this a declaration that Tanzania is a failed state?
 
Jamani mwee kama anavyuosema Nyani Ngabu.. hakuna sababu kabisa ya sisi kuchukuliwa Utumwa..Historia ya Utumwa inaendelea hadi kesho na Uhuru wetu ulikuwa ni kuondokana na Utumwa ambao tumeurudisha sisi wenyewe. Rostam sii tatizo ila sisi wenyewe (Masikini) ndio tatizo la Umaskini wenyewe wa kufikiria.

Ebu tazameni jamani maisha yale yanavyofanana na haya.. Waarabu wawili tu wenye migobole ya kushindilia risasi waliweza kuchukua watumwa 1,000 toka Zaire hadi Bagamoyo tena kwa miaka sijui zaidi ya 500..Hivi mnafikiri walitumia njia gani kama sio kuspread fear..
Na kibaya zaidi weusi wenzetu ndio walikuwa Manyapala wanaotuchunga tusitoroke..Kuna waliosema au kuandika ati watumwa walifungwa minyororo na kukatwa visigino, huu ulikuwa uongo mkubwa kwa sababu mtumwa kama pruduct anatakiwa afike pwani akiwa na afya na mwenye uzezo wa kufanya kazi ndipo huweza kununuliwa kwa bei nzuri hivyoi hatukuwa na kisingizio hata kidogo.
- HAYA NAYAONA leo..Tunaendeshwa na kundi dogo sana la Mafisadi na Manyapala ni viongozi wazalendo wenzetu kama yule Tippu TiP mtu mweusi aliyetisha wengi.. Na sisi watumwa ktk mfumo huu hatujakosa sababu...kama kawa!

Waarabu walipotufikisha Pwani kwa wazungu nasikia watumwa wenyewe waligombania kununuliwa kwanza na wakaona sifa kuchaguliwa kwanza kwa bei kubwa..What?..Majisifa yao yalikuwa ni nani kanunuliwa kwa bei kubwa na aliheshimika while wote hawa wanakwenda kuwa watumwa..Leo hii watumwa hao hao wa Amerika na Ulaya tunawaona wameukata na pengine tunajutia kwa nini wazazi wetu hawakuwepo ktk kundi hilo.. Hizi ndizo fikra za kitumwa wakuu zangu.
Well, HAYA PIA NAYAONA hadi leo toka kwa Viongozi wetu, waandishi, Wakurugenzi, wafanyakazi hadi machinga na pengine kundi kubwa la wananchi wakulima wanapigania kuuzika kwa hawa Mafisadi na bahati mbaya au nzuri hawa mafisadi kwa uchache wao kama alivyosema Mengi ni rangi tofauti nasi (wanatambulika) sasa sijui tunafikiria watatupa pepo au kitu gani!..

Hivyo, kushinda mafisadi watashinda hiyo haina ubishi hata Kidogo na wala tusiweke matumaini ati akiondoka Kikwete tunaweza kubadilisha kitu..Nimeuliza sana kuhusiana na hili, Je, akionmdoka Kikwete nani anafaa?.. nani CCM yuko tayari kuwaangamisa Mafisadi.. Ni nani David wa CCM ambaye kweli tunaweza kusema atafanya tofauti na Kikwete. jamani sii huyu huyu Kikwete tulijenga naye matumaini dhidi ya Mafisadi wakati wa MKapa?.. Inakuwaje leo tunauzungumzia Ufisadi kama vile umeanza jana wakati ni tatizo sugu..

Wakuu zangu bila kutokea watu kama kina Kreist, pamoja na contraversial zao za imani ya dini au rangi hatuwezi kufikia kupata suluhu kwa sababu hakuna Mapinduzi yoyote duniani yameweza kufanikiwa bila kutumia tofauti hizi. Iwe Uhuru wa Marekani au South Afrika, France au Uingereza kote wameweza kuziorodhesha tofauti zao za kimwili iwe kabila, uzawa au rangi ili kupata support ya wananchi.
Huwezi kupigana na Ufisadi kwa sababu hauna rangi.. ni crime kama crime nyinginezo na kamwe hauwezi kwisha isipokuwa unaweza kupunguzwa. Ndio maana nasema jiungeni na chama cha Upinzani, mnasema hakuna chama cha Upinzani mnanikumbusha vizuri maneno ya wazee wangu waliponambia kwamba wananchi hawakuwa na imani kabisa na TAA..
Kila mtu alifikiria hakina nguvu, ni chama cha Waislaam hawawezi kushindana na Wazungu..lakini viongozi wa chama hicho hawakukata tamaa wakatafuta mbinu nyingine zaidi za kuwavuta wananchi..Siku TAA walipoweza kuonyesha tofauti ya rangi, uzawa na haki milki ya nchi yao against Wazungu ndipo watu wakaanza kufikiria kwamba alaa kumbe mali yote hii inatakiwa iwe yangu?.. Kumbe naweza kuwa kama mzungu ktk position aloshika na ni haki yangu... haya ndio Mapinduzi ya Kifikra na wala tusione aibu kabisa kutumia kila mbinu against mafisadi hata kama itahusiana na jambo lolote..
tatizo letu kubwa ni pale tunapofikiria kwamba Rostam ndiye Mungu mtu wa Mafisadi!.. hapana, Rostam katengenezwa na Rostam anatumiwa vile vile na kundi kubwa la Mafia ambalo hufanya vikao vyao kupanga mikakati. Rostam ni sawa na Dr. Slaa upande huu ambaye kaa utamwondoa leo, kesho atatokea Dr. Slaa mwingine kwa sababu unajaribu kupigana na mtu badala ya kilevi..
Hivyo Rostam is not a probel isipokuwa problem yetu kubwa ni Ufisadi, tukiweza kuuangamiza Ufisadi Rostam is nothing, utamwona mitaani akipuyanga.
 
Je kuna matumaini? Je, tuwaachie nchi kwani nasibu iko kinyume yetu? Je tukubali yaishe ili tuendelee kuzungumzia mambo mengine ya maendeleo? Je, Je tuwaachie nchi watawale wapendavyo!? Je tujiunga nao ili tuwabomoe kutoka "ndani"?

Naam kwa maoni yangu kuna matumaini makubwa sana dhidi ya mafisadi. Mafisadi sasa wameingiwa na woga na wameanza kutangatanga. Tukitumia umoja wetu tulionyesha hadi sasa Watanzania walio ndani na nje ya nchi nina hakika kabisa tutawashida mafisadi tena kwa kishindo. Kuwaachaia nchi yetu tunayoipenda mafisadi na kama kuisusa na kuitekeleza Tanzania ambayo wengi wetu tuna mapenzi ya kweli kabisa na nchi yetu. Tutawaambia nini vizazi vyetu vijavyo kama Tanzania ikiangamia kutokana na mafisadi. Vizazi vyetu vijavyo wakituuliza mlikuwa wapi Watanzania milioni 40 kupambana na mafisadi ambao hawafiki hata 1,000, tutawajibu nini!? Kwamba tuliamua kuisusa na kuitekeleza Tanzania yetu mikononi mwa mafisadi wasiozidi 1,000!? Kama tuna mapenzi ya kweli na nchi yetu basi ni lazima tuviendeleze vita dhidi ya mafisadi kwa hali na mali popote pale tulipo bila woga wala kificho.

Kwanini tuwaachie watawala uchwara ambao wameshindwa kufanya chochote kutetea maslahi ya nchi yetu? Waliahidi mambo makubwa wakati wa kampeni zao na Watanzania tukawaamini kwamba sasa tumepata wakombozi. Wakatumia maneno mazuri na kutwambia kwamba wataipitia upya mikataba ya uchimabji wa dhahabu, wataendesha nchi kwa i kwa ari mpya, kasi mpya na ngivu mpya na pia kutuhakikishia kwamba, Maisha Bora kwa Kila Mtanzania yanawezekana. Kumbe walikuwa wanafiki wakubwa baada ya kukaa madarakani miaka minne hakuna ahadi hata moja waliyoweza kuitimiza.

Pamoja na ushahidi chungu nzima dhidi ya mafisadi wa EPA, Kagoda, Richmond/Dowans, CIS, Twin Towers, ununuzi wa rada, ndege za jeshi na Helicopters, uporwaji wa mgodi wetu wa Kiwira, ufisadi ambao umeigharimu nchi yetu zaidi ta shilingi Trillioni moja hakuna hata mmoja waliyekwisha kumkamata tunachokiona ni kiini macho tu za kesi ambazo Serikali inaonyesha wazi kwamba haikuzipa kipaumbele chochote dhidi ya mafisadi wa EPA ambao wote wataachiwa huru kwa kukosa ushahidi wa kutosha dhidi yao. Watu kama hawa ni watu wa kuaminiwa kuachiwa nchi kweli!? Wametiwa mifukoni mwa mapapa mafisadi hata kufurukuta wanaogopa kutokana na kununuliwa na mabilioni ya mapapa wa mafisadi katika uchaguzi wa 2005. Hapana Watanzania wenzangu wanafiki hawa, waliojawa woga, wasio na sifa yoyote ile ya uongozi hawastahili kabisa kuachiwa nchi yetu na lazima tuwaambie wazi bila kificho kwamba hawastahili kuachiwa nchi yetu.

Hakuna sababu yoyote ya kujiunga na hawa wanafiki tunaweza kabisa kupambana nao tukiwa nje na mafanikio tuliyoyapata mpaka sasa pamoja na kuwa ni madogo lakini yanatutia motisha wengi wetu kwamba sasa Watanzania wanaanza kubadilika kidogo na ishara hizi ni kama kuzomewa viongozi mbali mbali wa chama na serikali wakiwemo Malecela na Msekwa.

Kwa kumalizia tu nawaomba Watanzania wenzangu tusichoke na wala tusibwage manyanga maana vita dhidi ya mafisadi ni vita ndefu sana. Umoja wetu utahakikisha tunashinda vita hivi dhidi ya mafisadi na watetezi wao wasiofika hata 5,000. Tunaweza kabisa kuwa na Tanzania isiyo na mafisadi. Na mimi naamini kabisa kwamba kama tutaendelea na ushirikiano katika vita hivi dhidi ya mafisadi basi tunaweza kabisa kuwashinda mafisadi. YES WE CAN JUST PLAY YOUR PART!

Alutta Continua!
 
Mimi ninatofautiana na hoja hii. Kwa mtizamo wangu naona hoja inatupa nafasi ya ku-posture na ku-grandstand bila kutueleza haswa namna gani tutaweza kufanikiwa katika vita hii. Badala yake imetupa jibu jepesi. Tatizo si kuchagua upande kati ya RA na Mengi. Cha msingi ni kusimamia haki bila kujali sura ya mhusika.

Hatujiulizi kuwa hao mafisadi tunaowaandama tukishawashinda, nini kitafuata? Jirani zetu Kenya waliing'oa KANu na kuweka matumaini yake kwa waliokuwa wakitema cheche dhidi ya ufisadi na sote tunajua yaliyotokea. Bila shaka kuna wengine wao wanaona heri wakati wa Moi. Na sisi hivyo hivyo. Tunadhani tukiitoa CCM, tukamfunga RA basi mambo yetu yatatunyookea! Si hivyo hata kidogo.

Tunachotakiwa kufanya ni kuangalia namna gani system yetu ilivyoruhusu na kulazimisha wakati mwingine vitendo vya ufisadi. Wenzetu Uingereza ilipoibuka scandal ya madai ya kurejeshewa expenses yaliyokuwa yakifanywa na wabunge, kitu cha kwanza walichofanya ni kuangalia ni namna gani ya kuzuia vitendo hivyo visije tokea tena. Nasi tunatakiwa kufanya hivyo.

Kwa mfano, tudai:
a) ulazima wa kuwepo na full disclosure kwa umma kwa mapato na kodi wanayolipa kila mwaka kwa wale wote walio katika nafasi za uongozi. Kila kiongozi atoe tax returns zake kila mwisho wa mwaka. Yake na ya spouse wake. Katika return hizo, mishahara, allowances, mapato kutoka biashara n.k. yote yawekwe wazi. Kama kiongozi anapewa allowance kwa ajili ya kulipia huduma alazimishwe kuwasilisha ushahidi wa kufanya malipo hayo. K.m. kama analipwa kwa ajili ya kuajiri dereva basi jina la huyo dereva, sifa zake na mshahara anaomlipa na ushahidi kuwa kweli analipa viambatanishwe.
b) ulazima wa kuwepo na full disclosure ya mapato na matumizi ya vyama vyote vya siasa. Mapato yaainishe makampuni na watu binafsi waliochangia na kiasi walichotoa.
c) pawe na limits cha kiasi ambacho mtu binafsi au kampuni anaweza kuchangia chama chochote kinachopokea ruzuku ya serikali.
e)Malipo na mapato ya Benki Kuuyawasilishwe kila quarter kwa kamati ya fedha ya bunge ambayo mwenyekiti wake atakuwa wa chama kikuu cha upinzani. Gavana wa Benki Kuu atoe ripoti kwa bunge kila mwaka kuhusu matumizi na mapato ya benki hiyo.
f) Nafasi zaote za watendaji wa juu wa serikali zipitishwe na bunge baada ya kuteuliwa na Rais.
g) Wakati wa uchaguzi, wagombea wote wawasilishe ripoti ya matumizi yao, gharama zao na michango yao. Ripoti iainishe nani katoa mchango na kiasi alichotoa pamoja na nani kalipwa, kwa nini kalipwa na kiasi alicholipwa.
h) Ripoti za utekelezaji wa bajeti kwa kila wizara zote ziwasilishwe kila robo mwaka kwa kamati ya bunge ya fedha niliyoitaja hapo juu. Kamati hiyo ndiyo itakayoamua kama ripoti hizo ziwe siri au ziwasilishwe kwa umma.
i) Usiri wa ripoti zote udumu kwa miaka mitatu isipokuwa zile zinazohusu usalama wa taifa. Maamuzi wa zipi zinastahili kuitwa za usalama wa taifa ufanywe na serikali ikishirikiana na kamati ya bunge husika. Ripoti hizi zifungiwe kwa kipindi kisichozidi miaka itano ambapo nazo ziwekwe wazi kwa umma.


Na kadhalika kadhalika.

Kwa kufanya hivi tutahakikisha kuwa yeyote atakaeingia, tutaweza kumbana. Ni system mbovu tuliyonayo ndiyo inaruhusu vitendo hivi. System hii hii ndiyo inayolazimisha wafanya biashara kujikomba kwa chama tawala ili mambo yao yawanyookee. Tukiondoa uwezo wa viongozi wa juu kutoa upendeleo bila kuhojiwa, basi ulazima huu utatoweka. Hakuna mfanyabiashara ambae atakuwa tayari kuwekeza mahali ambapo hana uhakika wa kufaidika!

Amandla.......
 


Hatujiulizi kuwa hao mafisadi tunaowaandama tukishawashinda, nini kitafuata? Jirani zetu Kenya waliing'oa KANu na kuweka matumaini yake kwa waliokuwa wakitema cheche dhidi ya ufisadi na sote tunajua yaliyotokea. Bila shaka kuna wengine wao wanaona heri wakati wa Moi. Na sisi hivyo hivyo. Tunadhani tukiitoa CCM, tukamfunga RA basi mambo yetu yatatunyookea! Si hivyo hata kidogo.

.

- Mkuu mfano hauko sawa, Kenya ni mafisadi wenyewe waliamua kujigeuza na kuwauza wananchi, Kibaki na Moi walikuwa kitu kimoja mpaka leo ni one thing, ilikuwa ni kanyabwoya tu hebu uliza Mwanawasa hakuwa fisadi alivyonyoosha huko Zambia, kama tunatka mabadiliko hatuhitaji hizi lame excuses, either uko na mafisadi yaani Makamba/Rostam/Manji au uko na wananchi/Mengi, hakuna nafasi ya neutrality hapo!.

Respect.

FMES!
 
Ni dhambi kubwa sana kwa wapiganaji wa ufisadi kukata tamaa au kujiunga na upande wa maadui na kuacha Taifa tukufu liangamizwena wachache.....na kuwaachia just a skeleton ya nchi kwa vizazi vijavyo!

Vizazi vijavyo vitawahukumu na kuwatia hatiani kwa udhaifu huo wa kushindwa kulikomboa taifa kutoka mikono ya wanyang'anyi!

Ni bora vita hivi vikachukua miongo kadhaa au karne kadhaa...kwa maana wajukuu, vijukuu,vilembwe vyetu vitakuja na impetus ya kuumalizia ufisadi ulionyong'onyezwa na mapambano ya tangu wakati huu hadi wakati huo ujao!.....kuliko kukataa tamaa, na kuacha ufisadi kujiimarisha zaidi Tanzania.......itakuwa ngumu zaidi kwa vizazi vijavyo kulimaliza tatizo hili kuliko ilivyo sasa!
 
- Obama ameshaaanza kuisafisha Democratic party akiwa ndani, yaani baada ya kujiunga nao kwanza.

- Mwanawasa alijiunga nao kwanza, Muluzi alijunga nao kwanza mifano ipo, tuache uvivu wa kufikiri!

FMES!
 

- Mkuu mfano hauko sawa, Kenya ni mafisadi wenyewe waliamua kujigeuza na kuwauza wananchi, Kibaki na Moi walikuwa kitu kimoja mpaka leo ni one thing, ilikuwa ni kanyabwoya tu hebu uliza Mwanawasa hakuwa fisadi alivyonyoosha huko Zambia, kama tunatka mabadiliko hatuhitaji hizi lame excuses, either uko na mafisadi yaani Makamba/Rostam/Manji au uko na wananchi/Mengi, hakuna nafasi ya neutrality hapo!.

Respect.

FMES!

Na point yako? Kwamba wakenya walimchagua Kibaki wakijua kuwa Moi ataendelea kupeta! Zambia kumenyooka? Tangu lini? Au kwa vile Chiluba ( another anti fisadi aliyegeuka kuwa fisadi) anasumbuliwa?

Kwa kifupi, hivi kweli unaamini kuwa Mengi akiwa Rais basi ufisadi utakwisha? Au Dr. Slaa? Bila kubadilisha system, temptation zitabaki pale pale. Mfano rahisi, ni wangapi kati ya hao wanaopiga kelele kuhusu ufisadi bungeni wamenyanyua sauti zao dhidi ya dhulma hii wanayotaka kufanya ya kujipandishia mishahara? Wangapi wako na Slaa katika kilio chake kuwa malipo yao ni kupita kiasi? Hawa ndio unadhani wakipata nafasi ya kutu-EPA wataacha kweli? Lame excuses ni zako. Kudhani kuwa tatizo ni personalities na si system! Mnaogopa kubadilisha system maana mnajua kuwa nanyi mkipata nafasi mtafanya haya haya mnayowalaumu wenzenu!

Amandla......
 
- Obama ameshaaanza kuisafisha Democratic party akiwa ndani, yaani baada ya kujiunga nao kwanza.

- Mwanawasa alijiunga nao kwanza, Muluzi alijunga nao kwanza mifano ipo, tuache uvivu wa kufikiri!

FMES!

Obama anasafishaje Democratic party? Mwanawasa alibadilishaje MDD? Umeishasahau ushindi wake ulivyojaa mizengwe? Alihakikishaje kuwa uchaguzi wowote utakaomfuata utakuwa fair? Angalia yaliyompata Michael Sata aliposhindana na Rupiah Banda! Kiini macho kile kile kilirudiwa. Rupiah Banda aliyepewa umakamu na Mwanawasa kama shukrani kwa watu wa mashiriki ya Zambia kwa kumpigia kura!

Unamtoa Muluzi kama mfano? Muluzi aliyetaka kubadili katiba ili aendelee kutawala.? Muluzi ambae serikali yake iliuza akiba ya mahindi ya nchi yake na kuleta janga la njaa Malawi? Mapato ya mauzo hayo ambayo hadi sasa hayajaonekana mahali! Muluzi ambae anashitakiwa na ACB ( Anti Corruption Bureau) kwa kubinafsisha mamilioni ya dola za wamalawi! Huyu ndiyo mfano wako wa wanaongoza mapambano dhidi ya mafisadi?

Mvivu wa kufikiri ni wewe, Mkuu!

Amandla......
 
- Obama ameshaaanza kuisafisha Democratic party akiwa ndani, yaani baada ya kujiunga nao kwanza.

- Mwanawasa alijiunga nao kwanza, Muluzi alijunga nao kwanza mifano ipo, tuache uvivu wa kufikiri!

FMES!
Huo uchafu unaousema wewe ni upi.Unalingalisha uchafu wa democrat ya akina Obama na huu wa CCM???
Muluzi na mwanawasa wako wapi??? You cant join them. hii thana ya kuungana nao haiwezi fanyakazi kila sehemu.Tanzania no either with them or with us. no way in fisadi chama.
 
mkuu mkjj tuwekee AUDIO YA HII THREAD!nakumbuka ile ya NANI ATASHINDA ninayo kwenye mafolder yangu ya audios
 
MKJJ, asante kwa hii mada, nilishadhani kuwa na wewe umechukuliwa na upepo huu mbaya.
Tuliosimama tupo, japo nguvu yetu ni ndogo, ila tumeshachagua siku nyingi kupigana na uzembe, wizi na udanganyifu kazini.
Mimi binafsi hata rushwa ya sh 1000 huwa sitoi wala sipokei, najua ni kero tu kwa kila ninayekutana nae, ila nimeshaamua nasimama upande gani.
Sisubiri kupata ubunge ndio nianze kukataa rushwa.
Najua rushwa kubwa haiwezi kuonana na mimi,kwa hio mimi part yangu ni hizi za trafic, hospitali, ajira, polisi nk. Nimeamua kukataa both kutoa na kupokea!!!
Hata kama wote mtaamua kukata tamaa na kuamua kulegeza.
Its my own commitment to myself!!
I keep it for me and my legacy.
I do not hate anybody (at least in actions) but I hate all corruption deals and deals to conceal them.
I hate inneficient people who claim to take rensponsibilities only in word, but do not put their hearts into the work!! (surprisingly more and more women are joining the group!! do mothers kill or give birth?)
I hate to think of the reason, why so many people claim to hate corruption, but still we can not win this! (this makes me afraid for my children)
Is there such a thing as the power of the people?
Which people by the way?

Nadhani hapa ndio tunaposema watanzania ni wanafiki sana
 
Mkjj,leo nilikuwa naongea na waziri mmoja ambaye alipata kuwa kiongozi wa vijana,akasema kuwa mwkjj anaongea mambo ya msingi sana,nimepitia hoja zako hapa kwa utaratibu mkubwa,naweza kusema kuwa zimejaa chuki binafsi dhidi ya rostam na harufu ya ubaguzi wa rangi,,haimzuii RA kuendelea kuishi maisha yake ya heshima mbele ya jamii...jamaa ana akili sana na tena wanaitajika wana JF kama mia kutoa kichwa kimoja kama cha RA

Duuh, angalia lakini usije ukawa hujui unachosema...Lini tutegemee ataitwa NASA akajiunge na wenzake kwenye tafiti za mambo ya anga badala ya kuhangaika na lobbying zisizokwisha TZ na tuhuma tele zinazomnyima usingizi? Waswahili wana usemi, ndege mjanja hunaswa na tundu bovu. Kuna mambo mengi RA na akili zake nyingi hayajui,mojawapo ni hili la watanzania kudhamiria kukata mzizi wa fitina za ufisadi. Kama angekuwa na akili nyingi angeanza kusoma alama za nyakati. Kupata support ya baadhi ya waheshimisha haijarishi kama ana akili nyingi. Mana bado kuna maswali juu yake hajatupatia majibu. Ushauri wa bure...times change
 
Hakuna kurudi nyuma. Historia (na hata dini) inatufundisha kwamba wanyonge hatimaye ushinda mradi wanapigania haki yao. Wayahudi walichomolewa Misri kutoka makucha ya Pharaoh ambaye alikuwa na hila na uwezo mkubwa sana. Nani alifikiria kwamba ANC ingetokomeza ubaguzi wa rangi huko Afrika ya Kusini pamoja na makaburu kuwa na akili, utajiri mkubwa, tekinologia na kuungwa mkono na mabeberu! Ubaguzi wa rangi uko USA ulikomeshwa kutokana na tendo moja la mama aliyekataa kumpisha kiti mzungu kwenye basi licha ya wazungu kuwa na raslimali kibao! Ufisadi wa Watergate huko Marekani ulishindwa kwa kutumia karamu! Kazi kama unayofanya Mwanakijiji unaweza kuona kama ni ndogo lakini ni kubwa mno. Kule kujua kwamba watanzania tunaibiwa (kujua tu) ni hatua moja kubwa sana ya kuelekea katika ushindi.

Biblia inasema ni kosa kubwa kukata tamaa. Hakuna silaha kubwa hapa duniani kama kusema ukweli. Kwa waamini wa dini ya kikiristu Bwana Yesu alichukiwa na mafarisayo, masadukayo na makuhani kwa kuwambia ukweli mpaka wakamsulubisha lakini hatimaye alishinda. Waache watumie "mahela" yao kutupinga tusichoke kusema ukweli kwamba: NI WEZI wakubwa.
 
Back
Top Bottom