Mafisadi watashinda! - A somber look

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Hatimaye nimefikia hitimisho kuwa juhudi za kupambana na ufisadi nchini hazitofanikiwa na ya kuwa upepo wa ushindi unavuma kuelekeza merikebu za mafisadi kuelekea ushindi! Zaidi ya watu kulalamika pembeni na kuonesha kuchukizwa na ufisadi, himaya ya ufisadi itazidi kujikita na kupenya katika vyombo vingi zaidi kwani sasa hivi dalili zote zinaonesha ufisadi haufanywi na mtu mmoja bali umekuwa ni mtandao wa uhalifu ambao umeundwa na wasomi, wanasiasa, wafanyabiashara na watu wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii.

Mwanzoni ilipotajwa kuwa ni Tanzanian Mafia nilidhani ni hyperbole lakini wiki hizi chache zilizopita na taarifa ambazo ninazipata hasa baada ya kuanza kuandika suala hili ni wazi kuwa ipo "familia ya kihalifu" ambayo imejipanga vilivyo na iko tayari kutumia nguvu zao zote kuzima juhudi zozote zile za kunyofoa meno yao kwenye migongo ya Watanzania.

Sitoshangaa joto linavyozidi kupanda waandishi mahiri wa uchunguzi wakajikuta wanashambuliwa na kitakachoelezewa kuwa ni "majambazi" na kwa mwendo huo kuleta hofu kubwa kwa waandishi na kuwalazimisha waoga kati yao kunywea na kuchukua upande wa familia hiyo.

Kama vile Jitu Kubwa linavyoshika kwa kuminya mkono wa mtoto mdogo na kumburuza ndivyo ufisadi utakavyoendelea kuburuza taifa na Watanzania wengi. Lengo kubwa ni kuhakikisha kuwa watawala wenye uwezo wa kifisadi wataendelea kutawala tena bila kuulizwa. Ufisadi utakaofunuliwa baadaye mwaka huu yawezekana ukawa ndiyo msumari wa mwisho kabisa utakaowafanya mafisadi kuja na silaha zao zote kuhakikisha Taifa zima linapiga magoti na kwa sauti kali kama ya wale nyani wa kwenye filamu ya Planet of the Apes watapiga ukelele "Bow"!

Kuelekea uchaguzi mkuu mwakani himaya hiyo imepanga sasa watu wapya kabisa kuanza kuingia katika safu za uongozi na hasa Bungeni ili hatimaye usalama wao uzidi kuhakikishwa. Kiwango kikubwa cha fedha kimeshatengwa kuhakikisha (na hili limeshasemwa na wengine) wabunge wote ambao wanapigia kelele ufisadi wanaaungushwa kwenye kura za maoni na watu wapya kuingia. Lengo la hilo ni kuhakikisha kuwa inapofika Bunge jipya ule upinzani ambao umekuwa ukisikika utakuwa umezimwa kwa kiasi cha kutosha na ukabakia kuwa ni upinzani wa magazetini.

Juhudi kubwa ya kujipanga huko sasa hivi ni kuelekea pia katika Mahakama za juu kitu ambacho kinafanywa kwa uangalifu mkubwa na tahadhari. Kwa macho ya uchunguzi tuangalie sana teuzi zinazokuja za Mahakama na kuzielewa vizuri.

Vyovyote vile ilivyo, naomba niwakatishe matumaini kabisa kuwa kufikiria kuwa "vita ya ufisadi ambayo bado inaendelea" kwa mujibu wa Mkuchika ni vita ambayo mafisadi watashinda. Watashinda kwa sababu kubwa tano.

a. Wamejipanga vizuri zaidi kuliko wanaopinga ufisadi (well organized). Wanaopinga ufisadi they are a fragmented bunch!

b. Wamewekeza fedha pale wanapokula na hawaoni haya kufanya hivyo (well funded). Wanaopinga ufisadi wanatumia maneno tu, wenye kuwekeza fedha wanaonekana wanataka kujitajirisha na wale ambao wanatumia fedha zao kupigana na ufisadi na wenyewe wanageuziwa kibano alimradi kuvuruga juhudi zao. Mtu mmoja (ambaye sistahili kufunga kamba za viatu vyake) ameniambia kwenye sakata hili la RA na RM nisichague upande kwa sababu nitaonekana nampendelea mmoja wao!

Yaani, mtu asichague upande kwa kuogopa kuonekana yuko upande mmoja. Ushauri wangu ni kuwa upande niliopo sihami, mtu anayetaka abadili yeye upande aje upande wangu, na ukija upande wangu wewe mwenzangu, ukiwa kinyume changu najua upande wako, neutrality is the position of the weak and the coward, I'm neither weak nor a coward!

Nawapongeza wale waliochagua upande mmoja kati ya hizi!

c. Wamejikita vizuri na kuwabana watawala na vyombo mbalimbali na hivyo kama utando wa buibui wanajua na wanaweza kujua chochote wanachotaka kujua (well connected). Wanaopinga ufisadi wachache walioko serikalini au madarakani wanafanya hivyo at their own risk hakuna wa kuwakinga na muda si mrefu wataanza kupukuchwa kama hindi.

d. Wanaogopesha; wanatumia serikali na vyombo vyake kuingiza hofu kwa watu wa kawaida kwa kauli za "kuvunjika kwa amani", "watachukuliwa hatua za kisheria", n.k (they command fear). Wanaopinga ufisadi bado hawajaanza kuleta itikadi ya matumaini na badala yake wamejikita na kupiga kambi kwenye mazungumzo ya ufisadi na kauli za dhidi ya CCM ambazo ni sawa (kwa maoni yangu) na mtu kuupuliza mbuyu, likianguka buyu moja anafikiri ni kwa sababu yake!!

e. Wako tayari kwenda umbali wowote ule kuhakikisha hawaondoki madarakani au mirija yao kukatwa (ready to sacrifice). Katika hili watawatoa sadaka wenzao wachache ili kutuliza munkari wa jamii lakini wakati huo huo wakiwapanga wengine.

Ninachosema kwa maneno mawili ni kuwa 'we are screwed!" (najua ni matatu!) hakuna matumaini, hakuna njia ya kutokea, na hakuna mashujaa wetu wa kutuongoza vitani. Tufike mahali aidha tusalimu amri, au tujiunge humo humo na kula nao "sahani moja". Tufike mahali aidha tuendelee kupiga kelele kwenye mtandao na kuibua mambo kadha wa kadha au tukubaliane kujiunga nao.

Huko tunakokwenda neutrality is not an option! Ni waoga na wasio na msimamo ndio watajifanya kuwa neutral wengine wetu itabidi tuchague upande au tukae kimya na kusubiri upande unaoshinda! aidha tuko kinyume na familia na himaya hii ya ufisadi (kwa vitendo siyo mawazo) au tuko sehemu ya familia hii na sisi tukipata nafasi tutakuwa hivyo hivyo!

Je kuna matumaini? Je, tuwaachie nchi kwani nasibu iko kinyume yetu? Je tukubali yaishe ili tuendelee kuzungumzia mambo mengine ya maendeleo? Je, Je tuwaachie nchi watawale wapendavyo!? Je tujiunga nao ili tuwabomoe kutoka "ndani"?
 
....

Je kuna matumaini? Je, tuwaachie nchi kwani nasibu iko kinyume yetu? Je tukubali yaishe ili tuendelee kuzungumzia mambo mengine ya maendeleo? Je, Je tuwaachie nchi watawale wapendavyo!? Je tujiunga nao ili tuwabomoe kutoka "ndani"?

Mhh..... kujiunga nao sio option (mtazamo wangu binafsi).
 
Mkjj kumbuka kwamba the only thing that can not change is the change itself. Mimi bado naamini vita hii mafisadi hawatashinda and for just one reason - Political dynamics. God forbid lakini say JK anavuta leo hii do you still think mambo yatabaki in the status quo???? Well huu ni mfano tu! Kumbuka pia hawa mafisadi hata wakishinda kwenye phase hii ya haka kavita things will never be the same as it is at the moment.
 
Dr. SLAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA.....................................
 
Ukijiunga hata siku mmoja huwezi kupinga kwani utakuwa umeona matunda yake na lazima utakuwa kama wao kulinda masilahi yako. Hutakubali kusikia mtu anakuita fisadi, hutakuwa tayari kusikia chombo cha habari kinakuandika, hutakuwa tayari kusikia mtu anataka kumtoa madarakani aliyesababisha wewe uwe fisadi!!

Hivyo dawa ni kuongeza nguvu za kuwasema hadharani kwa kutumia nguvu za wananchi, na kwa kuwa MUNGU yu pamoja nasi, Mimi naamini Upande unaopinga UFISADI UTASHINDA tena kwa kishindo kikubwa na utakuja shangaa.

Walikuwepo akina Mobutu nani aliwagusa, !! sasa wapo wapi, walikuwepo akina Boaz SA nani aliwagusa , sasa wapo wapi. Ilikuwepo imaya ya kirumi ilikuwa na nguvu kuliko lakini ilivunjika. Hivyo Mwanakijiji usikate tamaa endeleza mapigano, na kuna wengine wanazaliwa leo watakuja endeleza mapambano hata kama itapita miaka 10 vumilia utakuja ona matunda siku mmoja na utajisifu kwa hilo.
 
ufisadi wa Tanzania umejifunza sana kutokana na mafisadi wa nchi nyingine, wanajua ni vitu gani vya kufanya na vipi vya kutokufanya.. Wanajua hulka moja ya Watanzania nayo ni kuridhika kirahisi. Lakini zaidi wanajua pia kuwa ukiwaambia mambo ya "uvunjifu wa amani" siku chacha baada ya kilichotokea Mbagala wanajua kabisa Watanzania hawawezi kufikiria kukaa zaidi ya siku moja katika mazingira ya namna hiyo..
 
ufisadi wa Tanzania umejifunza sana kutokana na mafisadi wa nchi nyingine, wanajua ni vitu gani vya kufanya na vipi vya kutokufanya.. Wanajua hulka moja ya Watanzania nayo ni kuridhika kirahisi. Lakini zaidi wanajua pia kuwa ukiwaambia mambo ya "uvunjifu wa amani" siku chacha baada ya kilichotokea Mbagala wanajua kabisa Watanzania hawawezi kufikiria kukaa zaidi ya siku moja katika mazingira ya namna hiyo..

Na ndio maana Waafrika tulitawaliwa na kuchukuliwa watumwa!! Sijui kama kuna connection...but what the heck....watu wachache hivi watatufanyaje wote tuishi maisha ya dhiki na utiifu namna hii?
 
Kwanini tukubali kushindwa kirahisi ivi???? bado..bado..bado naamini kwa kutumia midomo yetu hii hii maana ndio utajiri tulio pewa na mola sis wana wa Tanzania tutashinda tu..inaweza isiwe kwa mwaka mmoja au miwili au mitatu..but iko siku ndoto zetu zitatatimia...tutapata nchi tuliyokua tunaiota na kuitamani kwa miaka mingi.....safari ya vitendo ianze 2010.!
 
Kuelekea uchaguzi mkuu mwakani himaya hiyo imepanga sasa watu wapya kabisa kuanza kuingia katika safu za uongozi na hasa Bungeni ili hatimaye usalama wao uzidi kuhakikishwa. Kiwango kikubwa cha fedha kimeshatengwa kuhakikisha (na hili limeshasemwa na wengine) wabunge wote ambao wanapigia kelele ufisadi wanaaungushwa kwenye kura za maoni na watu wapya kuingia. Lengo la hilo ni kuhakikisha kuwa inapofika Bunge jipya ule upinzani ambao umekuwa ukisikika utakuwa umezimwa kwa kiasi cha kutosha na ukabakia kuwa ni upinzani wa magazetini.
Mzee Mwanakijiji,

Lakini pia si kuna mipango imeandaliwa ya watu kulia wanaangushwa kwasababu ni wapinga ufisadi wakati wanajua sababu kubwa ni kushindwa kwao ku deliver waliyoahidi.

Mipango hiyo ni kuhakikisha kila atakayewapinga basi huyo anaunganishwa na mafisadi hata kama hana uhusiano na mafisadi.

Naamini mipango yote haitafanikiwa, hakuna ambaye ana mkataba na bunge, miaka mitano ikiisha kila mtu ana haki sawa ya kushiriki uchaguzi mahali popote.

Watu wanaanza kuzua mambo ya ajabu ajabu kupakazia watu wengine na kuwahusisha na vitendo ambavyo hata havipo, je huo sio ufisadi?

Kuna watu wanataka kutumia vita dhidi ya ufisadi kama mtaji wa kisiasa 2010. Nitaelewa kama mtu atasema yeye anafaa kwasababu amefanya A, B, C na pia amepigana na mafisadi. Lakini kuanza kusingizia kila anayeingia kwa mpambano kama ni fisadi, amepewa pesa na mafisadi nk. bila ushahidi wowote naamini huo ni ufisadi mkubwa sana.
 
Hii vita haitashindwa, pamoja na kupoteza wapiganaji mapambano yataendelea na atakayegeuka nyuma 'AGEUKE JIWE'

Wale wanaokumbuka miaka 30 ilyopita wakati tunapambana na Nduli Amin, wapiganaji wetu walipata 'KIPIGO CHA LUKAYA' wengi wao walipoteza maisha na baadhi yao wakakimbia kurudi nyuma, lakini kuna mashujaa waliamua kusonga mbele na miezi mitatu baadaye tukaikamata Kampala.

Kwanini tushindwe leo kuikomboa nchi yetu kutoka mikononi mwa mafisadi? ALUTA CONTINUA! na ushindi utapatikana.
 
Mzee Mwanakijiji,

Lakini pia si kuna mipango imeandaliwa ya watu kulia wanaangushwa kwasababu ni wapinga ufisadi wakati wanajua sababu kubwa ni kushindwa kwao ku deliver waliyoahidi.

Mipango hiyo ni kuhakikisha kila atakayewapinga basi huyo anaunganishwa na mafisadi hata kama hana uhusiano na mafisadi.

Naamini mipango yote haitafanikiwa, hakuna ambaye ana mkataba na bunge, miaka mitano ikiisha kila mtu ana haki sawa ya kushiriki uchaguzi mahali popote.

Watu wanaanza kuzua mambo ya ajabu ajabu kupakazia watu wengine na kuwahusisha na vitendo ambavyo hata havipo, je huo sio ufisadi?

Kuna watu wanataka kutumia vita dhidi ya ufisadi kama mtaji wa kisiasa 2010. Nitaelewa kama mtu atasema yeye anafaa kwasababu amefanya A, B, C na pia amepigana na mafisadi. Lakini kuanza kusingizia kila anayeingia kwa mpambano kama ni fisadi, amepewa pesa na mafisadi nk. bila ushahidi wowote naamini huo ni ufisadi mkubwa sana.

unachosema ni kweli kabisa na pia ni sehemu ya ufisadi ule ule.. fisadi ni fisadi tu na anajulikana kwa matendo.
 
If you can’t fight ‘em join ‘emMimi nafikiri kama mtu una nia njema na nchi hii na una nafasi ya kupata uongozi, join them. kama tukipata watu wengi wapenda nchi ndani ya bunge na uwaziri watasaidia hatimaye kubadilisha mwelekeo wa kutawala.hawa wenzetu akina Dr Slaa na Zitto (na wengine wa upinzani) na hata baadhi ya wabunge wa chama tawala wanasikia na wanaeleweka zaidi kuliko mtu uliye mtaani. labda kuwe na platform yenye nguvu na kusikika kwa wananchi waliowengi lakini humu kwenye jamiiforums na blogs mbalimbali ni watz asilimia ngapi wana access? utaona ni almost none
 
ufisadi wa Tanzania umejifunza sana kutokana na mafisadi wa nchi nyingine, wanajua ni vitu gani vya kufanya na vipi vya kutokufanya.. Wanajua hulka moja ya Watanzania nayo ni kuridhika kirahisi. Lakini zaidi wanajua pia kuwa ukiwaambia mambo ya "uvunjifu wa amani" siku chacha baada ya kilichotokea Mbagala wanajua kabisa Watanzania hawawezi kufikiria kukaa zaidi ya siku moja katika mazingira ya namna hiyo..
MMN Unajua wakati wanapanga na kubadilisha watu watakuwa wanaweka watu ambao watakuja kuwageuka baadae. Hata Mafia iligeukwa na watu ndani ya familia na hayo yatakuja kutokea, inaweza kuchukua muda lakini mwisho wao utafika.
Wananchi sina wasiwasi naoo, wataibiwa na kuja kushtuka tuu (Hata mbwa koko ukimfukuza sana akichoka anakugeukia na kubweka) Wananchi watapelekeshwa kwa sababu ya njaa zao sasa hivi, itafika kipindi watasema hata wakifa na njaa poa tuu ila lazima wapapmbane. Ila mtu wa kuwapa moyo na munkari hao wananchi ni lazima awepo. Ingawa vita inaweza kuchukua muda sana kama mafisadi wanaendelea kupanga watu wao.
 
Shida siyo pesa wala nguvu za mafisadi. Kumbuka hata wakoloni walikua na pesa na nguvu lakini tuka washinda. Tatizo siyo connection kwa maana hata wakoloni wali shika kila nyanja ya uongozi lakini tuka washinda. Tatizo siyo organization kwa kuwa hata wakoloni walikuwa well organized na vyama vyetu vya kutu letea uhuru saa nyingine vikawa vina pingana wenyewe kwa wenyewe. Tatizo siyo fafisadi kuoandikiza watu wao maana hata wakoloni wali pandikiza watu wao tena weusi kati ya watu waliokua wana tutetea. TATIZO Tanzania we lack courage. Tumezoea sana amani mpaka watu waki tishiwa tu kuwa jambo fulani lita leta kuvunjwa kwa amani watu wanaogopa. Mafisadi wana lead kwa bluffs "kutishia kufanya kitu". Kama kila tuki tishiwa kidogo tu tunaogopa basi hatuta fika mbali. What we need is courageous leaders & courageous citizens. Vita dhidi ya ufisadi una shindika. MAfisadi wana tutawala the same way wakoloni walivyo tuta wala, kwa kutu tenganisha sisi wenyewe kwa wenyewe, kwa vitisho na kwa kudivert attention sehemu nyingine.

The only way for us to win is to focus on what is really important instead of diverting attention to non important things. Hapa JF tu unaona members mbali mbali waki gombana but if you get to the roots of it most of them wana pinga ufisadi. Lets stop fighting with each other & fight with the real enemies. Tukumbuke kuwa the more we are divided the easier we make it for the fisadis. Kama Mwana kijiji alivyo sema wao wapo organized so why don't we be organized against them badala ya kupingana hapa bila msingi? Mtu mkiona thread yake au post yake ni obvious hayupo your side usi poteze muda kuanza kubishana nae manaake naona mara nyingi thread topic ni nyingine but watu waki shaanza kucomment topic ina badilika.

WE KNOW WHO OUR ENEMIES ARE, LETS FIGHT THEM & NOT EACH OTHER. MAFISADI NI WACHACHE KULIKO SISI SASA TUSI TENGANE SISI WENYEWE KATIKA MAKUNDI NA KUWAPA WAO THE NUMBER ADVANTAGE PIA.
 
Mmkijiji,SIJAELEWA UNA MAANA GANI NA THREAD HII.JE UNATAKA NAWE KUWATISHA WA TANZANIA KWAMBA HATUWEZI KUSHINDA VITA HII AU WAJIPANGE UPYA DHIDI YA MAFISADI?
Mimi sijui nipo upande gani wa vita hii ila najua sipo ktk nafasi ya kushauri/kushawishi jamii kubwa ila naamini naweza kuwaelezea watu wawili au watatu madhara ya ufisadi na wakanielewa na kuuchukia ufisadi.HIVYO NITAENDELEA KUWASHAURI NA KUWAELIMISHA HAO NIKIAMINI NAO WANAWEZA KUWAELIMISHA WENGINE.
Tatizo kubwa linaloikumba vita didhi ya UFISADI NI ELIMU,ELIMU YA KUPAMBANA NA BILA ELIMU HIYO KUWAFIKIA WENGI NA KUIELEWA ITAKUWA NGUMU.
Wananchi wengi wakielimishwa kuwa ufisadi sio mtu bali matendo na fisadi ni mtu basi tunaweza walao tukashinda.
 
hivi kweli 'tuliwashinda' wakoloni? Mi nadhani walirudi nyuma tu na kujipanga upya, na miaka ya hivi karibuni wamerudi tena kwa mikakati mipya

They have come back through what is called neo-colonialism(ukoloni mambo leo) because our weak & corrupt leaders have let them. Hata mwizi akikuibia ukamfukuza haimaanisha hata rudi tena uki zembea. There know they need us for the own interest kwa nini wasi jaribu kurudi? Swala la wao kuridi sishangai, hata wewe ukishindwa kitu si una jaribu kwa njia nyingine? Ukim tongoza yule dada aka kukataa si una tafuta njia ya pili kumpata? Tatizo ni serikali zetu hazina msimamo, tuliwa kataa kwa njia nyingine wakaja kwa njia nyingine tuka waruhusu. Wakoloni tuli washinda wakajipanga upya na kurudi kama ulivyo sema lakini si serikali zetu ndiyo zili wapokeo kwa mikono miwili.

Wamerudi kwa njia ya misaada. Anakuja na misaada halafu ana kuambia nataka uipe tenda kampuni ya nchi yangu, utakataa? Hizi vioesa tunavyo chukua ndiyo vina wapa ubavu wa kupangia serikali zetu. Angalia Chuna, ina gombana na Marekani kila siku ila kwa ajili wana jitegemea hawa babaishwi wala kuyumbishwa. I hope nime kujibu mkuu.
 
Mmkijiji,SIJAELEWA UNA MAANA GANI NA THREAD HII.JE UNATAKA NAWE KUWATISHA WA TANZANIA KWAMBA HATUWEZI KUSHINDA VITA HII AU WAJIPANGE UPYA DHIDI YA MAFISADI?
Mimi sijui nipo upande gani wa vita hii ila najua sipo ktk nafasi ya kushauri/kushawishi jamii kubwa ila naamini naweza kuwaelezea watu wawili au watatu madhara ya ufisadi na wakanielewa na kuuchukia ufisadi.HIVYO NITAENDELEA KUWASHAURI NA KUWAELIMISHA HAO NIKIAMINI NAO WANAWEZA KUWAELIMISHA WENGINE.
Tatizo kubwa linaloikumba vita didhi ya UFISADI NI ELIMU,ELIMU YA KUPAMBANA NA BILA ELIMU HIYO KUWAFIKIA WENGI NA KUIELEWA ITAKUWA NGUMU.
Wananchi wengi wakielimishwa kuwa ufisadi sio mtu bali matendo na fisadi ni mtu basi tunaweza walao tukashinda.

Nadhani nia na mazumuni yake kwenye thread hii ni kueleza hali halisi. Wewe hauoni tuna shindwa vita? Yeye kasema tunapo elekea kama tusipo badilika sasa ni juu ya watu kama mimi na wewe tubadilike ili tushinde vita. Siwezi kuku semea mwana kijiji kwa hiyo kama nime kosea niambie.
 
Back
Top Bottom