Namanga: Madereva 23 toka Tanzania wazuiliwa kuingia Kenya baada ya kukutwa na COVID-19

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Wewe Waziri wa Afya kweli ni mwanamke unayejua uchungu wa mtoto? Kwenye janga hili la Corona unafuata muongozo upi ambao unaelekea kuiua Tanzania?

Tumechoshwa na habari za aina hii kila siku. Pia nikueleze kuwa tunachoshwa na madhila tunayoyaona huku mitaani. Hatujazoea kuishi na maiti sisi! Kama unaona huwezi kufuata mwongozo sahihi kuukabili huu ugonjwa basi ondoka ili tujue tutachukua hatua gani.

KBC.JPG

Umefikia hatua sasa unatukera waziwazi!

Madereva 25 kutoka Tanzania wamezuiwa kuingia nchini Kenya baada ya kukutwa na virusi vya corona.

Kati ya madereva hao 23 ni raia wa Tanzania , mmoja wa Uganda na mmoja kutoka taifa la Rwanda.

Kulingana na wizara ya afya nchini Kenya raia hao wa taifa jirani la Tanzania walipimwa na kupatiwa matokeo yao katika kipindi cha saa 24.

Wizara hiyo imesema kwamba hatua hiyo inalenga kuwalinda Wakenya dhidi ya maambukizi kutoka kwa raia wa kigeni.

Katika mkutano wake na wanahabari naibu waziri wa Afya rashid Aman amesema kwamba maabara 2 za kuhama hama zitazinduliwa katika mpaka wa Namanga ili kuimarisha upimaji wa wagonjwa wapya.

Aman aidha amewataka Wakenya wanaoishi mipakani kuwaripoti watu wanaowashuku ambao wanajaribu kuingia nchini kwa njia haramu.
 
Serikali ya CCM pamoja na Rais, waitishe kikao cha dharura kulinusuru taifa. Hili swala halina chama wala kabila, ni swala la dharura la kitaifa. Mambo yanaelekea kubaya.

Tumefika babaya tunatengwa na majirani pamoja pamoja na jumuiya ya kimataifa, na hii inatokana na makasa tunayofayanya kama taifa. Hatujafika sehemu ya kujitenga na jumuiya ya kimataifa. Hili ni gazette la the The Standard la KenyaView attachment 1449158
Screenshot 2020-05-13 at 09.37.14.png
 
Hao waliotest positive wamelazwa wapi? If they are positive and are stil healthy and kicking we unapata tafsiri gani? Hata huko Kenya I am sure wakitest watu barabarani watajiona watawakuta wengi tu wako positive bila kuwa na dalili yeyote
 
Serikali ya CCM pamoja na Rais, waitishe kikao cha dharura kulinusuru taifa. Hili swala halina chama wala kabila, ni swala la dharura la kitaifa. Mambo yanaelekea kubaya.
Tumefika babaya tunatengwa na majirani pamoja pamoja na jumuiya ya kimataifa, na hii inatokana na makasa tunayofayanya kama taifa. Hatujafika sehemu ya kujitenga na jumuiya ya kimataifa. Hili ni gazette la the The Standard la KenyaView attachment 1449158
View attachment 1449163
Waliopanga unataka haohao waitishe kikao cha dharula! Waongelee nini.
CHAPA KAZI HATA KAMA HOTELI YENU IMEFUNGWA.
 
"waliopewa jukumu wametelekeza, wamebaki kupambana na upinzani"

kila mtu ajipambanie kivyake!!

Sent using kidore
 
😂😂 Kwa namna hii!!! Kama ni kweli! Natilia mashaka afya zetu, huenda tumeathirika karibu wote Ila cha ajabu, Watanzania wako Imara licha ya kutembea na virusi mwilini mwao, hii Nayo ni ajabu duniani.

Mimi nishauri, ikiwezekana, kuchukuliwe vipimo, virusi wale wapimwe utendaji wao wa kazi kwenye miili yetu Watanzania ili ibainike kama virusi hao hawawezi kutuathiri tuendelee kujichanganya zaidi.
 
Madereva 25 kutoka Tanzania wamezuiwa kuingia nchini Kenya baada ya kukutwa na virusi vya corona.

Kati ya madereva hao 23 ni raia wa Tanzania , mmoja wa Uganda na mmoja kutoka taifa la Rwanda.

Kulingana na wizara ya afya nchini Kenya raia hao wa taifa jirani la Tanzania walipimwa na kupatiwa matokeo yao katika kipindi cha saa 24.

Wizara hiyo imesema kwamba hatua hiyo inalenga kuwalinda Wakenya dhidi ya maambukizi kutoka kwa raia wa kigeni.

Katika mkutano wake na wanahabari naibu waziri wa Afya rashid Aman amesema kwamba maabara 2 za kuhama hama zitazinduliwa katika mpaka wa Namanga ili kuimarisha upimaji wa wagonjwa wapya.

Aman aidha amewataka Wakenya wanaoishi mipakani kuwaripoti watu wanaowashuku ambao wanajaribu kuingia nchini kwa njia haramu.
 
Back
Top Bottom