Wakuu mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii wa watumishi wa umma PSPF hauna hela na kinachofanyika sasa ni 'kuokoteza" fedha toka vyanzo mbalimbali hususani kodi wanazolipwa kutoka majengo yao waweze kuwalipa wastaafu mbalimbali wanaochangia katika mfuko huo. Hali hii inathibitishwa na kasi ndogo ya ulipaji mafao ya mirathi, kustaafu kazi ambapo mpaka sasa baadhi ya wastaafu wa mwaka 2013 bado hawajalipwa. Kila nikifuatilia ofcn kwao ni kalenda tu na sababu za hapa na pale ambazo kimsingi hazina mashiko.