Mademu wakimya mnakera mnoo

Mademu wakimya mnakera mnoo

Hongera sana mkuu,hilo sio tatizo hata kidogo kwanza jiponeze kua na mwanadada wa karama hiyo, jikite na uwezo wake chanya wadada wa leo wengi wanamapungufu yanayosononesha mioyo ya wakaka sasa hilo la kwako kwakweli ni maakuzi yake aliyonayo. usichokonoe sana mkuu wewe mjenge pole pole maana hiyo hali umemkuta nayo na amekua nayo kwa miongo kadhaa hiyo ukitaka kumould aendane na hitaji lako inabidi pia ikuchukue mda kumjenga na usichoke. nakupa heko tu kua na jembe la hivyo
Ahsante mkuu ushauri wako ni mzurii
 
Habari za majukumu wakuu?

Kiukweli mademu wakimya sana wana boa mno.. Una kuta demu mzurii kabisa na elimu yake lakini yupo kama bubu hawezi hata kuchangia maada yoyote katika vikao vya ukoo au familia. Yaani kila kitu mpaka mwanaume aseme, yeye ni kusikiliza tu yaani hachangii chochote mpaka kero..
Back to the main point..

Yaani huyu demu wangu nafikiri ndo rais wa mademu wakimya duniani, nisipo msemesha mimi jua siku hiyo nzima hata ongea.
Mashemeji zake na mawifi zake wote wanamuogopa yaani baada ya salamu tu hana time nao tena.
Mi huwa naongea nae kwa kumuuliza vi maswali vya hapa na pale ndo wakati anajibu hapo ndo tunapiga story hivo.. Sasa inafika wakati na mimi maswali ya kumuuliza yanaisha tunabaki tunatazamana tu.

Tuna miaka mitatu kwenye mahusiano ila yupo vile vile tu.. Nilipo jaribu kumuuliza kuhusu ukimya wake akasema ndivo alivo tuNi mtu anae penda sana kujifunza vitu vingi, akimaliza kazi zake anaenda kwenye tv kufatilia BBC na CNN news pia ni shabiki mzurii wa mpira wa miguu anaweza taja hata kikosi kizima cha buyern munchen..

Watu wanamuogopa mnoo hata wageni hawaji siku akiwepo home.. Yaani hata ushoboke vipi hana time na wewe.Ni mzurii sana wa sura na umbo na elimu nzuri anayo shida ipo hapo kwenye ukimya ulio pitiliza..Alafu yupo emotional sana, yaani nikimtia mkwara kidogo tu atashinda analia siku hiyo..
Kweli "too much of any thing is harmful"

Simaanishi napenda mademu wanaoongea kama chiriku.. Kila
kitu kiwe cha wastani

Location: dodoma
Napenda sana wanawake wakimya... mie mkimya pia....
 
Nooo mimi ni story za kuchekesha tu na miti
🤣🤣🤣🤣🤣 sasa huo ndio uke wema, sio kuanzishiana varangati. Mwenzio leo hata kazini hajaenda anajiuguza mgongo huko. Ukisikia mdomo uliponza kichwa ndio hivyo yani.
 
duuh kazi maana mimi pia niliwahi kuwa na demu wa hivyo machoni pa watu ni kauzu balaa ila ni kiwa naye mimi ananisimulia hadi chupi aliyovaa asubuhi...maybe try to tell her new jokes ...lakini mademu wakimya ni wa ukweli sana huwa hawana mazoea ya kucheka cheka na mabishoo hiyo pia inaongeza ka security fulani kwenye mahusiaono maana watakua wanamuogopa
Mkimya upate mwenye combination ya romantic and cool attitude hapo utafurahia maisha.
Haongei sana kwa watu wa nje ila mkiwa wawili ni kucheka na story kibao in a very friendly way...ila akiwa nje ya lovezone yenu anakuwa hataki mazoea kiasi kwamba raia wanamgwaya. Huyo mwanamke ndio safi sana.
 
Wangu yeye haongei na mtu,yaani mkiwa wote njiani wewe utasalimiana na jamaa zako na watu mnaofahamiana njiani yeye yupo kimya,hata kama utamtambulisha huyu ni flani ataishia kumsalimia siku hiyo na hata akikutana naye kesho hatamkumbuka,mimi na yeye tunaongea tu japo kuna zile unarudi home unamkuta yupo kimya tu,ukimuuliza shida nini anasema hamna tatizo lolote,ila akianza kuongea na ndugu zake kwenye simu mpaka unaweza kumwambia aende nje maana siyo kwa kelele hizo,kama mjuavyo wamaasai ila kwa ndugu na jamaa wanaokuja nyumbani wakishamaliza salamu basi ndiyo imetoka hiyo,ngoja tu niishie hapa ila mimi nilishamzoea sema kwa watu wanaonizunguka wanapata tabu sana.
 
Muulize "kwanini Punda anatoa mlio kila baada ya saa moja?" Nakuhakikishia mtapiga story siku nzima.

Watu wakimya wanapenda mental challenges sababu maisha yao yako kichwani zaidi kuliko mdomoni, kumtoa kichwani mwambie kitu ambacho kichwa chake hakiwezi kutatua.
Yeah inasaidia kuchezesha akili yake lazma ataongea tu. Mi napenda mwanamke mpole ambae anapenda kucheka cheka akiwa na mimi. Huyo ndio atanikuna mpaka ukoko wa moyoni. Hata tukigombana nikimfanyia vituko flani afurahie tusameheane maisha yaende.

Wanawake wa mipasho wanaboa kinoma.
 
Yaah anapenda sana utani japo huwa anafurahi napokuwa natania watu.. huwa anabaki kucheka tu
Sasa mwanamke kama anapenda utani means she can laugh on your jokes as well. Unataka nini kingine mzee baba au hata ukimchekesha anakaza uso tu?
 
Habari za majukumu wakuu?

Kiukweli mademu wakimya sana wana boa mno.. Una kuta demu mzurii kabisa na elimu yake lakini yupo kama bubu hawezi hata kuchangia maada yoyote katika vikao vya ukoo au familia. Yaani kila kitu mpaka mwanaume aseme, yeye ni kusikiliza tu yaani hachangii chochote mpaka kero..
Back to the main point..

Yaani huyu demu wangu nafikiri ndo rais wa mademu wakimya duniani, nisipo msemesha mimi jua siku hiyo nzima hata ongea.
Mashemeji zake na mawifi zake wote wanamuogopa yaani baada ya salamu tu hana time nao tena.
Mi huwa naongea nae kwa kumuuliza vi maswali vya hapa na pale ndo wakati anajibu hapo ndo tunapiga story hivo.. Sasa inafika wakati na mimi maswali ya kumuuliza yanaisha tunabaki tunatazamana tu.

Tuna miaka mitatu kwenye mahusiano ila yupo vile vile tu.. Nilipo jaribu kumuuliza kuhusu ukimya wake akasema ndivo alivo tuNi mtu anae penda sana kujifunza vitu vingi, akimaliza kazi zake anaenda kwenye tv kufatilia BBC na CNN news pia ni shabiki mzurii wa mpira wa miguu anaweza taja hata kikosi kizima cha buyern munchen..

Watu wanamuogopa mnoo hata wageni hawaji siku akiwepo home.. Yaani hata ushoboke vipi hana time na wewe.Ni mzurii sana wa sura na umbo na elimu nzuri anayo shida ipo hapo kwenye ukimya ulio pitiliza..Alafu yupo emotional sana, yaani nikimtia mkwara kidogo tu atashinda analia siku hiyo..
Kweli "too much of any thing is harmful"

Simaanishi napenda mademu wanaoongea kama chiriku.. Kila
kitu kiwe cha wastani

Location: dodoma
Mi wangu pia mkimya balaa sipendi, kimchepuko nakizidi umri twice yaan katundu kananirukia hadi mgongoni, nakependea hapo tu
 
Nadhani wengine wanakuwa na matatizo ya kisaikolojia tokea utotoni mwao, inawezekana kabisa wazazi/mzazi walichangia kwa kiasi huyo binti kuwa hivyo. Wengine ni kwasababu wazazi walikuwa wanamchunga sana na viboko na kukaripia mara kwa mara. Mtoto atakuwa kama unavyotaka sawa atakuwa successful kwenye masomo lakini anajenga uoga na kutojiamini kwa kiasi kikubwa sana na ndio maana ukimpiga mkwala unamuumiza sana maana huwa anakumbuka mateso matusi aliyokumbana nayo alipokuwa mtoto, wengine waliwahi kubakwa na wazazi wao na kuwatishia Maisha, kwa style hio hio ya Question and Answer unaweza kujifunza mengi toka kwake, ukianza na wewe kuelezea past zako ulipokuwa mtoto na shida ulizopitia naamini na yeye anaweza kufunguka.
Mkuu umemaliza kila kitu... Big up sana
 
Back
Top Bottom