Madeleka kufungua kesi ili ukweli ujulikane kama waliouawa Vingunguti ni panya road

Mkuu watu wanafanya kazi 2 mbili kawaida tu.
Mchana kkoo,jioni anashika mapanga kwenda kupora.
Ukiona polisi wamedeal nae kimyakimya Ujue wanamtambua vizuri tu,
Tusiwalaumu.
Raia Wema wanatoa info toka hapo mtaani wanakokaa.
Kesi zikiwa nyingi inakua kero maana wao wataonekana hawatimizi wajibu wao.
Ndio mwisho wanakupeleka kusikoeleweka.
Ni kweli mkuu. Kuna dogo mmoja alikuwa mwizi wa boda anatumia mademu kukodisha boda then wanamkaba na kupora. Baada ya hapo ni matanuzi na sherehe mtaani. Bia kama zote. Kuna jamaa polisi mtaani akamfuata akamwambia dogo acha hizi issue kabisa nakwambia kama mdogo wangu. Dogo akajiapiza pale braza sijui nmeacha sijui blah blah nyingi. Jamaa akaondoka. Haijapita siku 3 dogo kauawa nadhani makongo juu walikuwa wanaenda kuvunja godown. Ilitangazwa hata kwenye Media walikuwa katika noah nadhani wanaelekea kwenye tukio.
Na siku hiyo anakufa alikuwa grocery ya mtaani anakula bia mida ya saa 7,8 hivi akaacha washkaji zake akasema naarudi muda si mrefu kumbe ndo anaaenda kula chumba.
So hizi issue polisi wanajua vizuri tu. Ingekuwa polisi wanadeal nazo kisawasawa vijana wengi wangeshazikwa ila huwa wanatoa muda wa kumtaka ajirekebishe
 
Madeleka hayupo kwenye pay roll ya Police.
Aliacha kazi mara baada ya kutoka kozi ya G.O hakukaa sana kuitumikia nyota3
Sawa. Endeleeeni kuamini hivyohivyo.... Mje mshangae ameteuliwa cheo kikubwa kama Diwani Athumani au yule Mchungaji Kapilimba mara BoT mara NIDA mara paap Usalama.....
 
Wawe ni panya road au sio, kuna utawala wa sheria. Walipaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria baada ya uchunguzi na sio kuuawa kikatili namna hiyo. Tusitumie hisia kujadili mambo.
Ngoja nikuuulize mkuu wewe unadhani hawa panya road huwa hawakamatwi? Hawapelekwi jela? Wakitoka wanakuwa wema au wanarejea tena? Hivi unajua wakikamatwa wazazi wao wanawadhamini wanawatoa then wanarudia tena. Je umewahi kujeruhiwa au kushuhudia tukio lolote la panya road.
Mkuu acha kutetea jambo ambalo hulijui hao watoto ni hatari kuua au kumpa mtu kilema ni jambo dogo sana kwao.
 
Ila picha za hao wanaoitwa panya road, huyo wa kushoto ukiiangalia vizuri hiyo picha ana vichembechembe vya uhalifu. Huyo mwingine mwonekano wake sio mwalifu.
 
Iki ni kichak cha kuua watoto wetu polisi wanatakiwa kudhibitisha upanya road je wataweza?
Kudhibitisha maana yake kuzuia.

Kuthibitisha maana yake kuonyesha au kuhakikisha kwa kuonyesha ushahidi wa wazi.

Hivi vijana somo la kiswahili ni tatizo kwenu?
 
Ni kweli mkuu. Kuna dogo mmoja alikuwa mwizi wa boda anatumia mademu kukodisha boda then wanamkaba na kupora. Baada ya hapo ni matanuzi na sherehe mtaani. Bia kama zote. Kuna jamaa polisi mtaani akamfuata akamwambia dogo acha hizi issue kabisa nakwambia kama mdogo wangu. Dogo akajiapiza pale braza sijui nmeacha sijui blah blah nyingi. Jamaa akaondoka. Haijapita siku 3 dogo kauawa nadhani makongo juu walikuwa wanaenda kuvunja godown. Ilitangazwa hata kwenye Media walikuwa katika noah nadhani wanaelekea kwenye tukio.
Na siku hiyo anakufa alikuwa grocery ya mtaani anakula bia mida ya saa 7,8 hivi akaacha washkaji zake akasema naarudi muda si mrefu kumbe ndo anaaenda kula chumba.
So hizi issue polisi wanajua vizuri tu. Ingekuwa polisi wanadeal nazo kisawasawa vijana wengi wangeshazikwa ila huwa wanatoa muda wa kumtaka ajirekebishe
Lakini bado polisi hawana haki ya kuua mtuhumiwa yeyote.

Polisi kazi yao ni kumfikisha mtuhumiwa mahakamani, mahakama ndiyo ina wajibu na haki ya kuhukumu.
 
Ila picha za hao wanaoitwa panya road, huyo wa kushoto ukiiangalia vizuri hiyo picha ana vichembechembe vya uhalifu. Huyo mwingine mwonekano wake sio mwalifu.
Hivihivi ndiyo mtu anavaa suti kali, ananyoa vizuri, anaingia benki, anawapiga vizuri kwa wizi wa kalamu.

Huku mnamsifia kwa jinsi alivyo smart.
 
Ngoja nikuuulize mkuu wewe unadhani hawa panya road huwa hawakamatwi? Hawapelekwi jela? Wakitoka wanakuwa wema au wanarejea tena? Hivi unajua wakikamatwa wazazi wao wanawadhamini wanawatoa then wanarudia tena. Je umewahi kujeruhiwa au kushuhudia tukio lolote la panya road.
Mkuu acha kutetea jambo ambalo hulijui hao watoto ni hatari kuua au kumpa mtu kilema ni jambo dogo sana kwao.
Kama unaona tatizo kwenye mfumo wa kurekebisha tabia wahalifu, au mfumo wa mahakama, jikite huko kutatua matatizo hayo.

Ukisisitiza na kuhalalisha Panya Road wauawe na polisi bila kufuata process, hapo bila kujua umefungua mlango wa kumfanya polisi ambaye umegombana naye kwa sababu yoyote kukuwinda hata wewe usiku na kukuua kwa kisingizio cha kwamba wewe ni Panya Road.

Si ushakubali polisi waue watu kiholela kwa kisingizio cha Panya Road?
 
Huyu wakili anahangaika sana kutafuta attention ... he is all over the contry putting his hands on every case
Muache atafute haki kwa wasio na sauti.Na wewe tumia professional yako kusaidia jamii,acha kuonea wivu wanaojitahidi.What if hao waliouwawa siyo panya road?
 
Usilolijua usipende kulishadadia.

tulee watoto wetu katika namna ifaayo tutumie fimbo pindi inapobidi.

niliwahi shuhudia wahanga wa matukio ya uhalifu. siwez sema sana ila tuzuie uhalifu tokea kwenye familia zetu na haya malalamiko hayatakuwepo.
 
Anasaka umaarufu kwa nguvu kubwa
Jadili hoja, usimjadili mtu.

Kuacha kujadili hoja ya mtu na kuanza kumjadili mtu ni ishara ya kukosa hoja.

Ni logical fallacy, inaitwa ad hominem fallacy.

Madeleka katoa hoja, umeacha kuijadili hoja yake, huna points za kuipinga hoja.

Unakwenda kumshambulia yeye mtoa hoja.

Hiyo ni ishara kuwa umefilisika kihoja.
 
Wawe ni panya road au sio, kuna utawala wa sheria. Walipaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria baada ya uchunguzi na sio kuuawa kikatili namna hiyo. Tusitumie hisia kujadili mambo.
Siku wakikufikia wewe binafsi au ndugu yako utaelewa kwanini tunawapongeza hao polisi kwa kazi nzuri ya kumalizana na hao wahalifu hatari.
Ndugu yangu mmoja wa kike alikuwa anaenda kazini 12 asubuhi akavamiwa na kibaka boda boda.
Alipojaribu kujihami na kupiga kelele jamaa kachomoa kisu akataka kumchoma ndipo watu wakatokea akakimbia.
Wakati huo huyo mama alikuwa katoka kufanyiwa upasuaji (operation) mkubwa kibaka hakujali hayo alimsukuma chini alipo anguka ndiyo akataka kumpora mkoba na kumchoma kisu.
Huyo ni mama mwenye watoto 4 tena wa mwisho alikuwa na miezi 3 tu. Umefikiria watoto wake wangelelewa vipi mama yao angeuwawa na kibaka?
 
Siku wakikufikia wewe binafsi au ndugu yako utaelewa kwanini tunawapongeza hao polisi kwa kazi nzuri ya kumalizana na hao wahalifu hatari.
Ndugu yangu mmoja wa kike alikuwa anaenda kazini 12 asubuhi akavamiwa na kibaka boda boda.
Alipojaribu kujihami na kupiga kelele jamaa kachomoa kisu akataka kumchoma ndipo watu wakatokea akakimbia.
Wakati huo huyo mama alikuwa katoka kufanyiwa upasuaji (operation) mkubwa kibaka hakujali hayo alimsukuma chini alipo anguka ndiyo akataka kumpora mkoba na kumchoma kisu.
Huyo ni mama mwenye watoto 4 tena wa mwisho alikuwa na miezi 2 tu. Umefikiria watoto wake wangelelewa vipi mama yao angeuwawa na kibaka?
Kwa nini unataka kufanya kama vile polisi hawawezi kufanya makosa, au hawawezi kubambikia watu u panya road ambao haupo?

Siku polisi uliyegombana naye mtaani akikubambikia u panya road feki na kukuua bila simile hutapata hata nafasi ya kujitetea kwamba wewe si panya road.

Ndicho unachotaka hicho?
 
Sawa. Endeleeeni kuamini hivyohivyo.... Mje mshangae ameteuliwa cheo kikubwa kama Diwani Athumani au yule Mchungaji Kapilimba mara BoT mara NIDA mara paap Usalama.....
Kuteuliwa ni ishu nyingine, nani anajua ya mbeleni?

Tunaongelea kilichopo, kwani kuja kuteuliwa hizo nyadhifa huko mbeleni ni lazima kwamba awe kwenye pay roll ya police au awe police?

Sisi tunakuambieni Madeleka alishaacha upolisi kitambo, hayupo police, hata mkewe sio mtumishi wa uhamiaji tena!
 
Kama unaona tatizo kwenye mfumo wa kurekebisha tabia wahalifu, au mfumo wa mahakama, jikite huko kutatua matatizo hayo.

Ukisisitiza na kuhalalisha Panya Road wauawe na polisi bila kufuata process, hapo bila kujua umefungua mlango wa kumfanya polisi ambaye umegombana naye kwa sababu yoyote kukuwinda hata wewe usiku na kukuua kwa kisingizio cha kwamba wewe ni Panya Road.

Si ushakubali polisi waue watu kiholela kwa kisingizio cha Panya Road?
Naona tunashindwa kuelewana. Kama mtoto wa mtu anakamatwa na polisi, mzazi anakuja anamfhamini mwanae kwa maana ya kuenda kumkanya na anasisitiza ataacha. Polisi wanampa nafasi mzazi ya kufanya hizo. Miezi mitatu mingi anafanya tukio lingine na lingine. Anakamatwa akapelekwa jela kifungo kinaisha anatoka anakuja kulianzisha upya, unataka polisi wanafanye tena labda.
 
Kwa nini unataka kufanya kama vile polisi hawawezi kufanya makosa, au hawawezi kubambikia watu u panya road ambao haupo?

Siku polisi uliyegombana naye mtaani akikubambikia u panya road feki na kukuua bila simile hutapata hata nafasi ya kujitetea kwamba wewe si panya road.

Ndicho unachotaka hicho?
Kiranga
-Una kubali hao panya road wapo?
-Pasipo kujali unajua furani na furani wanafanya, kama jibu lako ni hapana, naishia hapa. Ila,kama jibu lako ni ndio,
-umewahi shuhudia athari za matokeo yao?
-kama imetokea wakamshambulia mtu na kumuumiza, nani anaechangia matibabu na maisha yake na ya familia yake kwa ujumla?
-kwa hiyo unamaanisha una akili sana kuliko vyombo vya usalama?
-wanaokamatwa na kupelekwa mahakamani,umewahi kufatilia wakitoka wanafanya kazi gani?
-Haya,polisi wamekosea kushambulia na kuua. Je,unafikilia bila kufyatua lisasi,wao ndo wangekubali kukatwa mapanga?
-kwa kifupi unamaanisha vyombo vya usalama ndo vina makosa, raia hawana hatia?
-usitumie hisia,kubali. Kwani hapa ukikusanya watu mji mzima,nani atakili kuwa ni panya road?
-Kikubwa uelewe kwamba wakikuibukia,si kwamba hawana taarifa za uhakika.
Ni kweli mtu wa mtu anauma,kila mtu ataongea weeee,kama ilivyo hujawahi sikia jambazi anasemwa kwenye mazishi kwamba alikuwa kauzu, na ujambazi wake hauzuii familia yake kumlilia, hivyo acha wafanye kazi yao.
Mbona hawakukupiga lisasi wewe? Ni kwamba wale ndo walikuwa maarufu jiji zima?
Katibu unayoyisema, inaruhusu watu kuwaumiza wenzao? Anayeilinda ni nani? Mbona hata viongozi hawaishi kulalamikiwa kuwa hawailindi?
Damu zote sawa,usiwaonee huruma waharifu
 
Kwa nini unataka kufanya kama vile polisi hawawezi kufanya makosa, au hawawezi kubambikia watu u panya road ambao haupo?

Siku polisi uliyegombana naye mtaani akikubambikia u panya road feki na kukuua bila simile hutapata hata nafasi ya kujitetea kwamba wewe si panya road.

Ndicho unachotaka hicho?
Wale vijana wa vingunguti mimi nilikuwa mzito sana kuwalaumu au kuwaunga mkono polisi.
Sababu jeshi la polisi lina historia mbaya rejea kesi ya kijana wa madini aliyeuwawa Mtwara mikononi mwa polisi, pia rejea wafanya biashara wa madini wa Mahenge kesi ya akina Zombe.

Ilibidi nifuatilie ukweli juu ya hao vijana wa Vingunguti. Kila kitu kipo wazi na Madeleka angeweza kupata taarifa.
Sidhani kama jeshi la polisi limekodi waandishi wa habari walio hoji wahanga wa hao vijana. Video za maoni yao zimejaa mitandaoni.

Yupo kijana mmoja mkoa wa Pwani alikuwa kibaka muuwaji akafikishwa polisi anaachiwa mara kadhaa sababu za ushahidi au anatoroka, na mara ya mwisho alipelekwa na mama yake polisi wakamuachia.
Kijana akauwa watu wengi zaidi aliporudi mtaani mpaka mara ya mwisho mwaka jana nadhani August aliuwa watu wawili girlfriend wake, na rafiki yake huyo kibaka. Polisi na wananchi wakamchoka akaishia kama hao madogo. Wananchi walipolaumiwa wanaficha mhalifu wakajibu huyo mtu amefikishwa kwenu mara kadhaa anatoka.

Mlitakata na hawa madogo wa Vingunguti waachwe uraiani wauwe watu wengi zaidi au wawatie vilema watu? Kuna mama kapiteza mtoto alichomwa kisu, kuna jamaa kapigwa mapanga, Kuna kijana kachomwa visu mgongoni na mbavuni utumbo ulionekana. Matukio yote hapo mtaani kwa hao vijana.
Watu wanawaona wanawajua kwa sura na wanasikia wanaitana kwa majina wakati wa matukio.

Watu kama hao wanastahili kuondoshwa mapema, wanao uwawa kimakosa na polisi haipiti siku 5 ungesikia polisi nao wako matatani kama kesi ya Mtwara au ya akina Zombe.
 
Madeleka ni Polisi na yuko kwenye Payroll ya mishahara, kama ikitokea kesi ambayo Jamhuri ina maslahi, huwa anatumika kuivuruga, na kuwatoa kwenye mstari wahusika.

Ni mtu wa kazi maalum, ila anatakiwa ajifanye kama raia
Hii nailewa sana na ndo maana kaivuruga ile kesi ya gekul kwaa makusudi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom