A
Anonymous
Guest
Sisi Watarajali (Interns) wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Hospitali ya Mawenzi) tunapitia katika changamoto zenye kuleta ugumu mkubwa katika maisha yetu ya kulitumikia Taifa katika kutoa Huduma za Afya.
Tunapambana kwa juhudi kubwa katika kutoa Huduma za Afya hapa hospitalini licha ya kuwa na mazingira magumu ya utendaji kazi.
Tumekuwa tukipata shida sana kupatiwa stahiki zetu za Posho ya Interns ya kila mwezi, ambazo zipo kwa mujibu wa Sheria, kumekuwa na desturi ya ucheleweshwaji mkubwa wa malipo ya posho zetu kila mwezi, ambapo huingiziwa posho zetu mwenzi wa mbeleni, tena tarehe zilizopitiliza.
Mfano posho ya mwezi wa Julai 2023, tulikuja tukaingiziwa tarehe 18 Agosti 2023 tena baada ya sisi wenyewe interns kuamua kukutana kujadiliana juu ya stahiki zetu, ndipo uongozi ulipata taarifa kuwa tunafanya kikao, wakaingiwa na hofu kwamba tunaweza kugoma, ndio wakaamua kulishughulikia na pesa tukaingiziwa jioni yake.
Hadi tarehe 17 Septemba 2023 posho yetu ya Agosti hatujapatiwa, tumefatilia kwa wahusika hakuna mwenye majibu yenye kueleweka kila mhusika anajibu “Mimi part yangu nimeshafanya”, hayo ni majibu tuliyoyazoea kila mwezi tukifatilia na huu ndio umekuwa utamaduni Hospitalini hapa kuchelewesha malipo ya Posho za Interns.
Hali hii imekuwa ikiiathiri sana maisha yetu kiasi ya kwamba hufikia miezi mingine watu hutolewa ndani ya vyumba vya watu kutokana na kushindwa kulipa kodi kwa wakati.
Kwa kweli tumekuwa wanyonge sana kwani wengi wetu, tumekuwa na hofu ya kufanyiwa figisu ya kuharibiwa Intership zetu endapo tukichukua hatu zitakao waudhi viongozi.
Tunadhalilika kwa kweli huku mtaani.
Tunapambana kwa juhudi kubwa katika kutoa Huduma za Afya hapa hospitalini licha ya kuwa na mazingira magumu ya utendaji kazi.
Tumekuwa tukipata shida sana kupatiwa stahiki zetu za Posho ya Interns ya kila mwezi, ambazo zipo kwa mujibu wa Sheria, kumekuwa na desturi ya ucheleweshwaji mkubwa wa malipo ya posho zetu kila mwezi, ambapo huingiziwa posho zetu mwenzi wa mbeleni, tena tarehe zilizopitiliza.
Mfano posho ya mwezi wa Julai 2023, tulikuja tukaingiziwa tarehe 18 Agosti 2023 tena baada ya sisi wenyewe interns kuamua kukutana kujadiliana juu ya stahiki zetu, ndipo uongozi ulipata taarifa kuwa tunafanya kikao, wakaingiwa na hofu kwamba tunaweza kugoma, ndio wakaamua kulishughulikia na pesa tukaingiziwa jioni yake.
Hadi tarehe 17 Septemba 2023 posho yetu ya Agosti hatujapatiwa, tumefatilia kwa wahusika hakuna mwenye majibu yenye kueleweka kila mhusika anajibu “Mimi part yangu nimeshafanya”, hayo ni majibu tuliyoyazoea kila mwezi tukifatilia na huu ndio umekuwa utamaduni Hospitalini hapa kuchelewesha malipo ya Posho za Interns.
Hali hii imekuwa ikiiathiri sana maisha yetu kiasi ya kwamba hufikia miezi mingine watu hutolewa ndani ya vyumba vya watu kutokana na kushindwa kulipa kodi kwa wakati.
Kwa kweli tumekuwa wanyonge sana kwani wengi wetu, tumekuwa na hofu ya kufanyiwa figisu ya kuharibiwa Intership zetu endapo tukichukua hatu zitakao waudhi viongozi.
Tunadhalilika kwa kweli huku mtaani.