Barua ya wazi ya Madaktari Watarajali kwenda kwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu

KwetuKwanza

Member
Mar 13, 2023
34
82
BARUA KWA WAZIRI WA AFYA

09/10/2023

YAH: - KUOMBA KUJUA UAMUZI WA WIZARA YA AFYA DHIDI YA MALALAMIKO YA MADAKTARI WATARAJALI.

Kwako Ummy A. Mwalimu, Waziri wa Afya.

Tunakusalimu kwa jina la Jamhuri.

Kwanza tuanze kwa kukupongeza kwa juhudi zako mbalimbali za kuliwajibikia Taifa ili lipate kuwa na afya njema itakayowezesha kuijenga Tanzania yetu.

Waziri, tunatambua una majukumu mengi sana kwa ajili ya ujenzi wa Taifa letu, hata hivyo tunaendelea kukupongeza kwa kutambua sehemu muhimu ya jukumu lako hata ukaamua kuunda Kamati ya Uchunguzi kwa ajili ya kufuatilia malalamiko yetu dhidi ya Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) na dosari zilizopo kwenye mtihani wa Pre na Post Internship kupitia barua yako ya tarehe 14/08/2023.

Waziri, tunatambua kuwa zoezi la uchunguzi liliendeshwa na Kamati kama ulivyoagiza na ni matumaini yetu kuwa zoezi hilo lilikamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Waziri, leo tumeamua kukuandika barua ili tupate kusikia neno kutoka kwako kwa kuwa tulihitaji msaada kutoka kwako na kwa Serikali yetu Tukufu ili tupate kuwa na mtihani usiokuwa na dosari nyingi.

Bahati mbaya, sisi Madaktari Watarajali hatukuwa na mwakilishi ndani ya Kamati uliyokuwa umeiunda na hivyo hatujui chochote au hatujui hatua iliyofikia Kamati au Wizara katika kutafuta ufumbuzi wa malalamiko yetu.

Waziri, kwa kutambua umuhimu wako na sisi jitihada zetu kugonga mwamba kutaka kujua hatua iliyopo katika kuyafumbua malalamiko yetu, kwa kuwa kumekuwa na ukimya mkubwa na sasa ni takribani inakaribia miezi miwili hatujui chochote kinachoendelea dhidi ya malalamiko yetu na msaada tunaoutazamia kutoka kwa wizara.

Tumeamua kuchukua hatua hii ili kukuomba utuweke wazi juu ya uamuzi wa Wizara yako kwa namna ya kutusaidia ili tuweze kuondoka na kipindi kigumu cha maisha na kusumbuliwa na msongo mkubwa wa mawazo unatukabili sisi Madaktari Watarajali.

Waziri, hata hivyo hatutakoma kukuomba msaada wako uzingatie pia barua yetu iliyoainisha dosari, maoni na maombi yetu ili walau tusaidike kupitia ‘panel assessment’ kwa kuwa si hospitali zote zilikuwa na ‘logbook’.

Ahsante na tunakutakia majukumu mema.

Madaktari Watarajali
 
Mwandishi hana jina??
Kama barua ya kwanza aliandikiwa Mhe. Rais na Waziri akaunda tume rudini kwa Rais
Ila in the meantime Zamu ya mtihani ikifika mnapaswa kuandika.Mwisho kazeni buti kusoma na Kuzingatia Rotations.Taaluma zote za afya (Wafamasia,Wataalam maabara,Wauguzi nk) wanafanya mitihani na mabaraza yanatoa matokeo ukifeli unarudia.Wanasheria na Wahasibu vivyo hivyo.
Punguzeni siasa
 
BARUA KWA WAZIRI WA AFYA

09/10/2023

YAH: - KUOMBA KUJUA UAMUZI WA WIZARA YA AFYA DHIDI YA MALALAMIKO YA MADAKTARI WATARAJALI.

Kwako Ummy A. Mwalimu, Waziri wa Afya.

Tunakusalimu kwa jina la Jamhuri.

Kwanza tuanze kwa kukupongeza kwa juhudi zako mbalimbali za kuliwajibikia Taifa ili lipate kuwa na afya njema itakayowezesha kuijenga Tanzania yetu.

Waziri, tunatambua una majukumu mengi sana kwa ajili ya ujenzi wa Taifa letu, hata hivyo tunaendelea kukupongeza kwa kutambua sehemu muhimu ya jukumu lako hata ukaamua kuunda Kamati ya Uchunguzi kwa ajili ya kufuatilia malalamiko yetu dhidi ya Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) na dosari zilizopo kwenye mtihani wa Pre na Post Internship kupitia barua yako ya tarehe 14/08/2023.

Waziri, tunatambua kuwa zoezi la uchunguzi liliendeshwa na Kamati kama ulivyoagiza na ni matumaini yetu kuwa zoezi hilo lilikamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Waziri, leo tumeamua kukuandika barua ili tupate kusikia neno kutoka kwako kwa kuwa tulihitaji msaada kutoka kwako na kwa Serikali yetu Tukufu ili tupate kuwa na mtihani usiokuwa na dosari nyingi.

Bahati mbaya, sisi Madaktari Watarajali hatukuwa na mwakilishi ndani ya Kamati uliyokuwa umeiunda na hivyo hatujui chochote au hatujui hatua iliyofikia Kamati au Wizara katika kutafuta ufumbuzi wa malalamiko yetu.

Waziri, kwa kutambua umuhimu wako na sisi jitihada zetu kugonga mwamba kutaka kujua hatua iliyopo katika kuyafumbua malalamiko yetu, kwa kuwa kumekuwa na ukimya mkubwa na sasa ni takribani inakaribia miezi miwili hatujui chochote kinachoendelea dhidi ya malalamiko yetu na msaada tunaoutazamia kutoka kwa wizara.

Tumeamua kuchukua hatua hii ili kukuomba utuweke wazi juu ya uamuzi wa Wizara yako kwa namna ya kutusaidia ili tuweze kuondoka na kipindi kigumu cha maisha na kusumbuliwa na msongo mkubwa wa mawazo unatukabili sisi Madaktari Watarajali.

Waziri, hata hivyo hatutakoma kukuomba msaada wako uzingatie pia barua yetu iliyoainisha dosari, maoni na maombi yetu ili walau tusaidike kupitia ‘panel assessment’ kwa kuwa si hospitali zote zilikuwa na ‘logbook’.

Ahsante na tunakutakia majukumu mema.

Madaktari Watarajali
Malalamiko hayakuwa na Tija
 
Mwandishi hana jina??
Kama barua ya kwanza aliandikiwa Mhe. Rais na Waziri akaunda tume rudini kwa Rais
Ila in the meantime Zamu ya mtihani ikifika mnapaswa kuandika.Mwisho kazeni buti kusoma na Kuzingatia Rotations.Taaluma zote za afya (Wafamasia,Wataalam maabara,Wauguzi nk) wanafanya mitihani na mabaraza yanatoa matokeo ukifeli unarudia.Wanasheria na Wahasibu vivyo hivyo.
Punguzeni siasa
Hakuna aliekataa mtihani bwana kabunguru, rejea barua zote za madaktari hao. Wanachodai ni mitihani hiyo ina mapungufu kwa sababu walizoahinisha, hivyo ufanyiwe marekebisho vinginevyo wengi watakua wakifeli na huku performance yao ya internship ilikua very good. Punguza mihemko unapochangia mada usioijua kiundani.
 
maamuzi ❌️
uamuzi ✅️


MTC ❌️
MCT ✅️

Waheshimiwa Madaktari Watarajali, kwani huko shuleni hamkufundishwa kanuni za uandishi?
Kuna watu huwa mnatazama mabaya tu kwenye kila zuri (Negative minds) ni hatari mno
 
yawekeni sawa Ili kuisave taaluma yenu......

Nje ya mada...
"Duh bongo raia waliotoboa Huwa wanaisumbua sana upcoming generation......hii imezaa chuki, uchawa, fitna, figisu, roho mbaya, vijicho, husda nk......"
Very true!!
 
Hiyo MTC wewe umeiona wapi. Siku wabongo tukiacha kukurupuka tutafanikiwa sana
Wewe fala; jifunze kwanza kutumia JF. Mleta mada ameelewa na amesharekebisha. Acha kukurupuka.

Wewe endelea tu kukurupuka
We bata; una msongo wa mawazo?

Kuna watu huwa mnatazama mabaya tu kwenye kila zuri (Negative minds) ni hatari mno
We kuku; kuwa na mema siyo kichaka cha kuficha ujinga wa Kanuni za Uandishi.

Wamesema wanamsongo wa mawazo,unategemea wataandika vizuri...wanapitia kipindi kigumu hawa vijana,kwa waliopitia medical school, wanaweza fahamu machungu yake.
I have been there. Ninaelewa kila kitu. Depression isiwe kisingizio cha makosa madogomadogo ya Uandishi.

Makosa madogomadogo yanawafanya muonekane unprofessional.
 
BARUA KWA WAZIRI WA AFYA

09/10/2023

YAH: - KUOMBA KUJUA UAMUZI WA WIZARA YA AFYA DHIDI YA MALALAMIKO YA MADAKTARI WATARAJALI.

Kwako Ummy A. Mwalimu, Waziri wa Afya.

Tunakusalimu kwa jina la Jamhuri.

Kwanza tuanze kwa kukupongeza kwa juhudi zako mbalimbali za kuliwajibikia Taifa ili lipate kuwa na afya njema itakayowezesha kuijenga Tanzania yetu.

Waziri, tunatambua una majukumu mengi sana kwa ajili ya ujenzi wa Taifa letu, hata hivyo tunaendelea kukupongeza kwa kutambua sehemu muhimu ya jukumu lako hata ukaamua kuunda Kamati ya Uchunguzi kwa ajili ya kufuatilia malalamiko yetu dhidi ya Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) na dosari zilizopo kwenye mtihani wa Pre na Post Internship kupitia barua yako ya tarehe 14/08/2023.

Waziri, tunatambua kuwa zoezi la uchunguzi liliendeshwa na Kamati kama ulivyoagiza na ni matumaini yetu kuwa zoezi hilo lilikamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Waziri, leo tumeamua kukuandika barua ili tupate kusikia neno kutoka kwako kwa kuwa tulihitaji msaada kutoka kwako na kwa Serikali yetu Tukufu ili tupate kuwa na mtihani usiokuwa na dosari nyingi.

Bahati mbaya, sisi Madaktari Watarajali hatukuwa na mwakilishi ndani ya Kamati uliyokuwa umeiunda na hivyo hatujui chochote au hatujui hatua iliyofikia Kamati au Wizara katika kutafuta ufumbuzi wa malalamiko yetu.

Waziri, kwa kutambua umuhimu wako na sisi jitihada zetu kugonga mwamba kutaka kujua hatua iliyopo katika kuyafumbua malalamiko yetu, kwa kuwa kumekuwa na ukimya mkubwa na sasa ni takribani inakaribia miezi miwili hatujui chochote kinachoendelea dhidi ya malalamiko yetu na msaada tunaoutazamia kutoka kwa wizara.

Tumeamua kuchukua hatua hii ili kukuomba utuweke wazi juu ya uamuzi wa Wizara yako kwa namna ya kutusaidia ili tuweze kuondoka na kipindi kigumu cha maisha na kusumbuliwa na msongo mkubwa wa mawazo unatukabili sisi Madaktari Watarajali.

Waziri, hata hivyo hatutakoma kukuomba msaada wako uzingatie pia barua yetu iliyoainisha dosari, maoni na maombi yetu ili walau tusaidike kupitia ‘panel assessment’ kwa kuwa si hospitali zote zilikuwa na ‘logbook’.

Ahsante na tunakutakia majukumu mema.

Madaktari Watarajali
Poleni sana
 
Hawa vijana wamemaliza masomo na kutunukiwa shahada zao za udaktari, figisu zote hizi za nini? hivi hawa watu wanajua ugumu wa kijana kukaa chuo miaka mitano apate shahada halafu uje kumhangaisha bila sababu za msingi!?​
 
Back
Top Bottom