DOKEZO Hospitali ya Kitete (Tabora) haijatulipa posho zetu za Oktoba Madaktari Wanafunzi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Mimi ni mmoja wa Madaktari Wanafunzi ambao tulikuwa tunajifunza kwa vitendo kwa muda wa mwaka mmoja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa (Kitete) iliyopo Tabora.

Moja ya changamoto ambayo tulikutana nayo kwenye mafunzo yetu ni ucheleweshwaji wa malipo yetu (posho) ya kila mwezi.

Mara kadhaa yalikuwa yakichelewa lakini inadaiwa kuwa wahusika walilazimika kulipa hata kwa kuchelewa wiki moja mbili hadi tatu kwa kuwa walihofia yakichelewa zaidi tunaweza kugoma.

Pamoja na hivyo, mwezi mmoja wa mwisho wa mafunzo yetu Oktoba 2023 hatukulipwa posho zetu, tulilzimika kusubiri kama ilivyo kawaida wiki moja, mbili au tatu lakini bado kukawa na ukimya.

Baada ya kuzungushwa kwa muda mrefu huku tukifuatilia, tukajulishwa kuwa fedha zimeshafika lakini zimepelekwa Hazina Ndogo, na huko ndipo zilipokwama.

Pamoja na hivyo tulipofuatilia hiospitli nyingine wenzetu wote wametuambiwa wao wameshalipwa na hakuna wanachodai, kwa sasa wanaendelea na maisha yao mengine.

Kwa nini Hospitali ya Kitete haijatulipa mpaka sasa na hakuna majibu tunayopewa ya kueleweka?

Kwa kawaida fedha zikitoka Hazina, zinaelekezwa kwenye kituo husika (hospitali) baada ya hapo nipo wahusika wanapewa, na uongozi wa Hospitali unakiri kuwa umepokea fedha lakini zipo Hazina Ndogo, huko zinafanya nini na tayari zimeshapita wiki tano hatujalipwa posho zetu?
 
Sisi Watumishi wa mkataba katika Hospitali ya Rufaa Kitete Mkoani Tabora hatujalipwa mishahara kwa miezi miwili sasa.

Malipo ya posho ambayo ndio kama mshahara kwetu ya Desemba (2023) tumelipwa siku chache zilizopita, lakini ile ya Januari na Februari (2024) hatujalipwa na hatuoni dalili za kulipwa hivi karibuni.

Hali hiyo imekuwa ikitokea kila mara, kukaa miezi miwili hadi mitatu au zaidi bila kulipwa ni jambo la kawaida.

Tunaomba Serikali ifuatilie hili kwa mamlaka husika maana limekuwa jambo sugu, kila mara linajirudia.

Hali hii inapunguza morali yetu ya kazi, unapambana lakini malipo yanakuwa shida, kama ni watu au mtu ndio wanahusika kukwamisha, hatua zichukuliwe mapema kwani pia tunaathirika kisaikolojia.
 
Not only contract employees who have been experiencing this, permanent employees have not received their extra and on-call allowances since November last year, the hospital management has lacked the #accountability to timely motivating their staff.
 
Back
Top Bottom