Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Kwa mtu asiyekusikiliza vizuri anaweza kuona vitu unavyoongea vinamashiko lakini nakuhakikishia unajichanganya sana ndugu yangu.

Wewe sio mchambuzi mzuri wa siasa ila ni msemaji wa chama cha mapinduzi. Jifunze kwa wachambuzi wa siasa kama Prof Kitila na Dr Bana. Wenzako wako dyanamics licha ya kuwa na vyama vyao saa nyingine kwenye ukweli wanasema ukweli hata kama ni ukweli mchungu kwa vyama vyao.

Sasa wewe umekazania Magufuli yuko sawa ata nyumba zilivyouzwa haikua kosa lake si asingeshiriki basi angejiuzuru.

Polepole punguza mahaba unakua unaboa

Awali ya yote Polepole anatakiwa kuwaeleza vijana wa Tanzania alitumiaje fedha kutoka kwa wafadhili mbali mbali alizopatiwa kupitia NGOs zake za kuendeleza vijana wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi na Mkapa chini ya mpango wa kuomdoa Umaskini MKUKUTA, moja ya taasisi hizo TANZANIA YOUTH COALITION (TYC).

NGOs hizi zilikuwa na ofisi zake Kijitonyama. Kabla ya kuwarukia wengine awaeleze vijana wenzake mabilioni ya fedha alizopatiwa na wafadhili mbali mbali ameweza kuwatoa vijana wangapi ktk lindi la umaskini? Pia awaeleze nini kilitokea hadi wafadhili wengi ikiwemo DANIDA kusitisha kutoa fedha za kuendeleza vijana. Akishaelza hayo ndipo Polepole atakuwa na Legitimacy ya kuwasema wengine
 
Kabla ya kuteuliwa kuwa mmoja wa makamishna wa Tume ya mabadiliko ya Katiba kuwakilisha vijana, Polepole kwa muda mrefu amekuwa akiongoza NGOs zinazolenga kusaidia vijana ikiwemo TANZANIA YOUTH COALITION (TYC) yenye ofisi zilizochoka pale Kijitonyama.

Katika kipindi cha utawala wa Mzee Mwinyi na Mkapa NGOs zake zilipatiwa fedha nyingi sana kuendeleza vijana. Baada ya impact ya fedha zao kutooneka donors wengi wakakata misaada ndipo akaubikia ktk Tume.

Hivyo vijana wa Tanzania wanalalamika kuwa hawana fursa,ajira n.k mmoja wa watu wanaotakiwa kutoa majibu ni Pole pole kwa sababu kwa miaka 20 amekuwa akipatiwa misaada na wafadhili ya kuendeleza vijana chini ya MKUKUTA. Hivyo hivi sasa anajaribu kujijengea kukubalika upya kupitia Katiba na Ukawa.

Wasiomjua huyu HP huwa wanafikiri ni mtu genius saaana na muadilifu saaaana lakini wanaomjua wanasema ana makashfa ya kula pesa na infact ashawahi pata hata grant ya kujiongezea elimu na still aliitafuna na shule hakwenda! Halafu form 6 si alipataga 0 huyu!

Tatizo la jamaa ni opportunist sana otherwise angeweza kuwa mweledi sana kwenye mambo ya social development, social change.Huyu ni watu wa calibre ya akina Nape, Makonda yuko tayari kujitoa ufahamu as long as pesa inaingia kwake!
 
Nimemsikiliza polepoole, anahangaikia tuzo kama za viti maalumu hivyo Kazi aifanyayo anafanya kwa bidii ila jamii ya Tanzania sasa ni tofauti sana na ile ya miaka iliyopita hatima yake Aibu kubwa Kwa polepole

There your are! jamaa anachokifanya ni kukikampenia CCM kwa gharama yoyote ile ili ikishika dola apate malipo ya kazi yake, watu wakumbuke ya Makonda! kamtukana EL, kampiga Warioba then nini kimefuata si ukuu wa wilaya tena Kinondoni! Kwa maana nyingine HP kila akichekiiiii na yeye anaona akikomaa kuichafua UKAWA na EL mbona cheo kinakujaa.Vilevile NGO hazimlipi tena maana donors now wamekuwa wakali ka nini wanataka wapate thamani ya pesa yao kwa kila senti wanayotoa, so HP hana mahali pa kula ka zamani kilichobaki lazima afanye siasa maana anajua itamlipa tena fasta!
 
Nimekuwa nikimsikiliza ndugu Humphrey kwa muda mwingi tangu aanze kuchambua siasa.lakini cha ajabu zaidi anamwingelea mhe.lowassa kuwa si mwadilifu je.chama anachotoka yeye polepole tangu lini kikawa kisafi mbona hasemi haya?

1.Mwenyekiti wa chama chake aliongoza bunge la katiba kuikanyaga katiba ya warioba kwa kutoa maelekezo kwa BMK je nani msafi CCM?
2.Magufuli alipiga kura ya NDIO kama lowassa kwenye katiba pendekezwa je.lini magufuli kawa msafi? mwadilifu? shem on u.
3.Uko CCM chama ambacho kinamsema lowassa ni kapi huku kikimpitisha Endrew chenge kutetea jimbo la bariadi magharibi na prof.Tibaijuka kule mureba!!! shem on u polepole.
4.Unajipa madaraka ya kuchambua nani msafi na mchafu huku unalelewa na chama kichafu nani akuelewe?
5.Unatoa povu kupinga katiba pendekezwa huku waliojitoa kuwaunga mkono na lowassa akiwemo leo hawafai unataka mabadiliko gani wewe dogo janja?

Lowassa kakili na kujitoa wewe umeufyata kila siku unalialia kwenye media katiba! katiba! lini magufuli alimtetea warioba? chama chako kimemvua nguo jaji warioba tukiwa tunaona leo hii nani tutamsikiliza kutoka ccm? wote wasaka tonge HATUKUTAKI.....SHAME ON U!
Pole pole ana MORAL AUTHORITY ya kuzungumzia tuhima zozote wala watuhumiwa wowote kwa sababu yeye pia ni mtuhumiwa wa ufisadi wa mabilioni yaliyotolewa na wafadhili mbali mbali kwa NGOs alizoanzisha na kuziongoza wakati wa utawala ws Mzee Mwinyi na Mkapa chini ya mpango wa MKUKUTA. Badala yake kwanza anatakiwa kuueleza umma kiasi cha fedha alizopewa na idadi ya vijana aliowaendeleza na kuwatoa katika umasikini. Aeleze pia ni kwanini wafadhili ikiwemo DANIDA walizisitishia misasda NGOs zake?
 
"Kama ccm wasingekuwa makini nchi ingenunuliwa mapema tu"Humphrey Polepili..
Cham Bee nchi inunuliwe mara ngapi?? wasio wananchi ndiyo walioshikilia njia kuu za uchumi wakifaidi rasilimali za nchi na wananchi hawanufaiki na chochote bali wanaonufaika ni wachache wakizidi kuwazuga walio wengi. Wananchi ni raia daraja la tatu japo nchi ni yao. Nchi kila kitu mpaka vijiti vya kuchokorea meno baada ya kula vinaagizwa kutoka nje bado haijanunuliwa tu?!!. Tuache masihara tunahitaji kuundoa mfumo kwa kwenda kupiga kura bila kuacha siku ya 25 Oktoba 2015.
 
Polepole anachanganya sana watu.

Kwanza aelewe ametambulika kuwa ni moja wa maadui.

Pili yeye ni mwanaharakati za kuwandeleza vijana iweje leo awe mchamabuzi wa mambo ya kisiasa?

Channel 10 watafute watu wengine wafanye majadiliano ambayo hayatamshirikisha Polepole kwababu haelewi anachokiongea isipokuwa kuendeleza chuki binafsi.

Kwa mfano kwenye moja ya ingizo zake katika mtandao wa Twitter anasema yeye angeeleza dhana ya mabadiliko na dhana ya mageuzi na kwamba he(Lowasa) can't bring transformation.

Sijawahi kuona mtu anaetumiwa kiasi hiki.
 
Kweli mtangazaji

alikuwa anambeba mtatiro
Polepole yuko vizuri
Polepe hana MORAL AUTHORITY ya kuzungumzia tuhuma zozote wala watuhumiwa wowote kwa sababu yeye pia ni mtuhumiwa wa utafunaji fedha zilizotolewa na wafadhili chini ya mpango wa MKUKUTA kuendeleza na kuwaondolea umaskini vijana kupitia NGOs zake mbali mbali ikiwemo TANZANIA YOUTH COALITION ( TYC).

Tatizo wanaoitaa ktk vipindi wanaanzia toka HP alipokuwa ktk Tume ya Warioba, hawafanyi homework kujua background yake kabla ya kuteuliwa kuwa kamishna wa tune hiyo. Kutokana na ufisadi sa fedha za wafadhili walizotoa kuendeleza vijana ndio maana baada ya tune kuvunjwa akawa jobless na sasa anatafuta pa kujipatia ajira.

Vijana waliopigika kwa umaskini wanatakiwa kumhoji HP namna alivyotumia mabilioni yaliyotolewa na wafadhili chini ya MKUKUTA kuendeleza na kuwaondolea umaskini vijana kabla hajakuwa na ujasiri wa kuwsema wengine
 
Ndugu Polepole kwa nini hujibu maswali unayoulizwa kuhusiana na tuhuma za mgombea wa CCM? Kama mgombea wa UKAWA aliyakataa maoni ya wananchi kupitia ile tume ya Mh.Warioba, je huyo wa CCM unayemkumbatia pamoja na mgombea mwenza wake waliyakubali maoni ya wananchi? Polepole nilikuheshimu sana wakati ukitetea maoni ya wanachi kutupwa na CCM lakini kwa sasa umepoteza mwelekeo. Nitakubaliana na wewe ukinijuza kama mgombea wa CCM na mgombea mwenza wake walikubaliana na maoni yetu sisi wananchi kupitia iliyokuwa tume ya mhe. Jaji Warioba.
 
Uchaguzi mwaka huu umekuwa wa moto sana ukikolezwa zaidi na wale tuliozoea kuona wakitetea wananchi ila kwa sasa wamekuwa wa tofauti, mawazo yao yamegeuka kwa miezi michache tu.

Ni vyema tukawajua kiundani zaidi hawa public figures wetu, mtu kama Dr. Slaa au Prof. Lipumba, wamekuwa kwenye siasa muda mrefu, tunawajua vizuri.

Huyu Polepole ni mgeni kwa wengi, ameibukia tume ya katiba, akionekana kama ni mtetea wanyonge, kwa sasa hali ni tofauti. Tukimjua vizuri itasaidia kuelewa mitazamo yake ya sasa imeshawishiwa na nini.

Binafsi nimemjua toka 2009 akiwa mwenyekiti/mwanzilishi Tanzania Youth Coalition (TYC) iliyopo Kijitonyama.

Wewe unamjua vipi huyu mtu?
TYC inategemea wafadhili pia ela toka serikalini kujiendesha, je huwa zinatumika vipi? Zinawafikia walengwa?

Kuna uwezekano wowote mitazamo yake imebadilika akiogopa kukosa misaada toka serikalini kama akitoa support kwa wapinzani?
Mahusiano yake na wafanyakazi wake yapo vipi?

Ameoa? Anawatoto? Michepuko je?
Tukimjua vizuri, itasaidia kuelewa mabadiliko yakifikra yaliyomkumba.
 
Mkuu WATANABE,you nailed it. Watu wengi humu JF hawajui background ya HP, hata hivyo credibility aliyojijengea akiwa mjumbe wa tume ya Warioba nayo inashuka muda sio Mrefu.
 
nyie mtu akiwaambia ukweli ndio mnaona anashusha credibility. baada ya mtatiro naye kupewa za uso leteni mbowe sasa
 
polepole leo alipwaya sana kwenye kipindi hasa kwa kumsafisha magufuli kwa tuhuma zake za kuuza nyumba na ufisadi kwenye tanroads..

Nyumba za serikali waliuziwa wafanyakazi wa serikali pamoja na Lowassa mtutajie waliouziwa nje ya mtumishi wa serikali kama sio unafiki ni nini
 
Nahisi kanunuliwa tayari huyu mtu, naomba mzee Warioba aingilie kati amkemee, anatuyumbisha.
 
Mwaka huu kila mtu anajenga hoja kwa kubalance mzani upande wa bwana wake yaani '' ALIYEMUAJIRI'' kufanya kazi hiyo ili kutimiza MATAKWA ya ajira yake na bwana wake! Pia HP ni nani hata Mungu huwa anaweza kubatilisha maamuzi ya kwanza dhidi ya mwanadamu sembuse yeye! Infact always TRUE IS RELATIVE BUT REALITY IS ABSOLUTE!!!
 
Jamaa toka yupo shule alikuwa bize kwenye makongamano mbalimbali ya maendeleo ya vijana 2001-2003 , kwa hiyo hakuweza kubalance kati ya shule na majukumu ya nje, kwa masomo ya science A level si rahisi kupita kama hautakuwa nayo makini. Angesoma HGL jamaa angepasua vizur tu.
 
Back
Top Bottom