Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,278
- 8,868
Leo channel 10 Ni zamu ya Mtatiro na Polepole. Don't miss saa 4 kamili usiku.
Polepole anasema kuwa wananchi wanataka mageuzi 'transformation' na sio mabadiliko kwa maana ya change.Akasema ukawa wanahubiri kuhusu mabadiliko wakati wananchi wanataka mageuzi.
Mifano aliyoitoa huyu polepole kuelezea hayo mageuzi amejikuta akijichanganya na kwakweli sasa naweza kusema kwa uhakika kabisa huyu jamaa ana agenga yake ya kukipigania chama cha mapinduzi hata kwa kujifanya haelewi ili tu malengo yake yatimie.
Ametaja Muungano.Kwamba watanzania wanataka mageuzi ya muungano.Huu uliopo haufai na umeshindwa.Hili lipo kwenye rasimu ya mzee Warioba ambayo ni moja ya misingi mikubwa ya muungano wa UKAWA.
Ametaja watanzania wanataka raisi ambaye madarajka yake yanadhibitiea na katiba.Yani hana mamlaka ya kupindukia kama ilivyo kwa katiba ya sasa hivi.Hili lipo kwenye rasimu ya katiba ya Warioba ambayo inasimamiwa na UKAWA na kubezwa na CCM na Polepole analijua hilo sana kuliko mimi..
Ametaja kitu kingine cha mageuzi ambacho wananchi wanataka ni kuwa na uwezo wakuwawajibisha wabunge easiowajibika kwenye majimbo yao.Hili pia ni moja ya msingi uliopo kwenye katiba ya mzee Warioba ambayo ni mwimbo ulioifanya UKAWA ukawepo......
.
Sasa najiuliza haya makusudi ya kutoa hoja za kijinga kabisa huku akijicontradict mwenyewe huyu Polepole ni kwa manufaa ya nani?Mifano yake ya hiyo anayoita transfomation yote ni mihimili ya katiba ya wananchi na haikubaliki kabisa CCM.Sasa bado anataka watu wachague CCM kupata transformation zipi wakati zote zipo kwenye agenda ya UKAWA?Na yeye ni shahidi kuwa ccm hawataki hayo mambo na ndo moja ya kitu kilichompa yeye umaarufu kwa kuwasema sana ccm kuwa wanapuuza maoni ya wananchi
Leo hii sarakasi anayopiga huyu polepole ni kwa manufaa ya nani?Polepole atueleze sasa kuwa hata kwenye mchakato wa katiba yeye alikuwa anaigiza tu kuwa anaiunga mkono katiba ya wananchi huku akijua chama chake hakiwezi kuipitisha ili tu kutafuta wafuasi ambao watamwamini ili aje kuwadrive upandevwa ccm kwenye uchaguzimkuu.Hapo nitamuelewa sana lakini kinyume na hapi anajichanganya sana huyu jamaa