Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Hata sisi tuliangalia kwanini unataka sema umedanganywa wapi?wewe ndie polepole hutaki kukubali kuwa ulipoteza fahamu hadi ukashindwa mpa mkono washiriki ukiwa unajifiria?Karibu ktk siasa..maji waliyoyashindwa makatibu kibao na viongozi wengine wa CCM...polisi na wakuu wa mikoa,wilaya wote wamechemsha.

Mimi huwa nawashangaa sana hawa ccm kwa nini hawataki kusikia yanayosemwa na wengi??au ndio ulevi wa madaraka?
 
leo walivaa utaifa maana hakuna sehemu mtatiro kakataa lowasa sio fisadi safi sana pole pole safi mtatiro nilijua utakua kama mchungaji wewe ni mwanasiasa ulie simamia itikad ya cuf kweli na usomi wako umeonekanaa leo
 
Mtatiro Kajitahd Kumatch Na Polepole Lakin Stl Bado Sana Kumzidi Huyu Kijana Wa Ccm...Tuache Unafiki Na Uvyama Pembeni Ukwel Tumeuona Mtatiro Kazidiwa Lakin Si Kama Msigwa....!!!

hajazidiwa mtu mnajipa moyo mtatiro alikuwa anaongea point polepole alikuwa shabiki wa ccm wapi na wapi tumefuatilia usitudanganye hapa, Mtatiro hajaongelea chama chochote.
 
Leo polepole amejidhihirisha kua na chuki binafsi na Lowasa ameshindwa hata kujua mahitaji ya watanzania. NA leo amekutana na kisiki cha mpingo

Yaani jamaa kila maelezo anayatafutia njia hadi yakutane na lowasa kwake magufuli ni msafi saaana na lowasa ni mchafu saaana
 
Magufuri katika utumishi wake wote, amehudumu wizara zisizo za muungano ambazo msimamizi wake ni Waziri mkuu. Maana yake majukumu yake ni ya utekelezaji wa maagizo ya Bosi wake, Waziri mkuu. Mfano uuzwaji wa nyumba za serikali.



Kwa nini Prof. Muhongo aliwekwa pembeni baada ya sakata la Escrow na si waziri mkuu?

Kwa nini Balozi Kagasheki aliwekwa pembeni kufuatia operesheni tokomeza na sio w/mkuu?
 
Pole pole anashida kubwa sana...aliniudhi sana. Alikuwa anjifanya anajua sana maana ya mfumo.. ila hajui alikuwa anaongea nini kati ya hivi: SUB SYSTEM, SYSTEM, SUPER SYSTEM ETC. Alianza ongea upofu wa ccm km ktk katiba hadi JK akawafafanulia kwa jinsi ya huyu poleopole.
 
nimemtazama ni mtu wa kulazimisha na mwenye njaa kali na chuki iliyo kuu anachanganya mambo na kudhani anajua leo kakamatwa vizuri
 
Polepole na ujuaji wake anashindwa kuelewa kuwa system inakuwa created na waendesha serikali na waendesha serikali ni chama sasa tukitaka kuchange system ni lazima sasa uchange chama yamemshinda kuyaelewa

ANAJUA isipokuwa anatimiza majukumu yake ya kueneza propaganda ikiwa ni maagizo rasmi toka LUMUMBA bila ya aibu eti aligombea ubunge kwa tiketi ya CDM.
Angeimaliza chama huyu,bora kalikatwa mapemaaaa.
Eboo!.
VIVA UKAWA.
 
Kifaurongo

Alikwa hajui anaongela sub -system, system,supersystem, multi systems etc. ... kwani mkuu wa waziri mkuu, ni nani? mwenyewe kasema urais TZ ni km uaskofu mkuu..halafu anataka mtoa huyo askofu mkuu ktk mamlaka ya mwisho na inayotakiwa wajibika.JK amebadili waziri mkuu ,baraza la mawaziri, wakuu wa wilaya, polisi, makatibu wa ccm ,wakuu wa miko etc bado mambo mabaya hayaishi.
 
Last edited by a moderator:
Polepole ni mpuuzi sana sio analytical yeye anadhani kuongea issues katika muda huu ni sawa na kuchambua vifungu vya katiba pendekezwa nimesikiliza kwa mara ya kwanza leo ni kamuona ni mjinga sana kiasi cha kwamba hana maono anataka kutuaminisha anachokiamini yeye ndio cha wananchi hopeless younf politician hafai na ameshadharaurika sana imeingia kwenye angle za Benson Bana na Kitila Mkumbo
 
Mengi yamezungumzwa na nimefatilia kwa umakini sana

Polepole
Daaah amejitahidi kichimba mambo nakueleza vitu vingi sana na vingine ni vizuri tuu kwa kukuza uelewa wa watu.ila
*Amechemka kujibu maswali kiufasha
* amechemka kuoanisha mambo

Hasa kwenye nini wanachotaka watanzani.yeye anatuambia watanzania wanataka mageuzi na wala sio mabadiliko

Mtatiro
Anajua vizuri na anajua kuelezea mambo ambayo watanzania wote kwa hali ya kawaida wanaweza kumuelewa.
*amejibu kwa ufasaha maswali yote
Hasa lile la watanzania wanataka mabadiliko ya mfumo mzima.

Kwa nini nasema hvyo.Polepole anatuambia kubadili mfumo ni sehemu ndogo iliyondani ya kufanya mageuzi.wakati huo huo anasema ili ufanye mageuzi lazima ubadili Sera,sheria na kanuni za idara mbali mbali ndani ya nchi.

Anasahau kuwa huwezi kubadili Sera,sheria na kanuni bila kubadili katiba iliyopo ili ziendane saw a.

Watanzania wanataka mabadiliko ya mfumo ili wapate katiba mpya ambayo itawasaidia kupata katiba iloyotakiwa na watanzania waliowengi ambayo iwaletea mageuzi yanayotakiwa.

Hicho ndicho tunachohitaji
 
Mtatiro kabebwa sana na Albert...Polepole kanyimwa muda wa hata kumalizia hoja zake..
 
Kwa nini Prof. Muhongo aliwekwa pembeni baada ya sakata la Escrow na si waziri mkuu?

Kwa nini Balozi Kagasheki aliwekwa pembeni kufuatia operesheni tokomeza na sio w/mkuu?

Kumuokoa Waziri mkuu, na serikali isidondoshwe, na wabunge wakaridhika.
 
Back
Top Bottom