Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Wananchi wataelewa tu anachosema Polepole. Ukawa wanasema wanataka kubadili mfuno lakibi wanachomaanisha ni kubadili chama kinachotawala tu kwa uchu wa madaraka. Cha kijiuliza ni kwamba kama ukawa inataka kubadili mfumo, nani wa kubadili huo mfumo? Rais wa jamhuri ana role kubwa sana ya kubadili mfumo mbovu uliopo.

Cha kujiuliza ni mgombea wa ukawa anadhamira ya kupambana na ufisadi? Anao uwezo wa kuwabana wafanyabiashara rafiki zake walipe kodi. Kumbuka ni michango ya hao wafanyabiashara ndiyo inayonunua vijana wa kumuandika vizuri mitandaoni. Inasafirisha kwa mabasi vikundi vya vijana wa kumshangilia nk. Kwa mtizamo wangu hawezi. Tumchague mtu asie na excess luggage. Ambae atafanya maamuzi bila kuwafikiria rafiki zake bali watz wote.
 
Pole pole ana MORAL AUTHORITY ya kuzungumzia tuhima zozote wala watuhumiwa wowote kwa sababu yeye pia ni mtuhumiwa wa ufisadi wa mabilioni yaliyotolewa na wafadhili mbali mbali kwa NGOs alizoanzisha na kuziongoza wakati wa utawala ws Mzee Mwinyi na Mkapa chini ya mpango wa MKUKUTA. Badala yake kwanza anatakiwa kuueleza umma kiasi cha fedha alizopewa na idadi ya vijana aliowaendeleza na kuwatoa katika umasikini. Aeleze pia ni kwanini wafadhili ikiwemo DANIDA walizisitishia misasda NGOs zake?
Mzee unafahamu historia ya mpango huu wa mkukuta japo kidogo???
 
haka ka bwana sijui kakoje kalikuwa kanaongea vzr sana (H.Polepole) sasa kamepotea kabisa
 
Alisema ukweli gani,
Mbona mtatiro alisema Wagombea wote ni watuhumiwa lakn hakuna aliembeza?

Kiufupi Polepole yuko so biased,subjective and so individualised one..tulimpa umaarufu na sasa tutauchukuwa

Umesema kweli. Polepole alinishangaza aliposema makosa ya Magufuli anayetakiwa kuwajibika ni waziri mkuu kwa sababu Magufuli anatumwa tu. Lakini hakusema kwa Lowassa nani alipaswa kuwajibika, hilo alikaa kimya! The guy was biased!
 
Tuliona chanell 10 Msigwa alipigwa vibaya mno na polepole siku ile mpaka akapoteza mwelekeo na kuanza kuongea kama muhuni wa mtaani,
Polepole ni kichwa anajitambua

kwa mara nyingine polepole baada ya kumpiga tatu bila Msigwa sasa atakuwa uwanjani na mtatiro, duh ila game la leo ni noma sijui km mtatiro atapona kweli, lkn nimegunduwa watu wa jf wengi wanashabikia kwa hisia mkumbuke game lililopita msigwa aligaragazwa vibaya sana mpaka akaanza kumsema polepole mambo yake ya personal,badala ya kusimamia mada iliyokuwa wanaijadili, kiukweli game la leo tamuuu,
jamaaa wote nawakubali Mtatiro pamoja na Polepole,
jambo la msingi tupime hoja tuache ushabiki wa vyama.:mod:
 
Ifike wakati pale tunapotaka kumpa uongozi mwanachama yeyote wa CCM tumpukutishe kwanza meno yote mdomoni maana tumechoka na kutafunwa kwa fedha zetu.
 
Now wait a minute! Kama anaiogopa serikali, ilikuwaje akaikomalia rasimu ambayo watu wa serikali ya sisiemu hawakuitaka? It seems to me anaonekana msaliti sasa kwa sababu tu haendi na upepo. What if you are wrong and he is right? Btw, ad hominem arguments hazosaidii sana.
 
jana ndio nimejua unafiki wa bwana pole pole,

hapo mwanzo wakati akijipambanua mpigania rasimu ya warioba,watu walimwelewa kama mpambanaji wa ukweli, kumbe alikua mnafiki mkubwa!

Jana katika kipindi cha mada moto pale chanel ten ndio nikamgundua huyu bwana ni wakuogopa kama ukoma,

anataka kutuaminisha kwamba kwa sasa chama cha mapinduzi ni kizuri sana tena hakuna mfano wake na magufuli na samia suluhu ni watu wakuchaguliwa?

Maali nilipo mdharau ni pale aliposema mgombea wa ukawa asichaguliwe kwa sababu alikataa katiba ya warioba.

Huku hakisahau magufuli tena alichangia kuisigina rasimu ya warioba?

Mbaya zaidi mgombea mwenza samia suluhu hasani, ndiye alikua makamu mwenyekiti wa bunge la katiba na kwa kiasi kikubwa yeye kwa maelekezo ya chama alitumika kuminya na kuchana chana maoni ya wananchi!

Sasa pole pole anakuja kutuaminisha nini? Ndani yake amekua na chuki ya wazi wazi kwa lowassa!

Nampongeza sana ndugu julius mtatiro uameongea vitu vya msingi sana,

ushauri wangu kwa pole pole, unajidhalilisha sana mgodo wangu wacha kutumika simamia ukweli hakuna msafi ndani ya ccm kama unavyotaka kuwa aminisha watanzania, wewe siyo MUNGU hata ugeuke kumwukumu lowassa, bila ushahidi wowote,

kama unao ushahidi wa tuhuma unazo zisema peleka mahakamani ili mahakama iamue lowassa ni mkosaji hau la. Tusilete vituhuma vya kisiasa kuchafuana kisiasa,

wadau naomba kuwasilisha:
 
bravo, well said, yaani ww una akili kama dunia nzima vile


Wananchi wataelewa tu anachosema Polepole. Ukawa wanasema wanataka kubadili mfuno lakibi wanachomaanisha ni kubadili chama kinachotawala tu kwa uchu wa madaraka. Cha kijiuliza ni kwamba kama ukawa inataka kubadili mfumo, nani wa kubadili huo mfumo? Rais wa jamhuri ana role kubwa sana ya kubadili mfumo mbovu uliopo. Cha kujiuliza ni mgombea wa ukawa anadhamira ya kupambana na ufisadi? Anao uwezo wa kuwabana wafanyabiashara rafiki zake walipe kodi. Kumbuka ni michango ya hao wafanyabiashara ndiyo inayonunua vijana wa kumuandika vizuri mitandaoni. Inasafirisha kwa mabasi vikundi vya vijana wa kumshangilia nk. Kwa mtizamo wangu hawezi. Tumchague mtu asie na excess luggage. Ambae atafanya maamuzi bila kuwafikiria rafiki zake bali watz wote.
 
Cham Bee nchi inunuliwe mara ngapi?? wasio wananchi ndiyo walioshikilia njia kuu za uchumi wakifaidi rasilimali za nchi na wananchi hawanufaiki na chochote bali wanaonufaika ni wachache wakizidi kuwazuga walio wengi. Wananchi ni raia daraja la tatu japo nchi ni yao. Nchi kila kitu mpaka vijiti vya kuchokorea meno baada ya kula vinaagizwa kutoka nje bado haijanunuliwa tu?!!. Tuache masihara tunahitaji kuundoa mfumo na sio kwa kuandika humu JF bali kwenda kupiga kura bila kuacha siku ya 25 Oktoba 2015.

UMEONGEA yaliyo ya kweli MTANZANIA mwenzangu!.
Hakikisha kikatio chako kiko ACTIVE hadi trh jumapili 25.10.2015 saa 1 asubuhi.
 
Last edited by a moderator:
Niongezee yafuatayo kwa ushauri mzuri wa Msonge.

Watanzania lazima tuwe waangalifu/makini na kikundi cha watu wachache wanaojitahidi kutuwekea agenda zao kama vipaumbele vya taifa tukielekea uchaguzi mkuu 2015. Hawa wanapewa airtime nyingi isivyostahili kwenye TVs kurudiarudia propaganda zao mbovu ili hatimaye watu waamini ni wakweli kwa staili za akina Hitler - " Ukiurudia uongo mara kwa mara, watu wengi wataamini kuwa ni ukweli".

Kwanza ieleweke kwa mfano, kutofautiana maoni katika mijadala ya katiba ni jambo la kawaida katika mfumo wa demokrasi. La msingi ni kutoa nafasi ya wazi kwa raia kupigia kura (referendum) rasimu au hoja zinazopendekezwa ili maoni ya wengi yapite - na hapa Tanzania ukiondoa uchakachuaji wa wazi uliyofanywa na CCM na mfumo usiofaa wa bunge la katiba ingewezekana kuwaachia wananchi kuamua muundo wa serikali ya muungano (2 au 3) kama swali la msingi kama CUF na raia wengi walivyodai miaka yote.

Hivyo ni upuuzi kwa Polepole kumshkia bango Lowasa na wengine kuhusu mawazo yao juu ya jambo hili. Hata Kenya baadhi ya viongozi waliopinga katiba mpya ndiyo wamechaguliwa (Ruto n.k.) kuongoza nchi na kuitekeleza. Kuhusu sakata la Richmond watu wakweli na wenye akili wanajua kabisa watu wengi na serikali yote ilihusika katika maamuzi.

Richmond ilitokea katika mazingira ya dharura ya taifa ya umeme (national emergency). Nchi ilikuwa inaelekea kuingia gizani na kusababisha hasara ya mabilioni kila siku. Mchakato wa tenda za kununua mejenereta usingefuata taratibu za kawaida hivyo ilibidi maamuzi yafanyike haraka - na tusisahau hata hizo bodi za tenda za mashirika ya umma kama Tanesco zimekumbwa na tuhuma/kashfa nyingi za ufisadi miaka yote zikisababisha hasara na utekelezaji wa miradi.

Kilichotokea wafanyabiashara wajanja wakajitokeza kama agents na hili ni jambo la kawaida pote duniani sababu huwezi kununua mitambo hiyo moja kwa moja kiwandani katika mazingira ya dharura. Issue ni kwamba Richmond waliposhindwa kumobilise pesa na logistics ndipo utapeli wao ulipogundulika!

Ni serikali iliyogundua tatizo wala siyo kamati ya Mwakyembe. Sasa Lowasa na Waziri wa Fedha Meghji wamethibitisha kwamba mpaka hatua hii hapakuwepo malipo yoyote yaliyofanyika! Ni baada ya hapo siasa na jazba zikaingia, Lowasa akajiuzuru na kupelekea nchi kulipa faini kwa amri ya mahakama - the rest is history.

Mapendekezo mazuri ya Zitto kuepusha faini hiyo na hasara yalipuuzwa na akina Sitta na wapambe wake ili watimize lengo lao kummaliza Lowasa. Wengine wanatuletea stori za Mwl. Nyerere zilizotokea zaidi ya miaka 20 iliyopita. Jamani Mwalimu alikuwa na maoni mengi tofauti kwa watu wengi na mabo mengi katika kipindi cha maisha yake. Nayeye alisema alifanya makosa mengi na hakuwa malaika! Yeyote anaye jitwisha jukuma la kumsemea mzee wetu huyu (iwe walipokuwa Msasani au Butiama) ni vizuri akaacha.

Watanzania wa leo wana uwezo wa kuwatambua viongozi wanaofaa kwa kuona matendo yao. As a nation we have moved on after demise of Mwalimu. Vinginevyo hao wanaomsemea Nyerere washinikize CCM irejeshe Azimio la Arusha na miiko ya viongozi kama ilivyokuwa wakati wake. Mwisho yupo Mzee mmoja ninaye mheshimi sana ambaye kwa kushirikiana na "kitengo" ndani ya CCM amekuwa mstali wa mbele kukata wagombea akiwemo Lowasa kwa hoja ya maadili, tamaa ya madaraka n.k.

Ni ajabu, Mzee huyu aliwahi kuwa Spika wa Bunge na wakati huohuo akakubali kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya VODACOM - kampuni kubwa ya mashirika binafsi! Nilimpenda mzee mwingine mkweli wa CCM aliyesema Lowasa amekatwa kutokana na nguvu kubwa aliyokuwa nayo miongoni mwa viongozi na wanachama wa CCM.

Hoja yangu hapa watanzania na hasa wana UKAWA tuungane kukabiliana na changamoto halisi na taifa ambazo ni mabadiriko ya katiba na mfumo wa utawala- ili tupate katiba itakayopunguza madaraka ya Rais, kupunguza ukubwa wa serikali, Kuimarisha taasisi huru za utawala bora (mahakama, bunge, taasisi ya kupambana na rushwa, uchaguzi) ikiwezo "vetting" ya viongozi, devolved government na uhuru wa vyombo vya habari na haki za binadamu, uwiano sahihi katika muungano.

Magenge ya wachambuzi uchwala (Polepole, Mkinga, Mtikila, Kasoli n.k.) yasiachwe kutupangia agenda ambazo zinajikita kuwachambua watu binafsi kwa maslahi ya kulinda watawala na "status quo", badala ya issues za msingi.
 
nyumba za serikali waliuziwa wafanyakazi wa serikali pamoja na lowasa mtutajie waliouziwa nje ya mtumishi wa serikali kama sio unafiki ni nini
Hawara WA makomeo pamoja na mdogo wake waliuziwa nyumba wakiwa wanafunzi WA chuo kikuu hawakuwa watumishi.
 
Samuel sitta hana hamu nae,alimuendesha mbaya bunge la katiba ya wananchi,jamali anagonga tu hajali uko upande gani Wa chama,yeye kwake Tanzania kwanza vyama baadae ndio mana watu wengi wanamfuatilia,lowassa inabidi amtafute tu hakuna namna nyingine zaidi ya kumhonga kama atakubali akae kimya
 
Yericko Nyerere katika ubora wake huko Twitter
 
Ukawa kumbe weupe aisee yani mtu mmoja anawatesa kwa hoja wiki nzima vichwa vyote ukawa vimemshindwa,sasa mumlete lowassa studio apambane na polepole
 
Back
Top Bottom