Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Ni bora Pepo "Jini" Linapobadilika na kutubu kuliko malaika akibadilika (kuhasi) maana Malaika akihasi anakuwa Shetani.

Ndicho kilichotokea kwa huyu polepole
 
mimi huyu Polepole eti tuhuma za Magufuli anasema abebeshwe Waziri Mkuu wakati huohuo anasema Membe awanibishwe ilhali Membe sio Waziri .mkuu

Na anasema anafurahi pinda, membe na lowasa walikatwa kama alivyotaka......hivi membe alikatwa?? Ccm ile tano bora yao si waliamini yeyote anaweza kuwa rais na membe kura hazikutosha tu
 
Polepole leo kakalishwa vibaya sana mtatiro kajenga hoja zake kwa ustadi mkubwa sana nimemkubali
 
Pole pole leo tena kadhihirisha anavyotumika kumchafua lowasa.....eti anasema magufuli alipouza nyumba za serikali kifisadi aliyetakiwa kuwajibishwa ni waziri mkuu .......shame.
 
Tuhuma ya Richmond; Lowasa alitaka kuvunja mkataba wa Richmond, mamlaka ya juu ikakataa na kuamuru mkataba uendelee>>Polepole: Lowasa ni fisadi hafai (Haoni kama mamlaka ya juu ina maslahi hapo) - Hatimaye Lowasa aliwajibika kwa kujiuzuru.

Tuhuma ya kuuza nyumba za serikali; Magufuli aliuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa na nyingine kawauzia ndugu zake wasiowafanyakazi wa serikali. Mpaka sasa wafanyakazi wa serikali wanahangaika kwa kukosa makazi na gharama kubwa za hotel>>>Polepole: Akamatwe waziri mkuu aliyekuwepo, Mgufuli hausiki alifuata maelekezo ya Mkubwa wake wa kazi. Magufuli si fisadi!!!

Hizi case zinafanana kabisaaaaa. ukimsafisha Magufuli msafishe na Lowasa vinginevyo bwana Polepole naona una upendeleo wa waziiiiiii kabisaaaaaaa kwa mgombea wa chama chako.
 
CCM,Kitendo Cha Kumtumia H. PolePole Ch. 10 Kina Hasara Zaidi Kulikoni Faida. PolePole Kila Siku Anarudia Yaleyale Ambayo Kimsingi Sio

Issue Tena. Kilichoonekana Leo Ni Kwamba HP Hana Ubavu Wa Kumtetea Mgombea Dr. Magufuli Kuhusu Uadilifu wake na Kinyume Chake

ni Kumvua Nguo Kwa expose Madhaifu Yake. Sisiem Kama Mnamtuma Kijana Huyu Anaendelea Kuharibu Kabisa.

Kilichoonekana HP Hana Ubavu Kabisa wa Kudebate Na Mwanasiasa Kama J. Mtatiro. CCM Chukua Hatua Huyu HP Ndo Kabisa Anawamaliza Mazima.
 
Wakuu habari
Leo ndiyo nimepata kujua huyu kijana wa Azania ndugu Humphrey Polepole anatumiwa na ccm chini wa mwanvuli wa katiba kuupinga upinzani usiingie madarakani....Leo nimepata kufuatilia kipindi cha television flan chaTz chenye mada inayo husu yanayo jili sasa kuelekea uchaguzi mkuu....nimshukuru ndugu yangu Mtatiro kwa utulivu wake na kutoa hoja zinazo endana na mada husika...Lakushangaza ndugu polepole ameonekana wazi akijaribu kutengeneza mianya ya kuchomoa mtu mmoja na kudili naye personally ili hali mada ilikuwa hamuhusu...MY TAKE: Akili za kuambiwa changanya na zako..Hakika polepole anatumiwa .
 
Kweli ukiambiwa jambo na akili za mtu mwingine changanya na akili zako. Wote walikuwa 50/50
Polepole alitaka kuhadaa watu eti Lowassa ndie aliichakachua katiba mpya watu wamsikubali....Julius Mtatiro akampa Live...kuwa asipotoshe watu...Mtu aliyechakachua katiba mpya sio Lowassa ni Mwenyekiti wa CCM JK...na aache kuhadaa watu sio Lowassa, MFUMO wa CCM ndio tatizo, na wananchi wanataka mabadiliko ya kuuondoa mfumo wa CCM...!!!

AKAJIDAI eti CCM ni kitu kidogo tu ktk mfumo...!!! Mtatiro akamwambia labda hajui anachosema...CCM ndio chama Dola..kwa miaka 50, hizi Rushwa, uchafu, uporaji wa mali ya umma, umaskini yote YANALETWA NA CCM... na CCM ndio MFUMO wenyewe...asiseme eti CCM ni kitu kidogo tu...in short Polepole alitaka kuaminisha watu CCM sio TATIZO...na MAGUFULI NI MSAFIIIIK KAMA MALAIKA...ameaibika sana sanaaaa...!!!
 
pole pole sasa anawakati mgumu maana alichokisema kwamba ccm wakate mafisadi hawajakata sijui amesemaje
 
Jamaa uelewa wake unatiaga shaka........ anajitaidi kutaka wamuamini na anataka kuwaaminisha kuwa yeye ni mjuaji.....
 
Mnyakatari

Mtangazaji alitaka maelezo tu wananchi wanavyoongelea mabadiliko wanamaanisha nini polepole katuzungusha kama ulivyoeleza ila mpiga simu toka pemba akaeleza kwa kifupi mabadiliko ya mfumo kwa lugha ya wananchi ni kuiondoa ccm
 
Last edited by a moderator:
Nilichojifunza toka kwa Polepole:

CCM katika mchakato wake wa kupata wagombea urais imefanikiwa kuwaondoa mafisadi wake wakubwa waliokuwa na matumizi makubwa ya fedha ili kushawishi wajumbe wawapitishe katika uteuzi.

Mfumo ni zaidi ya CCM. Mfumo ni utendaji mzima wa Watumishi wa Umma, Sekta binafsi, Mahakama, vyombo vya ulinzi na usalama na taasisi zake. Kumuondoa Rais peke yake Hakuondoi mfumo.

Watanzania hawahitaji mabadiliko (Change of regime), wanahitaji Mageuzi (Transformation). Mageuzi ndiyo yanayoweza kubadili mfumo na hauwezi kurudia mfumo wa awali tena lakini change inaweza kuwa reversed.
Lowassa si mtu binafsi bali ni taasisi yenye wafanya biashara wakubwa ndani yake, isiyoweza kudhibitiwa kwa maamuzi yake. Ila yeye anaweza kuwadhibiti wengine kama inavyotokea sasa katika baadhi ya viongozi wa vyama vya ukawa kudhibitiwa.

Magufuri katika utumishi wake wote, amehudumu wizara zisizo za muungano ambazo msimamizi wake ni Waziri mkuu. Maana yake majukumu yake ni ya utekelezaji wa maagizo ya Bosi wake, Waziri mkuu. Mfano uuzwaji wa nyumba za serikali.

 
Big up kwa brother Mtatiro. Polepole kinachomsaidia ni sauti tu ya kuongea lakini hana hoja zenye mashiko. Bila shaka polepole umetumwa na unachuki binafsi na Lowasa. Ila kaa ukijua Lowasa ndiye Rais, huyo Magufuli hawezipata Urais,hatuna imani na CCM tena. Tunataka mageuzi kama ulivyosema lakini ccm hana nia ya dhati ya kutupa hayo mageuzi kwa kuvikataa hivyo vitu ulivyoviainisha kwenye katiba ya warioba.
 
Chadema mtabadili wachambuzi tu ila huyu polepole hamumuwezi

Polepole ni msemaji wa CCM bana, aliwapa masharti na kuwachagulia mgombea, anajifanya CCM iko poa na kasahau kuwa walichakachua katiba ya Warioba, Anadeal na mtu maana ndiyo maagizo aliyopewa na CCM, Alipoulizwa kuhusu uuzwaji wa nyumba za serikali na Magufuli anajibu eti alipewa amri na mamlaka ya juu kasahau hata Lowasa ana mamlaka za juu ilimwamuru kuhusu Richmond.

Polepole kaweka katiba ya Warioba iliyochakachuliwa na CCM na sasa anafurahi katiba kubadilishwa.Kasahau kuwa katiba mbovu ndiyo vyanzo vya ufisadi nchini na CCM wanaikumbatia ili iendelee na UFISADI huku akiiunga mkono. Tumekuelewa maana ulikuwa unatafuta umaarufu kwa mgongo wa katiba ya Warioba sasa umewageuka wazee wako hiyo laana haitakuacha.Kawatie moyo Familia ya Magufuli na uwe sehemu ya familia yake Intaharamwe.

Channel ten acheni kumwita Polepole kama mchambuzi bali ni kada wa CCM, watafuteni wachambuzi makini siyo kudanganya watu kuwa ni wachambuzi kumbe makada wa vyama.
 
Back
Top Bottom