Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,924
- 831,404
- Thread starter
- #581
Mogadishu- 02 Julai, 2025
Somalia imeanza mradi wa ujenzi wa kiwanja kipya cha ndege cha kimataifa karibu na Mogadishu, katika eneo la Haawaay kilomita 35 kutoka Mogadishu katika eneo la Shabelle ili kupunguza msongamano katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Adde.
Kiwanja hicho kipya cha ndege, kilichopewa jina la Mogadishu International Airport, ni mradi wa dola milioni $800 uliobuniwa kuimarisha muunganisho na kusaidia ukuaji wa uchumi ambapo unatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitano.
Mradi huu utapunguza msongamano wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Adde na kuboresha muunganisho wa ndani na wa kikanda.
Mradi huo unaonekana kama ishara ya kuimarika kwa Somalia na uwezo wa kujijenga upya, pamoja na kukuza sekta ya usafiri wa anga na maendeleo ya taifa.
Kiwanja hicho cha ndege kinatarajiwa kuwa na angalau njia mbili sambamba za kuruka na kutua ndege, kila moja ikiwa na urefu wa takriban mita 4,000, ili kuhudumia ndege kubwa za kibiashara.
Somalia imeanza mradi wa ujenzi wa kiwanja kipya cha ndege cha kimataifa karibu na Mogadishu, katika eneo la Haawaay kilomita 35 kutoka Mogadishu katika eneo la Shabelle ili kupunguza msongamano katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Adde.
Kiwanja hicho kipya cha ndege, kilichopewa jina la Mogadishu International Airport, ni mradi wa dola milioni $800 uliobuniwa kuimarisha muunganisho na kusaidia ukuaji wa uchumi ambapo unatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitano.
Mradi huu utapunguza msongamano wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Adde na kuboresha muunganisho wa ndani na wa kikanda.
Mradi huo unaonekana kama ishara ya kuimarika kwa Somalia na uwezo wa kujijenga upya, pamoja na kukuza sekta ya usafiri wa anga na maendeleo ya taifa.
Kiwanja hicho cha ndege kinatarajiwa kuwa na angalau njia mbili sambamba za kuruka na kutua ndege, kila moja ikiwa na urefu wa takriban mita 4,000, ili kuhudumia ndege kubwa za kibiashara.