Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Rais na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa kampuni ya Boeing ametoa kauli yake inayoambatana na salamu za Rambirambi kuhusu ajali ya ndege aina ya Boeing 787 ya shirika la Air India iliyotokea mapema Alhamisi ya leo.

Kauli hiyo inasema;

"Rambirambi zetu za dhati ziwaendee wapendwa abiria na wafanyakazi kwenye ndege ya Air India Flight 171, vile vile
kila mtu aliyeathiriwa huko Ahmedabad."

"Nimezungumza na Mwenyekiti wa Air India, N.Chandrasekaran kutoa msaada kamili na timu ya Boeing inasimama tayari kuunga mkono uchunguzi unaoongozwa na ofisi ya Uchunguzi wa Ajali za Ndege ya India"

Mwisho wa nukuu

Kelly Ortberg
Rais wa Boeing na Mkurugenzi Mtendaji - BOEING
1749982463217.jpg
 
Ndege ya JetBlue yenye mruko namba B6312 iliyokuwa ikitokea uwanja wa ndege wa O'Hare (Chicago) imeacha njia katika uwanja wa ndege wa Boston Logan siku ya Alhamisi, maafisa wa eneo hilo walisema.

Ndege aina ya Airbus A220-300 yenye usajili N3242J iliacha njia na kuelekea kwenye nyasi kutoka kwenye njia ya 33L wakati ilipotua.

Mamlaka ya Uwanja wa ndege ilisema katika taarifa yake kwamba, hakuna majeruhi na njia ya kurukia ndege imefungwa.

Abiria wanaripotiwa kupandishwa kwenye Mabasi wakati ndege hiyo ikifanyiwa tathmini.
1749982902736.jpg
 
Ndege aina ya Airbus 380 kutoka shirika la ndege la Qantas - Australia, inatajwa kuwa mojawapo kati ya ndege zinazoongoza kwa kufanya njia ndefu zaidi ya kituo kimoja inayosafiri zaidi ya saa 24.

Ndege hiyo hufanya safari kati ya Uwanja wa Ndege wa Sydney Kingsford Smith (SYD), Australia, hadi London Heathrow (LHR), Uingereza, kupitia Uwanja wa Ndege wa Singapore Changi (SIN).

Ratiba hii ya safari inajulikana kama Njia ya Kangaroo "Kangaroo Route" ambayo huchukua takribani mwendo wa saa 24.75 kutoka Australia hadi kuwasili Uingereza.

Qantas hufanya safari 30 (sawa na safari 60 za kwenda na kurudi) kila mwezi, ambapo hubeba wastani wa abiria 485 kwa mruko mmoja.
1749992649231.jpg
 
Ndege iliyokuwa imebeba watu wawili ilianguka kwenye paa la kituo cha ndege cha New Century Air Center katika kaunti ya Johnson siku ya Jumatatu, Juni 16 majira saa 7 mchana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Uwanja wa Ndege wa Johnson County, Bryan Johnson, alisema, Wote waliokuwa ndani ya ndege hiyo waliweza kutoka na majeraha madogo madogo.

Wafanyakazi wa dharura walifika eneo la tukio kwa wakati kulingana na taarifa PulsePoint na kutumia ngazi kuwatoa watu wote wawili kutoka kwenye paa la hangar, Johnson alisema.

"Kulikuwa na watu wachache waliokuwa wakifanya kazi kwenye karakana hiyo wakati wa ndege hiyo kutua kwenye paa, Johnson alisema.

Taarifa zaidi: https://www.kansascity.com/news/local/article308768340.html#storylink=cpy
1750140475145.jpg
 
Kwa mujibu wa mtandao wa ufuatiliaji wa safari za ndege wa Flight Radar 24, katika muda mchache uliopita unaonyesha ndege mbili ikiwemo MAX9 ya Air Tanzania na Dash 8-100 ya Auric Air zikiwa zinasubiri angani (Hold) kabla ya kutua.

Bado hatufahamu sababu ya kusubirishwa huko.
1750248325260.jpg
 
Honda, kampuni ya kutengeneza magari ya Kijapani, imezindua na kufanikisha majaribio ya kutua roketi ya mfano inayoweza kutumika tena, ikiashiria hatua muhimu kuelekea lengo lake la kufikia anga za mbali za chini ifikapo 2029.

Honda R&D ilikamilisha kwa ufanisi jaribio la kwanza la uzinduzi na kutua roketi yake ya majaribio cha futi 20.6 inayoweza kutumika tena katika mwinuko wa futi 889 katika kituo chake cha majaribio cha Taiki Japani.

Jaribio lililenga kuonyesha teknolojia muhimu kwa ajili ya utumiaji tena wa roketi, kama vile uthabiti wa ndege wakati wa kupanda na kushuka, pamoja na uwezo wa kutua.

Honda pia ilianzisha kampuni ya kutengeneza ndege ndogo za kibinafsi mwaka wa 2006 ziitwazo HondaJet ikiwa kama kampuni tanzu ya Honda Motor Co.

Utafiti wa roketi wa Honda bado uko katika awamu ya kimsingi ya utafiti, lakini inapanga kuendelea kufanya maendeleo katika utafiti huo wa kimsingi kwa lengo la ukuzaji wa teknolojia ya kutambua uwezo wa kiteknolojia ili kuwezesha uzinduzi wa sehemu ndogo ifikapo 2029.
1750271799165.jpg
 
Shirika la ndege la RwandAir mnamo Juni 17 limepokea Tuzo kama "Shirika Bora la Ndege la Kanda" barani Afrika katika Tuzo za mashirika ya Ndege Duniani 2025 zilizoandaliwa na Skytrax mjini Paris.
1750273233281.jpg
 
Qatar Airways ilitangazwa mshindi katika tuzo za mwaka huu za Skytrax World Airline Awards - 2025.

Hii inakuwa mara ya 09 kwa mtoa huduma huyo kupokea heshima hiyo katika historia ya miaka 26 ya tuzo hizo, ambazo zinajulikana kama "Oscars of the aviation world"

Ikifafanua upya ubora wake juu ya clouds, Shirika la Ndege la Qatar linaendelea kutambuliwa kuwa "Shirika Bora la Ndege Ulimwenguni" kwenye Tuzo za Skytrax 2025, pamoja na kutawazwa tuzo nyingine kadhaa ikiwemo;
"Daraja Bora la Biashara Ulimwenguni" kwa mara ya 12

Soma zaidi;
1750284509134.jpg
 
Moto mkali uliweza kudhibitiwa kwenye eneo la uwanja wa ndege wa Kinshasa N'Djili, (FIH), Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kabla ya kuenea zaidi siku ya Jumatano, Juni 18.

Moto ulilipuka kutoka kwenye trekta ya ATS mara baada ya kusukuma ndege ya ASKY, ikiwa inajiandaa kusukuma ndege ya Air Congo na ambapo dereva aliwahi kukimbia kutoka eneo la tukio.

Msemaji wa uwanja wa ndege alisema:
"Tuliita kikosi cha zima moto, ambacho kilidhibiti moto mara moja. Matairi ya ndege hiyo hayakushika moto, na hali ilirejea kuwa ya kawaida."
1750338764962.jpg
 
Ndege ya British Airways BA35 ilipata tukio la kiufundi siku ya Jumapili 15 Juni, lililowalazimu marubani kugeuka na kurejea London Heathrow.

Ndege hiyo ya British Airways BA35 iliondoka Uwanja wa Ndege wa London Heathrow kuelekea Chennai, India.

Ndege hiyo aina ya Boeing 787-8 BA35 (usajili G-ZBJG) iliondoka Uwanja wa Ndege wa London Heathrow kuelekea Chennai, India lakini ikasimamisha kupanda usawa wa futi 15,000 kisha ikaingia kwenye mzunguko angani wakati marubani wakishughulikia suala la "Flaps".

Kwa kuwa marubani hawakuweza kutatua tatizo hilo, uamuzi ulichukuliwa wa kurudi Heathrow ambapo kabla ya hapo, marubani walilazimika kumwaga mafuta ili kupunguza uzito wa ndege.

Ndege hiyo ilishuka hadi futi 12,000 juu ya mkondo bahari na kumwaga mafuta kwa takriban dakika 30.

Saa moja na dakika 45 baadae, ndege hiyo ya Boeing 787 ilitua kwenye njia ya 27L na kupokewa na magari ya dharura kisha kupelekwa kwenye Kituo cha 5, stendi ya C66.
FB_IMG_1750387723211.jpg
 
PARIS - 20 JUNI

Airbus imepata dola bilioni 21 katika oda mpya za ndege katika Maonyesho ya Anga ya Paris ya 2025, kuashiria uongozi bora dhidi ya mpinzani wake Boeing, ambaye alijizuia kutangaza mikataba yoyote mpya.

Kutoshiriki ipasavyo kwa Boeing kunafuatia ajali mbaya ya Air India (AI) Boeing 787 karibu na New Delhi (DEL), ikitoa picha ya huzuni ya tukio katika kalenda ya maonesho ya anga ya kimataifa.

Tukio hilo lililohusisha ndege ya Boeing 787 Dreamliner, ikiashiria ajali ya kwanza mbaya inayohusisha Boeing 787 Dreamliner tangu ianze huduma.

Licha ya kurudisha nyuma matangazo kwa kuzingatia janga la Air India, Airbus iliondoka kwenye Maonyesho ya Anga ya Paris ya 2025 na mafanikio makubwa ya kibiashara.

Vivutio muhimu ni pamoja na agizo la ndege 40 za A220 kutoka LOT Polish Airlines na makubaliano makubwa na VietJet ya hadi ndege 150.

Pia Airbus ilipata oda ya Saudi Arabia, na Riyadh Air, iliagiza ndege 25 za A350 na AviLease ilinunua ndege 40 kwa matumizi ya abiria na mizigo.

Timu ya uongozi ya Boeing, ikiwa ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu Kelly Ortberg na Mkuu wa Ndege za Biashara Stephanie Pope, walighairi kuhudhuria maonyesho ya anga kufuatia ajali ya Air India iliyoua zaidi ya watu 270.
1750405108208.jpg
 
Wakati wa majaribio ya ardhini mnamo 2017, Injini ya GE9X ilitoa matokeo ya kushangaza ya nguvu ya pauni 134,300 (597.396 kN) na kuweka rekodi mpya ya ulimwengu iliyotambuliwa rasmi na kitabu cha kumbukumbu za Dunia cha Guinness World Record.

Moja ya ndege kubwa zaidi ya abiria duniani, Boeing 777X, inatarajiwa kuanza kutoa huduma mwaka 2026 huku shirika la ndege la Ujerumani, Lufthansa, likiongoza shughuli za uzinduzi.

Ndege hiyo, ambayo ni mradi mkubwa zaidi wa ndege za kibiashara wa Boeing, imesimikwa GE9X, injini kubwa zaidi ya ndege za kibiashara duniani.

Toleo la Boeing 777-9, ambayo inaweza kuchukua zaidi ya abiria 425, inapita urefu wa Boeing 747-8 na Airbus A380 ya ghorofa mbili.

Injini za GE9X, kila moja ikiwa na uzito wa takriban pauni 21,000 (Sawa na tani 9.5) na kipenyo cha inchi 184 kwa ujumla, inaonesha mageuzi ya kazi bora ya teknolojia katika uhandisi wa anga.

Kipenyo cha feni kina urefu wa inchi 134, inchi 6 zaidi ya injini za GE90 zinazotumia ndege ya sasa ya Boeing 777-200 na 777-300.

Wachambuzi wa sekta ya anga wanajadili kuwa, nguvu ya upepo inayozalishwa na injizi za GE9X inaweza kuangusha kirahisi Gari kubwa ikiwa inakatiza nyuma yake.

Injini hizo 02 pacha za B777X zinatoa faida ya nguvu sawa ikilinganishwa na ndege nyingine kubwa za kibiashara zenye injini 04 kama vile Airbus A380 na Boeing B747-8.

1750422617836.jpg
 
Agosti 19, 1980 - Ndege ya Saudia namba 163 ilipaa kutoka Riyadh kuelekea Jeddah.

Dakika chache tu baada ya safari, kengele za moshi zilizuka.
Moto ulikuwa umezuka katika sehemu ya kubebea mizigo ya Lockheed L-1011 TriStar.

Wafanyakazi waligeuka nyuma, wakatangaza dharura, na kuweza kutua salama.

Injini zilizimwa, timu ya uokoaji chini walisubiri milango ya ifunguliwe, lakini ndani ya ndege moshi mbaya ulienea haraka. Watu wote 301 waliokuwa ndani abiria na wafanyakazi walipoteza kwa hewa ya fusho yenye sumu kabla ya timu za uokoaji hata kufungua milango.

Walikuwa karibu sana na usalama. Lakini bado, walichelewa.

Flight 163 inasalia kuwa mojawapo ya hitilafu mbaya zaidi katika historia ya usafiri wa anga, si kwa sababu ndege ilianguka, lakini kwa sababu hakuna mtu aliyetoka hai ndege ilipotua.

Tukio hilo lilibadilisha kila kitu, itifaki za uokoaji haraka, uboreshaji wa lazima wa kuzima moto, na mafunzo makali ya wafanyakazi.

Kunusurika kwa kutua kwa ndege haitoshi, inabidi utoke nje.
1750479842581.jpg
 
Video kutoka kwenye chumba cha marubani "Cockpit" hapo juzi, inaonyesha kurushwa kwa makombora ya balistiki kutoka Iran.

Video hiyo iliyoripotiwa kuchukuliwa kutoka kwenye chumba cha marubani cha ndege ya kibiashara kwenye Rasi ya Uarabuni inaonyesha makombora hayo yakifika anga ya juu kutoka Iran kuelekea Israel.

Iran ilirusha takriban makombora 280 ya balestiki dhidi ya Israel katika mashambulio kadhaa tangu Jeshi la Ulinzi la Israel lianze operesheni yake dhidi ya mpango wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu mapema Ijumaa asubuhi, kwa mujibu wa takwimu zilizosasishwa na jeshi siku ya Jumapili.

Chapisho kutoka pic.twitter.com/d0h1SsTsG7 liliandika

"Picha za kustaajabisha zinazoonyesha kurushwa kwa makombora ya balestiki mapema leo na Iran dhidi ya Israel, kutoka kwenye chumba cha marubani cha ndege ya kibiashara iliyokuwa ikiruka juu ya Dubai"

Makombora kadhaa "yamepenya" ulinzi wa anga, kulingana na IDF, yakishambulia maeneo ya Tel Aviv, Ramat Gan, Rishon Lezion, Bat Yam na Rehovot katikati mwa Israeli, na Haifa na Tamra kaskazini, na kusababisha hasara na uharibifu.

Kulingana na makadirio ya Marekani, Iran ilikuwa na orodha ya makombora 3,000 ya balestiki kabla ya mashambulio ya hivi karibuni
1750481177097.jpg
ya Israeli.
 
Kikosi cha Tathmini ya usalama kimeundwa katika kambi za kijeshi za Uingereza baada ya wanaharakati wanaoiunga mkono Palestina kuvamia kwa kutoboa uzio wa kambi ya RAF Brize Norton na kunyunyizia ndege mbili za kijeshi rangi nyekundu.

Waziri Mkuu Sir Keir Starmer alilaani kitendo hicho na kusema ni cha aibu, na "kitendo cha uharibifu".

Picha zilizochapishwa mtandaoni na 'Palestine Action' mnamo Ijumaa zilionyesha watu wawili ndani ya uwanja wa ndege wa Oxfordshire wakiwa gizani, mmoja akiwa amepanda baiskeli ya skuta hadi kwenye ndege ya Airbus Voyager na kunyunyizia rangi kwenye injini.

Polisi wa kukabiliana na ugaidi Kusini Mashariki baadaye walithibitisha kuwa maafisa wake maalum walikuwa wakichunguza tukio hilo pamoja na Polisi wa Thames Valley na Wizara ya Ulinzi (MoD).
1750519356222.jpg
 
Takriban watu wanane wamepoteza maisha kufuatia ajali iliyohusisha puto la hewa moto katika eneo la kusini mwa Brazil la Santa Catarina siku ya Jumamosi ya leo, taarifa ya gavana wa eneo hilo inasema.

"Sote tumeshtushwa na ajali iliyohusisha puto huko Praia Grande, Jumamosi hii asubuhi. Timu yetu ya uokoaji tayari imewasili kwenye eneo husika na tumethibitisha vifo vinane" gavana wa eneo hilo Jorginho Mello alisema kwenye mtandao wa X.

Alisema watu 21 walikuwa ndani ya ndege hiyo, ambapo watu 13 walinusurika.

Video iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii inaonyesha puto ya hewa moto ikishika moto ikiwa angani.
Kisha puto kuungua na kuanguka chini.

"Tuliona watu wawili wakianguka kutoka juu, na mara baada ya kikapu kuvunjika, na puto ikaanguka," Shuhuda aliambia vyombo vya habari vya ndani Jornal Razão.

Shahidi huyo alisema alikimbia ili kuona mahali puto lilianguka na kuona manusura wawili, "mwanamke aliyefunikwa na matope na katika hali ya mshtuko, na mwanamume ambaye alikuwa akichechemea," pamoja na miili miwili.

Rais Luiz Inácio Lula da Silva alionyesha mshikamano wake na familia za wahanga kwenye mtandao wa X.
"Ningependa kuiweka Serikali ya Shirikisho kwa wahathiriwa na vikosi vya serikali na manispaa ambavyo vinafanya kazi ya uokoaji na utunzaji wa walionusurika," alisema.
1750522859211.jpg
 
GARDNER, Kan (KCTV) - Hitilafu ya kiufundi imetajwa kusababisha ajali ya ndege yenye injini mbili kuanguka juu ya paa la karakana, ambayo ilijeruhi rubani na abiria waliokuwa ndani.

Maafisa wa Kaunti ya Johnson walithibitisha kuanguka kwa ndege hiyo juu ya hangar ya Butler Avionics tarehe 16 Juni, katika New Century AirCenter nje ya Gardner, Kansas

Askari wa Kansas Highway Patrol walisema kuwa ndege ya Beech King Air ilikuwa ikiruka kusini wakati hitilafu ya kiufundi iliposababisha injini ya kushoto ya ndege hiyo kushindwa kufanya kazi.

Leslie Gordon, rubani mwenye umri wa miaka 73 wa ndege hiyo kutoka Lee’s Summit, alipoteza udhibiti wa ndege hiyo ilipogeuka upande wa kushoto na kuanguka kwenye hangar.

Askari wa Jimbo walionyesha kuwa Leslie na abiria wake, Delaney Rindal, 30, wa Wasilla, Arkansas, wote walipelekwa katika Kituo cha Afya cha Mkoa wa Overland Park na majeraha yasiyo ya kutishia maisha.

Hakuna mtu ndani ya hangar aliyejeruhiwa katika tukio hilo na shughuli zimeendelea kama kawaida katika uwanja wa ndege.
1750523733229.jpg
 
Katika tukio hilo waliloita "Operation Midnight Hummer" ilihusisha zaidi ya ndege 125 zikiwemo B-2 Spirit zilizoruka kwenye Bahari ya Pasifiki kama "udanganyifu," kulingana na maafisa wa Amerika.

Wakati huo, ndege nyingine za B-2 ziliingizwa kudondosha dazeni ya mabomu makubwa wanayoita "bunker buster" kwenye vituo vya Iran vya Fordow na Natanz, huku makombora ya Tomahawk yakirushwa kwenye kituo kimoja huko Isfahan.

Taarifa inasema, ndege za B-2 ziliruka urefu wa futi 40,000, kuangusha mabomu zaidi ya tani 12 yanayodondoka kwa kufuata mvuto wa ardhi pasipo kuendeshwa na injini.

'Bunker Buster' ziliongozwa na Satelaiti kulenga shabaha huku ikidhibiti uelekeo kwa kutumia mapezi ya mkia yanayotembea mfano wa 'rudder na elevator' za mkia wa ndege.

Uzito mkubwa hufanya nishati kubwa ya 'kinetic' inapofikia uso na kupenya hadi mita 60 chini ya ardhi kabla ya 'Fuse' kulipua kilo 2,400 za vilipuzi.

Waziri wa Ulinzi Pete Hegseth alidai operesheni hiyo "ilifuta" malengo ya nyuklia ya Iran.
1750612428291.jpg
 
Alberto Santos-Dumont, anayejulikana kama "Baba wa Usafiri wa Anga" huko Brazili, alijiua mnamo 1932 kutokana na mfadhaiko mkubwa na dalili za kisaikolojia zinazohusiana na matumizi ya ndege aliyobuni kwaajili ya usafiri wa anga, kutumika kuangamiza binaadamu katika vita ya kwanza ya Dunia mnamo 1914-18.

Albert Santos alikuwa mwanaanga wa Brazili, mwanamichezo, na mvumbuzi ambaye alichangia pakubwa katika ukuzaji wa mapema wa ndege nyepesi kuliko hewa na nzito kuliko hewa (Lighter and Heavier than Air Aircraft).

Puto ya kwanza "Hot Air Balloon" ya Santos-Dumont, aliyoita "Brésil," ilifanyaa safari yake ya kwanza huko Paris mnamo 1898.

Albert Santos alibuni na kuunda ndege kadhaa, ikijumuisha safari ya kwanza iliyofaulu ya ndege inayotumia nguvu (Powered flight) huko Ulaya.

Anasifiwa kwa kufanya safari ya kwanza ya ndege iliyoshuhudiwa hadharani na kurekodiwa na watu huko Ulaya aina ya 14-bis Biplane 14 mnamo 1906.
1750660728166.jpg
 
Back
Top Bottom