Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Nyenzo za kipekee za mchanganyiko zinazotumiwa katika muundo wa B-2 zinaweza kukabiliwa na kutu ikiwa zinahifadhiwa kwenye mazingira yasiyodhibitiwa.

Karakana 'Hangar' zenye kiyoyozi huhakikisha hali ya utulivu ambayo inazuia uharibifu wa taratibu wa nyenzo hizi muhimu.

Uwezo wa siri wa B-2 Spirit unategemea sana nyenzo za ngozi yake kunyonya mawimbi ya rada.

Nyenzo hiyo ni dhaifu kwa unyevu, mabadiliko ya joto, na vumbi hali inaweza kukabiliwa na kutu.

Ili kudumisha hali yake ya kutoonekana kirahisi kwenye rada, ndege lazima ihifadhiwe katika karakana zinazodhibitiwa na hali ya hewa ambazo hudhibiti halijoto na unyevu.

Ikizingatiwa kuwa kila B-2 inagharimu takriban dola bilioni 2, Jeshi la anga la Marekani huchukua tahadhari kubwa kulinda uwekezaji huu.
1750700480894.jpg
 
Ndege ya Qantas QF33 iliondoka Perth, Magharibi mwa Australia Jumatatu, Juni 23 2025 saa 20:01 (AWST) kwa muda uliopangwa wa safari ya saa 17 na dakika 10.

Ndege hiyo ya Boeing 787-9 yenye usajili VH-ZNM iliondoka katika Uwanja wa Ndege wa Perth na kupanda usawa wa futi 38,000 safari ndefu katika bahari ya Hindi.

Lakini kutokana na mashambulio ya makombora ya Iran dhidi ya kambi ya anga ya Marekani ya Al Udeid, Qatar na UAE zilifunga anga na kuwalazimu marubani kugeuka pwani ya India.

Ndege ilirejea kutua tena Perth, siku iliyofuata, Jumanne, Juni 24 2025 ikitumia saa 17 na dakika 7 za safari tangu kuondoka.
1750740583997.jpg
 
Airplanes Africa Limited (AAL) ni kampuni ya Kitanzania ambayo imeidhinishwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kuunda na kutengeneza ndege ndogo za watu wawili hususan aina ya Skyleader 400, 500 na Skyleader 600.
Ingawa pia ina lengo la kuunda ndege za watu wanne hapo baadae.

Kampuni hii iliyopo mkoani Morogoro,imekuwa ya kwanza nchini Tanzania kufikia uthibitisho huu wa uundaji na utengenezaji wa ndege ambapo inalenga kusambaza soko la Afrika Mashariki.

Wakati wa matembezi yangu binafsi siku ya leo, nilipata fursa ya kipekee ya kushuhudia mchakato mgumu wa kutengeneza ndege hizo, pamoja na juhudi inayochanganya teknolojia na ufundi wa kitamaduni kuanzia uundaji sahihi wa mabawa hadi mkusanyiko wa sehemu za chumba cha marubani.

Naweza kusema, matembezi haya yamenizindua kushuhudia ustadi mkubwa ambao unaweza kuchochea kukua kwa tasnia hii ya usafiri wa anga inayochipukia.

Kampuni ya AAL imejikita katika utengenezaji wa ndege zinazoundwa kwa madhumuni mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mafunzo, binafsi, kilimo, Ufuatiliaji (Doria), Utalii na kadhalika.

Nimeshuhudia jinsi mafundi stadi wakitengeneza kwa uangalifu sehemu mbalimbali za ndege kama mabawa, mikia, mifumo ya umeme na nguzo muhimu zinazoshikilia uimara wa ndege vikiundwa kwa umakini wa hali ya juu kuhakikisha usalama na utendakazi angani.

Wanachokifanya hapa sio kuunga mapande tu, bali ni mchanganyiko wa uhandisi, ufundi na uzalishaji.

Lakini pia nilipata kutembelea mtambo wao wa kufundishia ndege wa kisasa (Flight simulator) unaoigiza hali halisi ya ndege angani na ardhini katika kila hali ya hewa.

Kwa kumalizia naweza kusema, uelekeo wa Airplanes Africa Limited sio tu utachangia uchumi wa taifa lakini kusaidia kuinua uwepo wa Afrika katika sekta ya anga ya kimataifa na kutimiza ndoto za wanaotaka kuwa marubani na watumiaji wa usafiri wa anga.

Shukrani sana uongozi na timu nzima ya utendaji kazi kwa kuwataja wachchache;
~Paulo Ihuya
~Meyoyu Kampuni
~Abdulmalik Zumo
~John Haule
~Lilian Petro
~Engelbert Sengati
~Claude Moga
~Kaysan Khakoo
~Naumu Siloma
~Nickson Kaduma
~Michael Seni
~Mark Makalanga
~Salim Goliama

Usikose kufuatiliaya 'Special Flight Demonstration Day' ambayo ni maonyesho ya usafiri wa anga ya ndege wanazozalisha AAL (Skyleader) kuanzia tarehe 24 hadi 27 Juni.
1750754899629.jpg
 
Mwigizaji Suchitra Krishnamoorthi alihoji hadithi ya mtu pekee aliyenusurika kwenye ajali ya Air India 171, Vishwas Kumar Ramesh.

Kufuatia ajali mbaya ya ndege ya Air India ya Boeing 787 Dreamliner mnamo Juni 12, ambayo iligharimu maisha ya watu 270, mwigizaji Suchitra Krishnamoorthi alituma maoni X yanayohoji hadithi ya manusura pekee, Vishwas Kumar Ramesh aadhibiwe ikiwa hadithi yake itakuwa ya uwongo.

Baada ya kukabiliwa na maoni ya chuki kwenye mitandao ya kijamii, Suchitra alifuta chapisho lake na kujilaumu kwa kuenea kwa habari ghushi.

Chapisho lililofutwa lilisomeka, "Kwa hiyo huyu vishwas kumar ramesh alidanganya kuwa ni abiria kwenye ndege na ndiye pekee aliyesalimika? Hii ni ajabu sana.."

"Je, familia yake huko Uingereza haikuthibitisha hadithi yake? Anastahili sio tu adhabu kubwa lakini awekwe kwenye tiba ya akili."

Baadaye Suchita alifuta chapisho hilo na kuomba radhi.
1750761640820.jpg
 
Jeshi la Anga la Kifalme la Uingereza (RAF) limenunua ndege 12 mpya za kizazi cha tano za F-35A kama sehemu ya Mapitio ya Ulinzi wa Usalama, kuashiria kurejea kwa jukumu la nyuklia kwa RAF kwa mara ya kwanza tangu kuisha kwa Vita Baridi.

F-35A itapatikana kwa misheni ya nyuklia ya NATO wakati wa migogoro, ikiimarisha mchango wa Uingereza katika ugawanaji mizigo ya nyuklia wa NATO na kuimarisha kuzuia dhidi ya vitisho kwa Uingereza na Washirika wake.
1750940220911.jpg
 
Ndege ya Air India AI2354 kutoka Mumbai kuelekea Bangkok ilichelewa kwa saa tatu baada ya kiota cha ndege kupatikana ndani ya bawa la ndege hiyo kabla ya kuruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Mumbai mnamo Juni 25.

Ndege hiyo, iliyopangwa kuondoka saa 1:45 asubuhi, ilikabiliwa na dharura hiyo huku wafanyakazi wa ardhini wakiondoa kwa uangalifu kiota kilichotengenezwa kwa nyasi na vijiti.

Shirika hilo lilichukua uamuzi wa kubadili ndege nyingine.
Abiria wote walirejeshwa kwenye Terminal 2 ili kupanda ndege mpya, iliyopangwa upya kuondoka saa 12 jioni.

Credit:
pic.twitter.com/Q0
1750942383251.jpg
E1JVG724
 
Graham Cooke, Rais wa Tuzo za World Travel (WTA) pamoja na Makamu wa Rais na timu nzima ya ufundi wametua rasmi jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) ikiwa Tanzania mwenyeji mteule katika tuzo za WTA mwaka 2025.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) uliteuliwa kuwania Tuzo hiyo katika kipengele cha "Kiwanja cha Ndege Bora/Kinachoongoza Afrika" kwa mwaka 2025 ikiwa sambamba na viwanja vingine vya ndege vilivyoteuliwa katika kipengele hicho ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Tambo O.R.

Sherehe za "The Africa & Indian Ocean Gala Ceremony" zinahodhi tuzo hizo, zitafanyika katika Hotel ya Johari Rotana, Dar es Salaam mnamo 28 Juni, 2025.

Chanzo:
Tanzania Unforgettable
1750990077752.jpg
 
Marubani wa ndege ya kijeshi ya B-2 Spirit (Bomber) huvaa nguo za ndani zinazonyonya taka, zinazojulikana kama "Pilot Relief Bags" au "Astronaut Diapers," au Nepi wakati wa misheni ndefu.

Chumba cha marubani cha B-2 kimebana na kifupi, kilichoundwa kwaajili ya umbo la siri la ndege na ufanisi na sio faraja.

Marubani hukaa hivyo ndani kwa saa nyingi wakiwa na nafasi ndogo ya kusimama, kutembea ili kupata huduma za haja.

Ndege za B-2 zilitumiwa katika mapigano ya masafa marefu juu ya Afghanistan, Iraqi, Libya na pengine juu ya Iran.

Wakati wa misheni hii, marubani huvaa nepi kama kawaida, wakipata faraja na uhuru unaohitajika wa kusimama, kutembea na kufikia maliwato kwa wakati unaohitajika.
1751073772257.jpg
 
Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia Boeing 787 Dreamliner ET640 iliyokuwa ikielekea Mumbai kutoka Addis Ababa, ilitua kwa dharura mapema Ijumaa asubuhi kutokana na kabini kushuka shinikizo la hewa.

Abiria Saba walipata mfadhaiko wa kiafya na kusababisha kutua kwa dharura mjini Mumbai. Wanane walipata matibabu ya haraka na mmoja alilazwa hospitalini.

Tukio hilo lilitokea umbali wa futi 33,000 juu ya Bahari ya Arabia, njiani kutoka Addis Ababa kuelekea Mumbai, wakati abiria saba walihitaji msaada wa matibabu walipotua, mmoja wao kulazwa.

Kwa kawaida, kabini ya ndege huongezwa shinikizo na hewa iliyotibiwa na oksijeni (Oxygenated Cabin Pressurization) ili kukidhi miinuko ya juu ambapo viwango vya oksijeni ni kidogo.

Tukio la Ethiopian Airlines linaashiria hitilafu isiyo ya kawaida ya mifumo hii, na kusababisha kushuka kwa shinikizo la kabini na pengine kuzua hofu miongoni mwa walio ndani.
1751109859481.jpg
 
Ndege nyingi (hasa kubwa) inapoinuka kutoka kwenye njia ya kurukia, magurudumu yake bado yanazunguka kwa kasi inayoweza kufikia mzunguko wa 2,000 kwa dakika (rpm).

Ikiwa mzunguko huu hautadhibitiwa, mzunguko huu unaweza kusababisha uharibifu wakati magurudumu yanarudi kwenye chumba chake (Landing Gear Bay).

Ili kuzuia hili, ndege za kisasa zina mifumo ya breki ya kiotomatiki ambayo huwashwa mara baada ya kupaa.

Mifumo hii ya udhibiti wa breki usimamisha mzunguko wa gurudumu kabla ya kuingia ndani ambayo wakati mwingine husababisha mtetemo mfupi au kelele kidogo ambayo mara nyingine abiria wanaweza kuhisi.

#Mhandisiwetu na
#AlphaMikeTango
1751278130561.jpg
 
Umahiri wa helikopta unaifanya kuwa chombo chenye matumizi mengi katika nyanja mbalimbali, ikiwa ni pamoja na usafiri wa kijeshi na kiraia.

Helikopta ni aina ya ndege yenye uhuru zaidi kwa kuzingatia urukaji wake wa chini chini na uwezo wa kutua katika eneo dogo au eneo lenye changamoto.

Pamoja na hivyo, ndege hiyo haiwezi kutua popote ambapo rubani atachagua kutokana na vikwazo vya kisheria, masuala ya usalama na mambo ya kiutendaji.

Serikali karibu ulimwenguni kote zimeweka kanuni kuhusu mahali ambapo helikopta zinaweza kutua, huku viwanja vya ndege vya umma vilivyoteuliwa na helikopta zikiwa ndiyo maeneo ya kawaida.

Katika hali za dharura, rubani lazima afanye uamuzi makini ili kuhakikisha Helikopta inatua kwa usalama bila hatari kwa mazingira ikiambatana na taarifa kwa mamlaka husika.

Ukiwa unamiliki Helikopta unaweza kutua kwenye sehemu binafsi, tofauti na hivyo inahitaji idhini ya mwenye eneo na mamlaka.

Pia Sheria hutofautiana kwa maeneo yenye vikwazo kama vile maeneo ya kijeshi, na helikopta zinapaswa kuepuka kuruka juu au kutua maeneo hayo.

Vigezo vya mazingira kama vile hali ya hewa na ardhi vinaweza pia kuathiri mahali ambapo rubani anaweza kutua helikopta.

Marubani wenye uzoefu wanaweza kupata urahisi wa kutua katika hali ya hewa yenye misukosuko au kwenye miteremko.

Aina ya helikopta pia ni muhimu, kwani helikopta za kijeshi zinafaa zaidi kwa hali na maeneo yenye changamoto kuliko za kiraia.

© Alpha Mike Tango
1751282063827.jpg
 
Kuzingatia kwa Iran kuhusu J-10C kumeripotiwa kunatokana na kusikitishwa na kuongezeka kwa kucheleweshwa kwa muda mrefu katika jaribio lake la kununua mpiganaji wa uzito wa juu wa kizazi cha 4.5 Su-35 "Flanker-E" ambazo ziliagizwa awali na Misri kisha kufuta mpango huo chini ya shinikizo la Marekani.

Iran inaripotiwa kutathmini upatikanaji wa ndege ya J-10C inayotengenezwaa na China maarufu "Vigorous Dragon" ndege ya kivita yenye uwezo mkubwa ambayo tayari imepewa jina la "Rafale Killer" katika duru za ulinzi za kikanda.

Nia hii inayoongezeka inakuja kufuatia madai yaliyoenea kwamba mpiganaji wa J-10C ya Pakistani, ikiwa na Kombora la anga la PL-15E (Beyond Visual Range), ambapo yalidungua ndege za Dassault Rafale za Jeshi la Anga la India.

Ziara ya hivi majuzi ya Waziri wa Ulinzi wa Iran Aziz Nasirzadeh huko Qingdao, Uchina, kwa mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) - muungano ulioongozwa na Urusi na China - iliambatana na uvumi ulioongezeka juu ya mkakati wa ununuzi huo wa Tehran.
1751282325533.jpg
 
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) kimeshinda Tuzo ya Kiwanja Bora Barani Afrika katika Tuzo za World Travel Awards (WTA) 2025.

Tuzo hizo zilitolewa usiku wa Juni 28, 2025 katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam.

JNIA imewashinda wapinzani wake wakuu wakiwemo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Cape Town (Afrika Kusini), Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Jomo Kenyatta (Kenya), na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha O.R. Tambo (Afrika Kusini), katika kipengele cha "Africa’s Leading Airport 2025"

Tuzo nyingine ni;

Africa’s Leading Balloon Ride Operator – Miracle Experience – Balloon Safaris Tanzania

Africa’s Leading Destination – Tanzania

Africa’s Leading Tourist Board – Tanzania Tourist BoardAfrica’s

Leading Beach Destination – Zanzibar

Africa’s Leading Honeymoon Destination – Kitulo National Park

Africa’s Leading Tourist Attraction – Ngorongoro Conservation Area

Africa’s Leading National Park – Serengeti National Park

Africa’s Leading Big 5 National Park – Serengeti National Park

Africa’s Leading Mountain National Park – Kilimanjaro National Park

Africa’s Leading Cultural National Park – Ruaha National Park

Africa’s Leading Scenic National Park – Nyerere National Park

Africa’s Leading Elephant Paradise National Park – Tarangire National Park

Africa’s Leading Cruise Port – Port of Dar es Salaam

Tanzania’s Leading Tour Operator – Altezza Travel

Africa’s Leading Adventure Tour Operator – Zara Tanzania Adventures

Africa’s Leading Tour Operator – Pollman’s Tours & Safaris

Tuzo hizi hutolewa kila mwaka na World Travel Awards kwa lengo la kutambua taasisi zinazotoa huduma bora na za viwango vya juu katika sekta ya usafiri na utalii duniani, zikiwemo viwanja vya ndege, mashirika ya ndege, hoteli na kampuni nyingine za usafiri.
1751284989811.jpg
 
Katika usiku wa hafla ya Tuzo za World Travel Awards (WTA) 2025, zilitolewa tarehe 28 Juni, 2025 katika hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es Salaam, Shirika la ndege la Kenya (KQ) lilitangazwa kuwa Shirika Bora la Ndege Barani Afrika likiwapiku wagombea wenza wa Tuzo hizo ambao ni Ethiopian Airlines, EgyptAir, RwandAir na South African Airways.

WTA hutangaza ushindi wa Tuzo hizo kutokana na kura zilizopigwa na wadau mbalimbali wa sekta ya usafiri na utalii kutoka maeneo mbalimbali duniani, wakitambua ubora wa huduma, usalama, ratiba na uzoefu katika kipengele husika.
1751285543142.jpg
 
Kampuni ya Uendeshaji wa Maputo ya Hewa Joto ya Miracle Experience Balloon Safaris Tanzania imeshinda Tuzo ya World Travel Awards (WTA) 2025 kama Mwendeshaji Anayeongoza Uendesha Puto Afrika.

Miracle Experience imeshinda Tuzo hiyo katika kipengele cha "Africa’s Leading Balloon Ride Operator" zilizofanyika usiku wa tarehe 28 Juni, katika Hotel ya Johari Rotana - Dar es Salaa
1751285877895.jpg
m.
 
Ndege ya kivita ya Kifalme ya Uingereza F-35B Lightning Il, yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 100, imekwama katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Thiruvananthapuram huko Kerala, India, kwa takriban zaidi ya siku 10 kutokana na hitilafu ya mfumo wa haidroliki.

Ndege hiyo, sehemu ya HMS Prince of Wales Carrier Strike Group, ilitua kwa dharura tarehe 14 Juni 2025, kwa sababu ya mafuta kidogo, hali mbaya ya hewa na hitilafu ya haidroliki.

Ndege hiyo sasa inakabiliwa na ada ya kuegesha ya INR 26,261 ambazo ni sawa na kiasi cha shilingi za kitanzania 810,000/- kwa siku huku mamlaka ya uwanja wa ndege ikikokotoa gharama kulingana na vipimo vyake.

Ndege hiyo imeegeshwa katika eneo la Bay 4 chini ya ulinzi mkali unaotolewa na Kikosi cha Usalama cha Viwanda cha Kati "Central Industrial Security Force" (CISF).

Mafundi wa Jeshi la Wanamaji wa Kifalme wa Uingereza wamejaribu kurekebisha mfumo huo, ambalo ni muhimu kwa uwezo wa ndege hiyo Kuruka kwa Muda Mfupi na Kutua Wima (STOVL), lakini hawakufaulu.

Timu zaidi ya wahandisi kutoka Uingereza na Marekani inatarajiwa kuwasili hivi karibuni kushughulikia suala hilo, lakini ikiwa matengenezo hayatafaulu, huenda ndege hiyo ikahitaji kusafirishwa hadi Uingereza kwa kutumia ndege ya mizigo ya RAF aina ya C-17 Globemaster llI.

Jeshi la Wanamaji la Kifalme la Uingereza lilikataa ofa kutoka kwa Air India ya kuhamisha ndege hiyo kwenye karakana yao kutokana na wasiwasi juu ya kulinda siri yake nyetiteknolojia na 'avionics' ya hali ya juu.
1751414690300.jpg
 
Kijana Sullivan Vande Voort alisherehekea miaka 16 ya siku ya kuzaliwa kwake mnamo 16 Mei 26, 2025, kwa kukamilisha safari za ndege akiwa peke yake (Solo flight) katika aina 13 tofauti za ndege.

Familia ya Sullivan inamiliki Classic Aviation, kampuni ya huduma za usafiri wa anga na shule ya urubani katika Uwanja wa Ndege wa Manispaa ya Pella (KPEA) na Uwanja wa Ndege wa Manispaa ya Oskaloosa (KOOA) huko Iowa - Marekani.

"Rubani lazima awe na umri wa miaka 16 ili kuendesha ndege peke yake na Sullivan alikuwa ameweka lengo la kuruka zaidi ya ndege 10 katika siku yake ya kuzaliwa kutimiza miaka16,"
Alisema Shane Vande Voort, babake Sullivan.

Sullivan alikuwa amepata mafunzo ya saa 210 katika aina 24 za ndege tofauti kabla ya kutimiza umri wa miaka 16.

Sullivan ni rubani wa kizazi cha tatu ambaye alianza kufundishwa ndege akiwa na umri wa miaka 6 alipoweza kufikia usukani na vikanyagio.

Alikuwa amepata mafunzo ya saa 210 katika aina 24 za ndege kabla kufanya safari zake za peke yake, kulingana na Shane.

Ndege alizorusha Sullivan katika kusherekea siku yake ya kuzaliwa ni;

1946 Aeronca Champ,
1946 Piper J-3 Cub,
1940 Meyers OTW,
1947 Cessna 120,
1947 Stinson 108-2,
1992 Van’s RV-6,
1943 Taylorcraft L-2M,
2021 Rans S-21,
1999 American Champion 7GCBC Citabria,
1977 Cessna 172N Skyhawk,
2006 Cirrus SR-20,
2003 Cirrus SR22, pamoja na
1977 Piper PA28-140 Cherokee.

"Ndege nyingi alizorusha zinamilikiwa katika biashara ya familia, baadhi zinamilikiwa na washauri wake, baadhi babu yake, na mbili zilimilikiwa na mjomba wake mkubwa"
Alisema Shane.
1751429161089.jpg
 
CANADA - 02 Julai 2025

Kampuni ya kutengeneza ndege za biashara ya Canada - Bombardier imepata agizo la ndege 50 za Bombardier Challenger na Global-family kutoka kwa mteja wa mara ya kwanza ambaye jina lake halikujulikana.

Bombardier inasema mpango huo una thamani ya dola bilioni 1.7, na uwasilishaji unatarajiwa kuanza mnamo 2027.

Zilizojumuishwa katika mkataba huo ni chaguzi za ndege 70 zaidi ambazo, ikiwa zikitekelezwa, zingeongeza thamani agizo hadi wastani wa dola bilioni 4 pamoja na makubaliano ya huduma yaliyoelezewa kama ya kwanza ya aina yake kati ya Mzalishaji na Mwendeshaji.

"Mteja amechagua kutofichua jina lake hadharani," Bombardier ilisema.

Eric Martel, mtendaji mkuu wa Bombardier, anasema agizo hilo "linaonesha faida ya ushindani ya wa bidhaa na huduma za Bombardier kwa wateja katika matumizi ya ndege, kutoka kwa kuundwa hadi uwasilishaji, kisha katika huduma ya ndani ya ndege ".
1751463639477.jpg
 
Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya UAE (GCAA) imeacha rasmi kutoa huduma za ndege zisizo na rubani za moja kwa moja na kutangaza kwamba maombi yote na michakato inayohusiana lazima sasa ikamilishwe kupitia jukwaa jipya la huduma za ndege zisizo na rubani katika nchi hizo.

Waombaji sasa wanatakiwa kujisajili kama marubani wa ndege zisizo na rubani maarufu 'Drones'

UAE imeweka kati shughuli za ndege zisizo na rubani kupitia jukwaa jipya la drones.gov.ae, linalosimamiwa kwa pamoja na Baraza la Usalama wa Mtandao "Cyber Security na Mamlaka ya usafiri wa anga - GCAA.

Jukwaa hili hurahisisha usajili, masasisho ya anga, na uidhinishaji wa misheni kwa watumiaji wote wa ndege zisizo na rubani.

Kufuatia marufuku ya hapo awali, matumizi ya ndege zisizo na rubani sasa zimeruhusiwa chini ya kanuni kali, huku jukwaa likitoa nyenzo za mafunzo, utiifu na uendeshaji salama.

Mabadiliko haya ya udhibiti yanafuatia juhudi za kitaifa za kusawazisha utendakazi wa ndege zisizo na rubani na kuepuka matumizi mabaya.

Mnamo 2022, UAE ilipiga marufuku matumizi ya ndege zisizo na rubani baada ya ukiukaji kadhaa.

Hata hivyo, mnamo Januari 7, 2025, Wizara ya Mambo ya Ndani iliondoa marufuku hiyo kwa kiasi, ikiruhusu utumiaji wa ndege zisizo na rubani chini ya kanuni kali za usalama na matakwa ya kufuata serikali.
1751478647404.jpg
 
Back
Top Bottom