Alikimbia hadi uwanja wa ndege, moyo wake ukimwenda mbio, lakini alifika dakika 10 akiwa amechelewa.
Ndege yake ilikuwa tayari imeondoka.
Kuchanganyikiwa na hatia kulimuelemea.
Lakini saa chache baadaye, habari ya kuhuzunisha iliibuka, ndege ambayo alikusudiwa kuwa ilianguka kwa bahati mbaya.
Machozi yalijaza macho yake, na kupiga magoti - si kwa huzuni, lakini kutokana na wimbi la shukrani la kuokoa maisha yake.
Katika wakati huo, aligundua kuwa, wakati mwingine, kile unachohisi kama hakipo sawa ndiyo kinakuokoa na janga usilofahamu.
Mwanadada Bhoomi Chauhan kutoka Bharuch aliponea chupuchupu katika ajali mbaya zaidi ya anga nchini India kuwahi kutokea katika miaka ya hivi karibuni, yote hayo kwa sababu ya kuchelewa kwa dakika 10.
Bhoomi alitakiwa kupanda ndege ya Air India 171, ambayo ilianguka baada tu ya kupaa kutoka Ahmedabad siku ya Alhamisi, na kuua watu 241 waliokuwa ndani.
Mtu pekee aliyeokoka kutoka kwenye ndege hiyo ni Muingereza-Mhindi.
Bhoomi alikosa safari ya ndege kwa sababu ya msongamano wa magari.
Katika mazungumzo na ANI, Bhoomi alikumbuka wakati ambao ulibadilisha maisha yake. Alisema,
"Tulifika lango la kuingia kwa dakika kumi nyuma kwa sababu ya foleni ya magari huko Ahmedabad.."
"Niliwasihi, lakini hawakuniruhusu kupanda, wakisema ningechelewesha safari ya ndege zaidi."
Aliongeza, "Niliposikia imeanguka, nilizimia, namshukuru kuwa niko hai. Lakini tukio hilo linatisha sana."
Alisema mwanadada Bhoomi.