Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

1749815843028.jpg
 
A plane crash in Ahmedabad, India, took the lives of at least 290 people.💔 Today, we want to remember some of the victims of the horrific tragedy:
Akeel Nanabawa, Hannaa Vorajee, and their daughter Sara
Fiongal and Jamie Greenlaw-Meek
Dr. Pratik Joshi, his wife, Dr. Kaumi Vyas, and their three children — Miraya Joshi, Pradyut Joshi, and Nakul Joshi
Javed Ali and Mariam Syed
We extend our deepest condolences to their families and loved ones. 🕊️
1749816502086.jpg
 
Hawa ni marubani wawili waliokuwa kwenye chumba cha marubani cha Air India Boeing 787 Dreamliner iliyopata ajali Alhamisi ya jana huko Ahmedabad nchini India.

Nahodha (Captain) Sumeet Sabharwal (kushoto) ni
Rubani mwenye uzoefu na anayeheshimika mwenye zaidi ya saa 8,200 za uzoefu wa kuruka na ndege.

Alijulikana miongoni mwa wafanyakazi wenzake kwa utulivu na taaluma yake angani.
Nahodha huyo alikuwa ametumia miaka mingi kuruka njia za kimataifa na Air India.
Alikuwa kamanda wa ndege wakati wa safari yake ya mwisho.

Afisa wa Kwanza (First Officer au FO), Clive Kunder
Rubani mwenza kijana kutoka Mumbai.
Clive alikuwa amemaliza mafunzo yake hivi majuzi katika Shule ya Paris Air Flight huko Florida na alikuwa amepata saa 1,100 za ujuzi wa kuruka.

Marubani wote wawili walikuwa wakifanya walichopenda kabla ya ajali kutokea.

Maisha yao, kama wengine wengi kwenye ndege hiyo yalikatizwa.

Tupo pamoja kimaombi na familia ndugu, jamaa, marafiki na kila aliyeguswa na ajali hiyo.
FB_IMG_1749832690648.jpg
 
Walitabasamu kwa kujipiga picha kabla ya kuondoka,
Maisha mapya yalikuwa yakiwangoja,
Kisha... Kimya.

Pratik Joshi alikuwa amekaa miaka sita London akijenga mustakabali na kudunduliza kibaba, kila malipo, kila sikukuu aliyokosa kurudi nyumbani, kila fomu iliyojazwa yote ilikuwa kwa jambo moja tu, kumleta mke wake Komi na watoto wao wadogo watatu Uingereza.
Lakini Wiki hii hatimaye alifanikiwa.

Komi alikuwa amejipa likizo kazi yake ya hospitali, akaenda kufungasha Familia yake. Akasema kwaheri.

Mnamo Juni 12, walipanda Air India Flight 171 kutoka Ahmedabad, kuelekea London kupitia Mumbai.

Picha hiyo waliyopiga ilijaa matumaini na unaweza kuona machoni mwao.

Lakini dakika chache tu baada ya kupaa, ndege ilianguka na hakuna aliyenusurika kati yao.
Maisha yao yamepita, Juhudi za miaka Sita zimezima ndani ya sekunde.

Mwenyezi awalaze pema.

Chanzo:
FlightDrama
FB_IMG_1749833276043.jpg
 
Mtandao wa Flight Radar 24 unaonesha ndege ya Air Tanzania, Boeing 787 Dreamliner aka "ROMEO" (5H-TCR) ikiwa Bloemfontein - Afrika Kusini ikitokea Mwanza - Tanzania.
1749842209993.jpg
 
Pichani (Juu) ni muonekano wa ujenzi wa jengo la Mnara wa Waongozaji Ndege (Air Traffic Control Tower) katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Msalato kilichopo Dodoma.

Picha mbili za chini ni Njia ya kuruka na kutuanndege (Runway) pamoja na Jengo la Abiria (Terminal Building)
1749957356820.jpg
 
Mwanadada, Aya Gertrude Konan, amekuwa Rubani wa kwanza wa kike kurusha ndege za kibiashara nchini Ivory Coast.
Kwa sasa yeye ni Afisa wa Kwanza katika shirika la ndege la Air Côte D'Ivoire, akirusha Airbus A320.

Alianza kazi yake katika tasnia ya anga kama Mhudumu wa Ndege mnamo Aprili 2013, nafasi ambayo alishikilia hadi Oktoba 2015.

Katika robo ya mwisho ya 2014, shirika la ndege la Air Côte D'Ivoire ilizindua shindano kwa lengo la kuwaajiri na kuwafunza vijana wa Ivory Coast katika taaluma za angani (marubani na umekanika wa ndege).

Aya hakuacha fursa hiyo hivyo aliomba.
Mwishoni mwa mchakato, watu 15 walichaguliwa kati ya watahiniwa takriban 1500 na Aya Gertrude Konan alikuwa mwanamke pekee kati yao.

Mwishoni mwa mafunzo yalioyodumu miaka 2 na miezi 4, (kuanzia Oktoba 2015 hadi Februari 2017) alikua Rubani wa Kibiashara wa kwanza aliyefunzwa kutoka nchini Côte D'Ivoire.
FB_IMG_1749963713259.jpg
 
"Mchelewa Aliyeokolewa"
Baraka iliyojificha. ❤️🙏

Alikimbilia uwanja wa ndege, moyo wake ukidunda kwa kasi, lakini alichelewa kwa dakika 20. Ndege yake ilikuwa tayari imeondoka. Alijawa na hasira na majuto — aliendelea kukumbuka kila tukio lililomchelewesha.

Lakini saa chache baadaye, habari za kusikitisha zilifika: ndege aliyopaswa kupanda ilikuwa imeanguka kwa ajali mbaya.

Macho yake yalijaa machozi, na magoti yake yakalegea — si kwa huzuni, bali kwa wimbi la shukrani lililompitia.

Katika wakati huo, alitambua: wakati mwingine, kile kinachoonekana kama maisha kuharibika ni maisha kuokolewa.

Hakika, huyu ni mwanamke mwenye bahati zaidi duniani. ❤️🙏
FB_IMG_1749963858567.jpg
 
Mnamo tarehe 02 Juni, 2025,
Ndege ya Shirika la American Airlines namba AA780 kutoka Philadelphia - Marekani kuelekea Naples - Italy ilibadilisha njia katikati ya safari baada ya kugundua kuwa ndege hiyo aina ya Boeing 787-9 Dreamliner haikuwa imeidhinishwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Naples.

Safari hiyo, ambayo kwa kawaida inaendeshwa na Boeing 787-8, ilibadilishiwa ndege na kuendeshwa na Boeing 787-9 kubwa zaidi kwa sababu za kiutendaji.

Marubani walibadilisha njia na kuelekeza Uwanja wa Ndege wa Rome Fiumicino (FCO), takriban maili 124 kutoka mahali ilipokusudiwa kutua.

Toleo la Boeing 787-9 iliyotumika siku hiyo haikuidhinishwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Naples.

Tofauti kuu kati ya B787-8 na B787-9 huenda zilisababisha kizuizi hiko kwani 787-9 ni ndefu kidogo, ina uzito wa juu zaidi wa kupaa na ina sifa tofauti za utendaji kazi.
FB_IMG_1749964502773.jpg
 
Jaji wa Uingereza ameamuru makampuni ya bima lazima yawafidie wakodishaji wa ndege kulipwa ndege 147 pamoja na injini zilizokwama nchini Urusi baada ya serikali ya Putin kuzuia kurudi.

Uamuzi huo ulitolewa katika Mahakama Kuu ya London mnamo Juni 11.

Jaji Christopher Butcher aligundua kwamba ndege hizo "zilibinafsishwa" wakati Moscow ilipolipiza vikwazo vya marufuku ya usafirishaji bidhaa mnamo Machi 2022, wiki kadhaa baada ya kuivamia Ukrainia.

Korti ilisema ndege hizo hazikuwa katika uharibifu wa kivita bali uzuiaji serikali, hivyo ina kampuni za bima zinadaiwa.

Rasilimali hizo zilizozuiliwa na Urusi zimeenea katika mashirika ya ndege kama vile Aeroflot, S7, na Ural Airlines zikijumuisha ndege za kisasa kama vile Airbus A321neo na Boeing 737 MAX 8.

Nyingi hazikurejea nyumbani tangu vikwazo kuanza, hivyo ndege chache tu zilizosafirishwa kigendo kwa wakati.

Kwa miezi kadhaa, watoa huduma za bima walibishana ikiwa hasara hiyo ilitokana na siasa au maamuzi ya kibiashara.

Wakodishaji wa ndege hizo walisubiri zaidi ya miaka miwili kupata majibu, kukiwa na hasara zaidi ya dola bilioni 4.5.

"Bima Lazima Walipe ndege 147 Zilizokamatwa na Urusi.."
Sheria iliyotolewa na Jaji wa Uingereza.
1749977196161.jpg
 
Ndege ya shirika la Emirates kutoka Dubai ilitua Iran huku Israel ikianza mashambulizi ya anga.

Ndege ya Emirates yenye mruko #EK977 kutoka Dubai ilitua Tehran Ijumaa, Juni 13 2025 saa 03:48 IRST (saa za ndani), iliyoratibiwa saa 03:00.

Ndege hiyo aina ya Boeing 777-300ER (yenye usajili A6-EGE) ilitua njia namba 29 huku milipuko ikiripotiwa kote Tehran wakati Israel ilipoanzisha Operesheni Rising Lion.

Mamlaka ya usafiri wa anga ya Iran ilitangaza kwamba anga ya nchi hiyo imefungwa "hadi taarifa zaidi," vyombo vya habari vya serikali viliripoti.

"Hakuna safari za ndege zitakazoendeshwa katika viwanja vya ndege vyovyote nchini ili kulinda usalama wa abiria hadi ilani nyingine,"
shirika rasmi la habari la IRNA lilisema.

Ndege ya kurudi EK978 ilighairiwa. Ilitakiwa kuondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Imam Khomeini saa 04:35 (saa
1749977291631.jpg
za ndani).
 
Alikimbia hadi uwanja wa ndege, moyo wake ukimwenda mbio, lakini alifika dakika 10 akiwa amechelewa.

Ndege yake ilikuwa tayari imeondoka.
Kuchanganyikiwa na hatia kulimuelemea.

Lakini saa chache baadaye, habari ya kuhuzunisha iliibuka, ndege ambayo alikusudiwa kuwa ilianguka kwa bahati mbaya.

Machozi yalijaza macho yake, na kupiga magoti - si kwa huzuni, lakini kutokana na wimbi la shukrani la kuokoa maisha yake.

Katika wakati huo, aligundua kuwa, wakati mwingine, kile unachohisi kama hakipo sawa ndiyo kinakuokoa na janga usilofahamu.

Mwanadada Bhoomi Chauhan kutoka Bharuch aliponea chupuchupu katika ajali mbaya zaidi ya anga nchini India kuwahi kutokea katika miaka ya hivi karibuni, yote hayo kwa sababu ya kuchelewa kwa dakika 10.

Bhoomi alitakiwa kupanda ndege ya Air India 171, ambayo ilianguka baada tu ya kupaa kutoka Ahmedabad siku ya Alhamisi, na kuua watu 241 waliokuwa ndani.

Mtu pekee aliyeokoka kutoka kwenye ndege hiyo ni Muingereza-Mhindi.

Bhoomi alikosa safari ya ndege kwa sababu ya msongamano wa magari.

Katika mazungumzo na ANI, Bhoomi alikumbuka wakati ambao ulibadilisha maisha yake. Alisema,

"Tulifika lango la kuingia kwa dakika kumi nyuma kwa sababu ya foleni ya magari huko Ahmedabad.."
"Niliwasihi, lakini hawakuniruhusu kupanda, wakisema ningechelewesha safari ya ndege zaidi."

Aliongeza, "Niliposikia imeanguka, nilizimia, namshukuru kuwa niko hai. Lakini tukio hilo linatisha sana."

1749977436099.jpg
Alisema mwanadada Bhoomi.
 
Ndege aina ya Bombardier DASH-8 Q 400 inayoendeshwa na kampuni ya Air Tanzania imetua kwa mara ya kwanza katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Msalato jijini Dodoma leo tarehe 13 Juni 2025.

Ndege hiyo imetua kwenye kiwanja hicho kwa majaribio kikiwa katika hatua za Mwisho kukamilika.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo amesema kuwa hii ni hatua kubwa na TAA ipo tayari kutoa huduma za uendeshaji mara baada ya kukamilika kwa miundombinu miezi michache baadae.
1749977997277.jpg
 
Mamlaka za usafiri wa anga za nchini India na Japani zimeamuru ukaguzi wa ndege ya Boeing 787 Dreamliner kufuatia ajali ya ndege ya Air India siku ya Alhamisi, huku maafisa wa uchukuzi wa Marekani wakisema hawakuona sababu ya kusimamisha ndege hiyo.

Kulingana na gazeti la The Times of India, Kurugenzi Kuu ya Usafiri wa Anga ya India inahitaji ukaguzi wa ndege zote za 787-8 na 787-9 zinazoendeshwa na Air India. Air Kwa sasa Shirika la ndege la India linaendesha jumla ya Dreamliner 33.

DGCA iliiambia Air India kuangalia idadi ya mifumo ya ndege, ikiwa ni pamoja na hydraulics, compressor hewa ya cabin, na kitengo cha kudhibiti injini cha kielektroniki.

Japan pia imechukua hatua sawa. Mainichi Shimbun iliripoti Ijumaa kwamba Wizara ya Ardhi, Miundombinu, Uchukuzi, na Utalii ya nchi hiyo imeagiza Shirika la Ndege la All Nippon, Shirika la Ndege la Japan, na mtoa huduma wa bei ya chini Zipair Tokyo kuangalia injini na fremu za ndege zao za 787, ingawa ndege hizo hazijasimamishwa, wizara ilifafanua.

Maafisa wa uchukuzi wa Marekani hawajadokeza kwamba wataagiza ukaguzi mpya wa ndege 787.

Alipoulizwa na mwandishi wa habari ikiwa alikuwa na wasiwasi wowote kuhusu usalama wa ndege hiyo au anadhani inapaswa kuzuiwa, kaimu msimamizi wa FAA Chris Rocheleau alisema ilikuwa mapema mno kufanya uamuzi huo.
1749978930669.jpg
 
Familia ya Mzee Shirima imefanya Misa ya kumuombea marehemu Michael Ngaleku Shirima, amabaye ni mwanzilishi wa kampuni ya Precision Air.

Misa hiyo iliyofanyika jana Rombo - Tarakea mkoani Kilimanjaro iliudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Rombo Mhe. Raymond Steven Mwangwala, Mkurugenzi
Mkuu wa kampuni ya Precision Air, Bw. Patrick Mwanri, wafanyakazi wa kampuni hiyo pamoja na wananchi na wakazi wa Rombo.

Michael Ngaleku Shirima alifariki dunia mnamo 09 Juni 2023 katika Hospitali ya Aga Khan iliyopo Dar es salaam.

Mzee Shirima anatajwa kwa sifa ya kuishi maisha ya kawaida licha ya kuwa na rasilimali nyingi ikiwemo kampuni ya Precision Air.
1749979570576.jpg
 
GUAM - MAREKANI 12 JUNI

Aliyekuwa Rais na Mkurugenzi Mtendaji Hansen Helicopters Bw. John D. Walker mwenye umri wa miaka 60, amehukumiwa kwenda jela miaka 33 na miezi 09 siku ya Jumanne jioni baada ya kutiwa hatiani kwa makosa 110 ya uhalifu, ikiwa ni pamoja na kula njama, ulaghai, utakatishaji pesa, rushwa na udanganyifu wa kumbukumbu za ndege.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Wilaya ya Guam Frances Tydingco-Gatewood alitoa hukumu hiyo baada ya siku tatu za kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Walker amekuwa kizuizini tangu Septemba 2022 na alipatikana na hatia ya kuandaa mpango unaohusisha helikopta zilizoharibika, nyaraka bandi, uendeshaji usio salama wa ndege, kuajiri marubani wasio na leseni na mafundi ndege kitu ambacho klisababisha majeraha na vifo.

Mahakama pia ilimtoza faini ya dola $250,000 na kutaifisha Mali zake.
1749981947474.jpg
 
ZANZIBAR - 12 JUNI 2025

Zanzibar iko kwenye majadiliano na wawekezaji ili kuanzisha shirika la ndege la kitaifa.
Hatua hiyo ya kimkakati inalenga kuimarisha uunganishaji wa visiwa hivyo na uwezekano wa kuendelea kukuza utalii.

Taarifa inasema, Serikali iko kwenye mazungumzo na shirika la EgyptAir na imefikia makubaliano ya awali ya kuchunguza uwezekano wa kuzindua shirika hilo.

Katika kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar
wa Wawakilishi uliofanyika Chukwani, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano, na Uchukuzi Bw. Nadir Abdulatif Yussuf alitangaza maendeleo hayo siku ya Jumatatu.

Mbunge wa Mtambwe Dkt. Mohamed Ali Suleiman alitoa wasiwasi wake kuhusu ucheleweshwaji wa huduma za anga kisiwani Pemba na kueleza kuwa kwa muda mrefu wakaazi wamekuwa wakiomba safari za mara kwa mara kutoka Air Tanzania.

Hata hivyo, Shirika la ndege la Air Tanzania linatazamiwa kuzindua safari zilizopangwa kuelekea Pemba kuanzia Julai 2025, kama sehemu ya juhudi za kuimarisha usafiri kati ya visiwa.

Mpango huo unakuja huku kukiwa na ongezeko la mahitaji ya kuboreshwa kwa muunganisho wa safari za anga katika visiwa hivyo na juhudi zinazoendelea za kuimarisha mazingira ya utalii na uwekezaji
1749982317392.jpg
katika kanda.
 
Back
Top Bottom