Tofauti yangu na yako ni kuwa mimi naandika uhalisia wewe unaandika mtazamo.
Ngoja nikuzindue kwa jambo moja ili nikuonyeshe ya kuwa kumjua mwanamke unaweza kumjua hata chini ya dakika tano na ukamuoa (Hivi ndivyo huwa tunafanya sisi na wake zetu tunamshukuru Mola tuko mpaka muda huu) zaidi, kisha nikwambie ya kuwa kwa kawaida mwanamke huolewa kwa moja ya sifa nne, ila katika sifa hizo nne ni moja ambayo ndiyo msingi na haipo katika sifa hizo ambayo ni tabia njema, napa ndipo tunaizungumzia hii tabia njema.
Mathalani mimi nikitaka kuongeza mke mwingine situmii nguvu, na wasiliana au kuwatafuta wanaume wanao mjua, siyo kila mwanaume anaye mjua bali wake ambao wanasifika kwa sifa ya ukweli na uchamungu. Hatutumi mashushu sababu kinachotakiwa si utafiti wa jambo kubwa bali kupata majibu ya kuwa binti ana faa au la!