Mabinti ambao hamjaingia kwenye ndoa

Mabinti ambao hamjaingia kwenye ndoa

Pesa kiasi gani inayotakiwa ili uwe na ndoa nzuri?

Jeff bozzes ni bilionea namba moja lakini pesa zake hazikuweza kumsaidia kuinusuru ndoa yake iwe nzuri....so what's your recommendation here?
Hujaelewa kitu. Jeff kawekeza kwenye dollars. Mwenzi wake namba moja ni makampuni yake, siyo mkewe. Nazungumzia kutafuta pesa za kutumia kimkakati. Baadhi ya matajiri wameruhusu utajiri uingie ndani na akili zitoke nje. Pesa should serve your ndoa, na siyo anything the other way round.
 
Pesa kiasi gani inayotakiwa ili uwe na ndoa nzuri?

Jeff bozzes ni bilionea namba moja lakini pesa zake hazikuweza kumsaidia kuinusuru ndoa yake iwe nzuri....so what's your recommendation here?

Jamaa amejibu hii hoja au kalala mbele
 
Wapo wanaume wenye mapesa mengi lakini ndoa bado zimekua ngumu. Pesa ni muhimu ili maisha yaende lakini kupata mke sahihi ni muhimu zaidi
Ukiwa na pesa, na kama haujaoa, una-attract kila aina ya mdada wanapambana wawe nawe. Halafu warembo ni kibao wanakuja, ila unakuta wote sio majembe na unaona akiwa mke kama ukiondoka hatamudu kusiamamia mali. Hapo ndio kazi sababu ni ngumu kuacha mrembo anayekutaka, na kuoa wa kawaida tu. Kila mtu anataka kitu kizuri na kirembo. Afadhali mtu uoe kabla ya kupata pesa sana. Upambane na huyo mkeo mjijenge pamoja. Ila sasa tena asilimia kubwa wadada hawataki mtu asiye na pesa. Yani ni double edge sword hapo. Manake panga la kukata pande mbili. Ndoa ni changamoto tu sana siku hizi. Uwe na pesa au usiwe nayo. Kupata mtu sahihi imekuwa ngumu sana
 
Ukiwa na pesa, na kama haujaoa, una-attract kila aina ya mdada wanapambana wawe nawe. Halafu warembo ni kibao wanakuja, ila unakuta wote sio majembe na unaona akiwa mke kama ukiondoka hatamudu kusiamamia mali. Hapo ndio kazi sababu ni ngumu kuacha mrembo anayekutaka, na kuoa wa kawaida tu. Kila mtu anataka kitu kizuri na kirembo. Afadhali mtu uoe kabla ya kupata pesa sana. Upambane na huyo mkeo mjijenge pamoja. Ila sasa tena asilimia kubwa wadada hawataki mtu asiye na pesa. Yani ni double edge sword hapo. Manake panga la kukata pande mbili. Ndoa ni changamoto tu sana siku hizi. Uwe na pesa au usiwe nayo. Kupata mtu sahihi imekuwa ngumu sana
Pole sana, kama bado hujao badilisha strategies za kutafuta mke.... wasije kujipanga na wewe wakakupanga, ukapangika halafu ukaingia cha kike
 
Siku hizi ili uwe na ndoa yenye furaha itakuhitaji utumie muda na nguvu nyingi kitu ambacho ni ngumu sana ku-maintain kulingana na circumstances ya kiutafutaji
Scars ukiona unafanya wajibu wako na bado unatumia nguvu nyingi kuipata furaha kwenye ndoa huyo sio saizi yako.... kama angekua kiatu tungesema ni either anakupwaya au anakubana hadi huwezi kutembea.
Kama ni girlfriend tafuta mwingine, kama ni mke mwombe Mungu tuu yeye ndio anaweza ifanya nature ichukue mkondo wake
 
Pole sana, kama bado hujao badilisha strategies za kutafuta mke.... wasije kujipanga na wewe wakakupanga, ukapangika halafu ukaingia cha kike
Binafsi nafikiri hakuna strategy yenye guarantee. Wengine wanasema uombe sana (biblia yenyewe inasema maombi bila kazi ni sifuri), maombi pekee hayatoshi. Na wengi walipata wake kwa maombi ndoa zikavurugika tena za kanisani.

Ni kupata tu mtu mwenye ambitions na mchapa kazi kama ww. Na huyo ndio shida kumpata. Wengi tunapenda warembo, ila sababu wanasifiwa na wengi wanajionaga sana, na sio wachapa kazi na hawana ambitions.

Ukiwa na pesa unakuta wadada wanakuja wanafuata pesa na maisha mazuri. Hawafikirii kuendeleza mali, biashara nk. Ila kuna strategy moja nimeigundua recently, naamini hio ni lazima itoboe sababu hio sijaijaribisha bado. Nitaifanyia kazi hopefully soon.

Ps: suala la ndoa lina zero chance for errors. Manake usifanye makosa hapo. Kwa hio kuliko kuoa matatizo, afadhali utulie tu zako kwanza. Nyumba iliyokosewa inarekebishika, ndoa mbaya ndio zimewaua wakina bilionea msuya na wengineo
 
Binafsi nafikiri hakuna strategy yenye guarantee. Wengine wanasema uombe sana (biblia yenyewe inasema maombi bila kazi ni sifuri), maombi pekee hayatoshi. Na wengi walipata wake kwa maombi ndoa zikavurugika tena za kanisani.

Ni kupata tu mtu mwenye ambitions na mchapa kazi kama ww. Na huyo ndio shida kumpata. Wengi tunapenda warembo, ila sababu wanasifiwa na wengi wanajionaga sana, na sio wachapa kazi na hawana ambitions.

Ukiwa na pesa unakuta wadada wanakuja wanafuata pesa na maisha mazuri. Hawafikirii kuendeleza mali, biashara nk. Ila kuna strategy moja nimeigundua recently, naamini hio ni lazima itoboe sababu hio sijaijaribisha bado. Nitaifanyia kazi hopefully soon.

Ps: suala la ndoa lina zero chance for errors. Manake usifanye makosa hapo. Kwa hio kuliko kuoa matatizo, afadhali utulie tu zako kwanza. Nyumba iliyokosewa inarekebishika, ndoa mbaya ndio zimewaua wakina bilionea msuya na wengineo
Hongera kwa kuwa na strategy mpya ila yote ya yote tafuta pesa na mali kwaajili ya future yako na familia yako ila kamwe usitumie pesa zako kumshawishi au kumpata mwanamke wa kufunga nae ndoa
 
Vijana wakitaka mke waulize wanaume wanaonzunguka, mabinti wakitaka mme pia waangalie wanaume wanaomzunguka... inaonekana wanaume tu ndo wajuvi wa yote!
Swadakta sisi ndiyo wajuzi wa haya mambo.
 
Hongera kwa kuwa na strategy mpya ila yote ya yote tafuta pesa na mali kwaajili ya future yako na familia yako ila kamwe usitumie pesa zako kumshawishi au kumpata mwanamke wa kufunga nae ndoa
Wala situmii hela yangu kumshawishi mtu. Inaonekana tu automatically sababu ya biashara, zangu, majengo, magari nk. Nina uwezo mzuri kifedha, na inafahamika sijaoa, kwa hio automatically inajulikana na wanajileta tu ili wawe mother house, mke wa boss, wapate financial freedom nk.

Strategy niliyoongelea sio hii, ila hii ni nyingine na niliifikiria kwanza. Nikasema niende sehemu nisiyofahamika kabisa, ndio nitafute mtu hapo. Ila kazi za kibiashara na safari zangu hiyo strategy hainiruhusu sababu itabidi nikae hapo hata kwa mwaka au zaidi undercover. My business operations might suffer. Ila yes, kuna strategy nyingine, i will try it as soon as possible to do so.
 
Watu wanaishi kwa ku fake na hata uwe na intelijensia ya mossad ila kwa mwanamke huwezi kupata info zote
Ninacho kiandika ndiyo naishi nacho, na hakuna jambo rahisi kama kupata ukweli wa mja katika uso wa ardhi hii, hasa mtoto wa kike.

Lakini si lazima upate taarifa zote ili umjue mwanamke, bali kuna mambo ya msingi ambayo hutosheleza mengine.
Kitaa Watu walifanya investigation wakaridhia mpaka kutoa mahali baada ya pande zote mbili kuridhika na tafiti zao wakakubaliana waoane kumbe mtoto wa kike ana ngoma yakuzaliwa nayo na wazazi waliweka siri
Ninapo sema au nilipo andika ukitaka mke basi waulize wanaume wanao mjua huyo binti, mjue kabisa walio pewa kazi ya kufanya utafiti si mahiri na hawakujua kipi cha kufanya, sababu kuhusu suala la maradhi watu hupimana siku hizi, tena hili hasa husimamiwa na pande zote mbili.

Nilichokiandika bado ni sahihi, sabababu ndiyo ukweli wenyewe, labda kama huwajui wanaume ninao wakusudia hapa.

Nipo.....
 
Sasa unategemea angekuwa bora bila kuwa na vigezo hivyo??? Nashauri tena wazidi kuvipandisha juu hadi mbinguni ili vicholechole vishindwe kuvifikia, au vikipanda vinakutana na Malaika Gabrieli angani, mpaka waokoke ndipo mengine yaendeleee.
Stupidity
 
Kwakifupi usipokuwa na uwezo kiuchumi mwanaume mwenzangu sahau ndoa bora.Sahau.
 
Sasa kama huna pesa endelea kuzitafuta. Mwanaume ndio kichwa kiongozi na mlinzi wa familia yake.
Kuwa mume ni jukumu kubwa sana, muombe pia Mungu akupe mke atayekusaidia kwa maombi na kukusaidia kupata amani ya moyo

Uko sahihi sana Mama D, ukiwa huna hela mambo mengi utayaona kama unabebeshwa wewe tu as if kuna ntu unataka naye awe anahudumia.!
Wanaume tutafuteni pesa, Pesa ndio heshima yenyewe, ukiikosa pesa utadharauliwa hadi utajutia kwanini ulifanya maamuzi hayo.!
TUTAFUTENI PESA!
 
Uko sahihi sana Mama D, ukiwa huna hela mambo mengi utayaona kama unabebeshwa wewe tu as if kuna ntu unataka naye awe anahudumia.!
Wanaume tutafuteni pesa, Pesa ndio heshima yenyewe, ukiikosa pesa utadharauliwa hadi utajutia kwanini ulifanya maamuzi hayo.!
TUTAFUTENI PESA!
Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia mwanamke, “Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa, kwa uchungu utazaa watoto. Hata hivyo utakuwa na hamu na mumeo, naye atakutawala.”

Kisha akamwambia huyo mwanamume, “Kwa kuwa wewe umemsikiliza mkeo, ukala matunda ya mti ambayo nilikuamuru usile; kwa hiyo, kwa kosa lako ardhi imelaaniwa. Kwa jasho utajipatia humo riziki yako, siku zote za maisha yako. Ardhi itakuzalia michongoma na magugu, nawe itakubidi kula majani ya shambani. Kwa jasho lako utajipatia chakula mpaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa;
 
Ni kweli, ndoa nzuri ni foundation ya jamii iliyostaarabika. Vijana waingie kwenye ndoa ili kujenga familia bora na jamii nzuri.

Ila sasa....
Ndoa nazo zaweza kuwa chanzo cha jamii mbovu, hasa kama wawili hao hawataishi katika misingi yake, watatengeneza jamii mbovu kabisa.
 
Hujaelewa kitu. Jeff kawekeza kwenye dollars. Mwenzi wake namba moja ni makampuni yake, siyo mkewe. Nazungumzia kutafuta pesa za kutumia kimkakati. Baadhi ya matajiri wameruhusu utajiri uingie ndani na akili zitoke nje. Pesa should serve your ndoa, na siyo anything the other way round.
so hapa mkuu unapingana na kauli yako ya mwanzo kuonesha pesa haina mchango wowote kuifanya ndoa yako iwe nzuri?

ili pesa itumike kimkakati inatakiwa itumikaje?

kiasi gani cha pesa kinacho hitajika ku serve ndoa?

ndoa ambayo inahitaji fungu la pesa ili iendelee ku-survive haina upendo. so vile viapo vya kuishi katika hali zote za shida na raha wakati wa harusi ni uzushi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom