Mabilioni ya MCC: Tanzania 'kitanzini' March 28

Mabilioni ya MCC: Tanzania 'kitanzini' March 28

Jumatatu ya pasaka ya tarehe 28 mwezi huu,mkutano wa Bodi ya Wakurugenzi wa Millenium Challenge Corporation almaarufu kama MCC inakutana kuijadili Tanzania. Tanzania itajadiliwa kama ipewe au isipewe mabilioni ya MCC.

Nyaraka za shirika hilo zinaonesha kuwa Tanzania ilipewa masharti mawili ili iyapate mabilioni hayo. Kwanza,Tanzania ilitakiwa kupambana na rushwa pamoja na ufisadi. Pili,Tanzania ilitakiwa kuumaliza mgogoro wa kikatiba na kisiasa wa Zanzibar.

Tanzania itapata mabilioni ya MCC? Imetimiza masharti?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Pemba,Zanzibar)

Pesa zetu ya makusanya zatosha kabisa ndio maana Magufuli hajatoka kwenda kutembeza bakuli.
 
Tanzania ya Magufuli itakuwa Donor country badala ya kuwa ombaomba. Watupe wasitupe we dont care
kumbe na wewe ndugu unakubali kabisa kwamba Awamu iliyopita ilikuwa "OMBA" "OMBA" !!! Haaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Kweli kabisa hamna shida maana Magufuli kakusanya mapesa mengi na hivi sasa hakuna mwanafunzi anayekaa chini.. Hospitali zote zimejaa madawa na vifaa tiba hata wazazi wako si mafukara tena.
Hata bibi yako pale anakiti cha kuzunguka,ndo unataka tufikie hatua hiyo.
 
lakini hayo masharti ni kwa manufaa yetu wenyewe!! wanasema tupambane na ufisadi je hii ni kwa manufaa ya nani? wanasema wamalize mgogoro wa zanzibar je hii ni kwa manufaa ya nani?? si yetu?

Kuwa mtumwa ndiyo huko, ufisadi uache kupambana nao wewe mwenyewe ungoje mpaka upewe pipi? Yaani tu mapunguani kiasi hicho?

Mahathir Muhammad wa Malaysia alikataa huo utumwa na akaihakikishia dunia kuwa wao wenyewe wanaweza na wameweza kweli.
 
Ningekuwa na uwezo kubadili mawazo ya hao watoa ela za MCC ningewalazimisha watunyime ela hizo. Tujitegemee kuendesha shughuli zetu za kimaendeleo kwa rasilimali zote. Nadhani Rais wangu anawaza kama mimi kuhusu hili.
================
Nikwambie kitu, wanahaha mahala pa kuzipeleka hizo ela. Hivyo kazeni uzi maamuzi ya mustakabali wa utawala na maendeleo yetu yatoke kwetu, na kamwe yastoke kwao.
 
Tanzania ya Magufuli itakuwa Donor country badala ya kuwa ombaomba. Watupe wasitupe we dont care
Ccm wote wanatakiwa wawe na moyo wa uvumilivu kama wewe maana zile nafasi za kulipana fadhila za uRC umekosa lakin upo ngangari tu.ila vuta subira kuna nafasi za uDC zinakuja huwezi kukosa maana huwa zinatolewa kwa watu wanaotukana viongozi wa upinzani na kufunga wakubwa kamba za viatu.
 
Ccm wote wanatakiwa wawe na moyo wa uvumilivu kama wewe maana zile nafasi za kulipana fadhila za uRC umekosa lakin upo ngangari tu.ila vuta subira kuna nafasi za uDC zinakuja huwezi kukosa maana huwa zinatolewa kwa watu wanaotukana viongozi wa upinzani na kufunga wakubwa kamba za viatu.
Huyo dada nasikia kisomo hana ... Jamvi la wageni.
 
Ningekuwa na uwezo kubadili mawazo ya hao watoa ela za MCC ningewalazimisha watunyime ela hizo. Tujitegemee kuendesha shughuli zetu za kimaendeleo kwa rasilimali zote. Nadhani Rais wangu anawaza kama mimi kuhusu hili.
================
Nikwambie kitu, wanahaha mahala pa kuzipeleka hizo ela. Hivyo kazeni uzi maamuzi ya mustakabali wa utawala na maendeleo yetu yatoke kwetu, na kamwe yastoke kwao.
Mkuu TUJITEGEMEE, hilo ni kweli kabisa.
Hakuna taifa linatoa fedha bure bila kutegemea kitu chochote in return.
 
Mkuu unalala mlango wazi na kutazamia neema itaingia mlangoni!!
MCC ni chombo chenye malengo ya maslahi na matakwa ya Marekani.
JPM amefanya vema kujikita katika kuondoa taswira ya kuonekana kujikomba kutekeleza matakwa yao.
Na pale wabunge wa Marekani walipokuja bila itifaki aliwatolea nje.
Ni vizuri kama nchi tukawa na moyo wa kujiamini na kujua kile tunachotaka na si kudhalilishwa kwa vimisaada vyenye masharti ya kuondoa heshima ya nchi.

Kimsingi mimi sitegemei MCC kama watabadili maslahi ya nchi yao ili tu walete misaada Tanzania.
Hiyo hela isahau!!!
Tanzania ya Magufuli itakuwa Donor country badala ya kuwa ombaomba. Watupe wasitupe we dont care
Mbona kipindi cha JK hamkuyaona haya!! Wakati serikali ina sign Mliweza nini!? Pamoja na mapungufu yake msimdhalilishe JK kwa kusign MCA!!

Inaelekea nyie watu hampendi Magufuli afanikiwe!!
 
Kweli kabisa hamna shida maana Magufuli kakusanya mapesa mengi na hivi sasa hakuna mwanafunzi anayekaa chini.. Hospitali zote zimejaa madawa na vifaa tiba hata wazazi wako si mafukara tena.[/QUOTE
Amekusanaya wapi... Umesikia makusanyo ya march ni sh ngap... Naamini mwez ujao warudi kulekule kwa mzee wa msoga
 
Mbona kipindi cha JK hamkuyaona haya!! Wakati serikali ina sign Mliweza nini!? Pamoja na mapungufu yake msimdhalilishe JK kwa kusign MCA!!

Inaelekea nyie watu hampendi Magufuli afanikiwe!!
Soma majarida yapo kibao.
MCC haikuanza na JK, bali baada tu ya utawala wa Ben Mkapa alyeweka mazingira ya Utawala Bora
Na tatizo lililopo si kupokea fedha za MCC, bali masharti yaliyowekwa sasa, ya Zanzibar, masharti hayo hayakuwepo wakati MCC ina sainiwa.
Be informed!
 
Jumatatu ya pasaka ya tarehe 28 mwezi huu,mkutano wa Bodi ya Wakurugenzi wa Millenium Challenge Corporation almaarufu kama MCC inakutana kuijadili Tanzania. Tanzania itajadiliwa kama ipewe au isipewe mabilioni ya MCC.

Nyaraka za shirika hilo zinaonesha kuwa Tanzania ilipewa masharti mawili ili iyapate mabilioni hayo. Kwanza,Tanzania ilitakiwa kupambana na rushwa pamoja na ufisadi. Pili,Tanzania ilitakiwa kuumaliza mgogoro wa kikatiba na kisiasa wa Zanzibar.

Tanzania itapata mabilioni ya MCC? Imetimiza masharti?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Pemba,Zanzibar)
TUNA WEZA SONGA MBELE HATA BILA YA HIZO PESA ZA MCC NA KAMA TUTAKOSA PESA HIZO KUTOKANA NA MISIMAMO YETU BASI WAKAWAPE NDUGU ZAO AMBAO WENGINE HULALA MITAANI KWA KUKOSA MAHALA PA KUISHI
 
Kweli kabisa hamna shida maana Magufuli kakusanya mapesa mengi na hivi sasa hakuna mwanafunzi anayekaa chini.. Hospitali zote zimejaa madawa na vifaa tiba hata wazazi wako si mafukara tena.

Toka waanze kutupa hizo pesa tumemaliza matatizo yetu yote? Tufanye kazi tujenge nchi...anayekulisha lazima ataku control tu
 
Back
Top Bottom