Siwahi kuona umuhimu wa trafic kuongoza magari sehemu zenye taa zinazofanya kazi vizuri na mara nyingi huwa trafic wanaongeza foleni sehemu zenye mataa. Trafic I natakiwa awepo kuhakikisha kila mtu anafuata utaratibu na sio kuongoza.
Mkuu laptop2016 na figganigga binafsi sioni umuhimu wa askari wa usalama barabarani kuongoza sehemu yeyote ile amabyo taa zinafanya kazi vizuri. Katika nchi zote zilizoendelea hata ufike busy town kama Tokyo, New York, Shanghai, Bombay na Amsterdam huwezi kukuta eti askari anaongoza kama umeme upo na traffic light au taa za barabarani zinafanya kazi, huu ni ulimbukeni ama mazoea ya wawahusika na Road Safety. Wameona wapi huo utaratibu? Mtakuja kuua watu kwa kazi ambayo hamstahili kuifanya.
Mimi na declare interest ni Profesional Registered member wa International logistics & Transport Institute-London UK. Moyo unaniuma sana ninavyoona wana violate roles za transport, kinachofanyika its only happened in Tanzania. Hawa askari wetu wa barabarani wengi unakuta wamesoma cert.za vehicle inspector pale NIT ukikuta waliosoma BACHELOR ama zamani ADVANCED DIPLOMA IN LOGISTICS AND TRANSPORT MANAGEMENT. ADTM, ADLTM, BLTM pale chuo cha Taifa cha usafirishaji, mara nyingi wanakuwa maofsa hivyo ni mara chache na pia hawako entitled na kazi za kuongoza magari. Ama ukiwakuta njiani basi ujue mkubwa anapita au kuna operation maalum ya kukamata magari .wakimaliza wanarudi maofosini kwakuwa ethics za kazi huwezi kumpa officer hiyo role.
Road Transport is a feeder of all other modes of transport. Maritime Transport ambayo ni sea and ocean kwakuwa waterways ina-include lake transport na River transport hizo zote ni water transport na zina-depend on road transport, Air Transport ina-depend on road transport, Rail Transport ina-depend on road transport kupata pax -(abiria) wake.
Transporting goods and service from one place to another or people from one point of destination to where there's a demand for transport is what we call TRANSPORT. That is why transport become a "necessary devil in human life" to cater for a need of economic development, to any developed or developing country like Tanzania. It's where Road Traffic engineers, Logisticians & Transport Officers team up a solution of TRAFFIC LIGHTS MANAGEMENT to an area of road congestion as a result of junction. kwenye msongamano wa magari unaotokana na makutano ya barabara. hili wazo la traffic lights ni la kitaalamu siyo kutumia nguvu kuongoza magari.na ule muda wa traffic light unaotolewa kwa kila gari kwa highway na barabara za kona uko calculated kitaaalamu na body ya professional people kama nilivyo waainisha hapo juu.
Don't tell me hao wataalam ambao wote wako registered na body ya International logistics wengine ni foreigners na wamehusika kurekebisha miji kama Tokyo, New York, New Dell, na china wako wrong unachukua askari aliyekuwa malindo au ametoka ccp pale moshi au ametoka NIT kasoma miezi 3 au 6 Vehicle Inspector unamuweka barabarani unamwambia akaongoze magari, wakati yeye kajifunza ukaguzi wa magari. Mwenye shahada yake huwezi kumgusa labda akiwa anasubiri cheo. ACHENI TAA ZIFANYE KAZI ZIMEPIMWA, ZIMECALCULATIWA KITAAALAM na pia SERIKALI IMEZIGHARAMIA SANA. naomba wahusika zingatieni hilo. jifunzeni kwa nchi za watu. penye taa huoni askari anaongoza, wanakuwepo kuangalia usalama barabarani na wale ambao hawafuati hizo taa.
Kwa mfano pale TAZARA na UBUNGO ni shida tupu mpaka hizo fly over ziishe watu watakuwa hoi. askari pale Tazara anaruhusu magari yanayotoka njia ya bandarini kuelekea buguruni almost one & a half hour. Mpaka asikie gari la msafara wa magereza linawahi kuelekea mjini au yule mzee wa nyota tatu na gari yake ya kijani na escot ndiyo wananchi wakawaida wanaoenda Airport kuwahi Air transport wanaruhusiwa tena pale mara nyingi wasafairi kwa maana ya abiria wa ndege huwa wan-cancel trip na kuingia gharama mara mbili shauri ya foleni. Sasa huoni tuna athiri hata abiria na crew wa zile BOMBADIER zetu? na akisha pita mkubwa utaratibu ni ule ule siyo asubuhi,siyo mchana wala sio jioni utasema wale wamiliki wa malori wametoa maelekezo kwa askari wetu kuna malori yetu yatapita muda Fulani.
Na ukithubutu kupiga honi kama kutaka kumu-alert askari wetu kuwa labda umetusahau sisi upande huu umetuweka sana. Utanyooshewa kidole na hawezi tena kuruhusu upande huo umewaponza wenzako wote mtawekwa zaidi ya two hrs. huku akiendelea kuongea na simu yake ya mkononi.na kama kuna mwenzake pembeni atamuita kati aendelee na kuvuta upande mwingine kwa maelekezo yake. Unakuja kukamatwa, utawekwa pembeni, utanyanganywa leseni, funguo ya gari utaelezewa kusudio la kupelekwa central police traffic na inspection inaanza hapohapo. Na kwa magari yetu haya ya second hand from Dubai na Japan lazima ukutwe na kosa imekula kwako. Kazini huendi utacheleweshwa mpaka utajuta kupiga hiyo honi. Nafasi ya kuonywa hapo haipo ni adhabu kali utapewa na Inabidi uwe mpole usikilize maelekezo
Kama ingekuwa ni traffic lights zingetoa haki kwa kuruhusu magari kwa muda wa kitaalamu uliowekwa. Kama mnadhani kuna umuhimu wa upande Fulani upewe muda mrefu kidogo jamani zipo taa za kisasa zina setting. Matokeo ya kudharau wataalam walioweka taa ndiyo hizo ajali zinazo-onekana pichani na kusababisha ulemavu wa kudumu na upotevu wa roho za watu wasio na hatia. ACHENI TAA ZIFANYE KAZI. Kama resources ni nyingi basi wakae barabarani kuangalia drivers na pedestrians wanao kiuka alama za barabarani. Ni mawazo yangu siyo lazima yafuatwe na wahusika