Naiomba serikali ipokee ushauri wetu kuhusu kuboresha huduma ya mabasi ya mwendokasi

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,592
29,711
Lengo la serikali kuwekeza katika mkundombinu iliyotuletea huduma ya mabasi ya mwendokasi ni kupunguza usumbufu utokanao.na foleni kubwa za magari wakati wa kuingia na kutoka mijini. Hasa nyakati za ahsubuhi na jioni.

Mimi na baadhi ya wadau tunaamini kuwa huduma hii inapaswa kurahisisha movement ya wananchi hususani wanaotingia na kutoka mijini hasa wanaoishi pembezoni mwa miji.

Jiji la Dar es Salaam limegawanyika katika maeneo makubwa matatu.
  1. Maeneo yenye shughuli za biashara, haya maeneo yameunganika na vituo muhimu vya usafiri wa abiria wengi
  2. Maeneo ya ofisi mbalimbali ambayo yapo katikati ya jiji
  3. Maeneo ya makazi ambayo yamesambaa kutola.kati hadi.pembezoni mwa mji
Maeneo hayo yote yanaunganoshwa na vituo.mahususi vya usafiri ws abiria. Vituo hivyo vingi vinahudumia muda mwingi sana kwa sababu ya uhalisia wa shughuli na pilika pilika za jiji.

Kwa mfano kituo cha Mbagala hakijawahi kukauliwa abiria kwa saa 24 muda wote wa mwaka. Hata kibiashara mbalimbali eneo hilo lipo hai muda wote wa saa 24.

VIvyo hivyo maeneo ya Mbezi Luis yaani Mbezi mwisho kunakuwa na polika za ussfiri saa 24 ambapo inapofikia usiku wa saa 5 hivi kituo kinahamia barabara kuu ya Morogoro. Ukizunguka jiji la Dar usiku utagundua kuna maeneo watu hawakauki katika saa 24 za siku. Eneo la Kariakoo hususani makutano ya Uhuru na Msimbazi ni eneo ambalo linakuwa kama mchana muda wote.

Serikali kwa kujali ama kuangalia namna ya kurahisisha usafiri wa katikati ya jiji, ingeweka mkakati wa kuhakikisha huduma ya usafiri wa mwendokasi unapatikana muda wote. Sipendekezi mabasi yote yatumike kusafirisha abiria bali kuweka utaratibu wa basi mbili au tatu ambazo zinaanzia Kimara, kupitia Moroko, Gerezani hadi Kivukoni. Nasema hivyo kwa sababu wakati jiji limelala wapo watu ambao wanatoa huduma muhimu usiku wanapaswa kuwahi ama.kurejea makwao. Manesi, askari, sexual workers, wafanyabiashara na abiria wanaoingia kutoka mikoani usiku wote wanahitaji kufika either destinations zilizopo njia inayopita mwendokasi au katikati ya mji ambapo wanachukua feeders za daladala kutoka nje ya jiji.

Kwa mapenzi mema na kuzingatia lengo la huduma ya mabasi ya UDART, serikali izimgatie kuruhusu mzunguko wa uchumi kufanyika saa 24 na hatimaye tutazoea kufanyakazi kwa shift ili kukuza uchumi wetu.

Je Great Thinkers wenzangu mnalionaje suala hili la kuwepo kwa basi moja au matatu ya Mwendokasi yatakayotoa huduma kuanzia saa 6.00 usiku hadi saa 10.00 alfajiri?
 
Mwendokasi ina shida nyingi sana..

Mabasi kuchelewa. Na unayaona yanapita matupu ...sielewagi kabisa..

Kuruhusu watu hasa watoto Kula ndani ya mwendokasi...unaekutana na watoto wa shule ya msingi wanakula maembe na basi limejaa..
Unachafuliwa unnecessary wakati wangeweka ban ya kila mtu asiingie na chakula cha Aina yeyote kuondoa usumbufu Kwa wengine...

Mziki WA singeli Kwa sauti kubwa ..
Yaani mziki umejaa matusi unapigwa Kwa sauti ..nilishangaa Sana..

Ile sauti ya kutaja vituo kama Imekufa kabisa ..sio wote wenyeji....irudishwe ...

Kusubiri chenji huku basi unaliona lile linaondoka...why wasiweke kadi kama pantoni??


Kero ni nyingi Sana Kwa kweli
 
Mwendokasi ina shida nyingi sana..

Mabasi kuchelewa. Na unayaona yanapita matupu ...sielewagi kabisa..

Kuruhusu watu hasa watoto Kula ndani ya mwendokasi...unaekutana na watoto wa shule ya msingi wanakula maembe na basi limejaa..
Unachafuliwa unnecessary wakati wangeweka ban ya kila mtu asiingie na chakula cha Aina yeyote kuondoa usumbufu Kwa wengine...

Mziki WA singeli Kwa sauti kubwa ..
Yaani mziki umejaa matusi unapigwa Kwa sauti ..nilishangaa Sana..

Ile sauti ya kutaja vituo kama Imekufa kabisa ..sio wote wenyeji....irudishwe ...

Kusubiri chenji huku basi unaliona lile linaondoka...why wasiweke kadi kama pantoni??


Kero ni nyingi Sana Kwa kweli
Upo sahihi
Nadhani tunahitaji kuona tunahudumiwa kwa ufanisi hivyo tusiache kupaza sauti zetu.

Ni kweli unakuta gari inatoka Kimara mwisho likiwa tupu linaelekea Jangwani kupaki. Hapo Kimara limeacha abiria lukuki ambapo lingeweza kuwabeba na kiwasogeza hadi mapipa likawashusha na kumalizia destination yake.

Tukubali kwamba, watendaji serikalini hawana mtazamo chanya katika kuboresha huduma za maeneo au viteno vyao.

UPo sahihi mluu
 
Dawa ni kuweka kampuni zaidi ya moja zishindane...na ticket iwe Kwa card za electronic kila kampuni ioneshe ushindani
Hili ni wazo mujarab.
Lakini kwa utawala usiozingatia sheria na taratibu kama Tanzania, hizo kampuni zitapiga loss.

TUkipata katiba inayowajibisha kwa vitendo, hayo yote yamawezekana
 
Hili ni wazo mujarab.
Lakini kwa utawala usiozingatia sheria na taratibu kama Tanzania, hizo kampuni zitapiga loss.

TUkipata katiba inayowajibisha kwa vitendo, hayo yote yamawezekana

Mwendokasi kuboreshwa nalo lisiburi katiba mpya???

Mmezidi aisee....

Sasa hata soko la Kkoo mtasema kusubiri katiba mpya kusafishwa
 
Mwendokasi kuboreshwa nalo lisiburi katiba mpya???

Mmezidi aisee....

Sasa hata soko la Kkoo mtasema kusubiri katiba mpya kusafishwa
Mkuu wala mimi na wazalendo wenzangu hatupo bias kabisa.

Katika sheria na kanuni za utendaji kazini zikitegemea ukali wa aliyepo juu na siyo uwajibikaji wa kisekta hilo ni tatizo kunwa kimfumo.

Tujiongeze kwa sasa kisha katiba ikija tunakuwa na uhakika
 
Watalam wa IT mnajionaje? mwendokasi wanarudi nyuma kila leo,kivipi?wakati mradi unaanza yale maneno ya basi linaenda wapi yalikuwa digital na kila kituo kinachofuata kinatajwa sasa baada ya kuachiwa tumeanza kubandika vibao vya mbao vimeandikwa kwa mkaa.
 
Back
Top Bottom