Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Hatimaye imesalia siku moja kufikia 24/1/2024 ambayo ni siku ya kihistoria Tanzania. Ni siku ya mageuzi halisi. Yameandaliwa na kuratibiwa na Chadema kupinga miswada ya sheria za uchaguzi kama ilivyokubaliwa kwenye maridhiano.
Hata hivyo tukiweka Kandi lengo la kisiasa tunaomba wananchi hasa wa kipato Cha chini nao tujitokeze kuyaunga mkono maandamano hayo tukiwa na mabango ya ugumu wa maisha na kupanda kwa bei za bidhaa hasa domestics kama vyakula nk.
Hii ni fursa adhimu mno kuieleza Serikali mateso yetu. Uthubutu wetu na wingi wetu utaweza kuleta mageuzi katika maisha ya kila siku.
Tuhamasishane hata Kwa wenzetu wasio na smartphone. Inyeshe mvua au jua tuiambie Dunia kuwa Watanzania wanaishi jehanam katikati ya watu wachache wanaokula keki ya nchi Hadi kuvimbiwa.
Sambaza ujumbe huu walau Kwa watu 100 tu.
Wabeja.
Hata hivyo tukiweka Kandi lengo la kisiasa tunaomba wananchi hasa wa kipato Cha chini nao tujitokeze kuyaunga mkono maandamano hayo tukiwa na mabango ya ugumu wa maisha na kupanda kwa bei za bidhaa hasa domestics kama vyakula nk.
Hii ni fursa adhimu mno kuieleza Serikali mateso yetu. Uthubutu wetu na wingi wetu utaweza kuleta mageuzi katika maisha ya kila siku.
Tuhamasishane hata Kwa wenzetu wasio na smartphone. Inyeshe mvua au jua tuiambie Dunia kuwa Watanzania wanaishi jehanam katikati ya watu wachache wanaokula keki ya nchi Hadi kuvimbiwa.
Sambaza ujumbe huu walau Kwa watu 100 tu.
Wabeja.