Hizi ndizo sababu za kwanini Serikali ya CCM haitaki Maandamano ya CHADEMA

Lidafo

JF-Expert Member
Sep 26, 2019
551
747
Habari wanajamvi!
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikifuatilia siasa za Tanzania na kuna mengi ya kuzungumza japo muda ni mchache ila kwa hili la maandamano ya chadema yanayotarajiwa kufanyika tar 24 mwezi huu wa kwanza nikaona si vibaya na mimi nikatoa mtazamo wangu hasa baada ya nguvu kubwa ambayo serikali inatumia kukwamisha maandamano hayo.
Nianze kwa kusema kuwa CCM kama chama tawala kimepitia siasa za panda shuka tangu kuanzishwa kwake na wanauzoefu wa kutosha juu ya siasa za Tanzania na wanajua ya kuwa hali ya nchi kwa sasa si yamatumaini na raia wengi hawana matumaini na serikali hii ya CCM.

Tokea CHADEMA itangaze kutakuwa na maandamano tuliona reaction ya serikali, Kwanza kabisa Mh. Chalamila mkuu wa mkoa husika ambao maandamano yamepangwa kufanyika yaani Dar es salaam alitangaza kutakuwa na usafi ambao utafanywa na Jeshi La Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na jeshi la polisi lakini pia Mh. Paul Makonda Katibu mwenezi wa CCM huyu nae akasema anataka mdahalo na CHADEMA kwani haoni sabaabu ya Chadema kuandamana hasa kupinga miswaada ya sheria za uchaguzi, Tatu baadhi ya kundli la wanasiasa wa vyama vingine tofauti na CHADEMA wakasema hawaungi mkono maandamano hayo, Nne Baadhi ya wafanyabiashara wa kariakoo wakasema hawataandamana, Tano baadhi ya viongozi wa dini.

Swali la msingi ni Kwanini nguvu kubwa inatumika kuyazuia maandamano hayo? Hali yakuwa ni haki ya kikatiba na ni maandamano ya Amani?

Kwanza ni lazima tujue siasa ni Sayansi yenye sanaa ndani yake na kutokana na hili zifuatazo ndio sababu serikali haitaki CHADEMA waandamane.

1. HOFU JUU YA HASIRA WALIZONAZO WANACHI DHIDI YA SERIKALI.
Tutambue kuwa CHADEMA wanataka kuandamana kupinga miswaada ya sheria za uchaguzi lakini hiki ni kipindi ambacho kundi kubwa la wanachi lina hasira na serikali kwakuwa Umeme unasumbua, Huduma mbaya za maji, Elimu lakini Ufisadi umetamalaki kwa kiwango kikubwa na uwajibikaji na uwajibishwaji umeshuka kwa kiwango kilekile ambacho Ufisadi umepanda.
Hili halihitaji jicho la msomi wa PHD kugundua kila mwenye macho anajionea jinsi mambo yalivyo tafrani, Katika kipindi kama hichi serikali haiwezi kuruhusu maandano kwani huenda yakaanza kama maandamano ya kupinga mswaada wa sheria za uchaguzi mwisho yakamalizika kama maandamano ya kupinga mfumuko wa bei, Umeme ,Ufisadi , Rushwa n.k mambo ambayo yanamgusa kila Mtanzania na kwa kiasi kikubwa litawafungua macho watu wengi kitu ambacho CCM hawataki kukisikia kabisa kwani ujinga wa watanzania wengi ni mtaji wao wa Kisiasa.

2. KUIZUIA CHADEMA KURUDISHA NGUVU WALIYOIPOTEZA KWA JAMII.
CCM hawataki CHADEMA wawe karibu na raia kwa namna yeyote kwani wanajua hapo ndipo nguvu ya CHADEMA ilipo. Hivyo kuruhusu maandamano ni kuwafanya CHADEMA kuwa karibu na wanachi jambo ambalo CCM wameshajifunza katika uchaguzi wa 2010 na 2015 kuwa Wananchi wananguvu kubwa hivyo hawawezi kuruhusu nguvu ile CHADEMA waliokuwa nayo wawe nayo tena.

Kwa sababu hizo ndio maana Serikali ya CCM imeamua kuanza hatua za kiushawishi za kuzuia maandamano hayo na njia watakazotumia ni mbili tu.
Moja, ni kuyazuia kabisa kwa kutumia vyombo vya dola jambo ambalo pia linaweza leta taswira mbaya kimataifa kuwa hakuna demokrasia au Mbili kuyaruhusu ila kwa kuyapunguza nguvu maandamano hayo yaani hapa wanatumia mlango wa nyuma alafu wanatokea palepale kwa aliyetumia mlango wa mbele na hii ndio njia ambayo wameamua kuanza nayo kitendo cha kumtumia chalamila na viongozi wa Kisiasa na wafanyabiashara na jeshi kufanya usafi hii yote ni kudhoofisha nguvu ya maandamano hayo na usishangae siku hiyo ya maandano kama yatakuwepo kukajitokeza watu na mabango ya mama anaupiga mwingi, Hili usishangae likitokea ndio siasa za Tanzania lakini pia vyombo vya habari havitaruhusiwa kurusha habari za maandano hapa zitabaki online TV chache ambazo chadema zina mkono wake na labda JF hapa ambapo wamekuwa wakitoa habari pasi upendeleo.
Endapo hili la njia ya pili litatokea maana yake ni kuwa Serikali itakuwa imewapa CHADEMA maji ya vuguvugu ambayo hayakati kiu yaani wamewaruhusu waandamane lakini maandamano yasiyo na matokeo yaliyo kusudiwa.

Katika kuyaepuka yote haya ili CHADEMA Waweze kufanya maandano yenye matokeo waliyoyakusudia ni lazima wachukue hatua mbadala na wao watumie mlango wa mbele na watokee palepale sawa na aliyetumia mlango wa nyuma.
Swali la msingi ambalo Mh.Freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla wanatakiwa kujiuliza ni nini Kifanyike ili Maandamano waliyokusudia yatimie kwa matokeo makubwa?.. Nitarudi baadae Kwasasa ngoja kwanza nitoke nikatafute mlo wa Mtanzania aneishi chini ya dola moja.

Kabla sija-log off niseme tu kwa yanayoendelea kwa sasa Nchini katika mawanda ya Kisiasa tunapata picha ya kuwa Mama anataka kugombea 2025 na yupo serious na hilo , CCM imepoteza nguvu yake kama chama na tumaini pekee lipo kwa vyombo vya dola na mwisho ni kuwa CHADEMA imepoteza ushawishi wake kwa jamii.
Asanteni.
 
CCM wanaogopa maandamano ya CDM.🤣🤣🤣🤣🤣
Kwasasa raia wamechoka hivyo kikitokea kitu cha ku-trigger hasira za wananchi kama maandamano au mikutano ya kisiasa ya wazi ni tishio kwa uhai wa CCM hasa 2025 ukizingatia CCM yenyewe ina internal conflicts nyingi.
Ndio maana nguvu kubwa inatumika kuzuia maandamano.
 
Kwasasa raia wamechoka hivyo kikitokea kitu cha ku-trigger hasira za wananchi kama maandamano au mikutano ya kisiasa ya wazi ni tishio kwa uhai wa CCM hasa 2025 ukizingatia CCM yenyewe ina internal conflicts nyingi.
Ndio maana nguvu kubwa inatumika kuzuia maandamano.
Hapa kijijini kwetu huwa wanasema waliambiwa na mwenyekiti wa kijiji kwamba CHADEMA imekufa.Sasa wanaogopa maiti?🤣🤣🤣🤣
 
Hapa kijijini kwetu huwa wanasema waliambiwa na mwenyekiti wa kijiji kwamba CHADEMA imekufa.Sasa wanaogopa maiti?🤣🤣🤣🤣
Kama Hayati Magufuli angekuwa hai ni wazi kuwa chadema ingepoteza wafuasi wengi. Lakini kadari ya Mungu ikatangulia,
Kwa kuwa Magufuli alikuwa na wapinzani inactive ndani ya CCM sasa ndio wamejitokeza na kwa asilimia kubwa wale anti- Magufuli sasa ndio wamehodhi madaraka na ili kuonyesha kuwa magu alikuwa hafai wamejaribu kidogo kuachia pale alipokuwa amebana Magufuli, Sasa changamoto ni kadri wanavyoachia ndio wanajiweka hatarini na kuipa nguvu CHADEMA ndio maana kwa sasa hofu ni kubwa sana kuhusu Maandamano.
 
CCM inakufa Natural Death kama ilivyokuwa kwa UNIP KANU na UPC.

Hata huko South ANC inazidi kuchokwa siku hadi siku huko Zimbabwe ZANU-PF imebakia madarakani kwa kuiba kura kuua na kuwatisha wale wote wasioitaka ZANU-PF

Sisi Watanzania tumekichoka Chama Cha Mapinduzi iwapo kutakuwa na Uchaguzi HURU na HAKI bora hata tuchague Chama cha Ndondi kuliko CCM.
 
Habari wanajamvi!
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikifuatilia siasa za Tanzania na kuna mengi ya kuzungumza japo muda ni mchache ila kwa hili la maandamano ya chadema yanayotarajiwa kufanyika tar 24 mwezi huu wa kwanza nikaona si vibaya na mimi nikatoa mtazamo wangu hasa baada ya nguvu kubwa ambayo serikali inatumia kukwamisha maandamano hayo.
Nianze kwa kusema kuwa CCM kama chama tawala kimepitia siasa za panda shuka tangu kuanzishwa kwake na wanauzoefu wa kutosha juu ya siasa za Tanzania na wanajua ya kuwa hali ya nchi kwa sasa si yamatumaini na raia wengi hawana matumaini na serikali hii ya CCM.

Tokea CHADEMA itangaze kutakuwa na maandamano tuliona reaction ya serikali, Kwanza kabisa Mh. Chalamila mkuu wa mkoa husika ambao maandamano yamepangwa kufanyika yaani Dar es salaam alitangaza kutakuwa na usafi ambao utafanywa na Jeshi La Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na jeshi la polisi lakini pia Mh. Paul Makonda Katibu mwenezi wa CCM huyu nae akasema anataka mdahalo na CHADEMA kwani haoni sabaabu ya Chadema kuandamana hasa kupinga miswaada ya sheria za uchaguzi, Tatu baadhi ya kundli la wanasiasa wa vyama vingine tofauti na CHADEMA wakasema hawaungi mkono maandamano hayo, Nne Baadhi ya wafanyabiashara wa kariakoo wakasema hawataandamana, Tano baadhi ya viongozi wa dini.

Swali la msingi ni Kwanini nguvu kubwa inatumika kuyazuia maandamano hayo? Hali yakuwa ni haki ya kikatiba na ni maandamano ya Amani?

Kwanza ni lazima tujue siasa ni Sayansi yenye sanaa ndani yake na kutokana na hili zifuatazo ndio sababu serikali haitaki CHADEMA waandamane.

1. HOFU JUU YA HASIRA WALIZONAZO WANACHI DHIDI YA SERIKALI.
Tutambue kuwa CHADEMA wanataka kuandamana kupinga miswaada ya sheria za uchaguzi lakini hiki ni kipindi ambacho kundi kubwa la wanachi lina hasira na serikali kwakuwa Umeme unasumbua, Huduma mbaya za maji, Elimu lakini Ufisadi umetamalaki kwa kiwango kikubwa na uwajibikaji na uwajibishwaji umeshuka kwa kiwango kilekile ambacho Ufisadi umepanda.
Hili halihitaji jicho la msomi wa PHD kugundua kila mwenye macho anajionea jinsi mambo yalivyo tafrani, Katika kipindi kama hichi serikali haiwezi kuruhusu maandano kwani huenda yakaanza kama maandamano ya kupinga mswaada wa sheria za uchaguzi mwisho yakamalizika kama maandamano ya kupinga mfumuko wa bei, Umeme ,Ufisadi , Rushwa n.k mambo ambayo yanamgusa kila Mtanzania na kwa kiasi kikubwa litawafungua macho watu wengi kitu ambacho CCM hawataki kukisikia kabisa kwani ujinga wa watanzania wengi ni mtaji wao wa Kisiasa.

2. KUIZUIA CHADEMA KURUDISHA NGUVU WALIYOIPOTEZA KWA JAMII.
CCM hawataki CHADEMA wawe karibu na raia kwa namna yeyote kwani wanajua hapo ndipo nguvu ya CHADEMA ilipo. Hivyo kuruhusu maandamano ni kuwafanya CHADEMA kuwa karibu na wanachi jambo ambalo CCM wameshajifunza katika uchaguzi wa 2010 na 2015 kuwa Wananchi wananguvu kubwa hivyo hawawezi kuruhusu nguvu ile CHADEMA waliokuwa nayo wawe nayo tena.

Kwa sababu hizo ndio maana Serikali ya CCM imeamua kuanza hatua za kiushawishi za kuzuia maandamano hayo na njia watakazotumia ni mbili tu.
Moja, ni kuyazuia kabisa kwa kutumia vyombo vya dola jambo ambalo pia linaweza leta taswira mbaya kimataifa kuwa hakuna demokrasia au Mbili kuyaruhusu ila kwa kuyapunguza nguvu maandamano hayo yaani hapa wanatumia mlango wa nyuma alafu wanatokea palepale kwa aliyetumia mlango wa mbele na hii ndio njia ambayo wameamua kuanza nayo kitendo cha kumtumia chalamila na viongozi wa Kisiasa na wafanyabiashara na jeshi kufanya usafi hii yote ni kudhoofisha nguvu ya maandamano hayo na usishangae siku hiyo ya maandano kama yatakuwepo kukajitokeza watu na mabango ya mama anaupiga mwingi, Hili usishangae likitokea ndio siasa za Tanzania lakini pia vyombo vya habari havitaruhusiwa kurusha habari za maandano hapa zitabaki online TV chache ambazo chadema zina mkono wake na labda JF hapa ambapo wamekuwa wakitoa habari pasi upendeleo.
Endapo hili la njia ya pili litatokea maana yake ni kuwa Serikali itakuwa imewapa CHADEMA maji ya vuguvugu ambayo hayakati kiu yaani wamewaruhusu waandamane lakini maandamano yasiyo na matokeo yaliyo kusudiwa.

Katika kuyaepuka yote haya ili CHADEMA Waweze kufanya maandano yenye matokeo waliyoyakusudia ni lazima wachukue hatua mbadala na wao watumie mlango wa mbele na watokee palepale sawa na aliyetumia mlango wa nyuma.
Swali la msingi ambalo Mh.Freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla wanatakiwa kujiuliza ni nini Kifanyike ili Maandamano waliyokusudia yatimie kwa matokeo makubwa?.. Nitarudi baadae Kwasasa ngoja kwanza nitoke nikatafute mlo wa Mtanzania aneishi chini ya dola moja.

Kabla sija-log off niseme tu kwa yanayoendelea kwa sasa Nchini katika mawanda ya Kisiasa tunapata picha ya kuwa Mama anataka kugombea 2025 na yupo serious na hilo , CCM imepoteza nguvu yake kama chama na tumaini pekee lipo kwa vyombo vya dola na mwisho ni kuwa CHADEMA imepoteza ushawishi wake kwa jamii.
Asanteni.
maandamano au fujo na ujambazi wa mapanyarodi na manyumbu 🐒
 
maandamano au fujo na ujambazi wa mapanyarodi na manyumbu 🐒
Kwani Maandamano ya amani si polisi wanakuwepo kuhakikisha ulinzi na usalama?
Yaani mtu atake kuleta fujo alafu akatoe taarifa polisi kuwa siku fulani nitaenda kuleta fujo?
CCM wanajua CHADEMA hawawezi leta fujo ila wanajua kuwaruhusu CHADEMA waandamane ni kujichimbia kaburi lao wao kama chama tawala kisiasa.
Na jambo hilo CCM hawako tayari.
 
Changamoto ninayoiona kwa vyama vikongwe Afrika hususani kusini mwa Sahara km Afrika kusini,Zimbabwe, Msumbiji, Tanzania kuna anguko kubwa linakuja kama ilvyokuwa kwenye Anguko la ukomunisti duniani majukumu ya vyama hivyo ya ukombozi wa kisiasa yanaonekana ku exipire na wakati na historia.Ngoja tuone
 
Kwani Maandamano ya amani si polisi wanakuwepo kuhakikisha ulinzi na usalama?
Yaani mtu atake kuleta fujo alafu akatoe taarifa polisi kuwa siku fulani nitaenda kuleta fujo?
CCM wanajua CHADEMA hawawezi leta fujo ila wanajua kuwaruhusu CHADEMA waandamane ni kujichimbia kaburi lao wao kama chama tawala kisiasa.
Na jambo hilo CCM hawako tayari.
amani ipi na nyumbu bana 🐒

we nyumbu ana amani ya wap tangu lini akati wenzie tu hawamtaki🐒
 
Mbona nyinyi WanaCCM huwa mnaandamana kumsifia Mama yenu? Maandamano ya Amani ni haki ya Mtanzania ya Kikatiba.

Msilete Zengwe zenu.
ndio ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania,

Lakini sio ya manyumbu na mapanyarodi muleta fujo, uharibifu na uporaji 🐒

hiyo haiwezekani NG'Oo 🐒
 
Changamoto ninayoiona kwa vyama vikongwe Afrika hususani kusini mwa Sahara km Afrika kusini,Zimbabwe, Msumbiji, Tanzania kuna anguko kubwa linakuja kama ilvyokuwa kwenye Anguko la ukomunisti duniani majukumu ya vyama hivyo ya ukombozi wa kisiasa yanaonekana ku exipire na wakati na historia.Ngoja tuone
Na hii ni kutokana na vyama hivi kunga'ng'ania njia na mbinu za zamani kuendesha nchi.
Vyama vingi vikongwe kusini mwa Sahara vimekuwa vikitumia nguvu kubwa kubaki madarakani badala ya kuleta maendeleo.
Jambo ambalo ni sawa na kujiangamiza mwenyewe. Kwani kadri ugumu wa maisha unavyozidi ndivyo wananchi wanakosa uvumilivu kwa serikali.
 
Lakini sio ya manyumbu na mapanyarodi muleta fujo, uharibifu na uporaji
Sijui una maana gani lakini ngoja nijibu kama ulivyoandika.

•Nyumbu- Hawa ni Wanyamapori wanapatikana huko Serengeti na maswala yao waulizwe TAWA na TANAPA.

•Panyarodi-Hawa ni Vijana waliokosa Ajira na wakaamua kujihusisha na Uhalifu Jeshi la Polisi Tanzania lilishasema limeshawamaliza.
 
Habari wanajamvi!
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikifuatilia siasa za Tanzania na kuna mengi ya kuzungumza japo muda ni mchache ila kwa hili la maandamano ya chadema yanayotarajiwa kufanyika tar 24 mwezi huu wa kwanza nikaona si vibaya na mimi nikatoa mtazamo wangu hasa baada ya nguvu kubwa ambayo serikali inatumia kukwamisha maandamano hayo.
Nianze kwa kusema kuwa CCM kama chama tawala kimepitia siasa za panda shuka tangu kuanzishwa kwake na wanauzoefu wa kutosha juu ya siasa za Tanzania na wanajua ya kuwa hali ya nchi kwa sasa si yamatumaini na raia wengi hawana matumaini na serikali hii ya CCM.

Tokea CHADEMA itangaze kutakuwa na maandamano tuliona reaction ya serikali, Kwanza kabisa Mh. Chalamila mkuu wa mkoa husika ambao maandamano yamepangwa kufanyika yaani Dar es salaam alitangaza kutakuwa na usafi ambao utafanywa na Jeshi La Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na jeshi la polisi lakini pia Mh. Paul Makonda Katibu mwenezi wa CCM huyu nae akasema anataka mdahalo na CHADEMA kwani haoni sabaabu ya Chadema kuandamana hasa kupinga miswaada ya sheria za uchaguzi, Tatu baadhi ya kundli la wanasiasa wa vyama vingine tofauti na CHADEMA wakasema hawaungi mkono maandamano hayo, Nne Baadhi ya wafanyabiashara wa kariakoo wakasema hawataandamana, Tano baadhi ya viongozi wa dini.

Swali la msingi ni Kwanini nguvu kubwa inatumika kuyazuia maandamano hayo? Hali yakuwa ni haki ya kikatiba na ni maandamano ya Amani?

Kwanza ni lazima tujue siasa ni Sayansi yenye sanaa ndani yake na kutokana na hili zifuatazo ndio sababu serikali haitaki CHADEMA waandamane.

1. HOFU JUU YA HASIRA WALIZONAZO WANACHI DHIDI YA SERIKALI.
Tutambue kuwa CHADEMA wanataka kuandamana kupinga miswaada ya sheria za uchaguzi lakini hiki ni kipindi ambacho kundi kubwa la wanachi lina hasira na serikali kwakuwa Umeme unasumbua, Huduma mbaya za maji, Elimu lakini Ufisadi umetamalaki kwa kiwango kikubwa na uwajibikaji na uwajibishwaji umeshuka kwa kiwango kilekile ambacho Ufisadi umepanda.
Hili halihitaji jicho la msomi wa PHD kugundua kila mwenye macho anajionea jinsi mambo yalivyo tafrani, Katika kipindi kama hichi serikali haiwezi kuruhusu maandano kwani huenda yakaanza kama maandamano ya kupinga mswaada wa sheria za uchaguzi mwisho yakamalizika kama maandamano ya kupinga mfumuko wa bei, Umeme ,Ufisadi , Rushwa n.k mambo ambayo yanamgusa kila Mtanzania na kwa kiasi kikubwa litawafungua macho watu wengi kitu ambacho CCM hawataki kukisikia kabisa kwani ujinga wa watanzania wengi ni mtaji wao wa Kisiasa.

2. KUIZUIA CHADEMA KURUDISHA NGUVU WALIYOIPOTEZA KWA JAMII.
CCM hawataki CHADEMA wawe karibu na raia kwa namna yeyote kwani wanajua hapo ndipo nguvu ya CHADEMA ilipo. Hivyo kuruhusu maandamano ni kuwafanya CHADEMA kuwa karibu na wanachi jambo ambalo CCM wameshajifunza katika uchaguzi wa 2010 na 2015 kuwa Wananchi wananguvu kubwa hivyo hawawezi kuruhusu nguvu ile CHADEMA waliokuwa nayo wawe nayo tena.

Kwa sababu hizo ndio maana Serikali ya CCM imeamua kuanza hatua za kiushawishi za kuzuia maandamano hayo na njia watakazotumia ni mbili tu.
Moja, ni kuyazuia kabisa kwa kutumia vyombo vya dola jambo ambalo pia linaweza leta taswira mbaya kimataifa kuwa hakuna demokrasia au Mbili kuyaruhusu ila kwa kuyapunguza nguvu maandamano hayo yaani hapa wanatumia mlango wa nyuma alafu wanatokea palepale kwa aliyetumia mlango wa mbele na hii ndio njia ambayo wameamua kuanza nayo kitendo cha kumtumia chalamila na viongozi wa Kisiasa na wafanyabiashara na jeshi kufanya usafi hii yote ni kudhoofisha nguvu ya maandamano hayo na usishangae siku hiyo ya maandano kama yatakuwepo kukajitokeza watu na mabango ya mama anaupiga mwingi, Hili usishangae likitokea ndio siasa za Tanzania lakini pia vyombo vya habari havitaruhusiwa kurusha habari za maandano hapa zitabaki online TV chache ambazo chadema zina mkono wake na labda JF hapa ambapo wamekuwa wakitoa habari pasi upendeleo.
Endapo hili la njia ya pili litatokea maana yake ni kuwa Serikali itakuwa imewapa CHADEMA maji ya vuguvugu ambayo hayakati kiu yaani wamewaruhusu waandamane lakini maandamano yasiyo na matokeo yaliyo kusudiwa.

Katika kuyaepuka yote haya ili CHADEMA Waweze kufanya maandano yenye matokeo waliyoyakusudia ni lazima wachukue hatua mbadala na wao watumie mlango wa mbele na watokee palepale sawa na aliyetumia mlango wa nyuma.
Swali la msingi ambalo Mh.Freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla wanatakiwa kujiuliza ni nini Kifanyike ili Maandamano waliyokusudia yatimie kwa matokeo makubwa?.. Nitarudi baadae Kwasasa ngoja kwanza nitoke nikatafute mlo wa Mtanzania aneishi chini ya dola moja.

Kabla sija-log off niseme tu kwa yanayoendelea kwa sasa Nchini katika mawanda ya Kisiasa tunapata picha ya kuwa Mama anataka kugombea 2025 na yupo serious na hilo , CCM imepoteza nguvu yake kama chama na tumaini pekee lipo kwa vyombo vya dola na mwisho ni kuwa CHADEMA imepoteza ushawishi wake kwa jamii.
Asanteni.
Chama Cha Mabwege
 
Back
Top Bottom